“BONANZA LA MICHEZO LA WALIMU NA WADAU WA MICHEZO KUFANYIKA MEI 20 MWAKA HUU MJINI KOROGWE”

April 09, 2017


NA MWANDISHI WETU, KOROGWE.
BONANZA la Michezo la siku sita litakalohusisha walimu wa michezo na wadau mbalimbali linatarajiwa kufanyika Mei 20 mwaka huu kwenye viwanja vya Halmashauri ya Korogwe .
Bonanza hilo limefadhiliwa na asasi ya Inuka wenye lengo la kupiga vita madawa ya kulevya na kuhamasisha michezo na nidhamu kwa jamii
Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kaimu Mratibu wa Inuka Kanda ya Ziwa,Gaudance Msuya alisema lengo kubwa litakuwa kuiamsha jamii na kupenda kushiriki kwenye michezo ili kuimarisha afya zao.
Alisema katika bonanza hilo michezo itakayokuwepo ni mpira wa  miguu,riadhaa ,mpira wa pete,kuvuta kamba  na kukimbiza kuku na kutembea na magunia.
Aidha alisema washindi kwenye michezo hiyo wata zawadiwa zawadi mbalimbali ambapo zaidi ya milioni mbili zimetengwa kwa ajili ya zawadi kwa washiriki watakofanya vizuri.
“Ndugu zangu watu wa Korogwe hii ni fursa ya kipekee hivyo ninawaomba mjitokeze kwa wingi kushiriki kwenye bonanza hili ambalo litakuwa na faida kubwa licha ya kuwepo kwa zawadi hizo”Alisema.
Hata hivyo alisema kwa washiriki ambao wangependa kushiriki wawasiliane na Ofisa Michezo wilaya ya Korogwe ili kuweza kuthibitisha ushiriki wao.
Mratibu huyo aliyataka mashirika mbalimbali ikiwemo mabenki kuona namna ya kuunga mkono jambo hilo kwa kuona namna ya kufadhili ambapo wanaweza kuwasiliana na mratibu huyo kwa simu namna 0683122320/0683122340.

UAMUZI WA KIKAO CHA SAA 72

April 09, 2017




Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji wa Ligi Tanzania au Kamati ya Saa 72, ilifanya kikao chake juzi Ijumaa Aprili 7, 2017 jijini Dar es Salaam na kufikia uamuzi ufuatao. 

Kuhusu kupulizwa dawa vyumbani Uwanja wa Kambarage
Daktari wa Uwanja wa Kambarage, Dk. Abel Kimuntu amekataa kuwasilisha taarifa yake kuhusu tuhuma za kupuliziwa dawa kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha timu ya Majimaji katika mechi namba 170 ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya wenyeji Stand United. Klabu ya Majimaji iliwasilisha malalamiko yake kwa Bodi ya Ligi kuhusu suala hilo.

Hivyo, Kamati imeagiza suala la daktari huyo lipelekwe kwenye Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa ajili ya hatua za kinidhamu dhidi yake kutokana na kukataa kutoa ushirikiano kwa mwendeshaji wa Ligi juu ya jambo hilo. Kamati ya Nidhamu inatarajiwa kukaa wakati wowote wiki ijayo.

Kuhusu Mchezaji Abdi Banda Mechi namba 194 Kagera Sugar 2 vs Simba 1). Beki wa Simba, Abdi Banda jezi namba 24 amesimamishwa kucheza Ligi Kuu wakati akisubiri suala lake la kumpiga ngumi kiungo wa Kagera Sugar, George Kavilla jezi namba 15 wakati akiwa hana mpira kusikilizwa na kutolewa uamuzi na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Alifanya kitendo hicho ambacho hakikuonwa na waamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Aprili 2, 2017 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Uamuzi wa Kamati umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu.

Pia Kamati ilibaini kuwa Banda alifanya kitendo cha aina hiyo kwenye mechi namba 169 kati ya Simba na Yanga iliyofanyika Februari 25, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Awali, Klabu ya Kagera Sugar iliwasilisha malalamiko dhidi ya kitendo cha beki wa Simba, Abdi Banda kumpiga ngumi kiungo wao George Kavilla wakati akiwa hana mpira, na Mwamuzi wa mechi hiyo kutochukua hatua yoyote.

Kwa vile kosa hilo ni la kinidhamu, Kamati imemsimamisha Abdi Banda kwa mujibu wa Kanuni ya 9(5) wakati akisubiri suala lake kusikilizwa na kutolewa uamuzi na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Kamati ya Nidhamu inatarajiwa kukaa wakati wowote wiki ijayo.

Kadhalika Klabu ya Simba iliwasilisha malalamiko ikitaka ipewe ushindi wa pointi tatu na mabao matatu kutokana na timu ya Kagera Sugar kumchezesha mchezaji Mohamed Fakhi Gharib wakati akiwa na kadi tatu za njano katika mechi yao namba 194 iliyofanyika Aprili 2, 2017 Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Kamati baada ya kupitia malalamiko hayo, imeahirisha shauri hilo hadi Alhamisi Aprili 13, 2017 kwa vile bado inafuatilia baadhi ya vielelezo kuhusu malalamiko hayo kabla ya kufanya uamuzi.

Mechi namba 195 (Yanga 1 vs Azam 0). Yanga haikuingia kwenye chumba chake cha kubadilishia nguo, kutokana na kuwa na maji yaliyomwagwa na wanachama wa klabu hiyo (makomandoo) muda mfupi kabla ya timu hiyo kuwasili uwanjani.

Kamati imeelekeza klabu ya Yanga iandikiwe barua ya onyo, na kuitaka kuhakikisha wanachama wake wanaacha mara moja mtindo wa kumwaga maji vyumbani baada ya kuwa vimeshafanyiwa usafi na wafanyakazi wa uwanja tayari kwa ajili ya matumizi ya timu yao.

MAMA MAGUFULI ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTOA MISAADA KWA WAGONJWA KATIKA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD JIJINI DAR ES SALAAM LEO

April 09, 2017

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akilakiwa na Dkt. Julius Mwaisalage Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road   jijini Dar es salaam   alikoenda kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo ambako ndiko alikozaliwa yeye.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na mganga mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dkt. Grace Magembe wakati alipowasili kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Saratani ya Oceanm Road jijini Dar es salaam.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na  Diwani wa Kata ya Kivukoni Mhe. Henry Sato Massaba  wakati alipowasili kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Saratani ya Oceanm Road jijini Dar es salaam.
  Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na  Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo alipowasili kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Saratani ya Oceanm Road jijini Dar es salaam.
 Sehemu ya wageni na wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road wakifuatilia hotuba zikitolewa wakati wa hafla hiyo
 Sehemu ya wageni na wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road wakifuatilia hotuba zikitolewa wakati wa hafla hiyo
 Sehemu ya wageni na wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road wakifuatilia hotuba zikitolewa wakati wa hafla hiyo

KAMPUNI YA TATA YAWAFADHILI WATANZANIA KWENDA NCHINI INDIA KWA MAFUNZO YA KUTENGENEZA MAGARI

April 09, 2017
 Mkuu wa Kitengo cha Magari wa Kampuni ya Tata Tanzania, Prashant Shukla (kulia), akizungumza Makao Makuu ya Kampuni hiyo Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam jana, wakati wa  hafla ya kuwaaga vijana wanne wa kitanzania ambao wanakwenda nchini India kwa mafunzo ya miezi tisa ya kutengeneza magari. Kutoka kushoto ni viongozi wa kampuni hiyo, Sarvan Keshri na Udayagiri Veeru.