MPENZI MFUATILIAJI WA MATUKIO KWENYE BLOG HII YA KIJAMII YA TANGA RAHA PATA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI LEO JUMAMOSI

May 06, 2016






















zanchick yajipanga kushirikiana na wizara ya kilimo,maliasili,mifugo na uvuvi kuwasaidia wafugaji na wakulima wadogowadogo.

May 06, 2016


Uongozi wa Shamba la Kuku Maruhubi { Zanchick } umejipanga kushirikiana na Wizara ya Kilimo,  Maliasili, Mifugo na Uvuvi katika kuwasaidia wafugaji na wakulima wadogo wadogo Nchini ili waendeshe miradi yao ya uzalishaji katika misingi ya kitaaluma.

Mkuu na muanzilishi wa Shamba hilo Dr. David Elua akiuongoza ujumbe wa Viongozi watatu wa shamba hilo alieleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisini kwake vuga Mjini Zanzibar.

Dr. David Elua alisema mpango huo uliolenga kutekelezwa pande zote mbili za Muungano, Tanzania Bara na Zanzibar utawanufaisha wanachi wa kipato cha chini zaidi ya 45,000 kwa kupata ajira katika uendeshaji wa miradi ya ufugaji kuku kwa kutumia njia ya kisasa.Alisema katika hatua ya awali shamba hilo tayari limeshatoa ajira zipatazo 300 katika kiwanda chake cha kutotoa vifaranga vya Kuku kiliopo Maruhubi juhudi zikiwekwa zaidi katika kuunga mkono azma ya Serikali Kuu katika uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo.

Dr. David alimfahamisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Sera hiyo iliyoanzishwa na Serikali na kuanza kukubalika kwa baadhi ya mashirika na taasisi za uwekezaji ndani na nje ya nchi itawasaidia zaidi vijana kupata ajira badala ya kusubiri ajira za serikali ambazo ni finyu kwa miaka ya sasa.

Akizungumzia ugonjwa wa kuambukiza wa kipindupindu ulioikumba Zanzibar katika Kipindi hichi Mkuu na Muanzilishi wa Shamba hilo la Kuku Maruhubi Dr. David alisema Uongozi wake umepata mshtuko kutokana na janga hilo linaloendelea kusumbua wananchi hasa Watoto wadogo.

Dr. David alisema Zanchick imeahidi kutoa mchango wa shilingi Milioni 10,000,000/- ili zisaidie nguvu ya Serikali katika mapambano yake dhidi ya maradhi hayo yaliyopoteza maisha ya watu wasiopungua 53 tokea yavikumbe Visiwa vya Zanzibar mwezi septemba mwaka uliopita.

Akitoa shukrani zake kwa Uongozi wa Shamba hilo la Kuku Maruhubi {Zanchick} Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kuzifanyia kazi changamoto zote zinazoikumba Taasisi hiyo katika kuendesha miradi yake ya uwekezaji hapa Nchini.

Balozi Seif alisema Serikali imeamua kuimarisha miundombinu katika sekta mbali mbali za Uwekezaji ili kujenga mazingira bora yatakayotoa fursa kwa Taasisi na Makampuni ndani na nje kuwekeza miradi yao ya kiuchumi ili hatimae isaidie uchumi wa Taifa.

Shamba la Kuku Maruhubi ni miongoni mwa Taasisi za uwekezaji zilizohamasika kuja kuwekeza miradi yao Nchini kufuatia ziara ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif aliyoifanya Nchini Marekani mwezi Oktoba mwaka 2011 kwa mualiko wa shirika la uwekezaji vitega uchumi Barani Afrika la Nchini Marekani.

Ziara hiyo ya Balozi Seif ililenga kuitangaza Zanzibar kwa taasisi na mashirika ya Marekani kuangalia uwezekano wa kuwekeza miradi yao katika maeneo yaliyomo ndani ya Sekta za Utalii, Biashara, Elimu, Kilimo, Afya, Miundombinu pamoja na Mazingira.
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
6/5/2016. 
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akisalimiana na Ujumbe wa Viongozi wa Shamba la Kuku Maruhubi { Zanzchick } uliofika ofisini kwake kubadilishana mawazo juu ya sekta ya uwekezaji.Aliyempa mkono ni Mkuu na muanzilishi wa shamba hilo Dr. David Elua, wa kwanza kutoka kulia ni Meneja operesheni wa Shamba hilo Bw. Christopher Kontonasios na wa kwanza kutoka kushoto ni Nd. Issa Kassim.
 Balozi Seif akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Shamba la Kuku Maruhubi { Zanzchick } ukiongozwa na Mkuu na muanzilishi wa Shamba hilo Dr. David Elua.
Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Viongozi wa Shamba la Kuku Maruhubi { Zanzchick } mara baada ya mazungumzo yao.Kulia ya Balozi Seif ni Mkuu na muanzilishi wa Shamba hilo Dr. David Elua, Bwana Michael Mantheakis, Nd. Issa Kassim na kushoto ya Balozi Seif ni Meneja operesheni wa Shamba hilo Bw. Christopher Kontonasios.Picha na – OMPR – ZNZ.

102.5 LAKE FM MWANZA YAWATEMBELEA WASOMI WA CHUO KIKUU SAUT MWANZA.

May 06, 2016
Kama kawaida, Kampeni ya "Raha yako ya Rock City ni nini"? inayoendeshwa na 102.5 Lake Fm, Raha ya Rock City #RadioYaWananzengo iliyopo Jijini Mwanza, inaendelea.
RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANACHI ALIPOKUWA SAFARINI KUTOKEA DODOMA KUELEKEA ARUSHA

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANACHI ALIPOKUWA SAFARINI KUTOKEA DODOMA KUELEKEA ARUSHA

May 06, 2016

kat01 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha sehemu mbalimbali wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha kwa njia ya barabara leo Mei 6, 2016. PICHA NA IKULU
kat1 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha.
kat2 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha.
kat3 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua karanga kutoka kwa mjasiriamali mara baada ya kuwahutubia mamia ya wakazi wa Babati mkoani Manyara waliojitokeza katika eneo la Stendi ya Mabasi ya Babati Mkoani Manyara.
kat4 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Magugu mkoani Manyara wakati akielekea  Mkoani Arusha.
kat5 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wafanyabiashara wa Stendi ya Mabasi ya Singida wakati alipokuwa njiania kuelekea Arusha.
kat6 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wakazi wa Endasak mkoani Manyara wakati akitokea Dodoma kuelekea Arusha kwa njia ya barabara.
kat7 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Dareda mkoani Manyara waliojitokeza kumsalimia wakati akitokea Dodoma kuelekea mkoani Arusha. PICHA NA IKULU
Wizara ya Afya yapokea vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.4

Wizara ya Afya yapokea vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.4

May 06, 2016

AF1Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila (kushoto) akiongea na Waandishi wa Habari leo 6 Mei, 2016 Jijini Dar es Salaam kuhusu msaada walioupokea toka Shirika la Afya Duniani (WHO) wenye thamani ya shilingi bilioni 1.4.
AF2Mkurugenzi wa Huduma za Kinga,Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila (kushoto) pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro wakisaini hati za makabidhiano ya vifaa tiba leo 6 Mei, 2016 jijini Dar es Salaam.
AF3Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila (kushoto) pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro wakikabidhiana hati za makabidhiano ya vifaa tiba leo 6 Mei, 2016 jijini Dar es Salaam.
AF5 
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro (kulia) akikabidhi jokofu kwa kwa jaili ya huduma za chanjo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila leo 6 Mei, 2016 jijini Dar es Salaam.
AF6 
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro (kulia) akikabidhi jokofu kwa kwa jaili ya huduma za chanjo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila leo 6 Mei, 2016 jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.4 ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kutoa chanjo kwa akina mama na watoto dhidi ya magonjwa mbalimbali nchini.
Akiongea na waandishi wa habari Wizarani hapo, Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila ameeleza kuwa vifaa tiba hivyo vitasaidia uhifadhi wa chanjo katika mikoa mbalimbali pamoja halmashauri nchini.
‘’Ni msaada mkubwa tulioupata toka WHO na nina amini kuwa utatusaidia sana katika kufanikisha suala la chanjo kwa akina mama na watoto nchini na pia tunaamini wataendela kushirikiana na Wizara ili tuweze kufikia malengo tuliyojiwekea’’, alisema Dkt. Rusibimayila.
Ameongeza kuwa, kwa sasa vituo vipya vinavyofunguliwa nchini vikiwemo vile ambavyo havikuwa na majokofu vitakuwa na uwezo wa kupata vifaa hivyo kama vile majokofu na vifaa vingine vya tiba ili huduma za chanjo ziweze kutolewa katika kila kituo nchini.
Akikabidhi vifaa hivyo Wizarani hapo, Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro  amesema kuwa vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.4 ni pamoja na majokofu 200 pamoja na vifaa vitumikavyo kwa ajili ya kutolea chanjo.
Kwa upande wake Mratibu Chanjo Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bwana Emmanuel Yohana ameeleza kuwa, majokofu hayo pia yatapelekewa katika wilaya ambayo yana upungufu wa majokofu pamoja na vituo vipya kwa ajili ya kupunguza umbali kwa wagonjwa wa chanjo na pia ni moja ya kuweka huduma karibu na wananchi nchini.
Aidha, ameongeza kuwa spesimeni za polio na surua zilizotolewa na WHO zitapalekwa pia katika vituo kwa jili ya kuchukua damu kwa ajili ya vipimo na kuletwa Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi wa maabara.
‘’Wanufaika wa huu msaada kutoka WHO ni wananchi wote wa Tanzania kwani utaenda katika vituo vyote vya chini zikiwemo Zahanati’’, alisema Yohana.
Kupitia wadau mbalimbali Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kushirikiana na wadau hao katika kutafuta vifaa tiba mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kuwa sekta ya afya nchini inaimarika kwani Tanzania kwa sasa imeweza kudhibiti polio kwa kiasi kikubwa.
UN NA EU WAFURAHISHWA NA MIRADI WALIYOIFADHILI JIJINI MWANZA

UN NA EU WAFURAHISHWA NA MIRADI WALIYOIFADHILI JIJINI MWANZA

May 06, 2016
RC Mwanza, John Mongella
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (kulia) akisalimiana na kumkaribisha ofisini kwake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale (katikati) walipowasili jijini Mwanza kabla ya ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa pamoja na Umoja wa Ulaya.
MRATIBU Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Alvaro Rodriguez pamoja na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale, wamesema wameridhishwa na miradi inayofadhili maeneo kadhaa jijini Mwanza.
Wakizungumza baada ya kutembelea Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Mwauwasa), Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC), Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) na Radio ya Kijamii (Saut), walisema utekelezaji wa miradi hiyo imewatia hamasa kubwa.
Awali akizungumza katika ofisi za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa), Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka hiyo, Anthony Sanga, alisema mradi unaoendelea sasa wa kusambaza maji safi utakapokamilika utaweza kuwafikia wakazi 54,000 badala ya 23,000 wa sasa.
Sanga alisema mradi huo utakapokamilika Mei mwaka huu, utawafikia wakazi kwa asilimia 90 badala ya 68 za sasa.
“Mradi ukishakamilika utafanikisha makusanyo ya Sh. Bilioni 1.4 kwa mwezi badala ya kukusanya Sh. milioni 316 za sasa kwa mwezi, ukiwa na matanki ya ujazo wa lita 33,400,” alisema Sanga.
Akizungumzia hilo, Rodriguez alisema baada ya kushuhudia miradi hiyo ukiwamo wa maji taka chini ya ufadhili wa EU, amefurahishwa na hali ya miradi hiyo.
“Timu yetu imetembelea Mwauwasa na kushuhudia miradi hiyo inayofadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya kwa ajili ya huduma ya maji kwa wananchi, pia tumeenda kuangalia chanzo cha maji na yanapowekwa maji taka,” alisema Rodriguez.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Bugando, Prof. Kien Mteta, alishukuru UN na EU kwa miradi hiyo na kuja kushuhudia ufadhili wao.
“Ufadhili umelenga katika mambo matatu, moja kwenye maabara ambako vilinunuliwa vifaa vya mbalimbali vikiwamo vya kutambua kansa, pili vifaa vya mionzi kwa ajili kutambua vyanzo vya magonjwa,” alisema Prof. Mteta.
Aidha, alisema pia wafadhili hao walitembelea kitengo cha kutoa matibabu ya mionzi ya kansa, ambacho kinawafunza baadhi ya watumishi wake na upatikanaji wa mashine.
Luana Reale, EU Tanzania
Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale (katikati) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella mara baada ya kuwasili ofisini kwake mwishoni mwa wiki.
Hospitali ya Bungando yenye uwezo wa vitanda 950 iliyoanzishwa mwaka 1972 ni miongoni mwa hospitali nne kubwa nchini ambazo hutoa tiba maalumu ikihudumia watu milioni 16 katika mikoa minane ya kanda ya ziwa.
Hospitali hii inatoa tiba ya ugonjwa wa saratani kwa mifumo miwili. Moja kwa kutumia onkolojia au patholojia na tiba kwa kutumia mionzi.
Toka mwaka 2000 hospitali ya Bugando imekuwa ikifanyakazi kwa karibu na kampuni ya kitaliano ya TISSON ASSOCIATION ili kuboresha huduma zake patholiojia na pia kuanza kutibu kansa mwaka 2009.
Wataliano wamewezesha kufundishwa kwa wataalamu wa patholojia na onkolojia ya tiba, vifaa tiba, dawa na kuwezesha ziara za za kifundi za watu wa patholojia na utafiti.
Uangalizi wa wagonjwa wa kansa na matibabu yao ulianza mwaka 2009 na kuelezwa kuwa kwa mwaka wagonjwa 3500 wa kansa huangaliwa.
Huduma ya uangalizi ni pamoja na kufanya utambuzi, upasuaji na utoaji wa tiba ya kemo.
Hoyce Temu
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akitoa utambulisho wa ujumbe alioambatana nao kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.
Hata hivyo wagonjwa wanaohitaji huduma ya mionzi hukatiwa rufaa hospitali ya kansa ya Ocean (ORCI).
Kutokana na kuzidiwa kwa hospitali ya Ocean Road katika tiba ya mionzi, serikali iliamua kutanua huduma zake na kuzifikisha Bugando.
Ili kuwezesha haja ya serikali taasisi ya nguvu za atomiki duniani na ile ya hapa nchini kupitia mpango wa ushirikiano wa kiufundi walianzisha miradi kadha yenye lengo la kuwezesha huduma yenye tija kwa wagonjwa wa kansa.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo yanachangia miradi hiyo imekuwa ikisaidia serikali ya Tanzania kuwezesha tiba ya mionzi katika hospitali ya Bugando.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale katika ziara maalum ya kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na UN pamoja na EU jijini humo.
Alvaro Rodriguez
Kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza CP. Clodwig Mtweve, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella pamoja na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale wakiwa wameshilikilia kuhamasisha utekelezaji wa malengo mapya ya maendeleo endelevu (SDGs) ambayo yamewafikia wakazi wa jiji la Mwanza.
Luana Reale
Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa) mara baada ya kuwasili katika ofisi hizo jijini Mwanza.
Eng. Anthony Sanga
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa), Mhandisi Anthony Sanga, akitoa 'power point presentation' ya maendeleo ya mradi wa maji unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya jijini Mwanza kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale aliyeambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.
Anthony Sanga
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa), Mhandisi Anthony Sanga akitoa maelezo ya mradi kwa ugeni ulioambata na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.
Mwauwasa 1
Maji yakiwa kwenye hatua ya kutakatishwa ili yawe salama kwa watumiaji.
Godadi Mgwatu
Mhandisi wa ubora wa maji Mwauwasa, Godadi Mgwatu akitoa maelezo kwa mgeni ugeni huo ulioambatana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kukagua mradi wa maji wa Mwauwasa jijini Mwanza.
Mhandisi, Anthony Sanga-Mwauwasa Mwanza
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa), Mhandisi Anthony Sanga akitoa maelezo kwa ugeni huo ya namna ya maji yanavyochujwa na kusafisha kwa kutumia mtambo maalum uliopo mbele yao. (Picha zaidi za ziara hii Bofya hapa)