PSSSF YATENGA MUDA MAALUM WA MAJUMA MANNE KUSIKILIZA NA KUZIPATIA UFUMBUZI CHANGAMOTO ZA WANACHAMA NCHI NZIMA TANZANIA NA ZANZIBAR.

November 23, 2023

 

NA K-VIS BLOG/KHALFANS AID, ARUSHA

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetenga muda maalum wa majuma manne kuanzia Novemba 27 hadi Disemba 22, 2023, kwa lengo la kusikiliza na kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali za wanachama, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, CPA. Hosea Kashimba, amesema.

CPA. Kashimba amesema hayo kwenye banda la PSSSF katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Novemba 24, 2023.

“Iwapo kuna mwanachama yeyote mwenye changamoto yoyote inayohusu uanachama, michango na mafao, afike katika ofisi za PSSSF zilizo jirani naye Tanzania bara na Zanzibar, tutamsikiliza na kutatua changamoto yake.” Alisisitiza.

Alisema zoezi hilo litakuwa likifanyika kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni, Jumatatu hadi Ijumaa.

“Lakini hata baada ya kipindi hicho maalum kufikia ukomo, bado tutaendelea kuwapatia huduma wanachama wetu, lengo hasa ni kuhakikisha wanachama wetu wanafurahia huduma zetu wakati wote.” Alisema CPA. Kashimba.

Pia amerejelea angalizo kwa wanachama na wastaafu, kuwa wasikubali kupokea maelekezo yoyote kutoka kwa watu wasiowajua endapo wanahisi wanachangamoto yoyote kuhusiana na uanachama wao au mafao yao.

“Tunawaasa wanachama wetu hususan wale wanaokaribia kustaafu, watambue kuwa huduma zetu zinatolewa bure bila malipo yoyote, na kama wanachangamoto yoyote wapige simu namba ya bure 0800 110 040 au kupitia mitandao yetu ya kijamii kupitia anuani ya PSSSFTZ.” Alifafanua CPA. Kashimba.

CPA. Hosea Kashimba, Mkurugenzi Mkuu PSSSF,

KITANDULA ATOA MSAADA WA VYAKULA NA FEDHA KWA WALIOKUMBWA NA MAFURIKO JIMBONI KWAKE

November 23, 2023




Na Mwandishi Wetu, MKINGA.

MBUNGE wa Jimbo la Mkinga (CCM) Dastan Kitandula ametoa msaada wa Vyakula na Fedha kwa Kaya 36 zilizopo kwenye Kata ya Manza na Mtimbwani wananchi katika Kijiji cha Msimbazi ambao walikumbwa na kadhia ya mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali hapa nchini

Kitandula ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii aliamua kutoa msaada huo wakati akiwa kwenye ziara ya Jimbo hilo  ili kuhakikisha wananchi hao wanaaondokana na changamoto ambazo wamekumbana nazo kutokana na uwepo wa mafuriko hayo

Akizungumza wakati akiwa kwenye ziara hiyo pamoja alipokwenda kushuhudia zoezi la ukoaji wa wananachi katika Kijiji cha Msimbazi Kata ya Manza kutokana na mvua kubwa zinazoendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kitandula aliwaeleza wananchi hapo kwamba yupo pamoja nao na kuhaidia kuendelea kuwasaidia kuhakikisha wanaondokana na changamoto mbalimbali ili kuweza kujikwamua kiuchumi

Katika hatua nyengine Mbunge Kitandula alitoa msaada wa Pikipiki kwa kikundi cha wafugaji kwa ajili ya kukusanya maziwa kutoka kwa wafugaji wadogo wilayani humo.

Baada ya kuwakabidhi Pikipiki hiyo alimshukuru Mkuu wa wilaya hiyo Kanali Maulid Surumbu kwa kumshirikisha kwenye jambo hili ni kazi kubwa na nzuri ambazo zimekuwa zikifanywa kwa ajili ya kuwakwamua kiuchumi wafugaji hao

 “Nimeona niwaunge mkono kwa kuwapatia pikipiki hii naamini utakuwa chachu kwenu lakini pia niwaambie kwamba tupo pamoja na tutaendelea kushirikiana “Alisema

Awali akizungumza mmoja wa wanakikundi hao Abdala Mwajasi alimshukuru Mbunge huyo kwa msaada aliowasaidia huku akieleza mbunge huyo ni mahiri sana kuwasaidia wananchi hasa wanapokuwa wamekumbana na changamoto mbalimbali.

“Tunakushuru Mhe Mbunge Wetu kwa kutusaidia jambo hilo la umuhimu mkubwa kwa sababu sisi tauna uwezo wa kununua pikipiki “Alisema