AFRICAN SPORTS WAANZA VEMA MAANDALIZI YA LIGI DARAJA LA KWANZA.
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
TIMU YA African Sports “Wanakimanumanu “jana ilianza
vema maandalizi ya kuelekea michuano ya Ligi daraja la kwanza baada ya
kuibamiza timu ya Maafande wa Jeshi la Magereza mkoani hapa Small Prison mabao
2-0.
Mchezo huo wa kirafiki ulichezwa kwenye uwanja wa
CCM Mkwakwani na kushuhudiwa na mashabiki mbalimbali wa soka mkoani hapa.
African Sports iliyopanda daraja msimu huu na
kufanikiwa kucheza ligi daraja la kwanza ikwisha kucheza michezo mbalimbali ya
majaribio ili kuweza kukipa makali kikosi hicho ambacho kitashiriki ligi hiyo
kwa mara ya kwanza tokea iliposhuka daraja miaka.
Katika mchezo huo bao la kwanza la African Sports
lilifungwa dakika ya 42 kupitia Mohamed Farid ambaye aliweza kutumia uzembe wa
mabeki wa wapinzani wao kupachika wavuini bao hilo kabla ya timu hizo
haijakwenda mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote
ziliingia uwanjani zikiwa na nguvu mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi
ya wachezaji wao.
Wakionekana kujipanga kwwenye mchezo huo, African
Sports waliweza kuongeza wimbi la mashambulizi langoni mwa timu pinzani hali
iliyopelekea kuongeza bao la pili ambalo lilifuingwa na Evalisti Joseph ambaye
alimaliza kazi nzuri iliyofanywa na Mohamed Farid.
Akizungumza baada ya kumalizika mchezo huo,Ofisa
Habari wa timu ya African Sports ,Saidi Karsandas alisema kuwa mipango ya timu
hiyo ni kucheza mechi nyingi za majaribio ili kuweza kukiweka kikosi hicho
imara kwa ajili ya michuano ya ligi daraja la kwanza.
MWAMBOA WAPANGA KUTOA ELIMU YA UFUNDI SEREMALA KWA VIJANA .
KUSHOTO NI RAIS JAKAYA KIKWETE AKISALIMIA NA MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO MKOANI TANGA,ALHAJ MAJID MWANGA WAKATI ALIPOFANYA ZIARA WILAYANI HUMO. |
NA MWANDISHI WETU,LUSHOTO.
KIKUNDI cha Ufugaji wa Nyuki na Hifadhi ya Mazingira cha Mwamboa kilichopo Kata ya Mwangoi wilayani Lushoto mkoani Tanga kimepanga kutoa mafunzo kwa vijana wa kike na wa kiume kwenye fani za ufundi seremala kwa ajili ya kutengeneza mizinga ya kisasa,uchakataji wa asali na Nta ifikapo Juni 2015.
Wakiwa na madhumuni ya kutoa ajira kwa vijana wasiopungua 20 lengo likiwa kuwakomboa na limbi la umaskini pamoja na kuwaepusha kukaa vijiweni ambapo hutumia muda mwingi kufanya vitendo viovu kwenye jamii zao ikiwemo matumizi ya madawa ya kulevya.
Hayo yalielezwa na Ofisa Ugani wa Kata hiyo, Julius Mshauri wakati akizungumza na blog hii ambapo alisema kuwa licha ya hivyo wamepanga kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki kutoka kilo 1,000 iliyopo sasa hadi kufikia 2,500 ifikapo Juni 2015.
Mashauri alisema kuwa katika kuhakikisha jambo hilo linapata mafanikio tayari wamekwisha kustawisha miche ya miti ya aina tofauti tofauti ipatayo 15,000 na kuiuza kwa wananchi kulingana na mahitaji yao ikiwemo kuigawa kwa wanavikundi kwa lengo la kuhifadhi mazingira wakati msimu wa mvua unapoanza mwaka huu.
Akizungumzia chimbuko la kikundi hicho alisema kuwa ni mradi wa
utafiti wa chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo kupitia program yao
ijulikanavyo ASARECA(Associationfor Strehgttening Agricultural
Research in Eastern and Central Africa).
Alisema kuwa ndani ya program hiyo kikundi hicho kimeweza kushiriki kwenye mafunzo ya aina mbalimbali hasa ya ufugaji bora wa nyuki na utafutaji wa masoko kwa kushiriki kwenye maenyesho hususani ya kibiashara ya kimataifa na pia yale ya nanenane.
Ofisa ugani huyo alisema kikundi hicho kilipata ufadhili kutoka
serikali ya Poland kwa kupitia shirika la Poland East Africa Economic Foundation ambapo waliweza kufanya nao kazi kwa kipidi cha mwaka mmoja.
Hata hivyo alisema kuwa ndani ya kipindi hicho walifanya mambo
mbalimbali ikiwemo ujenzi wa kituo cha kikundi hicho ambapo ujenzi huo uligharimu kiasi cha sh.milioni 45 zilitumika mbali na nguvu za wananchi zilizotumika kwa wanakikundi zilikuwa ni tsh milioni 9.
KIKUNDI cha Ufugaji wa Nyuki na Hifadhi ya Mazingira cha Mwamboa kilichopo Kata ya Mwangoi wilayani Lushoto mkoani Tanga kimepanga kutoa mafunzo kwa vijana wa kike na wa kiume kwenye fani za ufundi seremala kwa ajili ya kutengeneza mizinga ya kisasa,uchakataji wa asali na Nta ifikapo Juni 2015.
Wakiwa na madhumuni ya kutoa ajira kwa vijana wasiopungua 20 lengo likiwa kuwakomboa na limbi la umaskini pamoja na kuwaepusha kukaa vijiweni ambapo hutumia muda mwingi kufanya vitendo viovu kwenye jamii zao ikiwemo matumizi ya madawa ya kulevya.
Hayo yalielezwa na Ofisa Ugani wa Kata hiyo, Julius Mshauri wakati akizungumza na blog hii ambapo alisema kuwa licha ya hivyo wamepanga kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki kutoka kilo 1,000 iliyopo sasa hadi kufikia 2,500 ifikapo Juni 2015.
Mashauri alisema kuwa katika kuhakikisha jambo hilo linapata mafanikio tayari wamekwisha kustawisha miche ya miti ya aina tofauti tofauti ipatayo 15,000 na kuiuza kwa wananchi kulingana na mahitaji yao ikiwemo kuigawa kwa wanavikundi kwa lengo la kuhifadhi mazingira wakati msimu wa mvua unapoanza mwaka huu.
Akizungumzia chimbuko la kikundi hicho alisema kuwa ni mradi wa
utafiti wa chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo kupitia program yao
ijulikanavyo ASARECA(Associationfor Strehgttening Agricultural
Research in Eastern and Central Africa).
Alisema kuwa ndani ya program hiyo kikundi hicho kimeweza kushiriki kwenye mafunzo ya aina mbalimbali hasa ya ufugaji bora wa nyuki na utafutaji wa masoko kwa kushiriki kwenye maenyesho hususani ya kibiashara ya kimataifa na pia yale ya nanenane.
Ofisa ugani huyo alisema kikundi hicho kilipata ufadhili kutoka
serikali ya Poland kwa kupitia shirika la Poland East Africa Economic Foundation ambapo waliweza kufanya nao kazi kwa kipidi cha mwaka mmoja.
Hata hivyo alisema kuwa ndani ya kipindi hicho walifanya mambo
mbalimbali ikiwemo ujenzi wa kituo cha kikundi hicho ambapo ujenzi huo uligharimu kiasi cha sh.milioni 45 zilitumika mbali na nguvu za wananchi zilizotumika kwa wanakikundi zilikuwa ni tsh milioni 9.
WEMA SEPETU ANENA HAYA BAADA YA DIAMOND PLATINUMZ KUTANGAZA NDOA
BINTI APOTEZA MAISHA ZIKIWA ZIMEBAKI SIKU CHACHE AFUNGE NDOA
Binti
ambaye hakuweza kufahamika jina lake kwa haraka (pichani chini), ambaye
alikuwa afunge ndoa na mchumba wake hivi karibuni, amepata ajali na
kufariki dunia akiwa na 'mchepuko'.
Aidha
imeelezwa kuwa wakati mchumba wake akiwa katika harakati za kukamilisha
mipango ya ndoa akapata taarifa kuwa mchumba wake huyo amefariki kwa
ajali ambapo hakuweza kuamini hadi alipoonyeshwa picha za ajali hiyo.
Imeelezwa
kuwa marehemu alimuaga mchumba wake huyo kuwa anakwenda kulala kwa dada
yake na kwenda kinyume na alivyoaga na kukutwa na ajali hiyo
iliyompelekea umauti. Katika ajali ya gari hilo lililokuwa na wapenzi
wawili wote wamepoteza maisha papo hapo huko mkoani Geita.
marehemu enzi za uhai wake (pichani chini na juu)
Baada ya kupata ajali. Habari na picha kwa hisani ya mdau, Tarime
OKWI AJIFUNGA TENA SIMBA MIAKA MIWILI.
STAILI
ile ile waliyotumia Yanga SC kumpata mshambuliaji Emmanuel Arnold Okwi ndiyo
ambayo klabu yake ya zamani, Simba SC inaitumia kumrejesha kundini Mganda huyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jioni hii mjini Dar es Salaam, Okwi amesema
kwamba amesaini Simba SC mkataba huru wa muda, baada ya Yanga SC kumpa barua ya
kusitisha mkataba naye jana pamoja na kumshitaki Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF).
Okwi amesema ameamua kuomba kuichezea Simba SC kipindi hiki ambacho ana
matatizo na Yanga SC ili kulinda kipaji chake, kwa kuwa hata FIFA haitaki
mchezaji akae bila kucheza.
“Sasa wakati Yanga wanaendelea na kesi yao, mimi ninaomba nichezee
Simba SC ili kulinda kipaji changu. Nimewaandikia barua TFF na FIFA pia na nina
matumaini usajili wangu utaidhinishwa, kwa sababu mimi si tatizo katika
hili,”amesema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans
Poppe amesema kwamba wamemsaini mchezaji huyo baada ya kupitia kwa kina suala
lake na Yanga SC na kugundua haki ipo upande wa mchezaji.
“Baada ya kulipitia suala lake na Yanga kwa undani kabisa na vielelezo ambavyo
mchezaji mwenyewe ametupatia, tumejiridhisha tuko sahihi kumsaini ili acheze
mpira kunusuru kipaji chake kipindi hiki ambacho ana matatizo na Yanga
SC,”amesema Poppe.
Yanga mtanikoma; Okwi
akiwa ameshika jezi yake nbamba 25 kwa pamoja na Hans Poppe
Tayari Simba SC imetuma jina la mchezaji huyo katika usajili wake TFF
na ataungana na Mganda mwenzake, Joseph Owino, Warundi Pierre Kwizera na Amisi
Tambwe na Mkenya, Paul Kiongera katika wachezaji watano wa kigeni.
“Tumewaandikia barua TFF kuomba kumtumia mchezaji huyu kwa muda wakati kesi
yake na Yanga inaendelea, tumeambatanisha na barua yake ambayo yeye anatuomba
kucheza kwetu kulinda kipaji chake,”amesema Poppe.
Okwi aliichezea Simba SC tangu mwaka 2009 kabla ya Januari mwaka jana
kuuzwa kwa dola za Kimarekani 300,000 Etoile du Sahel ya Tunisia. Etoile
haikulipa fedha hizo Simba SC na baadaye ikaingia kwenye mgogoro na Okwi,
aliyedai hakulipwa pia mishahara yake kwa miezi mitatu. Okwi akawafungulia
Etoile kesi FIFA na akaomba wakati mgogoro wao unaendelea, aruhusiwe kuchezea
timu yoyote kulinda kipaji chake, ndipo akajiunga na SC Villa ya kwao.
Akiwa SC Villa ndipo aliposaini Yanga SC Desemba mwaka jana na pamoja na
mapingamizi yaliyoanzia ndani, na baadaye klabu yake, Etoile- lakini Okwi
aliidhinishwa kuichezea timu hiyo ya Jangwani.
Okwi aliichezea Yanga
SC mechi 11 na kuifungia mabao matano- lakini kuelekea mechi tano za mwisho za
Ligi Kuu msimu uliopita akaingia kwenye mgogoro na klabu hiyo. Okwi
alisusa kushinikiza amaliziwe fedha zake za usajili na mgogoro wao umeendelea
huku mchezaji huyo akiwa amesusa tangu Machi, miezi minne tu baadaye tangu
asajiliwe.
Vikao kadhaa
vimekwishafanyika baina ya Okwi na Yanga SC tangu hapo kutafuta suluhu ya suala
hilo na kikao cha mwisho leo baina ya mchezo huyo na Mwenyekiti wa klabu hiyo,
Yussuf Manji matokeo yake ni nyota huyo kurejea Msimbazi.
Kuhusu deni lao la
dola 300,000 kumuuza mchezaji huyo Etoile, Poppe amesema haihusiani kabisa na
usajili wake huu wa sasa. “Ile kesi yetu ya madai ya fedha zetu kule FIFA
ilikwishamalizika na vielelezo vyote vilipelekwa, bado kutolewa hukumu tu,”
amesema
Subscribe to:
Posts (Atom)