WATEJA WA TIGO JIJINI TANGA KUNUFAIKA KWA KUPATA MTANDAO WA INTANETI WENYE KAZI KUBWA ZAIDI BAADA YA UPANUZI WA HUDUMA YA 4GLTE

November 26, 2015





WATEJA wa Tigo waishio jijini Tanga wanatarajia kunufaika kwa kupata mtandano wa intaneti wenye kasi kubwa zaidi kufuatia upanuzi wa upatikanaji wa huduma ya 4GLTE hadi kufikia kwenye jiji hili lililopo kaskazini mwa Tanzania.
Teknologia ya 4GLTE ina kasi mara tano zaidi kuliko teknolojia ya 3G inayopatikana nchini kwa sasa.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Kanda ya Pwani, Goodluck Charles wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kutangaza uzinduzi wa Upatikanaji wa Teknologia ya 4GLTE jijini Tanga, uliofanyika kwenye ofisi za Kampuni hiyo Jijini hapa.

Alisema kuwa upanuzi huo umetokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika majaribio ya awali ya utoaji wa huduma ya 4G jijini Dar es Salaam kuanzia mapema mwaka huu ambayo ni kielelezo cha jinsi ambayo Tigo imedhamiria kufanikisha kuleta mabadiliko ya kidigital katika maisha ya watanzania na pia kuwa katika mstari wa mbele wa kutumia teknologia ya kisasa na kibunifu nchini Tanzania.

Aidha alisema kuwa mtandao wa 4G LTE una kazi kubwa zaidi katika kuperuzi na kupakua kwa rahisi kutoka kwenye mtandano wa intaneti na pia katika kufanya mawasiliano kwa njia ya Skype kwani huduma hiyo inaharakisha urushwaji wa picha za video na ubora wa hali ya juu na kufanya mikutano kwa njia ya mtandao.

  “Tunapenda kuwahakikishia wateja wetu waisio Tanga kwamba sasa wanaweza kufurahia huduma bora zaidi za mawasiliano kutoka Tigo na intaneti yenye kasi zaidi,Tanga ni makao makuu ya taasisi nyingi za kimataifa ikiwemo Jumuiya ya Afrika Mashariki na kitovu cha Utalii nchini “Alisema Goodluck.
 

…..Tunapenda kuwatangazia wateja wetu wa Tigo kwamba bei ya vifurushi vyetu vya 4GLTE ni sawa na bei ya vifurushi vya intaneti vya 3G kwa hivyo mteja haitaji kulipia zaidi kwa ajili ya kutumia huduma ya 4GLTE na wateja wote wa Tigo 4GLTE watanufaika na promosheni ,kila watakapoongeza salio la shilingi elfu moja,atapata MB 500 za bure kama bonasi.
Alisema kuwa uzinduzi wa upatikanaji wa huduma ya 4GLTE kwa ufanisi jijini Dar es Salaam na Arusha na miji mingine katika mikoa sita ambapo huduma hiyo itaanza kupatikana hivi karibuni kuwa  ni Dodoma,Morogoro,Moshi na Mwanza.


Mkurugenzi huyo alisema kuwa jambo hilo linaifanya Tigo kuwa na mtandao mkubwa wa 4G LTE nchini Tanzania ambapo lengo lao kuu ni kufanikisha huduma hiyo katika kila kona ya nchi ifikapo mwaka ujao.
Muhimbili Yapokea Mashine ya kusaidia wagonjwa kupumua

Muhimbili Yapokea Mashine ya kusaidia wagonjwa kupumua

November 26, 2015


MU1
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN), Profesa Lawrence Mseru akipokea mashine ya ventilator ya kusaidia wagonjwa kupumua  endapo wamezidiwa baada ya kuugua. Kushoto ni Mkurugenzi Mauzo wa Mashariki ya Kati na Afrika, Qasem Sumrein akikabidhi mashine hiyo leo.
MU2
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN), Profesa Lawrence Mseru akitoa ufafanuzi baada ya kupokea mashine hiyo
MU3
Daktari Bingwa wa Magonjwa Mahututi na Uzingizi, Moa Kalunga katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akiwaeleza waandishi wa habari umuhimu wa mashine hiyo kwa wagonjwa.
MU4 MU5
Meneja Mauzo barani Afrika, Gordon Blair akimalizia kufunga mashine ya ventilator ambayo imekabidhiwa leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
…………………………………………………………………………………………..
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imepokea msaada wa mashine mojaya Ventilator  ya kumsaidia mgonjwa kupumua yenye thamani ya Dola za Kimarekani 36,000  sawa na Shilingi milioni 80.
Msaada huo umetolewa leo na Kituo cha kitabibu cha Halmiton chenye makao yake makuu nchini Switzerland .
Akikabidhi mashine hiyo  mpya na  kisasa , Mkurugenzi Mauzo wa Mashariki ya Kati na Afrika kutoka Halmiton , Qasem Sumrein amesema pamoja na kutoa msaada huo wataendelea kutembela MHN ili kutoa mafunzo jinsi ya kuitumia pamoja kufanya matengenezo endapo itahitajika kwa kuwa mashine hiyo ina waranti ya miaka miwili.
Akipokea msaada huo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MHN, Profesa Lawrence Mseru ameshukuru msaada huo ambao una lenga kuboresha huduma za afya na kueleza kwamba hospitali hiyo inahitaji kutengeneza ICU nyingine ikiwamo ya mama na mtoto hivyo bado zinahitajika mashine 120 kwa sababu MHN inapokea wagonjwa wengi.
Akielezea  kuhusu mashine hiyo Daktari Bingwa wa Magonjwa Mahututi na Usingizi Moa Kalunga amesema  mashine hiyo itamsaidia mgonjwa aliye mahututi kupumua na hivyo kuokoa maisha yake na mgonjwa akirejea katika hali ya kawaida mashine hiyo  inaonyesha .

WIZARA YA MAMBO YA NJE YASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 45 YA TAIFA LA OMAN

November 26, 2015

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akitoa hotuba wakati wa Maadhimisho ya miaka 45 ya Taifa la Oman yaliyoandaliwa na Ubalozi wa Oman hapa nchini na kufanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) tarehe 24 Novemba, 2015. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu, Mhe. Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Salim Ahmed Salim. Katika hotuba yake Balozi Yahya alisifu uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Oman na kuitakia heri nchi hiyo katika kuadhimisha miaka 45. 
Balozi wa Oman hapa nchini, Mhe. Soud Al Mohammed Al-Ruqaish akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za miaka 45 ya Taifa la Oman. Pia alisifu ushirikiano kati ya Tanzania na nchi yake na kuahidi kuuendeleza na kuuimarisha. 
Mhe. Mwinyi (wa kwanza kushoto) kwa pamoja na Mhe. Salim (wa pili kushoto) na Balozi wa Misri nchini, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf (wa pili kulia) wakiwa kwenye sherehe hizo pamoja na wageni wengine waalikwa. 
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Abdallah Kilima (kulia) akiwa na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Tahir Khamis (mwenye suti ya kijivu) pamoja na wageni mbalimbali walioshiriki maadhimisho ya Miaka 45 ya Taifa la Oman. 
Kiongozi wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Balozi Juma Halfan Mpango (kushoto mwenye suti ya kijivu) akiwa na Balozi wa Burundi hapa nchini, Mhe. Issa Ntambuka wakati wa maadhimisho ya sherehe ya miaka 45 ya Taifa la Oman. 
Balozi wa Oman, Mhe. Al-Ruqaish akiwaongoza Viongozi Wastaafu, Mabalozi na Mgeni rasmi Balozi Yahya kukata keki kama ishara ya kusherehekea siku hiyo kubwa kwa Taifa la Oman. 
Wageni waalikwa wakifuatilia sherehe hizo akiwemo Afisa Mambo ya Nje kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Batholomeo Jungu (mwenye suti ya kijivu). 
Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia sherehe za miaka 45 ya Taifa la Oman. Kutoka kulia ni Bw. Ali Ubwa, Bw. Seif Kamtunda na Bw. Hangi Mgaka. 
Mhe. Mwinyi akijadili jambo na Mhe. Salim kabla ya kuanza kwa sherehe hizo za miaka 45 ya Taifa la Oman. 
Picha ya Juu na Chini ni Sehemu ya Wageni waalikwa wakati wa sherehe za miaka 45 ya Taifa la Oman. 
Sehemu nyingine ya Wageni waalikwa.
Wageni waalikwa. 

JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. OTHMAN CHANDE ATOA SOMO KWA WAANDISHI WA HABARI

November 26, 2015
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akitoa ufafanuzi kwa wanabari (hawapo pichani) kuhusu uandishi bora wa habari za Mahakama wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande (kushoto) na Meneja wa Maadili wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Allan Lawa (kulia) wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari za Mahakama yaliyoandaliwa na Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
Rais wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari namna wanavyoweza kuandika habari za Mahakama kwa kuzingatia weledi wa taaluma zao.
Washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es salaam.

Na. Aron Msigwa –MAELEZO.

Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuzingatia weledi wa taaluma zao wanapoandika habari za Mahakama ili kuepuka kuandika habari zinazowatia hatiani watuhumiwa na kushindwa kutofautisha kati ya  mshitakiwa na mtuhumiwa pamoja na haki zake.

Akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es Salaam, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande  amesema waandishi wa habari  wanalojukumu la kuwapatia wananchi taarifa sahihi kuhusu masuala yanayowahusu na kuepuka uandishi wa habari zenye kuhukumu.

Amesema  kisheria mtuhumiwa huwa hana hatia mpaka itakapothibitishwa na mahakama kuwa ametenda kosa na kuongeza kuwa kukosekana kwa weledi katika uandishi wa habari za mahakama  huleta mkanganyiko  miongoni mwa jamii  kuhusu ukweli na kuondoa imani ya watu kwa mahakama.

Ameongeza kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa Vikitoa  habari zisizo mpatia mtu  fursa na haki ya kujibu tuhuma huku vingine vikitoa taarifa nusunusu na kushindwa kuwa na mwendelezo wa habari za mashauri mbalimbali mahakamani.

Mhe.Chande ameeleza kuwa waandishi wamejikita katika uandishi wa taarifa zenye mvuto kwa jamii na kusahau nyingine walizo anza nazo jambo  linalosababisha wananchi kuachwa  njia panda bila kupata taarifa za kina kuhusu mwisho wa mambo yanayoanzishwa.

" Mimi sitaki kuingilia utendaji wa kazi zenu za kila siku ila nachotaka kusema ni kuweka msisitizo wa utoaji wa habari za mashauri mbalimbali mnayoanza kuyaripoti kwa mwendelezo ili msiwachanganye wananchi" Amesisitiza.

Amewataka waandishi wa habari kuandika habari sahihi na kuepuka upendeleo na maslahi binafsi ili kulinda taaluma na imani katika jamii juu ya utendaji wa vyombo vya habari.

Mhe. Chande ametoa wito kwa waandishi wa habari kuepuka uandishi wa habari zilizojaa chuki zinazoweza kuleta mgawanyiko katika jamii na kusisitiza habari za kuisaidia jamii kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Kuhusu Mahakama amesema itaendelea kuboresha huduma na miundombinu yake katika maeneo yasiyofikiwa ili kuendelea kutoa haki kwa wakati pia  kushirikiana na waandishi wa habari wa ndani ili kuimarisha utendaji wao.

Aidha amevipongeza vyombo vya habari kwa ukomavu  viliouonyesha wakati wa utoaji wa taarifa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kwa upande wake Rais wa Baraza la Habari Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu Mhe.Thomas Mihayo  akizungumza kwa niaba ya Baraza hilo ametoa wito kwa waandishi wa habari kuzingatia weledi katika uandishi wa habari za mahakama ili kuepusha madhara katika jamii.

Amewataka waandishi kujikita zaidi katika uandishi wa habari zenye uhakika kuliko kuwa na taarifa zenye mlengo wa kuuza gazeti.

Amesema kuwepo kwa mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Mahakama ya Tanzania ni ishara nzuri ya uboreshaji wa taaluma ya habari hasa uongezaji wa ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya  kimahakama hapa nchini.

Amewataka wanahabari kujifunza na kufuatilia miongozo na kufuatilia taarifa mbalimbali zinazoweza kuboresha uandishi wao kwa kupata maneno sahihi ya kimahakama.Amesema Semina hiyo itawasaidia waandishi wa habari kujenga weledi katika uandishi wa habari za mahakama.

Ametoa tahadhari kwa waandishi kuepuka uandishi wa habari zenye uchochezi ili kuepuka kushtakiwa na jamii, kuepuka lugha za kishabiki na upendeleo.

Naye Meneja wa Maadili wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Allan Lawa akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo amewataka kuepuka kuandika habari zinaonyesha upendeleo na  kubainisha kuwa kuwa ipo haja kwa vyombo vya habari kutenga maeneo madawati ya habari hizo

KAMPUNI YA MEGATRADE INVESTMENT LTD YAVIPIGA JEKI CHUKO KIKUU CHA USHIRIKA NA BIASHARA,MOSHI PAMOJA NA CHAMA CHA SOKA CHA MKOA WA KILIMANJARO.

November 26, 2015
Meneja masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akimkabidhi hundi ya kiasi cha shilingi Milioni 1.5 ,katibu wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro ,KRFA,Mohamed Musa kwa ajili ya kusadia ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa iliyoanza hivi karibuni.
Mweka hazina wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro,Kusianga Kiata,akitizama hundi iliyotolewa na kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha.
Baadhi ya wadau wa soka waliofika kushuhudia makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo jengo la Voda House.
Meneja Masoko kanda ya Kaskazini ,Edmund Rutaraka akimkabidhi Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ushirika na Biashara ,Moshi,( MOCU),Profesa Faustine Bee hundi ya kiasi cha shilingi Mil 2 kusaidia maeneo mbalimbali yenye changamoto chuoni hapo.
Meneja Masoko wa kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akizungumza jambo mara baada ya kukabidhi hundi kwa mkuu huyo wa chuo.
Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ushirika na Bashara (MOCU) Profesa Faustine Bee akizungumza mara naada ya kukabidhiwa hundi hiyo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
MUULIZE MO!: TUANDIKIE MASWALI YAKO KUMUULIZA MOHAMMED DEWJI (CEO WA METL GROUP) TUTAKUWA NA MAHOJIANO NAYE HIVI KARIBUNI

MUULIZE MO!: TUANDIKIE MASWALI YAKO KUMUULIZA MOHAMMED DEWJI (CEO WA METL GROUP) TUTAKUWA NA MAHOJIANO NAYE HIVI KARIBUNI

November 26, 2015
mo
Msomaji na mdau wa mtandao wako wa habari www.modewjiblog.com unakupa nafasi wewe kumuuliza maswali/swali lolote lile Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL Group, Mohammed Dewji. Maswali yote yatajibiwa na kutolewa ufafanuzi wa kina. Tutakuwa na mahojiano naye karibuni. Asanteni sana.
Utaratibu wa kumuuliza maswali ni kwa kukomenti kwenye post hii kisanduku cha maoni, Zingatia Kanuni na sheria ikiwemo kutotumia lugha zisizo rasmi.
Pia waweza kutoa maoni yako kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ukiwemo ukurasa wa Mohammed Dewji : https://www.facebook.com/mohammeddewjitz/
au Ukurasa wa Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL):

HATIMA YA MWILI WA MAWAZO KUAGWA AMA KUTOAGWA JIJINI MWANZA KUJULIKANA KESHO.

November 26, 2015
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeahirisha kesi ya madai ya kuomba ridhaa ya kufanya ibada ya Mazishi ya aliekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoani Geita Marehemu Alphonce Mawazo iliyowasilishwa na Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mlezi wa marehemu Mawazo.

Katika kesi hiyo, mlalamikaji anaiomba mahakama kuondoa zuio la jeshi la polisi Mkoani Mwanza la kutoruhusu shughuli ya kuuaga mwili wa marehemu Mawazo kufanyika Jijini Mwanza, kabla ya kwenda kuzikwa Mkoani Geita.

John Mallya ambae ni miongoni mwa Mawakili watatu wa Chadema ambao wanaitetea kesi hiyo, amebainisha kuwa Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi kesho majira ya saa saba mchana, ambapo Jaji wa Mahakama hiyo Mhe.Lameck Mlacha anatarajiwa kutoa maamuzi yake baada ya leo kusikiliza utetezi wa pande zote mbili zinazohusika.

Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema bara Salum Mwalimu, amewasihi wanafamilia pamoja na wafuasi wa chama hicho kuendelea kuwa watulivu, wakati maamuzi ya mahakama hiyo yakisubiriwa ambapo ameeleza kuridhika na mwenendo wa kesi hiyo.

Nje ya Mahakama, ulinzi ulikuwa umeimarishwa zaidi ambapo kulikuwa na polisi wa kutuliza ghasia waliokuwa na bunduki za risasi za moto, mabomu ya machozi pamoja na mbwa ambapo baada ya kesi hiyo kuahirishwa, umati mkubwa wa wananchi uliokuwa umetanda mita chache kutoka Mahakamani hapo ulianza kuimba nyimbo za maombolezo na kuwasindikiza viongozi mbalimbali wa chedema hadi katika hoteli waliyofikia. 
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA BINAGI RADIO-HABARI 
John Mallya ambae ni mmoja wa Mawakili wa Chadema akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Katibu Mkuu Msaidizi Chadema bara, Salum Mwalimu akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Viongozi na makada wa Chadema wakiwa mahakamani
Viongozi na makada wa Chadema wakiwa mahakamani
Mawakili na Viongozi/Makada wa Chadema wakitoka Mahakamani
Wananchi na wafuasi wa Chadema wakitoka Mahakamani huku wakiimba nyimbo za maombolezo
Wananchi na wafuasi wa Chadema wakitoka Mahakamani huku wakiimba nyimbo za maombolezo
Wananchi hawa waliwasindikiza viongozi wa chadema hadi hotelini.

WAKAZI WA MIKOA YA MANYARA,ARUSHA NA KILIMANJARO WAJITOKEZA UZINDUZI WA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA.

November 26, 2015
Brass Band ya Chuo cha Polisi Moshi ikiongoza maandamano ya uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini .
Wanafunzi wa kozi ya awali ya Askari Polisi kutoka shule ya Polisi Tanania wakiwa katika manda,ano ya uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Kanda ya Kaskazini.
Maanda,mano ya lipita maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi.
Maandamano hayo yakipita eneo la kituo kuu cha Mabasi cha mjini Moshi yakieekea katia viwanja vya kituo hicho ambako uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini .
Mkuu wa wilaya ya Moshi Novatus Makunga aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kujinsia kanda ya kaskazini akimsikiliza Mwenyekiti wa Mwavuli wa Vikoba wa KIVINET ,Mama Mwingira wakati alipotembelea banda la KIVINET .
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akisikiliza malezo kutoka katika banda la shirika la NAFGEM linalopambana na vitendo vya Ukeketaji.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akisikiiza maelezo kutoka TAWREF ambao pia wameshiriki katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Afisa habari wa shirika la KWIECO ,Velonica Ollomi akitoa maelezo mbele ya mgeni rasmi katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini uliofanyika katika viwanja vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi,kulia kwake ni Afisa Kitengo cha elimu ya haki za binadamu na jinsia ,KWIECO ,Elizabeth Mushi.
Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi,MUWSA ,pia imeshiriki katika uzinduzi huo hapa ikiwasilishwa na afisa habari wake,Florah Nguma na mfanyakazi wa mamlaka hiyo,Kisingi.
Mwenyekiti wa kamati ya kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini,Honorata Nasuwa akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika viwanja vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.
Kikundi cha kwaya kutoka shule ya msingi Mweleni wakitoa ujumbe kwa njia ya wimbo wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya kaskazini.
Mkurugenzi wa shirika la Tusonge,Agnata Rutazaa akizungumza katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa TAWREF,Dafrosa Itemba akitoa mada katika uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini.
Mkurugenzi wa shirika la KWIECO,Elizabeth Minde akitoa mada katika uzinduzi huo.
Mwakilishi wa mkuu wa shule ya Polisi Tanzania na Mkufunzi mkuu wa shule hiyo Graifton Mushi ,akiwa na aliyekuwa mwenyekiti wa dawati la Jinsia mkoa wa Kilimanjaro,Grace Lyimo katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akiteta jambo na mkurugenzi wa shirika la KWIECO,Elizabeth Minde.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga aliyekuwa mgeni trasmi katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini akitoa hotuba yake.
Baadhi ya wasiriki katika uzinduzi huo wakifutilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya kaskazini.