NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
KOCHA Msaidizi timu ya Simba,Jamhuri Kiwelu "Julio"ameipiga vijembe timu ya Coastal Union ya Tanga kwa kusema yenye ni miongoni mwa makocha waliotoa mchango mkubwa kwenye timu hiyo na kuiambia kuwa watakutana kwenye ligi.
Julio alitoa kauli hiyo hivi karibuni mara baada ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki kati ya timu hiyo na Coastal Union,mchezo uliomalizika kwa Simba kukubali kichapo cha bao 1-0 bao ambalo lilifungwa na Chrispian Udula aliyetumia uzembe wa mabeki wa Simba kupachika wavuni bao hilo.
Alisema mchezo huo ulikuwa mzuri na wenye upinzani mkubwa kutokana na timu zote kucheza vema lakini pia ushindi huo wa wapinzani wao umewapa hasira ya kutaka kulipiza kisasi kwao kwenye mechi ya ligi kuu kwani huo ndio mpango wao ni kucheza ligi kwa mafanikio msimu ujao.
Kocha huyo alisema walifurahi kucheza mechi hiyo ambayo ilikuwa kipimo cha kuangalia aina ya uchezaji inaoucheza timu yao huku akitolea visingizio kuwa mwamuzi wa mchezo huo,Isihaka Shirikisho kuwa alichangia wao kukosa ushindi kwenye mchezo huo.
Kwa upande wake,Kocha Mkuu wa Coastal Union,Hemed Morroco alisema huo ni mwanzo mzuri kwa timu hiyo kwani malengo yao makubwa ni kuhakikisha wanazifunga timu zote zitakazocheza kwenye uwanja wao wa nyumbani na ugenini ili kuweza kurudisha heshima ya mwaka 1988 ya kuchukua ubingwa wa ligi hiyo.
KOCHA Msaidizi timu ya Simba,Jamhuri Kiwelu "Julio"ameipiga vijembe timu ya Coastal Union ya Tanga kwa kusema yenye ni miongoni mwa makocha waliotoa mchango mkubwa kwenye timu hiyo na kuiambia kuwa watakutana kwenye ligi.
Julio alitoa kauli hiyo hivi karibuni mara baada ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki kati ya timu hiyo na Coastal Union,mchezo uliomalizika kwa Simba kukubali kichapo cha bao 1-0 bao ambalo lilifungwa na Chrispian Udula aliyetumia uzembe wa mabeki wa Simba kupachika wavuni bao hilo.
Alisema mchezo huo ulikuwa mzuri na wenye upinzani mkubwa kutokana na timu zote kucheza vema lakini pia ushindi huo wa wapinzani wao umewapa hasira ya kutaka kulipiza kisasi kwao kwenye mechi ya ligi kuu kwani huo ndio mpango wao ni kucheza ligi kwa mafanikio msimu ujao.
Kocha huyo alisema walifurahi kucheza mechi hiyo ambayo ilikuwa kipimo cha kuangalia aina ya uchezaji inaoucheza timu yao huku akitolea visingizio kuwa mwamuzi wa mchezo huo,Isihaka Shirikisho kuwa alichangia wao kukosa ushindi kwenye mchezo huo.
Kwa upande wake,Kocha Mkuu wa Coastal Union,Hemed Morroco alisema huo ni mwanzo mzuri kwa timu hiyo kwani malengo yao makubwa ni kuhakikisha wanazifunga timu zote zitakazocheza kwenye uwanja wao wa nyumbani na ugenini ili kuweza kurudisha heshima ya mwaka 1988 ya kuchukua ubingwa wa ligi hiyo.