PICHA VURUGU KUBWA ZATOKEA MJINI IRINGA POLISI WALAZIMIKA KUTUMIA MABOMU,NI KATIKA ENEO LA IPOGOLO
Askari wa FFU wakiwa katika msako wa kuwasaka waliohusika na vurugu hizo eneo la Ipogolo mjini Iringa
MBOWE AKABIDHI AMBULANCE MBILI KWA HOSPITALI YA WILAYA YA HAI NA HOSPITALI YA MACHAME
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akiwa amembeba mtoto mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Kuni na kulakiwa na wananchi katika jimbo hilo. |
Naibu Waziri wa Nishati na Madini atembelea mgodi wa dhahabu bulyanhulu
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kushoto) akipeana mkono
na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad
Gordon, wakati alipowasili kutembelea mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu,
ulioko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili 11, 2015.
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (aliyesimama) akitoa
hotuba yake mwanzoni mwa ziara yake ya kutembelea mgodi wa dhahabu wa
Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili
11, 2015. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini
ya Acacia, Brad Gordon, na kulia ni makamu wa rais wa kampuni hiyo
anayeshughulikia masuala ya kampuni hapa Tanzania, Deo Mwanyika.
Kaimu
Meneja Mkuu mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala,
mkoani Shinyanga, Benedict Busunzu, akizungumza shughuli za uchimbaji
madini za mgodi huo na huduma zitolewazo kwa jamii, wakati naibu waziri
wa jishati na madini, Charles Kitwanga, alipofanya ziara ya kutembelea
mgodi huo, Jumamosi Aprili 11, 2015.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon,
akizungumza wakati wa uwasilishaji shughuli mbalimbali zifanywazo na
migodi inayomilikiwa na kampuni hiyo hapa nchini ya Bulyanhulu, North
Mara na Buzwagi, wakati wa ziara ya naibu waziri wa nishati na madini,
Charles Kitwanga, alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu uliko wilaya ya
Msalala mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili 11, 2015.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon,
(wapili kushoto), akimpa maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini,
Charles Kitwanga, (watatu kushoto), alipotembelea eneo la chini ya ardhi
la mgodiwa Bulyanhulu kiasi cha kilomita 1.5 chini ya bardhi, Jumamosi
Aprili 11, 2015. Kushoto ni mwenyekiti wa kampiuni ya uchimbaji dhahabu
ya Mlalo, Mohammed Hussein.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon,
(Kulia), akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 749.53, Afisa
Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shjinyanga, Mophen
Mwakajonga, ikiwa ni kodi ya huduma (service levy), huku Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Charles Kitwanga (katikati) akishuhudia. Hafla hiyo
ilifanyika kwenye mgodi wa Bulyanhulu ulioko wilayani humo April 11,
2015.
Sehemu
ya Ujumbe ulioambatana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles
Kitwanga katika ziara ya mgodi wa Bulyanhulu April 11, 2015.
Naibu
waziri wa nishati na madini, Charles Kitwanga, (wakwanza kushoto) na
ujumbe wake, wakipatiwa maelezo ya kiusalama muda mfupi kabla ya kuanza
ziara ya kutembelea shughuli za uchimbaji madini chini ya ardhi kwenye
mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu uliko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga
Jumamosi Aprili 11, 2015.
Naibu
waziri wa nishati na madini, Charles Kitwanga, (kushoto), na Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon,
(kulia), wakimsikiliza mtaalam wa shughuli za uchimbaji madini ardhini,
wa mgodi huo, wakati wa ziara ya naibu waziri Jumamosi Aprili 11, 2015.
IMETOSHA yaendeleza mkakati wake kimataifa kusafisha jina la nchi
Mkakati wa kutokomeza unyanyapaa na mauaji ya watu wenye ualbino nchini, uitwao IMETOSHA, jana ulianza rasmi kujitokeza kimataifa baada ya kushiriki katika pambano la kimataifa la kirafiki kati ya nyota wa zamani wa Barcelona na Veterani wa Afrika Mashariki.
Katika mpambano huo wa kimataifa uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadick na maafisa kutoka katika mkakati huo walipata nafasi ya kuongea na wachezaji hao nyota wa Barcelona kuhusiana na dhana iliyoko katika nchi za nje ambako inaaminika Tanzania wanauana wenyewe kwa wenyewe kutokana na imani za kishirikina.
Akiongea baada ya mpambano huo ambapo Barcelona waliibuka washindi, Balozi na muasisi wa mkakati huo unaoelekea na sura ya kizalendo na kitaifa, Bw. Henry Mdimu alisema kulikuwa na haja wachezaji hawa warudi na ujumbe kwao wenye majibu ya maswali wanayojiuliza kuhusiana na mauaji ya albino na kukosa majibu.
"Maneno haya ya kwamba sisi tunauana kwa imani za kishirikina, ingawa matukio mengi yapo kanda ya Ziwa lakini nchi nzima inachafuka kwa hiyo haja ya kusafisha jina la nchi kwa mataifa ya nje ipo na sisi IMETOSHA tumeamua kuchukua jukumu", alisema Balozi huyo ambaye pia ana ualbino.
Mdimu alibainisha kwamba katika mkakati wa kimataifa wameanza kwa kuanzisha tovuti (imetosha.or.tz) ambayo itakuwa ikionesha matukio mbali mbali yanayopinga mauaji na unyanyapaa ili wanaoamini vingine waone kwamba unyanyapaa na mauaji kwa watu wenye ualbino si kitu ambacho watanzania kama taifa wanakifurahia.
Balozi huyo pia alitoa wito kwa kila mtanzania kuuunga mkono mkakati wa IMETOSHA ili katika miaka 20 ijayo kizazi kijacho kiwe na jamii yenye watu wenye ualbino wanaoishi kwa amani katika nchi yao.
Wachezaji wa zamani wa timu ya Barcelona ya Hispania wakiongozwa na Patrick Kluivert (aliebeba mtoto) wakiingia uwanjani tayari kwa kukipiga na timu ya Tanzania Veterans katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. hadi mwisho wa mchezo, Barcelona ya Hispania ilishinda bao 2-1.
Mchezaji wa zamani wa timu ya Barcelona ya Hispania, Patrick Kluivert akifurahia jambo na Mtoto Sharifa mwenye Ualbino kabla ya kuanza kwa mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Tanzania Veterans uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara (wa pili kulia) akizungumza jambo na Mchezaji wa zamani wa timu ya Barcelona ya Hispania, Patrick Kluivert wakati akiwasalimia wachezaji hao kabla ya kuanza kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya Tanzania Veterans, uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jana.Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadick.
Sehemu ya Wachezaji wa timu ya Tanzania Veterans na Barcelona wakiwa kwenye picha ya pamoja na Watoto wenye Ualbino mbele ya Bango la Mkakati wa kutokomeza unyanyapaa na mauaji ya watu wenye ualbino nchini, uitwao IMETOSHA.Habari/Picha na Othman Michuzi
--
Othman Michuzi
Editorial Director & Chief Photographer
CELL: +255 713 775869 /+255 789 103610
WEB: issamichuzi.blogspot.com
othmanmichuzi.blogspot.com
michuzijr.blogspot.com
EMAIL: othmanmichuzi@gmail.com
Dar Es Salaam.
Tanzania.
East Africa.
Subscribe to:
Posts (Atom)