SERENGETI BOYS YAIFUNGA DYNAMO, KUTUA USIKU WA MANANE

SERENGETI BOYS YAIFUNGA DYNAMO, KUTUA USIKU WA MANANE

September 13, 2016
Timu ya Mpira wa Miguu ya vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imefanya kambi yake kwa mafanikio huko jijini Victoria kwenye Kisiwa cha Mahe, nchini Shelisheli baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya dhidi ya Northern Dynamo.
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Taifa wa Shelisheli, bao pekee la Serengeti Boys lilifungwa na Muhsin Makame katika dakika 75 ya mchezo huo uliokuwa na ushindani mkali katika vipindi vyote viwili kutokana na kushambuliaana mara kwa mara.

Serengeti Boys ambayo ilikuwa na kikosi cha nyota 21 na viongozi watano, wamemaliza kambi ya huko Shelisheli na hivyo inaondoka jioni ya leo Septemba 13, 2016 saa 11:00 jioni na ikitarajiwa kuingia nchini usiku wa saa 7:45 Septemba 14, 2016 ambako itakuwa kambini hadi siku ya mchezo Jumapili Septemba 18, mwaka huu.
Mchezo huo wa kuwania kucheza fainali za kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17. Fainali hizo zitafanyika jijini Antananarivo, Madagascar hapo Aprili, 2017.
Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Bakari Nyundo  Shime maarufu kwa jina la Mchawi Mweusi, amesema: “Sitaki kuwa na maneno mengi. Nataka Watanzania waje kuona wenyewe. Maana maneno maneno yakizidi inakuwa kama kero. Nataka kujenga utamaduni wa Watanzania kuja wenyewe uwanjani kuona timu yao.”
Katika hatua nyingine, wapinzani wa Serengeti Boys wanatarajiwa kutua Alhamisi wakiwa na kikosi cha watu 40 na kati ya hao ni 22 ni wachezaji. Miongoni kwa kundi hilo pia kuna wanahabari wanne.
Katika orodha ilitumwa TFF, wachezaji wa timu hiyo ni pamoja na Mathieu Lee Valtair, Balou Prince Joel, Bopoumela Chardon, Kiba Konde Ridrique, Kibasila Christ Benilde, Langa Lessen Bercy, Makouana Beni, Mantouari Juste Aldo, Mata Thomas, Mbemba Patchely Rael, Mbenza Kamboleke, Mboungou Prestige, Mebeza Egouep Craiche, Mouandza Mapata, Moungala Ikounga, Mountou Edouard, Ngakosso oko Alves, Ngaloukossi Jossy Ronel, Nguienda Mouanga Bernice, Nguimbi Exau, Ntoto Gedeon, Oboua Danish na Otang Jeordon.
Viongozi wa timu hiyo wamo Ntoto Lacombe ambaye ndiye Mkuu wa Msafara, Goma Ambroise Stephane ambaye ni Mratibu wa msafara, Ngami Gobard – Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Congo – Brazzavile.
Wengine ni maofisa mbalimbali Otende Charles, Moussavou Merrile, Badji Mombo, Berrettini Paulo, Ekariki Basile, Cesana Eraldo, Bakoua Loufouma Narcisse, Okandze Elenga Jean Pierre, Lounou Joste Feller, Mabila Kengue Francois, Loemba Jean Rufin, Mendome Ndoum, Batangounna Ntari na Mbemba Gervais.

DC IKUNGI AITAKA KAMPUNI YA SHANTA GOLD MINE KUWALIPA FIDIA WANANCHI WALIOFANYIWA TATHIMINI ILI KUPISHA UCHIMBAJI WA DHAHABU

September 13, 2016
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi
Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi wakijadili jambo nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya kabla ya kuingia kwenye kikao
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu akielezea namna ambavyo watawalipa wananchi 67 ndani ya wiki hii

WASOMI WAIPONGEZA MeTL GROUP KWA KUFANYA CAREERS FAIR, 25 KUPATA AJIRA

September 13, 2016
  Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza  vyuo  ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.(Habari picha na Modewjiblog).
 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Fatema Dewji-Jaffer akizungumzia idara yake ya masoko inavyofanya kazi wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa kilimo wa kampuni ya MeTL Group, Bw. George Mwamakula akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa masuala ya fedha wa MeTL Group, Bi. Hasina Ahmed akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
  Mtaalamu wa idara ya uzalishaji wa nyuzi na nguo ya MeTL Group, Bw. Clement Munisi akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.


Mtaalamu kutoka kitengo cha mauzo wa MeTL Group, Bw. Yusuf Ali, akizungumza kwenye Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa idara ya uzalishaji na matengenezo wa MeTL Group, Bw. Vijay Raghavan akizungumza kwenye Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.

 Washiriki wakiuliza maswali juu uendeshaji wa vitengo mbalimbali vya makampuni ya MeTL Group wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.

 Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji akijibu maswali yaliyoulizwa na washiriki wa kongamano hilo.
 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Fatema Dewji-Jaffer (katikati) akikabidhi box la zawadi kwa mmoja wa washiriki aliyejishindia kwenye mchezo wa kuokota majina wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji.

Na Mwandishi Wetu
Safari ya Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) kutoa ajira kwa Watanzania 100,000 hadi mwaka 2021 imeanza kufanyika kupitia Job Affairs ambapo limewapa nafasi wasomi mbalimbali nchini kutumia sehemu hiyo kuonyesha uwezo wao, na kati yao wasomi 25 wakipata nafasi ya kujiunga na familia ya zaidi ya wafanyakazi 28,000 wa kampuni ya MeTL Group.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanyika kwa kongamano hilo, wasomi mbalimbali waliipongeza kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited kwa kufanya kongamano la Job Affairs kwani licha ya kutoa nafasi za kazi lakini pia limewasaidia kujijengea uwezo mpya ambao hawakuwa nao awali.
Mmoja wa wasomi hao, Dennis Mtani alisema kupata nafasi ya kuhudhuria kumewajengea jambo lipya kuhusu jinsi ya kuomba nafasi za kazi hadi kuwa wafanyakazi bora katika kampuni.

Alisema kutokana na ukubwa wa kampuni ya Mohammed Enterprises kwa bara la Afrika ni matarajio yao kuwa wamejifunza jambo ambalo hata kama hawatapata nafasi za kazi basi watabaki na uwezo ambao utawasaidia kujua jinsi ya kuomba nafasi katika makampuni mengine ya kimataifa.

“Tumekuja katika kongamano hili wengine hata CV walikuwa hawajui jinsi ya kuandika ili kuomba nafasi na kuajiriwana na kutokana na ukubwa wa hii kampuni kwa nchi za Afrika tumepata elimu ambayo inaweza kutusaidia kwenda kufanya kazi kwa makampuni mengine,” alisema Mtani.

Nae Monica Mziray alisema alijumuika katika kongamano hilo ili kujaribu kutafuta nafasi ya kujiunga na kampuni ya Mohammed Enterprises kwani anaamini ni kampuni kubwa ambayo anaamini ana ndoto za kuifanyia kazi na ambayo inawajali wafanyakazi wake.

“Nimefanya kazi na kampuni zingine lakini niliacha sababu nataka kampuni ambayo inanilia vizuri na inanipa kitu na mimi naipa kitu, nilisoma historia ya Mohammed Enterprises, nimeona ni kampuni kubwa Afrika, nimeona bidhaa zake na naona inaweza niongezea kitu,” alisem Mziray.

Aidha akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Rasilimali wa Mohammed Enterprises, Hassan Dewji aliwambia washiriki ambao wametoka katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu, kwamba Idara ya Rasilimali Watu ya MeTL imekua ikitoa ajira, mafunzo ya kukuza vipaji kwa watanzania wa kada mbalimbali ili kuchukua nafasi za juu katika Makampuni shiriki ya MeTL.

Kuhusu kongamano hilo la kazi alisema linalengo la kupata wasomi wenye taaluma mbalimbali kutoka kwa vijana wa Kitanzania. Kwamba Idara ya Rasilimali Watu imelenga kupata wahitimu katika nyanja za Uhasibu wa fedha, Rasilimali watu, Masoko, Uhandisi, Kilimo na Viwanda vya nguo lakini pia vijana wasomi watapewa mafunzo kwa kipindi cha wiki 52 huku wakiwa wanalipwa na watakapomaliza mafunzo watapewa ajira na kuingizwa katika mfumo wa uwajibikaji.

“Kundi la Makampuni ya MeTL limepata umadhubuti wake kutokana na kuwa na utamaduni wa kuhakikisha kwamba wanakuwa karibu na wafanyakazi wake na kuwajali. Wafanyakazi wa Idara ya Rasimali Watu wamekua wakiandaa mafunzo kuboresha elimu ya wafanyakazi, maarifa na utaalamu,

“Ushiriki wa wafanyakazi ni sehemu ya maono ya wafanyakazi wa Idara ya Rasilimali Watu katika kundi hili la makampuni. Kampuni hii huhakikisha kwamba wafanyakazi wanapata mapumziko, kujitengeneza upya, wanakuwa na siku ya familia, siku ya michezo na kwamba shughuli hizo zinafanywa kwa mpangilio ili kuwezesha kuwepo kwa utamaduni  wa familia moja  inayofanya kazi kwa kushirikiana kwa kiwango cha juu,” alisema Dewji.

WASOMI WAIPONGEZA MeTL GROUP KWA KUFANYA CAREERS FAIR, 25 KUPATA AJIRA

September 13, 2016
  Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza  vyuo  ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.(Habari picha na Modewjiblog).
 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Fatema Dewji-Jaffer akizungumzia idara yake ya masoko inavyofanya kazi wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa kilimo wa kampuni ya MeTL Group, Bw. George Mwamakula akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa masuala ya fedha wa MeTL Group, Bi. Hasina Ahmed akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
  Mtaalamu wa idara ya uzalishaji wa nyuzi na nguo ya MeTL Group, Bw. Clement Munisi akizungumza wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.


Mtaalamu kutoka kitengo cha mauzo wa MeTL Group, Bw. Yusuf Ali, akizungumza kwenye Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.
 Mtaalamu wa idara ya uzalishaji na matengenezo wa MeTL Group, Bw. Vijay Raghavan akizungumza kwenye Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.

 Washiriki wakiuliza maswali juu uendeshaji wa vitengo mbalimbali vya makampuni ya MeTL Group wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise.

 Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji akijibu maswali yaliyoulizwa na washiriki wa kongamano hilo.
 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Fatema Dewji-Jaffer (katikati) akikabidhi box la zawadi kwa mmoja wa washiriki aliyejishindia kwenye mchezo wa kuokota majina wakati wa Kongamano la Ajira kwa Vijana waliomaliza vyuo ambao watapata fursa ya kupata ajira katika makampuni ya MeTL  Group, lililofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Alliance Francaise. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd, Hassan Dewji.

Na Mwandishi Wetu
Safari ya Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) kutoa ajira kwa Watanzania 100,000 hadi mwaka 2021 imeanza kufanyika kupitia Job Affairs ambapo limewapa nafasi wasomi mbalimbali nchini kutumia sehemu hiyo kuonyesha uwezo wao, na kati yao wasomi 25 wakipata nafasi ya kujiunga na familia ya zaidi ya wafanyakazi 28,000 wa kampuni ya MeTL Group.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanyika kwa kongamano hilo, wasomi mbalimbali waliipongeza kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited kwa kufanya kongamano la Job Affairs kwani licha ya kutoa nafasi za kazi lakini pia limewasaidia kujijengea uwezo mpya ambao hawakuwa nao awali.
Mmoja wa wasomi hao, Dennis Mtani alisema kupata nafasi ya kuhudhuria kumewajengea jambo lipya kuhusu jinsi ya kuomba nafasi za kazi hadi kuwa wafanyakazi bora katika kampuni.

Alisema kutokana na ukubwa wa kampuni ya Mohammed Enterprises kwa bara la Afrika ni matarajio yao kuwa wamejifunza jambo ambalo hata kama hawatapata nafasi za kazi basi watabaki na uwezo ambao utawasaidia kujua jinsi ya kuomba nafasi katika makampuni mengine ya kimataifa.

“Tumekuja katika kongamano hili wengine hata CV walikuwa hawajui jinsi ya kuandika ili kuomba nafasi na kuajiriwana na kutokana na ukubwa wa hii kampuni kwa nchi za Afrika tumepata elimu ambayo inaweza kutusaidia kwenda kufanya kazi kwa makampuni mengine,” alisema Mtani.

Nae Monica Mziray alisema alijumuika katika kongamano hilo ili kujaribu kutafuta nafasi ya kujiunga na kampuni ya Mohammed Enterprises kwani anaamini ni kampuni kubwa ambayo anaamini ana ndoto za kuifanyia kazi na ambayo inawajali wafanyakazi wake.

“Nimefanya kazi na kampuni zingine lakini niliacha sababu nataka kampuni ambayo inanilia vizuri na inanipa kitu na mimi naipa kitu, nilisoma historia ya Mohammed Enterprises, nimeona ni kampuni kubwa Afrika, nimeona bidhaa zake na naona inaweza niongezea kitu,” alisem Mziray.

Aidha akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Rasilimali wa Mohammed Enterprises, Hassan Dewji aliwambia washiriki ambao wametoka katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu, kwamba Idara ya Rasilimali Watu ya MeTL imekua ikitoa ajira, mafunzo ya kukuza vipaji kwa watanzania wa kada mbalimbali ili kuchukua nafasi za juu katika Makampuni shiriki ya MeTL.

Kuhusu kongamano hilo la kazi alisema linalengo la kupata wasomi wenye taaluma mbalimbali kutoka kwa vijana wa Kitanzania. Kwamba Idara ya Rasilimali Watu imelenga kupata wahitimu katika nyanja za Uhasibu wa fedha, Rasilimali watu, Masoko, Uhandisi, Kilimo na Viwanda vya nguo lakini pia vijana wasomi watapewa mafunzo kwa kipindi cha wiki 52 huku wakiwa wanalipwa na watakapomaliza mafunzo watapewa ajira na kuingizwa katika mfumo wa uwajibikaji.

“Kundi la Makampuni ya MeTL limepata umadhubuti wake kutokana na kuwa na utamaduni wa kuhakikisha kwamba wanakuwa karibu na wafanyakazi wake na kuwajali. Wafanyakazi wa Idara ya Rasimali Watu wamekua wakiandaa mafunzo kuboresha elimu ya wafanyakazi, maarifa na utaalamu,

“Ushiriki wa wafanyakazi ni sehemu ya maono ya wafanyakazi wa Idara ya Rasilimali Watu katika kundi hili la makampuni. Kampuni hii huhakikisha kwamba wafanyakazi wanapata mapumziko, kujitengeneza upya, wanakuwa na siku ya familia, siku ya michezo na kwamba shughuli hizo zinafanywa kwa mpangilio ili kuwezesha kuwepo kwa utamaduni  wa familia moja  inayofanya kazi kwa kushirikiana kwa kiwango cha juu,” alisema Dewji.

MUWSA WASAFISHA MIFEREJI YA MAJI TAKA KITUO KIKUU CHA MABASI MJINI MOSHI.

September 13, 2016
Tope zilizokuwa zimetuama katika mifereji ya kusafirisha maji taka katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi zikiondolewa.
Licha ya kuwepo na kampuni iliyopewa kandarasi ya usafi katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Moshi bado changamoto ya kuziba kwa mifereji ya kusafirisha maji taka imekuwepo .
Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) walishiriki kuzibua na kuondosha taka zote zilizokuwepo katika mifereji hiyo.
Kitengo cha maji taka cha Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi kilihusika zaidi kuhakikisha hakuna mfereji utakao kuwa umebaki na taka.
Taka ngumu zote ziliondolewa katika mifereji hiyo.
Baadhi ya wafanyabiashara katika kituo hicho kikuu cha mabasi walijitokeza pia katika kusaidia kufanya usafi .
Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukailisha zoezi la usafi katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MKOA WA SINGIDA WAPATWA NA KISHINDO CHA BURUDANI YA MSIMU WA TIGO FIESTA USIKU WA JANA

September 13, 2016
Msanii Ben Pol akiwa jukwaani  kuwapagawisha   wakazi   wa   Singida   kwenye  tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika  uwanja wa  Namfua  usiku  wa  kuamkia     jana.


Dj D Ommy akiwa katika kuhakikisha kuwa kila burudani inayotolewa na wasanii inakuwa katika utaratibu maalum katika usiku wa Tamasha la Tigo Fiesta mkoani Singida katika viwanja vya Namfua usiku wa jana.


FID Q akitumbuiza katika jukwaa la Tigo Fiesta mkoani Singida katika viwanja vya Namfua usiku wa jana












JUX akiwaburudisha wapenzi wa muziki waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Namfua mkoani Singida wakati wa  tamasha la Tigo Fiesta usiku wa jana


Niki wa pili akitumbuiza katika jukwaa la Tigo Fiesta usiku wa jana Mkoani Singida 


Malkia wa Uswazi Snura akiwa na madancer wake katika kuwapagawisha wakazi wa Singida katika usiku wa Tigo Fiesta usiku wa jana katika viwanja vya Namfua 
Maelfu ya wakazi wa SIngida waliojitokeza kwa wingi kushuhudia Tamasha kubwa la burudani Tigo Fiesta lilifanyika katika viwanja vya Namfua mkoani humo usiku wa jana.

Kamoga Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu aamua kuanza na Mungu

September 13, 2016
Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga, ambaye ameteuliwa mwishoni mwa wiki jana amesema anaamini ni Mungu aliyemuweka kwenye nafasi hiyo ili  awatumikie wananchi wa Mbulu kwa wakati huu. 

Akiongea kwenye ibada ya Jumapili hii  ndani ya  Kanisa la Living Water Center Kawe, wakati alipopewa nafasi na mtumishi wa  Mungu  Apostle Onesmo Ndegi  ili asalimia Kanisa Mheshimiwa Kamonga  alisema, anakwenda kwenye wilaya yenye changamoto nyingi za kimaendeleo ila anaamini Mungu atamwezesha kuzitatua kwa nafasi yake akishirikina na wananchi pamoja na  viongozi wengine kati halimashauri ya Mbulu.

Kamonga alisisitiza kuwa kwa kupata  nafasi hii ya  Ukurugenzi bado  ataendelea na utumishi wake kwa Mungu maana anaamini huo ndio uliomfanya kufikia hatua hiyo,hivyo kuamua kuwa anamtanguliza Mungu kaika kila atakachokuwa anafanya,alisema Kamoga

Pia alitoa shukurani za dhati kwa Mtumishi wa Mungu Apostle Ndegi pamoja na  watumishi wengine kanisani hapo na kusema kuwa kati ya vitu ambavyo hawezi kuvisahau na malezi mazuri ya kiroho pamoja na mafindisho ambayo amekuwa akiyapata kutoka  kwa Apostle Ndegi na watumishi wengine kanisani hapo, akisema mafundisho hayo yamesababisha kuwa vile alivyo sasa! Mwisho Mtumishi wa Mungu Mtume Onesmo Ndegi  na waumini walifanya maombi kwa ajili yake ili Mungu aambatane naye katika utumishi wake kwenye nafasi hiyo ya Ukurugenzi!.

Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga
Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga akiwa na Baba yake wa Kiroho Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimsiliza kwa makini akielezea uteuzi wake.
Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga akiwa na Baba yake wa Kiroho Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimsiliza kwa makini akielezea uteuzi wake.
Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimwombea Hudson Kamogaakiwa amepiga magoti
Waumini wa Kanisani Living Water Center Kawe wakiwa wamenyoosha mikono kwa Hudson Kamoga kuomba kwa ajili yake
Best Regards, gospelhabari.blogspot.com Tunu Bashemela Jr Managing Director Kingdom Heritage P.O.Box 11681 kingdomheritagetz@gmail.com +255 712116647 Dar es salaam Tanzania Better Community Better Life