Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kanda ya kaskazini,Amani Golugwa akizungumza na waandishi wa habari mapema jana kuhusu kupotea kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kwekitui Lushoto kupitia chama hicho Miraji
Kassimu ,kulia kwa katibu huyo ni Katibu wa Baraza la Vijana Chadema mkoa wa Tanga Jonathani Baweje na kushoto kwake ni Afisa kutoka chama hicho kanda hiyo Amina Thaguti "Aminata"
PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Pambalo
la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa
jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na
kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh.
500,390,000.
Mechi
hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo
msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi
kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh.
20,000 na sh. 30,000.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio
cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata
tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha
sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo
mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81,
tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi
sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
sh. 14,708,415.12.
Mwisho.
Mradi wa kituo cha Kupoozea umeme Sahare ni juhudi za Serikali Kuu.
Na Oscar Assenga, Tanga.
IMEELEZWA kuwa mradi wa
kituo cha kupozea umeme kilichopo Sahare (33/11Kv,15MVA)ni muendeleo wa Juhudi
za serikali kuu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hapa nchini kuendeleza
usambazaji wa umeme wa uhakika katika maeneo yote hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa
na Mkurugenzi wa Millenium Challenge Tanzania,Mhandisi,Ipack Chanji wakati
akitoa taarifa ya mradi wa kituo hicho kidogo cha kusambazia umeme Sahare kwa
kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa 2013 ambapo amesema mradi huo
ulianza Juanri mwaka 2011 na unatarajiwa kukamilika Julai 2013.
Chanji amesema mradi huo
ni utatumia kiasi cha (dola 1,541,408.95) ambazo ni sawa na shilingi za
kitanzania 2,508,643,066.12(Bilioni mbili milioni mia tano na nane,laki sita
arobaini na tatu elfu sitini na sita na senti kumi na mbili) zilizopatikana
kupitia akaunti ya changamoto za millennia ikiwa ni msaad wa watu wa marekani.
Amesema faida za mradi
huo ni kuongeza nguvu ya umeme hasa kwa maeneo ya viwandani kitendo ambacho
kitavutia wawekezaji ndani na nje pamoja na kupatikana umeme wa uhakika kwa mahitaji ya nyumbani na
maofisini na hivyo kuongeza tija kwenye uzalishaji mali hasa za viwandani
ikiwemo kukua kwa pato la Taifa.
Mwenge huo umezindua miradi 7 yenye thamani ya
bilioni 8 katika wilaya ya Tanga ambayo ni maabara katika shule ya sekondari
st.christina,barabara ya viwandani,chama cha ushirika wafugaji maziwa
kichangani,umeme,
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)