Release No. 132
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Julai 29, 2014
TAIFA STARS KWENDA AFRIKA KUSINI KESHO
Msafara wa watu 27 wa kikosi
cha timu ya Taifa (Taifa Stars) kinaondoka kesho (Julai 30 mwaka huu)
saa 10 jioni kwa ndege ya Air Tanzania kwenda Afrika Kusini ambapo
kitapiga kambi ya siku mbili kabla ya kuingia Maputo kuikabili Msumbiji
(Mambas).
Taifa Stars inayodhaminiwa na
Kilimanjaro Premium Lager itawasili saa 9 asubuhi kesho (Julai 30 mwaka
huu) kwa ndege ya Fastjet, na baadaye jioni kuunganisha safari ya Afrika
Kusini.
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi
ya pili ya michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji itachezwa Agosti 3 mwaka
huu Uwanja wa Taifa uliopo Zimpeto nje kidogo ya Jiji la Maputo.
Msafara huo wa Taifa Stars kwenda
Afrika Kusini unajumuisha wachezaji 19 na waliobaki ni maofisa wa Benchi
la Ufundi lililo chini ya Kocha Mkuu Mart Nooij kutoka Uholanzi.
Wakati kiungo Mwinyi Kazimoto
ametua leo (Julai 29 mwaka huu) nchini kuungana na wenzake,
washambuliaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wao wataungana na wenzao
kesho (Julai 30 mwaka huu) jijini Johannesburg wakitokea Lubumbashi,
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Wakati huo huo, Serengeti Boys
imewasili salama jana (Julai 28 mwaka huu) jijini Johannesburg, Afrika
Kusini kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri
chini ya miaka 17 dhidi Afrika Kusini (Amajimbos).
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi
ya pili itachezwa Jumamosi, Agosti 2 mwaka huu kwenye Uwanja wa
Dobsonville uliopo Soweto kuanzia saa 9 kamili mchana kwa saa za Afrika
Kusini.
Timu hizo zilitoka suluhu katika
mechi ya kwanza iliyofanyika Julai 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam
Complex, Dar es Salaam. Serengeti Boys inahitaji ushindi kwenye mechi
hiyo au aina yoyote ya sare ya mabao ili ifuzu kwa raundi ya tatu.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)