NAIBU KATIBU MKUU NISHATI-CHANGAMOTO YA UMEME NCHINI ITAKUWA HISTORIA

November 14, 2023
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Athumani Seleman wakati wa ziara ya kamati ya Kudumu ya bunge ya Nishati na madini kutembea vituo vya kuzalisha umeme vya Hale na Pangani Falls vilivyopo Mkoani Tanga

 

Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya bunge ya Nishati na madini David Mathayo akizungumza wakati wa ziara hiyo

Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Shirika la Umeme nchini (Tanesco) Balozi Meja Jenerali Paul Sesa akizungumza wakati wa ziara hiyo





Na Oscar Assenga,KOROGWE

Serikali imesema kuwa mpaka ifikapo Mwezi Aprili mwakani changamoto ya uhaba wa umeme nchini itakuwa historia baada ya kumalizika Kwa ukarabati wa vituo vya kuzalisha umeme pamoja na bwawa la Nyerere linalotarajiwa kuzalisha zaidi ya Megga watts 200 ifikapo Januari mwakani.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya nishati Athumani Seleman wakati wa ziara ya kamati ya Kudumu ya bunge ya Nishati na madini kutembea vituo vya kuzalisha umeme vya Hale na Pangani Falls vilivyopo Mkoani Tanga.

Alisema kuwa tayari serikali imeweza kufanya uwekezaji mkubwa wa kukarabati vituo vya kuzalisha umeme kwenye maeneo mbalimbali nchini ambapo utakapokamilika utasaidia kuongeza uzalishaji wa umeme nchini.

"Hadi ifikapo mwezi Januari mwakani Bwawa la Nyerere litazalisha Kwa mara ya kwanza mega watts 235 ambapo itasaidia kupunguza upungufu wa mega watts 132 ambazo zitaweza kumalizwa mwezi wa pili Kwa kuongeza uzalishaji hadi kufikia mega watts 470"alisema Naibu Katibu Mkuu.

Hata hivyo Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya bunge ya Nishati na madini David Mathayo aliitaka Wizara ya Nishati kuhakikisha miradi yote ya uboreshaji wa umeme inakamilika Kwa wakati na katika viwango bora

Alisema kuwa licha ya Miradi hiyo mingi kukamilika mwisho mwa mwezi Disemba mwaka 2025 lakini matarajio yetu ni kuona miradi hii inakamilika kabla ya muda Ili wananchi waweze kupata huduma

Dkt Mathayo alisema Serikali imewekeza kiasi cha Shilingi Bilioni 50 katika mradi wa ukarabati wa kituo cha kuzalisha umeme cha Hale lengo ni kuhakikisha Umeme unapatikana

Alisema kutokana na uwekezaji huo wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuwekeza kwenye Umeme kiasi cha shilingi bilioni 50 ambazo zimetolewa kufanya matengenezo katika kituo hicho ambapo mradi ulioanza tangu mwezi Agosti 2023 na utakamilika Agosti 2025.

Hata hivyo alitumia ziara hiyo kulitaka Shirika la Umeme nchini Tanesco, Wizara ya Nishati na wakandarasi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati.

Akiwa kwenye ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Shirika la Umeme nchini (Tanesco) Balozi Meja Jenerali Paul Sesa amesema kuwa hali ya umeme imeimarika kwan hapo awali kulikua na upungufu wa Megawati 410.

Alisema lakini mpaka sasa upungufu wa Umeme umebaki megawati 120 na mpaka kufikia mwezi Aprili 2024hakutakua na upungufu wa Umeme.



MRADI WA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA NCHINI UGANDA HADI CHONGOLEANI TANGA NI MUHIMU KWA WATANZANIA

November 14, 2023
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt David Mathayo katikati akiwa na ujumbe wake wakitembelea eneo la Mradi wa Bomba la Mafuta Chongoleani Jijini Tanga wa pili kulia ni Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Athumani Mbutuka
Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Athumani Mbutuka akizungumza 
Meneja wa eneo la mradi Mathiew Fayel akielezea jambo wakati wa ziara hiyo
Meneja wa eneo la mradi Mathiew Fayel akiwaonyesha kitu wajumbe wa kamati hiyo


Na Oscar Assenga,TANGA

MWENYEKITI wa Kamati ya kudumu ya Nishati na Madini ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt David Mathayo amesema kwamba mradi wa Bomba la Mafuta kutoka hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga Tanzania ni wa muhimu kwa watanzania,ueendelee na hauna madhara katika mradi huo hasa yale ya kimazingira.

Dkt Mathayo aliyasema hayo wakati kamati hiyo iliyopo kwenye ziara ya siku mbili ambapo ilitembelea katika eneo la Chongoleani na kukagua mradi wa bomba la mafuta toka Hoima nchini Uganda hadi Tanga ambapo mafuta ghafi yatasafirishwa kwenda nje ya Nchi

Alisema kwamba wanampongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kuhakikisha mradi huo unakwenda vizuri na ifikapo mwezi Desemba mwaka 2025 uwe umekamilika na kazi ya kuanza kusafirisha mafuta ghafi ianze.

“Kwa kweli tumpongeze Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kuhakikisha mradi huu unakwenda vizuri na ifikapo Desemba mwaka 2025 uwe umekamilika na kazi ya kuanza kusafirisha mafuta ghafi iianza huu mradi ni wa muhimu sana “Alisema

Alisema kwamba Bunge la Tanzania kupitia kamati hiyo inakanusha uvumi unaoenezwa wa uwepo wa uharibifu wa mazingira unaotokana na utekelezaji wa mradi wa Kimataifa wa Bomba la mafuta .

Mwenyekiti huyo alisema kwamba yapo madai yanayozungumzwa huko Duniani na hata watu toka nchi za Afrika Mashariki kuwa mradi huo ni mbaya kimazingira jambo ambalo sio la kweli.

Hata hivyo alisema kwamba wanaamini watu wanaopotosha kuhusiana na madhara ya kimazingira yatokanayo na mradi huu ni watu wasioitakia mema Tanzania ikiwemo kutaka watanzania wasifaidike nao

Katika hatua nyengine Mwenyekiti huyo wa Kamati alisema kwamba tayari wamekwisha kutoa maelekezo kwa watekelezaji wa mradi huo EACOP kuwa wajikite katika masuala ya kijamii ikiwemo elimu,afya,maji mengineyo

Pioa aliwataka kuhakikisha wana kuwa na idadi ya watumishi toka katika eneo la mradi ambao idadi yao bado ipo chini na wapatiwe mafunzo kwa ajili ya maslahi ya utekelezaji wa miradi huo.

Awali akizungumza katika ziara hiyo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Athumani Mbutuka alisema wamefurahishwa na kazi zinazoendelea katika mradi huo na kusema kazi kubwa ya Wabunge ni kuisimamia Serikali na imetoa maelekezo ya mambo ya msingi ya kuyafanya.

Athumani ambaye alimwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Madini Dkt Doto Biteko alisema kwamba Serikali imeyapokea maelekezo ya kamati hiyo na watahakikisha miradi yote ya maendeleo ambayo inafadhiliwa kwa dhana ya wajibu wa jamii kushiriki inaelekezwa katika maeneo yenye tija.

Alisema tayari Dola Mil 207 zimelipwa kati dola 308 kwa ajili ya hisa za Serikali ya Tanzania, ajira 4228 zimetolewa kwa Watazania ambapo sawa na asilimia 91,Makampuni na watoa huduma 146 wametoa huduma katika mradi huo na kufanikiwa kujiingizia Shs Bil 355.

Alieleza kwamba Sh,bil 35 zililipwa kupitia fidia kwa wananchi waliopitiwa na mradi huo na kuongeza kuwa Tanzania ilikuwa na jukumu la kufanya kama Serikali na wameendeleza kutekeleza majukumu na wataenda kutekeleza yote waliyoagizwa na kamati hiyo.

Hata hivyo Meneja wa eneo la mradi Mathiew Fayel alisema mradi huo unaendela vizuri na watumishi wapo katika eneo hilo la mradi kutekeleza majukumu yao kama kuandaa nguzo kwa ajili ya jeti itakapofunga meli na mategemeo mwaka 2025 mradi utakuwa umekamilika.