Asante
mungu Kwa kunipa uhai Na kipaji ambacho leo hii kina fanya naitwa Aslay
pia nakushukuru kwa kunifikisha kwenye mikono Ya mtu mwenye moyo wa
kibinaadamu. Najua kuna mengi makubwa ambayo boss wangu @mkubwafella
umenifanyia ambayo si vyema kuyataja yote kwasababu wakati wake
haujafikia ila naomba nichukue fulsa hii kukushukuru kwa
hiki ulichonifanyia leo katika sherehe Ya kusherehekea siku yangu Ya
kuzaliwa umenifanya nijione mwenye thamani kubwa duniani sikutegemea
kama leo itakuwa siku yangu ya kumbukumbu ambayo
sitoweza kuisahau hata Nije kuwa bilionea @mkubwafella asante kwa
kunipa hii zawadi ambayo mimi kama mimi sikuiwazia kabisa kama Leo
nitapata gari Na ninaushukuru uwongozi mziki Wa #mkubwanawanawe pamoja
na manager wangu @chambusso boss wangu @babutale @mhtemba na mama yangu
@sweatfella bila kuwasahau wasanii wenzangu wa @yamoto_band mungu ndie
atakaewalipa ... Nawatakia usiku mwema woote na Watu wa Dodoma Tukutane
kesho pale Matei
Akiongea wakati wa
uzinduzi Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Bwana Levi Nyakundi alisema”
uzinduzi wa punguzo la gharama za kupiga simu ni uthibitisho wa dhamira
ya kampuni ya Airtel kuwapatia watanzania dili lenye thamani halisia ya
fedha zao na kuwawezesha watu wengi zaidi nchini kuwasiliana kirahisi.
Lengo letu ni kuendelea kutoa huduma za kibunifu na zenye gharama nafuu
ili kukithi mahitaji ya watanzania wote. Wateja wetu watakaojiunga na
huduma ya “Airtel Zone” kuanzia leo, sasa hivi wataweza kupiga simu na
kupata punguzo la hadi asilimia 99 na punguzo hili litategemea mahali
alipo mteja”
“Hii ni punguzo
litakalosaidia sana wateja wa Airtel kupata unafuu wa kuwasiliana
kibiashara, masomo au kwa kuwasiliana na ndugu jamaa au wapendwa wao
bila kuwa na wasiwasi juu ya gharama zao za simu” alieleza bw, Nyakundi
Tunaamini huduma hii ya
“Airtel Zone” imekuja kwa wakati muafaka wakati mawasiliano ya simu za
mkononi ni nyenzo muhimu katika ukuzaji wa shughuli za kiuchumi na za
kijamii aliongeza Nyakundi
Akifafanua zaidi kuhusu
huduma hii Mkurugenzi wa Mawasilaiano Bi Beatrice Singano Mallya,
alisema” punguzo la gharama litategemea mahali mteja alipo na muda
anaopiga simu, mteja atapata ujumbe utakaomuonyesha kiwango cha punguzo
anachopata kwa mahali alipo, alikadhalika mteja anaweza kupiga
*149*39*0# ili kuangalia kiwango cha gharama ya kupiga simu. Huduma hii
ya “Airtel Zone” ni kwa wateja wa malipo ya awali na punguzo hili
litatumika kupiga simu za ndani tu .
Sambamba
na hilo mteja atakayekuwa na kifurushi cha muda wa maongezi kama vile
Airtel yatosha na vifurushi vingine punguzo litaanza pale tu kifurushi
chake cha muda wa maongezi kitakapoisha.
Kuujiunga ni rahisi, bure na mara moja tu, piga 107 ufate maelekezo au piga *149*39#” aliongeza, Singano Mallya.