TAWA YAPEWA TUZO NA OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE NA URATIBU

TAWA YAPEWA TUZO NA OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE NA URATIBU

September 12, 2023

 

Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu imeipatia Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) tuzo maalum kwa ajili ya kutambua na kuthamini mchango wake katika kufanikisha Kongamano la Pili la wiki ya Kitaifa ya Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza.

Tuzo hiyo imetolewa leo jijini Arusha na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Dotto Biteko wakati akifungua kongamano hilo ambapo ameipongeza TAWA huku akiwasilisha salamu za Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa za kuwasihi na kuwapongeza washiriki kwa kuweka ratiba ya kutembelea hifadhi za taifa, mapori tengefu na vivutio vingine vya utalii vilivyopo ukanda wa kaskazini mwa Tanzania.

“Mhe. Waziri Mkuu amenituma niwaambie amefurahi sana kusikia kuwa kwa mujibu wa ratiba yenu mtakwenda kutembelea vivutio vya utalii hivyo amewasihi sana mkirudi mlikotoka mkawe mabalozi wema kwa nchi yetu na kutangaza vyema Tanzania”

Kando na hilo, Naibu Waziri Mkuu Dkt. Biteko amewataka maafisa masuhuli wote nchini kuviwezesha vitengo vya ufuatiliaji na tathmini katika wizara na taasisi zao kwa kuhakikisha kunakuwa na wataalamu wa kutosha, vitendea kazi na rasilimali fedha ili viweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.



Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama amesema, wakati kongamano hili likifanyika kwa mara ya Pili hapa nchini, Serikali imefanyia kazi kwa Asilimia mia, (100%) utekelezwaji wa agizo la uanzishwaji wa Idara za Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara na Serikali.

Awali akiongea wakati wa Ufunguzi wa Kongamano hilo, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi, alisema kwa kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa kujipima matokeo, Taasisi za Umma zinaweza kujihakikishia kuwa zipo katika njia sahihi za utekelezaji katika kufikia malengo yake, hivyo Ufuatiliaji na Tathmini ni njia nzuri ya kujifunza na kuwajibika.


PSSSF YATOA MICHE YA MITI KWA WANACHAMA WAKE KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI

September 12, 2023

 

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, DAR ES SALAAM

Katika kutambua na
kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi,
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetoa miche kwa
wastaafu watarajiwa wa Mfuko huo waliokuwa wakihudhuria semina elekezi ya kujiandaa
na maisha ya kusataafu utumishi wa Umma.

Semina hiyo ambayo ilifunguliwa
Septemba 11, 2023 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira
na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, imefungwa Septemba 12, 2023
na Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba.



CPA.
Kashimba alisema, PSSSF inatarajia kuwa na wastaafu 11,000 katika mwaka wa
fedha wa 2023/24 na zoezi la ugawaji miche pia linafanyika kwenye mikoa mingine
ambako nako wastaafu watarajiwa wa Mfuko huo wanapatiwa semina kama hiyo.

“Mfuko
umepanga pia kugawa miche hiyo kwa wanachama wake 739,000 kote nchini.” Alisema

Akihutubia
katika kongamano la Mabadiliko ya Tabia Nchi lililofanyika jijini Nairobi
Nchini Kenya, Septemba 6, 2023, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisema kuna hatari kubwa, na hatua inapaswa
kuchukuliwa sio kesho bali leo na haswa sasa ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi.

Tayari
Jumuiya ya Kimataifa imemtambua Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo Septemba 12,
2023 Bodi ya Ushauri ya Kituo cha Dunia cha Uhimilivu wa Mabadiliko ya
Tabianchi (Advisory Board of the Global Centre on Adaptation – GCA), imemteua kuwa
Mjumbe wa bodi hiyo.

Akieleza
zaidi kuhusu umuhimu wa kupanda miti, Mkurugenzi Mkuu huyo wa PSSSF alisema  “Upandaji miti unasaidia sana katika
kukabiliana na janga hili la mabadiliko ya Tabianchi ambayo ni hatari si kwa
mazingira peke yake bali hata viumbe vilivyopo katika mazingira haya, tukiwemo
na sisi binadamu.” Alisema CPA. Kashimba

“Pia
kwa kushirikiana na watumishi wa Mfuko tutaendesha kampeni ya kuhakikisha kila
mtumishi anapanda na kuitunza miche kumi ya miti, kampeni hii itaendelea hadi
Disemba 2023 ambako tunatarajia tutakuwa tumepanda miche takribani million 7.

“Hivyo
ili kuanza kampeni hii mahsusi, katika semina hii kila mwanasemina na wafanyakazi
watapatiwa angalau mche mmoja wa mti kwa ajili ya kupanda na kutunza”

Aidha
CPA. Kashimba aliwaasa wastaafu hao watarajiwa kuzingatia yale waliyojifunza lakini
kubwa kujiepusha na matapeli ili wastaafu hao watarajiwa waendelee kuishi maisha
mazuri.

“Genge
hili lina nguvu sana tusilipuuze, Mafao ndio turufu yetu ya mwisho tuyatunze.” Aliasa.

Akizungumzia
uamuzi huo wa PSSSF, Msaatu mtarajiwa Bw. Laurian Mganga, alimpongeza Mkurugenzi
Mkuu wa PSSSF CPA. Hosea Kashimba na uongozi mzima wa Mfuko huo kwa uamuzi wa kuwapatia
elimu ya kujiandaa kabla ya kustaafu, lakini pia kuwapatia kila mstaafu mche mmoja
wa kupanda ili kutunza mazingira.

Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, akiwa amebeba mche wakati wa zoezi la ugawaji miche kwa wastaafu watarajiwa pamoja na watumishi wa Mfuko huo.

 

Watumishi wa PSSSF wakiwa wamebeba miche ya miti tayari kwa zoezi la kuigawa kwa washiriki

Mtumishi wa PSSSF, Bi. Nelu Mwalugaja (kushoto), akigawa miche kwa wastaafu watarajiwa

 

Baadhi ya wastaafu wakiangalia miche waliyopewa

CPA. Kashimba, akizungumza na wastaafu watarajiwa wakati wa kufunga semina hiyo Septemba 12, 2023

CPA. Kashimba, akiagana na mmoja wa wastaafu watarajiwa mwishoni mwa semina hiyo.

CPA. Kashimba akiongozana na Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa baada ya kufunga semina hiyo.

 

Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa, akizungumza na wastaafu watarajiwa wa mkoa wa Dar es Salaam, Septemba 12, 2023.

 

 

Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, PSSSF, Bw. James Mlowe, akizungumza na wastaafu watarajiwa wa mkoa wa Dar es Salaam, Septemba 12, 2023.
Mkurugenzi wa Fedha PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi (kushoto), akiteta jambo na Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, Bw. James Mlowe.

 

 

Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa, akizungumza na washtaafu watarajiwa wa mkoa wa Dar es Salaam, Septemba 12, 2023.

 

 

 

 

 

Meneja wa PSSSF, Kanda ya Ilala, Bi. Uphoo Swai

WAZIRI GWAJIMA ATOA ONYO KUWATUMIA WATOTO KUCHEZA NYIMBO ZISIZO NA MAADILI KWENYE KUMBI ZA STAREHE

September 12, 2023


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt.Dorothy Gwajima amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuunda Kamati mtambuka na kuipa jukumu la kuja na mpango wa haraka na wa muda mfupi wa kudhibiti uvunjifu wa sheria ya mtoto na sheria nyingine za nchi zinazohusika na kutunza maadili.

Ametoa maagizo hayo leo Septemba 12,2023 Jijini Dar es Salaam, wakati alipokutana na wadau mbalimbali kufuatia kwa kushamiri vitendo vya kusambaa kwa maudhui yanayohusisha watoto wakicheza muziki usio na maadili kwenye kumbi za starehe.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri Gwajima amesema kuwa kupitia mpango huo, wadau mbalimbali wakiwemo BASATA, TCRA, Wizara ya Katiba na Sheria, Bodi ya Filamu, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na wadau wengine muhimu waweze kushiriki kikamilifu katika kutokomeza yanayochochea mmomonyoko wa maadili kwa watoto wetu.

"Natoa siku 21 nipokee yatokanayo na kazi ya kamati hii ili nitoe mrejesho kwa jamii na kuandaa mjadala wa wazi ili jamii nayo itoe maoni yajumuishwe kwenye kazi ya kamati kwa ajili ya umiliki wa pamoja kama jamii". Amesema Waziri Dkt.Gwajima

Aidha Waziri Gwajima amewataka Wamiliki wa kumbi za starehe na Washereheshaji(MC) nchini, kuzingatia Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 ili kuwaepusha watoto na wimbi la mmomonyoko wa maadili.

Amesema kuwa washehereshaji na wamiliki wa kumbi za starehe, wapiga muziki (DJs) na Wazazi wana nafasi kubwa katika kumlinda mtoto ili kudhibiti mmomonyoko wa maadili dhidi va watoto kupitia Sheria ya mtoto, Sura ya 13 kifungu cha 158 cha Katazo la Jumla.

"Pamoja na juhudi zinazofanywa a Wizara kwa kushirikiana na Wadau, bado baadhi ya familia na jamii wakiwemo wazazi na walezi hawatimizi wajibu wao kwa ufanisi kwenye malezi na makuzi stahiki ya watoto". Ameeleza