February 17, 2014

Tuzo za KILI 2014 zimezinduliwa leo, haya ndio mabadiliko yaliyofanywa.

Screen Shot 2014-02-17 at 10.54.08 AM
Ni time ya kufahamu kuhusu tuzo ambazo hutolewa kwa Wanamuziki/Wasanii mbalimbali wa Tanzania zikiwa zimeanzishwa mwaka 1999 ambapo za mwaka huu 2014 zimezinduliwa leo February 17.
George Kavishe kutoka TBL ambao ndio Wadhamini wa tuzo hizi amesema >>> ‘Maboresho makubwa ambayo tumefanya mwaka huu ni tofauti na mara zote ambazo tumekua tukihusisha Watanzania dakika za kupiga kura tu hivyo wanakosa nafasi ya kupendekeza nani aingie kwenye category gani, mwaka huu tumebadilisha kutokana na matakwa ya soko hivyo Watanzania ndio watapendekeza nani aingizwe kwenye category gani’
‘Kupitia Magazeti, website ya Kilimanjaro na vipeperushi kuanzia kesho February 18 2014 kutaonyeshwa category zote za mwaka huu za kupigiwa kura na Wananchi, Watanzania watatuma kura zao kupitia simu ya mkononi kupitia 15440, unapendekeza msanii, kikundi au producer gani aingie kwenye kipengele’ – Kavishe
‘Kwa hiyo Mwaka huu Watanzania watapiga kura mara mbili ambapo ya kwanza ni nani aingie kwenye category alafu tutarudi tena kupiga kura nani awe mshindi wa kwanza, yani mwaka huu ile timu ya watu 100 ya Waandishi, Watangazaji na wadau wa muziki kuchagua nani na nani aingie kwenye category haitofanya hivyo bali itakutana kuhakikisha tu kama wimbo uliopendekezwa na Wananchi ni wa mwaka husika, uko sehemu husika na pia kama umekidhi vigezo vya kuingia KTMA’ – Kavishe

RC GALLAWA AFANYA ZIARA WILAYA YA MUHEZA ,AKAGUA MAENDELEO,KUZINDUA MIRADI YA MAJI NA MAABARA

February 17, 2014
 MKUU WA MKOA WA TANGA AKIZUNGUMZA NA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI POTWE WILAYANI MUHEZA WAKATI WA ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYANI HUMO
MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIZUNDUA CHUMBA CHA MAABARA KWENYE SHULE YA SEKONDARI POTWE WAKATI AKIWA KWENYE ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYANI HUMO ANAYESHUHUDIA NI MKUU WA WILAYA YA MUHEZA,SUBIRA MGALU.

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIGAWA KADI ZA CHF KWA WAZEE WILAYANI MUHEZA WAKATI WA ZIARA YAKE.

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIZUNGUMZA NA WAKAZI WA KIJIJI NDONDONDO KATA YA POTWE WILAYANI MUHEZAA.

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA WA KUTOKA PILI KULIA AKISISITIZA JAMBO WAKATI AKIWA KWENYE KITUO CHA AFYA MHAMBA WILAYANI MUHEZA AKIWA KWENYE ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYANI HUMO KUSHOTO NI MGANGA MKUU WA WILAYA YA MUHEZA,MATHEW MGANGA.

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIWAHUTUBIA WAZEE KWENYE KITUO CHA AFYA MHAMBA MARA BAADA YA KUWAKABIDHI KADI CHA CHF WA KWANZA KULIA NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA AMIRI KIROBOTO .


MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIVIKWA SKAFU NA WANAFUNZI WA SHULE YA SONGA WILAYANI MUHEZA.


MKUU WA MKOA WA TANGA.LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIPANDA MTI KWENYE SHULE YA SEKONDARI SONGA WILAYANI MUHEZA WAKATI WA ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYANI HUMO

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIZUNDUA KISIMA CHA MAJI KIJIJI CHA BWEMBWERA KATA YA MAMBOLEO WILAYANI MUHEZA WAKATI WA ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI.

  MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKISISITIZA JAMBO MARA BAADA YA KUZINDUA MRADI WA KISIMA CHA MAJI.

DC MTASIWA AIPONGEZA NMB

February 17, 2014
   
MKUU WA WILAYA YA PANGANI,HAFSA MTASIWA AKIZUNGUMZA WAKATI HAFLA YA KUPOKEA VITANDA 35 VILIVYOTOLEWA NA BENKI YA NMB KWA SHULE YA SEKONDARI TONGANI ILIYOPO KATA YA MKARAMO WILAYANI HUMO KULIA NI MENEJA WA NMNB TAWI LA PANGANI,ELISA MCHOME

MKUU WA WILAYA YA PANGANI ,HAFSA MTASIWA KUSHOTO AKIPOKEA VITANDA 35 TOKA KWA MENEJA WA NMB TAWI LA PANGANI ELISA MCHOME

HAPA NI MKUU WA WILAYA YA PANGANI HAFSA MTASIWA KUSHOTO AKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA WALIMU WA SHULE HIYO WA NNE KULIA NI MENEJA WA NMB BENKI TAWI LA PANGANI ELISA MCHOME.
.                           NA OSCAR ASSENGA, PANGANI
MKUU wa wilaya ya Pangani, Hafsa Mtasiwa amepongeza jitihada zinazofanywa na taasisi za kibenki hapa nchini kupitia sera zao za misaada kwa jamii ikiwemo kuchangia maendeleo ya elimu ikiwa ni sehemu ya kurudisha faida wanayoipata kwa jamii.

Mtasiwa alitoa kauli hiyo jana wakati akipokea vitanda 35 vya kulalia vilivyotolewa na benki ya NMB kwa ajili ya shule ya sekondari Tongani iliyopo kata ya Mkaramo wilayani humo ambapo vitanda hivyo vitatumika kwa matumizi ya wanafunzi wapatao 70 vyenye thamani ya sh.milioni tano (5000, 000)

SERIKALI YAOMBWA KUTENGA ENEO LA HEKTA 2000 ILI KUBORESHA MRADI ZA NG'OMBE WA NYAMA.

February 17, 2014
NA KHADIJA BARAGASHA,HANDENI.
SERIKALI imeombwa kutenga eneo lenye ukubwa wa hekta 2000  kwajili ya kuboresha mradi wa Ng'ombe wa nyama aina ya Borani na Sewali uliopo katika  kijiji cha Taula Kata ya Kwedizinga Wilaya ya  Handeni Mkoani Tanga.

Akizungumza na TANGA RAHA ,Mwenyekiti wa Kampuni ya Masaya Farm  Limited Sabas Woiso alisema kuwa matarajio yao ni kufikia hadi Ngombe 1500 wenye tija  ambao utawapelekea kuingia katika soko la ndani na nje ya nchi kwa kupitia mradi huo.

Owiso amesema hivi sasa wana eneo dogo ambalo ni hekta 120
ukilinganisha na mifugo iliyopo kuwa mingi na kila ngombe mmoja
anatakiwa kutengewa hekta moja kwa mzunguko wa mwaka tofauti na eneo walilonalo hivi sasa  ambapo  wana Ngombe 123, Ndama 21 na baadhi yao kuwa wajawazito hivyo itapelekea kuwa na msongamano mkubwa  katika eneo hilo.

SERIKALI YATAKIWA KUTOA KODI KATIKA NYUMBA ZA (NHC).

February 17, 2014
Na Khadija Baragsha, Mkinga.

KAMATI ya  kudumu ya Bunge ya  Ardhi, Maliasiri na Mazingira  imeitaka serikali kuondoa kodi  kwenye vifaa vya  mradi wa ujenzi wa nyumba za  gharama  nafuu unaoendeshwa na Shirika la Nyumba Tanzania (NHC)  ili kumuwezesha mwananchi wa hali ya chini kuondokana na makazi duni.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jemes  Lembeli aliyasema hayo baada ya  taarifa ya mradi huo iliyosomwa mbele ya kamati hiyo na Mkurugenzi wake, Benedict  Kilimba na kueleza kuwa kodi za serikali zimesababisha  bei ya nyumba hizo kuwa kubwa.