MFUMO WA BENKIWAKALA WA BIMA WAKUZA BIASHARA YA BIMA NCHINI

April 06, 2023


Na. Farida Ramadhani WFM, Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Mfumo wa Benkiwakala wa Bima umesaidia kukuza biashara ya Bima nchini.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Morogoro Kusini Mhe. Innocent Edward Kalogeris aliyetaka kujua kama Serikali haioni kuwa kuruhusu Benki kuwa Wakala wa Bima, Mawakala wengine watafunga biashara kwa kukosa wateja.

Mhe. Nchemba alisema Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na wadau wa bima ilianzisha Benkiwakala wa Bima ili kuongeza wigo wa usambazaji na upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi.

“Idadi ya Wakala wa Bima wa Kawaida imekuwa ikiongezeka sambamba na Benkiwakala wa Bima kwa sababu hali hii imechochea ushindani, ubunifu na kutegemeana”, alibainisha Mhe. Nchemba.

Alisema Takwimu zinaonesha Benkiwakala waliosajiliwa ni 14 (2020), 23 (2021), 27 (2022) na 30 hadi Machi 2023 huku Wakala wa Bima wa Kawaida waliosajiliwa ni 745 (2020), 789 (2021), 910 (2022) na 960 kati ya Julai 2022 na Machi 2023.




MAAFISA TEHAMA HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO WAPEWA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA MAZINGIRA YA MTOA HUDUMA

April 06, 2023


Mkuu wa Idara ya Udhibiti Ubora wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga  (Bombo ) Joseph Nzige akitoa mafunzo ya uboreshaji wa mazingira ya mtoa huduma kwa dhana ya 5S-KAIZEN kwa Maafisa Tehama wa Hospitali hiyo,Picha na Hospitali ya Rufaa ya Bombo   

Mkuu wa Idara ya Udhibiti Ubora wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga  (Bombo ) Joseph Nzige akitoa mafunzo ya uboreshaji wa mazingira ya mtoa huduma kwa dhana ya 5S-KAIZEN kwa Maafisa Tehama wa Hospitali hiyo,Picha na Hospitali ya Rufaa ya Bombo   
Mkuu wa Idara ya Tehama wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo William Masika  wa kwanza kulia akiwa na maafisa tehama wengine wakifuatilia mafunzo hayo
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini