RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA NAIROBI SOUTHERN BYPASS KATIKA ENEO LA KAREN NCHINI KENYA

November 01, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kuwasili katika eneo ka Karen jijini Nairobi kwa ajili ya kufungua rasmi barabara ya kupunguza msongamano ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati wa nyimbo za Taifa zikipigwa mara baada ya kuwasili katika eneo la Karen jijini Nairobi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Naibu Rais wa Kenya William Rutto pamoja na viongozi wengine, wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya kupunguza msongamano ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Karen nchini Kenya mara baada ya kufungua barabara ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.




Sehemu ya barabara hiyo ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakicheza wimbo pamoja na kikundi cha kwaya katika eneo la Karen mara baada ya kufungua barabara hiyo ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Bi. Lucy Karuga kuhusu usindikaji wa mazao ya chakula katika kiwanda cha Maziwa cha Eldoville katika eneo la Karen nchini Kenya.

KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA LEO

November 01, 2016
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akizungumza bungeni mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Tarime, Ester Matiko bungeni mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson akizungumza na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja, bungeni mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Singida Kaskazini , Lazaro Nyalandu kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wabunge wanawake kutoka bunge la Zimbabwe kwenye jengo la utawala la Bunge mjini Dodoma Novemba 1, 2016.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

WASHIRIKI WA TIGO FIESTA SUPER NYOTA WATAMBULISHWA JIJINI DAR ES SALAAM

November 01, 2016
 Mratibu wa Tamasha la Fiesta 2016 kutoka Tigo, Balla Shareeph(kushoto) akiongea na waandishi wa habari  kutambulisha udhamini wa Tigo kwenye shindano la Super Nyota, jumla ya washiriki 16 walipatikana mikoani ambao watashindana siku ya ijumaa kwenye fainali na kupata washindi wawili, Wengine pichani mshiriki Galla Bway(katikati) na Mratibu wa shindano la Super Nyota toka Clouds Nickson George.

Mratibu wa shindano la Super Nyota toka Clouds Nickson George(kulia)akiongea na waandishi wa habari kutambulisha washindi wa Super Nyota 16 waliopatikana mikoani ambao watashindana siku ya ijumaa kwenye fainali na kupata washindi wawili.

Mratibu wa Tamasha la Fiesta 2016 kutoka Tigo, Balla Shareeph(kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu mshiriki wa Super Nyota, Galla Bway wa Dsm kwa niaba wenzie 16, Kulia ni Nickson George kutoka Clouds Media.





Dar es Salaam  Novemba 1, 2016 Kampuni inayoongoza kwa maisha ya kidijitali ya Tigo Tanzania  leo imewatambulisha washindi 16 wa shindano la Tigo Fiesta Super Nyota lililofanyika katika mikoa 15 ya Tanzania Bara. Shindano hilo lililoratibiwa na Kampuni ya Prime Time Promotions liliendeshwa katika mikoa  hiyo kwa kipindi cha miezi miwili na nusu. Mshindi wa fainali yake atajulikana wakati wa fainali ya mwisho Novemba 5, 2016 itakayofanyika jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika mkutano wa vyombo vya habari  wakati wa kutangaza washindi hao, Mratibu wa mradi wa Tamasha la Fiesta 2016 kutoka Tigo, Balla Shareeph alisema, “ Tigo inaona fahari kuinyanyua sekta ya muziki ya Tanzania  kwa kuwapatia  wasanii  wanaoibukia  jukwaa la kuonesha  vipaji vyao waweze kufikia kiwango cha juu nchini na  wakati huo huo kuwawezesha kutambuliwa na chapa mbalimbali za muziki.”
Shareeph aliwapongeza  washindi  kwa kutumia nafasi hiyo kuwakumbusha  wao wenyewe pamoja na umma kwa ujumla kwamba wanaweza kupata tiketi  zao kwa  ajili ya fainali hiyo ya kuhitimisha tamasha la Fiesta 2016 ambalo litafanyika  katika viwanja vya Leaders Novemba 5, 2016  kwa kutumia mtandao wa Tigo Pesa.
Shareeph alifafanua, “Ili kupata tiketi kupitia Tigo Pesa  wateja wote wa Tigo na wasio katika mtandao huu  wanatakiwa kulipia tiketi kwenda namba 0678 888 888. Mkakati huu unalenga kuwapatia Watanzania njia ya kawaida na rahisi  ya kupata tiketi zao.”  
Washindi  Super Nyota 16  ambao majina yao ni Nchama Anton a.k.a Nchama, Raphael  Charles  Manengo  a.k.a Manengo kutoka (Mwanza), Ibrahim Juma   a.k.a   Mpanduji(Shinyanga) , Obed  Moses   a.k.a    O strings(Muleba), Salum Asman   a.k.a  Alinacha ( Kahama), Gasper Festo    a.k.a   YOW (Tabora)  Alex Joseph    .a.k.a  TIZO( Singida), Godfrey Andrew Mhoja  a.k.a  NEXUS( Dodoma) Hamad Hussein  a.k.a  Med Botion (Morogoro)  Cyril Henry Isidor a.k.a So Real(Tanga) Wilson Pascal     a.k.a  Willy Desmiller( Mtwara )   Charles Mariki  a.k.a Gerere(Moshi)    Mohammedy  Amiry  a.k.a  Croozy (Arusha), Amina Chibaba    a.k.a  Ammy Chiba  (Mbeya)   Leonard John  Haule   a.k.a sauti classic (Sumbawanga)    wata zawadiwa simu ya kisasa ya Tecno  Y3+ Music, ikiwa na muda wa maongezi.
 Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa pia na Mratibu wa shindano la Super Nyota  chini ya mrengo wa Tamasha la Fiesta 2016, Nickson George ambaye alisema, “Tunayofuhara  kubwa kutangaza  kwamba washindi 16 Super Nyota  ambao watashiriki katika Fainali Kuu  ya Fiesta 2016. Tunatarajia  kuendelea kishukuru jamii kwa kuandaa shindano kama hili  katika kuinyanyua sekta ya muziki na burudani ndani ya Tanzania.”
Tamasha ya Tigo Fiesta 2016  ni tukio linaloendeshwa kwa ubia baina Kampuni ya Prime Time Promotions na Tigo Tanzania na wakati huo huo Tigo ikiwa ndio mdhamini mkuu.