MATUKIO YA PICHA KATIKA MICHUANO YA LIGI YA WILAYA YA TANGA.

May 13, 2015
Mchezaji wa timu ya Majengo FC,Rashid Hamadi akiwania mpira na beki wa timu ya Boraska FC Amani Ally aliyekuwepo chini juzi ikiwa ni muendelezo wa michuano ya Ligi ya wilaya ya Tanga ambapo
Majengo FC ilishinda mabao 3-1, mchezo uliochezwa uwanja wa soka Lamore

Mshambuliaji wa timu ya Majengo FC,Rashid Shabani akipatiwa huduma ya kwanza mara baada ya kuumia katika mechi ya Ligi ya wilaya ya Tanga dhidi yao na Boraska FC ambapo majengo waliibuka na ushindi wa mabao 3-1,mchezo uliochezwa uwanja wa Lamore
RAIS NKURUNZIZA HAJULIKANI ALIKO, UWANJA WA NDEGE WAFUNGWA

RAIS NKURUNZIZA HAJULIKANI ALIKO, UWANJA WA NDEGE WAFUNGWA

May 13, 2015
Raisi Pierre Nkurunziza
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, inasemekana ameondoka nchini Tanzania saa moja baada ya kupatikana taarifa za kupinduliwa kwake na kiongozi mkuu wa majeshi yake Meja jenerali Godefroid Niyombare kutangaza kwamba amempindua.
Jenerali huyo mara baada ya tangazo lake, akaweka amri ya kufungwa kwa kiwanja cha kimataifa cha ndege nchini humo ikiwemo mipaka ya Burundi.
Hata hivyo haiko wazi ikiwa jeshi linamuunga mkono Meja jenerali Godefroid Niyombare. Naye msemaji wa rais wa Burundi, amesema kwamba wanajeshi watiifu kwa Rais ambaye alikuwa akihudhuria mkutano wa viongozi nchini Tanzania, amesema nchi iko shwari.
Maelfu ya watu wamekuwa katika shamra shamra katika mji mkuu wan chi hiyo Bujumbura baada ya wiki kadhaa za maandamano kumpinga katika maamuzi yake ya kugombea muhula wa tatu wa uongozi,na tayari mpaka sasa viongozi wakuu wa kanda wamelaani mapinduzi hayo.
Mgogoro wa Burundi umezusha wasi wasi wa kurejea katika ghasia baada ya miaka kumi na miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Zaidi ya watu elfu tatu walikufa katika vita vya kikabila kati ya wahutu na watutsi ,vita vilivyomalizwa muongo uliopita.na mgogoro wa sasa nchini humo umehusisha kwa kiasi kikubwa na masuala ya kisiasa. lakini,yaliyojiri Burundi hayana tofauti na kilichojiri katika nchi jirani ya Rwanda ambayo ilikumbwa na mauaji ya kimbari nayo ilikabiliwa na masuala ya ukabila.
Umoja wa mataifa umeonya hivi karibuni kwamba ikiwa ghasia zitasitishwa Burundi itakuwa na Amani na kama itakuwa vinginevyo basi nchi hiyo itarejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe .
CREDIT: BBC
TUME YA MIPANGO YATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

TUME YA MIPANGO YATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

May 13, 2015

1
Meneja wa Mipango na Mikakati wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Bw. Ntandu Mathayo (Kulia) akiukaribisha ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Kushoto ni Kiongozi wa Msafara huo, Bibi Florence Mwanri. Wengine pichani ni Bw. Aloyce Andrea (Wapili Kushoto), Bw. Robert Senya (Katikati) na Bw. Abel Shirima.   
2
Meneja wa Mipango na Mikakati wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Bw. Ntandu Mathayo (Wapili Kushoto) akizungumza wakati ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Wanaomsikiliza ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bibi Lucy Kazibure (Kushoto) na wageni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.
3
Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bibi Lucy Kazibure (Kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Ugeni huo uliongozwa na Naibu Katibu Mtendaji (Huduma za Jamii na Masuala ya Idadi ya Watu) Bibi Florence Mwanri (Wapili Kushoto).
4
Mkuu wa Sehemu ya Kushushia Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kapteni P. R. Paul (Kulia) akitoa maelezo kuhusu hali ya upakuaji wa mafuta kwa ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
5
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza wakati walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. a
7
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akikaribishwa na Mkuu wa Sehemu ya Kushushia Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kapteni P. R. Paul (Kulia) wakati walipotembelea kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
6  8
Pichani meli ikipakua shehena ya mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
PICHA NA SAIDI MKABAKULI

MWENYEKITI WA VUGUVUGU NCHINI BURUNDI AZUNGMZA NA WANAHABARI DAR ES SALAAM

May 13, 2015



Kikao Kikiwa kinaendelea leo usiku.
 Mwenyekiti wa Vuguvugu kutoka nchini Burundi Bw. Mugwengezo Chauvineau akiongea na
waandishi wa Habari  Serena Hotel Dar jana usiku .

Dkt. Christine Mbunyingingo Mwenyekiti wa wanawake na wasichana katika
harakati za usawa Nchini Burundi, Akiongea na waandishi wa Habari jana usiku . 

*****
Mwenyekiti
wa vuguvugu za Maandamano Burundi kwa Mara ya kwanza amefika Nchini
Tanzania ili kuweza kushuhudia Mkutano wa Dharula kati ya viongozi
watano wa Jumuia ya Afrika Mashariki  kuhusu nchi ya Burundi ambayo sasa
imeingia katika machafuko baada ya Rais aliyepo Madarakani kutaka
kuongeza muda wake.
 
Akiongea
na Waandishi wa Habari usiku huu Mkuu huyo wa vuguvugu wa Burundi
amesema kuwa wananchi hawaridhiki na Rais wao kuendelea kuwa madarakani
ambapo hata sheria na katiba hairuhusu na pia sasa ni wiki ya tatu
ambapo wananchi wanaendelea kupinga Rais kuendelea kuwania kwa Muhura wa
Tatu.
 
Amezungumzia
juu ya waandamanaji  baada ya wiki tatu bado wapo barabarani ambapo
wameweza kuwa ni kiungo, wameweza kuwa ni njia kwa sababu wanadai
kumekuwa na mabadiriko kuhusu Rais wao, na kuwashukuru waandamanaji hao
kwa kuonesha moyo wa uzalendo na kuwa wameweza kudhihilisha na kuwa
walikuwa ni watulivu na kutulia kungoja utekelezaji wa mambo ambayo
yamezungumziwa.
 
Amesema
kwamba anaomba vurugu hizi zipate kwisha ambapo watu zaidi ya laki
mbili wamekimbia nchi na anaomba vurugu ziishe ili wapate kurejea nchini
kwao.
 
Pia
ameiomba Jumuia ya kimatafa iweze kufuatilia kwa karibu hali
inayoendelea kwa sasa  Nchini Burundi ambapo jumuia iyo tangia zamani
imeweza kusimamia mambo ya usalama nchini Burundi na amani ili Burundi
iweze kufikia malengo ya Mkataba wa amani wa Arusha na kufikia malengo
ya katiba ambayo ndio uti wa mgongo wa taifa hilo.
 
Kuhusu jaribio la Mapinduzi kiongozi huyo amesema hayupo Miongoni mwa wale ambao wameandaa tukio hilo 
 
Kuhusu
jambo baya alilofanya Rais wa Burundi Kiongozi huyo amaesema kwamba ni
kuongezea Muhula wakati tayari alisha tawala kwa Miaka 10, na katika
miaka hiyo alishindwa kuweka usawa baina ya warundi, hajatekereza swala
la haki za Binadamu , aliongeza kuwa Muhura wake ni Muhura baki na
Haramu hauko sambamba na Katiba wala Sheria ya Burundi pamoja na Mkataba
wa Arusha na angetekeleza yote hayo hizi vurugu zisinge kuwepo. Pia
hata makubaliano ya Arusha yanasema hakuna Rais ataenda Mihula mitatu.
Pia warundi wanafanya hivyo kwa sababu hawataki shuhudia tena Damu
inamwagika.
 
Mwisho amewaomba Marais watano wamalize salama Mkutano na kuhakikisha maamuzi yote yanafanyiwa kazi.
 
Nae
Mwenyekiti wa wanawake na wasichana katika harakati za usawa
amewashukuru kwa uvumilivu wao na kuendelea kupinga Rais wao kuendelea
kuwa madarakani kwa awamu ya Tatu.

Balozi mpya wa Malawi nchini Marekani atembelea Ubalozi wa Tanzania Washington DC

May 13, 2015

 Mhe balozi mpya wa Malawi Nector Mhura akipokelewa na Afisa ubalozi Swahiba Mndeme alipotembelea ubalozi.
 Mhe, balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na mgeni wake balozi wa Malawi Nector Mhura.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani akiweka saini kwenye kitabu maalum cha wageni.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akimsikiliza kwa makini mwenyeji wake balozi Liberata Mulamula alipokua akijitambulisha.
  Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akiwa ameambata na mkuu wa utawala wa ubalozi wa Malawi bi, Jane Nankwenya.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akiwa ameambata na mkuu wa utawala wa ubalozi wa Malawi bi, Jane Nankwenya, kulia ni balozi wa Tanzania nchini Marekani Liberata Mulamula na Afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme.
 
                   PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI.

WIZARA YA FEDHA YAWAPA SEMINA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MRADI WA MABORESHO YA MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMAA

May 13, 2015

 
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma akifafanua jambo wakati wa warsha ya siku tano kuhusu mradi wa maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika Hoteli Njuweni Kibaha. 
 
Washiriki wa warsha kuhusu maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika Hoteli ya Njuweni Kibaha.
 Baadhi ya waandishi wakiwa katika warsha ya siku tano kuhusu kuhusu mradi wa maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika Hoteli ya Njuweni Kibaha. 


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Public Financial
Management Reform (
PFMRP) ni Mradi wa maboresho ya matumizi ya fedha za umma.

Serikali ya
Tanzania 
ilianzisha mradi huo kwa madhumuni ya kuimarisha mifumo ya matumizi ya fedha katika ngazi zote.  

Mradi huu umekuwa wa awamu 4 kutokana na mafanikio yanayojitokeza na changamoto.

Awamuya kwanza (I) ilikuwa kutoka mwaka
1998 – 2004 huu ulikuwa na malengo ya kudhibiti matumizi,
kuweka nidhamu ya fedha pamoja na kukuzana kuimarisha uchumi mpana.
Awamuyapili (II)
ilikuwa kutoka mwaka 2004 – 2008 malengo ya mradi huo yalikuwa ni kuimarisha na kuendeleza mifumo na njia zinazotumika katika malipo ya fedha za umma kwa kutumia njia rahisi na nyepesi.

Aidha awamu hiyo ilizingatia pia uimarishaji wa njia ya ukusanyaji mapato na jinsi ya kuweka mbinu ya kuzitumia rasilimali fedha na kuweka mikakati ya kipi kianze kwanza.
Awamu ya tatu (III)
ilikua kuanzia 2008 – 2011,
mradi huu ulikua na malengo ya kuhakikisha kuna kuwa na upatikanaji rasilimali fedha kutoka katikaTaasisi mbalimbali za kifedha.

Awamu ya nne (IV)
ya mradi ni kuanzia June 2012, mradi ulizinduliwa na kuanza rasmi tarehe 1 Julai,
2012.
Madhumuni ya mradi huu katika awamu ya nne umelenga katika kuonge za nguvu ambayo itawezesha kufikia malengo ya
Sera ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025,
 hiyo inaenda sanjari na mpango wa maendeleo wa miaka mitano yaani 2011/2012 – 2015/2016na
MKUKUTA (MkakatiwaKukuzauchumi Tanzania)/ MKUZA (Mkakati wa Kukuza uchumi
Zanzibar), ili kufika malengo ya ukuaji wa uchumi.
Mafanikio ya mradi huu katika kuimarisha matumizi mazuri ya fedha za umma yatafikiwa kwa kuwa na matokeo ya maeneo makuu matanokama
vile, usimaiziwaukusanyajikodi, mpangowabajeti, 
usimamizi wa bajeti, uwazi na uwajibikaji, 
usimamizi wa matumizi ya fedha zilizopangwa kutumika na kugundua matumizi ya nayoweza kujitokeza baadae na mabadiliko ya Uongozi pamoja na uangalizi na mawasiliano kwenye
mambo yafedha.
Maboresho ya fedha za umma yanaenda sanjari na maboresho katika sekta za umma ambayo yanalenga kuimarisha utendaji
bora na makini katika kutoa huduma  ambazo zinakuza uchumi ulioimara.
Mpango wa maboresho ya fedha za umma awamu ya nne
(IV) pia utaangalia/utalenga kwenye kuwajengea uwezo wale
wote wanaofanya shughuli za maboresho ya fedha za umma katika Nyanja tofauti tofauti.
Kufuatilia na kufanya tathmini katIka uwigo uliowekwa kwa kuangalia vipau mbele ambavyo vitatoa muelekeo na kufikia matokeo mazuri.
 
Kuhakikisha kuwa ripoti za fedha zinazotolewa zinakuwa za aina moja bila kuwa na utofauti wa aina yoyote.
 
Kuwa na uongozi mzuri ambao umepanga vizuri Taasisi za fedha.
 
Kuzilenga na kuzipa nguvu wakala ambazo zinaguswa moja kwa moja katika mifumo ya fedha za umma.
 
Mradi huu unafadhiliwa kwa pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika
(AfDB na Bank ya Dunia (WB),DfID, CIDA, DENMARK, IRELAND na KFW. Hawawote walisaini makubaliano ya kuchangia katika mradi huo.
 
Mpaka sasa hivi mradi huu umepata mafanikio makubwa hasa ya kuwekamfumomzuriwamalipo, muda wa kupitishwa kwa bajeti ya Taifa umeimarika na fedha zinatoka kwa wakati.  AidhabajetiyamwananchiinatangazwakatikaTovutiyaWizarayafedha

MTOTO WA BABA WA TAIFA AZIKWA LEO BUTIAMA

May 13, 2015

 Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mhashamu Michael Msonganzila akisali mbele ya jeneza la marehemu John Guido Nyerere kabla halijaingia kanisani kwa ajili ya ibada maalum iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya Butiama.
 Viongozi na wananchi wakishiriki ibada ya kumuombea marehemu John Gaudo Nyerere katika Kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya Butiama
 Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mhashamu Michael Msonganzila
akitoa heshima za mwisho kwa marehemu John Guido Nyerere baada ya kukamilika kwa ibada maalum iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki
la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya
Butiama.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Monduli na Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu Edward Lowassa wakati wa mazishi ya John Guido Nyerere yaliyofanyika nyumbani kwa Baba wa Taifa ,Butiama.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu John Guido Nyerere likiteremshwa kaburini na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
 Mama Maria Nyerere akiweka udongo kwenye kaburi la mtoto wake John Guido Nyerere.
 Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Asha-Rose Migiro akiweka udongo kwenye kaburi la John Guido Nyerere.
 Mtoto wa mwisho wa marehemu John Guido Nyerere anayefahamika kwa jina la Wanzagi akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na shangazi yake Anna Nyerere.
 Ni huzuni kwa kila mtu.
 Mama Maria Nyerere akiweka shada la mau kwenye kaburi la mtoto wake John Guido Nyerere.
 Mtoto wa Marehemu anayeishi Lusaka Zambia, Sofia Nyerere Mwape akiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba yake marehemu John Nyerere.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa heshima mbele ya kaburi la marehemu John Gaudo Nyerere mara baada ya kuweka taji la maua.
 Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Shyrose Bhanji akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu John Nyerere kwenye mazishi yaliofanyika nyumbani kwa marehemu Baba wa Taifa Butiama.
Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakishiriki kuweka mashada ya maua kwenye kaburi la John Guido Nyerere.
 Baadhi ya Watoto wa marehemu pamoja na ndugu wengine.
 Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Asha-Rose Migiro akisoma salaam za rambi rambi kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri wa Muungano wakati wa mazishi ya John Nyerere.
Emily Magige Nyerere akifafanua jambo wakati wa mazishi ya John Guido Nyerere.
(Picha zote na Adam H. Mzee)
MAPATO YA NDANI YAIMARISHWE KUFANIKISHA MALENGO YA MILLENIA

MAPATO YA NDANI YAIMARISHWE KUFANIKISHA MALENGO YA MILLENIA

May 13, 2015
IMG_7697
Mkurugenzi wa kupunguza umaskini kutoka Wizara ya Fedha, Ana Mwasha (kulia) akifungua kongamano, linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDG's ili kuhakikisha mafanikio katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF) Dk.Oswald Mashindano na Katikati ni Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama.(Picha na Zainul Mzige wa modewjiblog)
Na Mwandishi Wetu
MKURUGENZI wa Kupunguza Umasikini kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha amesema changamoto za uwezo wa kifedha kutekeleza miradi mbalimbali iliyokuwa katika Malengo ya Milennia, zinatoa ishara tosha ya kubadili mikakati ili kuwa na mafanikio katika Mipango ijayo ya Maendeleo Endelevu (SDGs)
Alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na washiriki wa kongamano, linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDGs ili kuhakikisha mafanikio.
Alisema ipo haja ya kuimarisha makusanyo ya fedha za ndani na kuacha kutegemea wahisani, kwa kuwa moja ya sababu za kushindwa kutekelezwa kwa Malengo ya Millenia ni ahadi za wahisani kutotekelezwa.
Alisema kipengele cha nane katika Malengo ya Millennia, kiligusia ushirikiano wa kimataifa, ahadi ambazo amesema ukiachia nchi za Luxemburg, Denmark, Sweden na Norway, mataifa mengi hayakutoa asilimia 0.7 ya pato lao la ndani, ambalo lilikubalika kimataifa kusaidia Malengo ya Millennia kwa nchi masikini.
Alisema ili kuwepo na mafanikio katika miradi mipya na ile inayoendelezwa kutoka MDGs, iko haja ya kuangalia jamii iliyopo vijijini, ambako ndiko kwenye umasikini wa kutisha, ingawa Tanzania imefanya vyema kuondokana na umasikini wa chakula.
Umasikini wa chakula umepungua hadi asilimia 9 wakati Malengo ya Millenia yalikuwa ni asilimia 11.
Alisema ipo haja ya kufungua mawasiliano ya vijijini, kuinua kilimo, kuwapatia nafasi ya masoko na kuinua huduma za jamii.
Pamoja na kuzungumzia uwezo wa kifedha, alisisitiza haja ya wadau kuangalia namna ya kushirikisha sekta binafsi katika kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ili kukabili umasikini.
IMG_7692
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama akizungumza kwenye kongamano la siku moja linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDG's ili kuhakikisha mafanikio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF).
Alisema mahitaji ya msingi katika kupunguza umasikini, hayajafikiwa kwani tumefikia asilimia 28.2 wakati tulitakiwa kuwa asilimia 19.
Alisema ipo haja kubwa ya kuangalia utekelezaji wa malengo endelevu kwa kuoanisha na mikakati mingine ya kidunia na ya kikanda, huku kazi kubwa ikiwa kuhakikisha malengo yote 17 yanatekelezwa katika muda uliopangwa.
Katika kongamano hilo, washiriki walipata nafasi ya kumsikia Balozi Celestine Mushy kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akichambua jinsi mataifa yalivyofikia SDGs, michakato inayoendelea na namna ambavyo anafikiri Tanzania inaweza kunufaika na mkakati mzima wa maendeleo.
Pia katika majadiliano, washiriki waliozungumzia haja ya kuangalia takwimu kwa kuoanisha kwani zimekuwa zikitafutwa na kila mtu mpaka hazijulikani nani yuko sahihi.
Aidha, walitaka mkakati wa kiviwanda ndio uzingatiwe kwani ndio unaoonesha dira ya kufanikisha maendeleo ya kitaifa, kikanda na kibara.
Kongamano hilo liliendeshwa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Uchumi (ESRF) kwa ufadhili wa UNDP.
IMG_7742
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF) Dk.Oswald Mashindano akizungumza kwenye kongamano hilo.
IMG_7724
Pichani juu na chini ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano Wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akiwasilisha mada jinsi mataifa yalivyofikia SDGs, michakato inayoendelea na namna ambavyo Tanzania inaweza kunufaika na mkakati mzima wa maendeleo.
IMG_7721 IMG_7771
Dk. Kenneth Mdadila kutoka kitengo cha uchumi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) akiwasilisha mada kwenye kongamano hilo.
IMG_7701
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kongamano hilo.
IMG_7707 IMG_7792
Pichani juu na chini baadhi ya wadau walioshiriki kwenye kongamano hilo wakichangia mada kwenye kongamano hilo.
IMG_7800