ASKOFU CHARLES GADI AWAONGOZA WAUMINI KUWAOMBEA WALIOATHIRIKA KWA KIMBUNGA FLORIDA NA TEXAS MAREKANI

September 11, 2017
 Askofu Charles Gadi  wa Huduma ya Good News for all Ministry (katikati), akiwaongoza waumini wa kanisa lake Dar es Salaam jana,wakati wa kuwaombea walioathirika kwa kimbunga katika miji ya  Florida na Texas nchini Marekani
 Askofu Charles Gadi  wa Huduma ya Good News for all Ministry (katikati), akiwaongoza waumini wa kanisa lake Dar es Salaam jana,wakati wa kuwaombea walioathirika kwa kimbunga katika miji ya  Florida na Texas nchini Marekani

Serikali Yawasilisha Bungeni Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi

Serikali Yawasilisha Bungeni Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi

September 11, 2017

PIX 1.
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Serikali imewasilisha Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Akiwasilisha Mkataba huo kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa Tanzania na Uganda ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo malengo yake ni pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama kwenye maeneo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii kiteknolojia , utafiti, ulinzi na masuala ya Kisheria.
Dkt. mwakyembe amesema kuwa Serikali ya Uganda kupitia kampuni za Kimataifa za TOTAL, TULLOW NA CNOOC iligundua uwepo wa mafuta ghafi takribani mapipa bilioni 6.5 katika eneo la Albertine nchini Uganda.
” Kufuatia ugunduzi huo, Serikali ya Uganda ilianza kutafuta njia ya kusafirisha mafuta hayo kwenda kwenye soko la kimataifa ambapo iliaanisha njia takribani tatu ikiwemo ile ya kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania” amesema Dkt. mwakyembe.
Aidha Dkt. mwakyembe amebainisha baadhi ya faida zitokanazo na Mkataba huo ikiwemo kuongezeka kwa mapato ya Serikali kutokana na Kodi ya zuio na Kodi ya Mapato ya Kampuni zitakazotozwa wakati wa ujenzi na uendeshaji wa Mradi.
Vilevile amesema kuwa Serikali ya Tanzania itanufaika katika kuongezeka kwa mapato ya Serikali kwa takribani Dola za Marekani 12.2 kwa kila pipa la mafuta ghafi litakalosafirishwa kupitia Bandari ya Tanga kulingana na kiwango cha Hisa za Serikali ya Tanzania.
” kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia, ulinzi na usalama kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda pamoja na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla sambamba na kuimarika kwa huduma mbalimbali katika bandari ya Tanga kutokana na shughuli za Mradi na miundombinu itakayojengwa” aliongeza Dkt. Mwakyembe
Pia ongezo kwa fursa za  ajira kwa Watanzania ambapo takribani watanzania 10, 000 wataajiriwa wakati wa ujenzi na ajira zipatazo 1,000 wakati wa uendeshaji, Amesema Dkt. Mwakyembe.
Kwa upande wake Deogratius Ngalawa akimuwakilisha  Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ameishauri Serikali kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa mkataba huo kwa kuzingatia mustakabali wa manufaa ya kiuchumi kwa Taifa.

RAIS DKT MAGUFULI AMUAPISHA JAJI MKUU WA TANZANIA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

September 11, 2017

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimwangalia Profesa Ibrahim Hamis Juma akitia sahihi hati ya kiapo baada ya kumuapisha kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiweka sahihi hati ya kiapo baada ya kumuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimkabidhi nyezo za kazi baada ya kumuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea baada ya kumuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai, Profesa Ibrahim Hamis Juma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba kabudi na Jaji Mkuu Mstaafu Mhe. Mohamed Chande Othman katika picha ya kumbukumbu baada ya Rais kumuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 11, 2017

MKURUGENZI MKUU WA TAWA, DKT. JAMES WAKIBARA NA KAIMU MKURUGENZI WA UTALII NA HUDUMA ZA BIASHARA WATEMBELEA OFISI ZA KDU NA MALIHAI CLUB ARUSHA

September 11, 2017
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Dkt. James Wakibara (wa tatu kushoto, mstari wa mbele ) akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka hiyo, Imani Nkuwi (kushoto kweke) na viongozi pamoja wafanyakazi wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha. Lengo la ziara hiyo ilikua kuona na kukagua shughuli zinazofanywa na kikosi hicho kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wake.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Dkt. James Wakibara (katikati) akisikiliza hoja mbalimbali kutoka kwa watumishi wa KDU alipotembelea ofisi zao hivi karibuni. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi wa Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka hiyo, Imani Nkuwi (kulia) na Mkuu wa Kikosi hicho Kanda ya Kaskazini, Ndugu Mkeni (kushoto). 
 Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, Dkt. James Wakibara wakati akitoa maelekezo mbalimbali ya kuboresha utendaji kazi wa kikosi hicho.
Baadhi ya watumishi na Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA (hayupo pichani).
Wafanyakazi na Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, Dkt. James Wakibara wakati wa mkutano huo. (PICHA NA TAWA)

KUHANI WA KANISA LA SILOAM NCHINI KENYA AFANYIWA IBADA KWA KUPATA UBUNGE

September 11, 2017
Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Siloamu, Mpaka Mafuta akimfanyia maombi rasmi ya kumbariki  Kuhani wa kanisa hilo nchini Kenya Agatha Mtindi, kwenye Ibada ya Mungu Baba, iliyofanyika jana katika Kanisa hilo, Mbezi Makonde jijini Dar es Salaam.  Agatha alifanyiwa maombi hayo maalum ya kumbariki kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mbunge kwenye Akaunti ya Machakosi nchini Kenya katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni.
Zifuatazo ni picha za tukio hilo, tangu mwanzo hadi mwisho wa ibada. Picha zote na Bashir Nkoromo


WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KUFUTWA TOZO NA ADA KUBORESHA KILIMO

September 11, 2017
Jovina Bujulu-MAELEZO.

Sekta ya kilimo nchini ni kitovu cha maendeleo ya viwanda kwa kutoa masoko na malighafi za viwandani ambapo inaajiri Watanzania wengi takribani zaidi ya asilimia 67.

Katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo, Serikali inaendelea kuimarisha mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya kilimo ikiwemo kuimarisha masoko ya kilimo ili sekta hiyo iendelee kuwa na tija kwa wakulimananchi na taifa kwa ujumla.

Hivi karibuni Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ilitangaza kufuta ada na tozo mbalimbali katika baadhi ya mazao ya biashara ili kumpa unafuu mkulima wakati wa kuuza mazao yake.

Hatua hiyo ni mwanzo mzuri wa kuimarisha sekta hiyo hasa wakati huu ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imetangaza nia yake ya kuimarisha uchumi wa kati na viwanda.

Serikali iliamua kufuta na kupunguza ada na tozo imedhamiria kumaliza kero na kilio cha muda mrefu cha wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia tozo hizo kwa madai kuwa zinawanyonya.

Aidha, uamuzi huo unategemea kuwapunguzia mzigo mkubwa wa malipo ambao umekuwa ukiwaelemea wakulima hao, hivyo kuwapa unafuu mkubwa na kuwapatia faida.

Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2017/18, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba alizitaja baadhi ya tozo zilizofutwa katika zao la tumbaku kuwa ni mchango wa ushirika wa mkoa, mchango kwa ajili ya gharama za masoko ya ushirika na chama cha msingi cha ushirika, dhamana ya benki kuu ya Tanzania na fomu ya maombi ya leseni za tumbaku.

Ada na tozo nyingine zilizotajwa kuwa ni kodi ya leseni ya kununua tumbaku kavu na mbichi kiwandani, leseni ya kuuza tumbaku nje ya nchi na tozo ya Baraza la Tumbaku.

Pamoja na kufuta tozo na ada katika baadhi ya mazao, Serikali pia imetoa punguzo katika zao la tumbaku ambapo kodi ya leseni ya tumbaku kavu itakuwa dola za kimarekani 2,000 badala ya dola 4,000.

Aidha, leseni ya kusindika tumbaku imepungua kutoka dola za kimarekani 10,000 hadi 5,000 ambapo Serikali imechukua hatua hizo ili kuhakikisha wakulima wananufaika na kilimo wakiwemo wakulima wadogo.

Kupitia bodi ya mazao, Serikali itaendelea kuimarisha soko la mazao ya asili hasa mazao ya jamii ya mikunde ili kukidhi mahitaji ya zao hilo katika soko la India na zao la muhogo kwa ajili ya soko la China.

SERIKALI YAINGIZA TANI 55,000 ZA MBOLEA ILI KUDHIBITI MFUMUKO WA BEI

September 11, 2017
Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Ubora wa Mbolea Tanzania(TFRA) Bw. Lazaro Kitandu (katikati) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wakati zoezi la upakuaji wa mbolea ya kupandia ukiendelea katika bandari ya Dar es Salaam mapema hii leo. 
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari nchini wakiendelea na zoezi la upakiaji wa mbolea ya kupandia tani elfu 23 tayari kwenda kwa wakulima mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari nchini wakiendelea na zoezi la kufunga mbolea ya kupandia katika mifuko tayari kwa kupakiwa na kusafirishwa kwenda kwa wakulima.Picha na Eliphace Marwa - Maelezo


Na. Eliphace Marwa - Maelezo

Serikali imeingiza nchini jumla ya tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia pamoja na tani elfu 23 za mbolea ya kupandia kupitia mfumo mpya wa uagizaji wa mbolea kwa pamoja, lengo likiwa ni kudhibiti bei kwa kuzingatia bei elekezi.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam wakati zoezi la upakuaji wa mbolea hiyo likiendelea Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Ubora wa Mbolea Tanzania(TFRA) Bw. Lazaro Kitandu amesema kuwa mpaka sasa jumla ya tani elfu 55 za mbolea zimewasili nchini.

Hii ni awamu ya kwanza ya kuingiza mbolea nchini kupitia mfumo mpya ya uagizaji mbolea kwapamoja ambapo kampuni ya OCP S.A ya nchini Morocco imeingiza jumla ya tani elfu 23 za mbolea ya kupandia na Kampuni ya Premium Agro Chem imeingiza tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia.

“Mpaka sasa zoezi la kupakua mbolea ya kupandia (DAP) tani elfu 23 linaendelea vizuri na mara baada ya kumaliza kupakua mbolea hii tutaanza zoezi la kupakua mbolea ya kukuzia (UREA) ambayo ni tani elfu 32,” alisema Bw. Kitandu.

Kitandu aliongeza kuwa Mheshimiwa Waziri wa kilimo juzi alipokuwa anaongea na waandishi wa habari mjini Dodoma na akasisitiza bei ambazo zimetolewa zisimamiwe na kila ngazi kwasababu taasisi peke yake haiwezi kuwa na watu kila mahali hivyo Tawala za mikoa, Serikali za mitaa mpaka Kijiji zitasaidia kusimamia bei ambazo zimetolewa. 

Pia Kitandu aliongeza kuwa kuhusiana suala la bei ya mbolea hiyo itatangazwa kupitia vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni na hivyo kutoa onyo kwa mawakala kujipangia bei kwa kuuza mbolea nje ya bei elekezi ya Serikali kwamba watachukuliwa hatua za kisheria kama kunyang’anywa leseni, kufungwa, faini au vyote kwa pamoja.

Aidha Kitandu alisisitiza kuwa mbolea hizi siyo mbolea za ruzuku kwani wakulima wengi wamekuwa wakichanganya mbolea hizi na mbolea za ruzuku na amefafanua kuwa mbolea hii imefanyiwa utaratibu wa kudhibiti toka kule inapotoka na hivyo serikali itahakikisha mbolea hii inauzwa kwa kulingana na bei ya soko la dunia.

GROUP LA WHATSAPP LA AFYA YANGU LATOA MSAADA KWA WAJAWAZITO KIBAHA MKOANI PWANI

September 11, 2017

 Msimamizi Mkuu wa Kundi la WhatsAPP la AFYA YANGU, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijamii wa Habarika 24, Shabani Lulale (kushoto), akimkabidhi Mbunge wa Kibaha Vijijini, Humoud Jumaa, vifaa vya kujifungulia wajawazito vilivyotolewa na kundi hilo kwa Kituo cha Afya cha Mlandizi jana. Kulia ni Mwanachama wa kundi hilo, Mudeme Elly.

WANANCHI WATAKIWA KUTUMIA NISHATI YA UMEME KUANZISHA VIWANDA VIDOGO VIDOGO KWENYE MAENEO YAO

September 11, 2017
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Dkt Juliana Pallangyo wakati wa uzinduzi wa mradi wa umeme wa Solar kwenye Kijiji hicho ambao utasaidia wananchi kuondokana na
changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo muhimu

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Dkt Juliana Pallangyo wa kwanza kushoto akipiga makofi mara baada ya  uzinduzi wa mradi wa umeme wa Solar kwenye Kijiji hicho ambao utasaidia wananchi kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo muhimu 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo katika akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali kushoto Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel mara baada ya  uzinduzi wa mradi wa umeme
wa Solar kwenye Kijiji hicho ambao utasaidia wananchi kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo muhimu

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati
na Madini,Dkt Juliana Pallangyo akicheza ngoma wakati wa  wa uzinduzi wa mradi wa umeme wa Solar kwenye Kijiji hicho ambao utasaidia wananchi kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo muhimu

 
WANANCHI wa Kijiji cha Mpale Kata ya Mpale wilayani Korogwe Mkoani Tanga wametakiwa kutumia nishati ya umeme waliopatiwa kwa shughuli za uzalishaji mali ikiwemo kuanzisha viwanda vidogo vidogo na miradi itakayoweza kuwaingizia fedha ili kujikwamua kiuchumi wao na jamii zao.

Hayo yalisema mwishoni mwa wiki na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo wakati wa uzinduzi wa mradi wa umeme wa Solar kwenye Kijiji hicho ambao utasaidia wananchi kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo muhimu.

Mradi huo umefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji na Maendeleo (The United Nations Capital Development Fund-UNCDF), ikishirikiana na kampuni ya Ensol Tanzania Ltd. (Ensol) hivyo kuwezesha umeme katika eneo hilo kwa mara ya kwanza.

Alisema uwepo wa nishati hiyo kwenye kijiji hicho utafungua fursa nyengine kwa wananchi kuweza kujikwamua kimaendeleo kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kusagia nafaka, mashine za useremala na kutengeneza samani.

“Licha ya hivyo lakini pia wataweza kufanya uchomeaji wa vyuma ambapo kwa kufanya hivyo ninyi wananchi wa hapa mpale mtakuwa mnaenda sambamba na mwamko mpya wa Tanzania ya Viwanda”Alisema Dkt Pallangyo.

Alisema upatikanaji wa nishati hiyo kwa wananchi hao ni maendeleo makubwa yaliyopatikana katika kipindi kifupi tangu wakala wa nishati vijiji ulipoanzioshwa mwaka 2005.

“Serikali sasa kupitia wakala wa Nishati imezindua rasmi mpango wa tatu wa kusambaza umeme maeneo ya vijijini na tumeweka lengo la kufikia vijiji vyote ifikapo mwaka 2022.

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradiu huo, Msimamizi Mkuu wa Mradi huo, Prosper Magali alisema alisema shughuli za mradi huo zilianza rasmi Machi mwaka 2014 baada ya kutembelea kijiji hicho pamoja na vyengine vilivyopo wilayani Korogwe.

Alisema licha ya kutembelea wilaya hiyo lakini pia walitembelea maeneo mengine Tanzania kutafuta vijiji na maeneo yanayofaa kwa miradi ya uzalishaji mdogo wa umeme kwa kutumia teknologia ya umeme wa Jua.

Aidha alieleza waliamua kuanza mradi wa mfano katika kijiji hicho
baada ya kuwa kijiji bora kwa vigezo walivyoweka vya kiuchumi, kijamii na kimakjazi ukilinganisha na vyengine walivyotembelea.

“Shughuli ya mradi zilifuatiwa na zoezi la kufanya upembuzi yakinifu, Mpango wa kibiashara (Bussines Plan) pamoja na makadirio ya kiufundi mambo ambayo yalitusaidia kuandaa nyaraka za kuwasilisha kwa wafadhili na wawekezaji mbalimbali “Alisema.

“Baada ya hapo mmwaka 2014 mwishoni, Taasisi ya Energy and Environment Partnership (EEP) Program yenye makao yake makuu huko Pretoria nchini Afrika kusini  inayopata ufadhili wa Serikali za Finland,Uingereza na Austria kupitia mpango wake wa kutoa ufadhili wa miradi ya nishati endelevu kwa nchi za kusini na mashariki ya Africa kwa mtindo wa ushindani.

“June 10 mwaka 2015 tuliweza kusaini makubaliano rasmi ya EEP ya ufadhili wa miaka miwili wa mradi huu uliokuwa na thamani ya Euro 263,000 ikiwa ni asilimia 63 ya gharama za mradi “Alisema.

Aliongeza kuwa bado wanaendelea na zoezi la kutafuta fedha zaidi za kutekeleza mradi huo lakini kwa bahati nzuri baada ya mazungumzo ya muda mfupi, Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Mitaji (United Nations Capital Development Fund ya UNCDF).

Aliongeza kuwa baada ya mazungumzo hayo taasisi hiyo ilikubali kutoa asilimia 22 ya gharama za mradi USD 124,000 na walitiliana saini ya makubaliano ya ufadhili wa fedha hizo Novemba mwaka 2015.