JESHI LA ZIMAMOTO TANGA WAJA NA PROGRAMU MBALIMBALI ZA KUELIMISHA UMMA NAMNA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO
Na Oscar Assenga,TANGA
JESHI la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tanga wameanzisha program mbalimbali za kuielimisha Umma kuweza kuwa na utambuzi ili majanga ya moto yanapotokea waweze kukabiliana nayo.
Hayo yalibainishwa leo na Afisa Operesheni wa Jeshi hilo mkoani Tanga Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo Yusuf Msuya wakati akizungumza na kuhusu namna walivyojipanga kukabiliana na matukio ya moto kwa wananchi.
Alisema katika kuzuia ajali za moto wameamua kuja na mpango huo ambao wanaamini utakuwa na mafanikio makubwa ambao utakwenda sambamba na
ukaguzi wa kinga na tahadhari kwa majanga katika maeneo mablimbali yakiwemo ya biashara,makazi na vyombo bya usafiri na usafirishaji.
“Lengo la ukaguzi huu ni kutambua yale mapungufu na risk zilizopo kwenye majengo ambayo ni hatari na kuyawasilisha kwa mmiliki ikiwemo kumpa mapendekezo na hatua za kufanya ili kuzuia moto usitokee “Alisema
Msuya alisema na endapo moto unapotokea madhara yake yawe machache kwa maisha ya wakazi wa Jengo au wafanyakazi wa eneo husika na ambaye atakidhi vigezo vya kukabuliana na majanga ya moto watatoa cheti kutoka Jeshi hilo cha kuonyesha eneo limekaguliwa na kukidhi vigezo vya usalama wa moto .
,”Katika kulipambanua hili nitoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Tanga kufika kwenye ofisi zetu zilizopo maeneo mbalimbali kwa ajili ya kupatiwa wataalamu kwa lengo la kwenda kukagua vyombo vyao vya usafiri iwe nchi kavu au majini pamoja na maeneo ya Biashara na ya makazi uli kuimarisha usalama dhidi ya majanga ya moto kwenye maeneo yao”Alisema
Awali akizungumzia mpango huo Mfanyabiashara katika soko la Mgandini Jijini Tanga Rashidi Said Kihondo alisema kwamba iwapo wataanzisha mpango huo utawasaidia kuweza kukabiliana na moto hivyo kupunguza majanga hayo katika maeneo yao.
“Huko nyuma tuliwahi kukutana na janga la moto na soko liliungua kutokana lakini kwa sasa kutokana na baadhi ya elimu ya kukabiliana na majanga hayo ya moto tulianza kuchukua tahadhari na hayajaweza kujitokeza tena”Alisema
Naye wa upande wake Mfanyabiashara wa soko Makorora Jijini Tanga Mwanahamisi Bakari alisema kwamba elimu hiyo iwapo elimu hiyo itatolewa kwa wafanyabiashara itawawezesha kukabiliana na majanga ya moto na kuweza kuyadhibiti pindi yanapojitokeza na hivyo kutokuwa na adhari kubwa kwao.
TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAHASIBU AFRIKA
Na. Peter Haule na Joseph Mahumi, WF, Arusha
Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Pili wa Wahasibu Barani Afrika (African Association of Accountants General Meeting (AAAG)) utakaofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 3 hadi 5 Disemba Mwaka 2024, ukiwahusisha zaidi wa washiriki 2,000 kutoka takriban nchi 55 za Bara la Afrika.
Hayo yameelezwa na Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude, wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari jijini Arusha, uliolenga kuujulisha umma kuhusu mkutano huo na fursa za kiuchumi na kijamii kwa watanzania.
CPA Mkude alisema kuwa mkutano huo unatarajia kuleta manufaa makubwa kiuchumi na kijamii pamoja na kuitangaza sekta ya utalii ya Tanzania, hususan kwa wajumbe kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko katika ukanda wa Kaskazini.
Alizitaja faida nyingine za mkutano huo kuwa ni pamoja na kuwa na Afrika yenye mafanikio yenye msingi wa ukuaji jumuishi na maendeleo endelevu, Bara jumuishi lililounganishwa kisiasa na kwa kuzingatia maadili ya Pan-Africanism.
Aliyataja manufaa mengine kuwa ni pamoja na kuwa na maono ya Mwamko wa Afrika na Afrika yenye utawala bora, demokrasia, kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria, Afrika yenye amani na usalama na Afrika yenye utambulisho thabiti wa kitamaduni, urithi wa pamoja na maadili.
CPA Mkude alisema kuwa Mkutano huo utawaleta Wahasibu wakuu wa Serikali Afrika watakaoambatana na Wahasibu Wakuu wa Wizara, Taasisi za umma na Wahasibu na wadau wengine ambao watapata fursa ya kusikiliza mada za masuala mbalimbali ya kitaaluma na kubadirishana mawazo na kujua fursa zinazopatikana katika nchi za Afrika.
Alisema wageni kutoka nje watakuja na fedha za kigeni ambazo watazitumia hapa Tanzania kwa kuwa watatembezwa kwenye mbuga za Wanyama na vituo mbalimbali vya utalii na hivyo kuunga mkono dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kuutangaza Utalii wa Tanzania.
Alitoa wito kwa wafanyabiashara wa nyumba za wageni (hoteli), usafiri, mamalishe na jamii kwa ujumla kuchangamkia fursa hiyo ya ujio wa wageni ili kunufaika kiuchumi na kijamii.
“Natoa wito kwa Maafisa Masuuli wa Wizara na Taasisi zote kuwaruhusu Wahasibu, wakaguzi na wadau wengine watakaoomba kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Pili wa Wahasibu wakuu wa Serikali Afrika, African Association of Accountants General (AAAG) utakaofanyika jijini Arusha mwezi Desemba, 2024”, alisema CPA Mkude
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Wahasibu wa Afrika, ambaye pia ni Mhasibu Mkuu wa nchi ya Lesotho, Bi. Malehlohonolo Mahase, alisema Mkutano wa Wahasibu Afrika unafanyika Tanzania kwa kuwa ni mwanachama anayeaminika na amekuwa mshiriki mwaminifu katika umoja huo, na kwamba wajumbe wa mkutano huo wanakuja kujifunza namna Tanzania ilivyopiga hatua kubwa katika matumizi ya mifumo ya fedha.
Alisema kuwa Tanzania ipo vizuri katika kutekeleza viwango vya kimataifa vya kihasibu, imekuwa ya mfano katika ukuaji wa Uchumi, imeimarika katika suala la ukarimu wa wageni, maendeleo katika teknolojia ya Habari na Mawasiliano na ni miongoni mwa nchi zenye vivutio vingi vya utalii hivyo wanachama kuna mambo mengi ya kujifunza.
Aidha alieleza kuwa Mkutano huo utakao wakutanisha pia Jumuiya za wafanyabiashara watapata fursa ya kujua ni namna gani Afrika ipo tayari katika suala la uwekezaji na namna ya kuripoti hali ya Uchumi ya Afrika, jambo ambalo litaongeza uwazi na uwajibikaji.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bi. Christine Mwakatobe alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wageni wanapokuja wanapata huduma bora kwa kuwa wanaamini watakuwa mabalozi wa Tanzania na watatembelea vivutio mbalimbali vya utalii.
Alisema anamshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuitangaza nchi yetu Duniani na kwamba hauo ni matunda ambayo Taasisi za Serikali kwa ujumla zinafaidi kwa kazi yake anayoifanya, huku Kituo chake cha Mikutano kikihudumia mikutano mingi ya Kitaifa na Kimataifa.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Arusha)
BENKI YA CRDB YATUNUKIWA TUZO YA UBORA KUHUDUMIA WAJASIRIAMALI WADOGO NA JARIDA LA EUROMONEY
KETI JIFUNZE YA BENKI YA CRDB YAIFIKIA SHULE YA WANAFUNZI MAALUM, MAJIMOTO KATAVI
Benki ya CRDB kupitia sera yake ya kurudisha kwa jamii sehemu ya asilimia moja ya faida yake, imeweza kutoa msaada wa magodoro 68 pamoja na viti 24 na meza 2 kwa matumizi ya wanafunzi wenye changamoto za usikivu na madawati 25 kwa ajili ya wanafunzi wenye changamoto ya uoni hafifu na viungo katika Shule ya Msingi ya Majimoto (Shule Maalum) , iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, mkoani Katavi.
Akipokea msada huo, Mkuu wa Wilaya ya Mlele anayesimamia pia Wilaya ya Mpimbwe, Majid Mwanga ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuona umuhimu wa kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutatua changamoto mbalimbali za elimu hapa nchini. Ameishuru Benki ya CRDB kwa msaada huo wa magodoro, viti pamoja na meza.
Msaada huo ni muendelezo wa programu maalumu ya benki hiyo iitwayo 'Keti
Jifunze' yenye lengo la kuwawezesha wanafunzi kujifunza wakiwa wameketi
katika mazingira mazuri na salama. Shule Maalum ni zile zinazohudumia
wanafunzi wenye changamoto mbalimbali kama vile uoni, usikivu na viungo.