RAIS KIKWETE AENDELEA KUIMARIKA AANZA KAZI NYEPESI

November 11, 2014

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea na kazi ndogo ndogo wakati akiendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Johns Hopkins huko Baltimore Maryland nchini Marekani leo. 
Rais jakaya Kikwete akizungumza na daktari wake. Picha na Fredy Maro
 SERIKALI KUWALINDA WAHADZABE – WAZIRI MKUU

SERIKALI KUWALINDA WAHADZABE – WAZIRI MKUU

November 11, 2014
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipokea tuzo ya Uhamasishaji na Ufugaji bora wa nyuki  kutoka kwa Rais wa Chama cha Wafugaji Nyuki Duniani, Gilles  Ratia  katika kongamani la ufugaji nyuki barani Afrika lililofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Novemba 11, 2014. Katikati ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 5 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaonyesha wazee wa kabila la Wahadzabe asali iliyofungashwa tayari kwa kuuzwa katika Kongamano la Ufugaji nyuki barani Afrika lililofanyika kwenye  Kituo cha Mikutano cha Kimataifa chaArusha ( AICC)  Novemba 11, 2014. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Vincent Ole Kone, wapili kulia ni Maidona Wazael  na watatu kulia ni Jacob Edward. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
2 
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akitazama mazao mbalimbali yanayotokana na nyuki katika maonyesho yaliyokwenda sambambamba na Kongamano la  Ufugaji Nyuki Afrika  kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Novemba 11, 2014. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na kushoto kwake ni Mhamasishaji wa ufugaji nyuki na usindikaji asali  wilayani Loliondo, Krystern Erickson.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
1 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaonyesha wazee wa kabila la Wahadzabe asali iliyofungashwa tayari kwa kuuzwa katika Kongamano la Ufugaji nyuki barani Afrika lililofanyika kwenye  Kituo cha Mikutano cha Kimataifa chaArusha ( AICC)  Novemba 11, 2014. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Vincent Ole Kone, wapili kulia ni Maidona Wazael  na watatu kulia ni Jacob Edward. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama ngoma kabla ya kufungua kongamno la ufugaji nyuki Afrika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Novemba 11, 2014. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 6 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihutubia  wakati alipofungua Kongamano la Ufugaji Nyuki Barani Afrika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Novemba 11, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
7 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipata maelezo kuhusu vifaa vya kukamulia asali kutoka kwa watalaam wa Kichina, Huang Hejie (kushoto) na  Zhinyong Wang (watatu kushoto) katika kongamano la Ufugaji Nyuki Afrika  lililofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha  (AICC) Novemba 11, 2014.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………..
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali itaendelea kuyalinda makabila madogo nchini yakiwemo ya Wahdazabe na Wasandawe ambayo yanategemea rasilmali misitu kwa maisha yao na ustawi wao.
 “Tutakuwa tunafanya makosa kama tutawanyang’anya rasilmali misitu makabila madogo hapa nchini kama vile Wahadzabe, Wandorobo na Wasandawe kwani ndiyo rasilami pekee inayowawezesha wapate chakula cha kutosha,” alisema.
 Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Novemba 11, 2014) wakati akifungua Kongamano la Kwanza la Ufugaji Nyuki Barani Afrika la Mwaka 2014 lililoanza leo kwenye ukumbi wa AICC, jijini Arusha. Kongamano hilo linashirikisha wajumbe 590 kutoka ndani na nje ya nchi. Nchi za nje zinazoshiriki kongamano hilo ni 24, ambapo kati ya nchi hizo nchi 12 ni za bara la Afrika.
 Kongamano hilo la siku tatu limeandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kuwakutanisha wafugaji nyuki, wafanyabiashara, wataalamu na wawakilishi wa taasisi za ndani na nje ya nchi ili kujadili njia za kuboresha ufugaji nyuki na kukabiliana na changamoto za ufugaji nyuki hapa nchini na barani Afrika kwa ujumla.
 Waziri Mkuu aliwataka viongozi wa Halmashauri na watu wenye maamuzi wasiwasumbue kwa kuwalazimisha wabadili maisha yao na kutoka kwenye mfumo wa ikolojia (ecosystem) ambao wameuzoea. “Tusiwabugudhi, tusiwatoe kwenye mfumo wao wa ikolojia. Tuwasaidie kuwapa teknolojia mpya ili waweze kufuga kisasa na kupata faida huku wakiishi kwenye mazingira hayohayo waliyoyazoea mpaka hapo watakapozoea na kuamua kubadilika kwa kubaini kuwa njia zao za zamani haziwasaidii sana.”
 Akizungumzia kuhusu ufugaji nyuki barani Afrika, Waziri Mkuu alisema ufugaji nyuki umeegemea zaidi katika rasilimali misitu na kilimo ambapo Afrika kwa asilimia kubwa shughuli ya ufugaji nyuki hufanyika katika misitu.
 “Bara la Afrika lina ukubwa wa eneo la kilometa za mraba milioni 30.2 na asilimia 20 ya eneo hilo ni misitu. Asilimia 40 ni misitu ya Savanna ambayo ni muhimu kwa ajili ya ufugaji nyuki. Mapori haya pamoja na maeneo ya kilimo yana uwezo mkubwa wa kuzalisha mazao ya nyuki kwa wingi,” alisema Waziri Mkuu.
 Akizungumzia kuhusu ufugaji nyuki nchini Tanzania, Waziri Mkuu alisema takwimu za Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) zinaonesha kuwa Tanzania ni nchi ya pili barani Afrika inayozalisha asali kwa wingi (tani 34,000 kwa mwaka), ya kwanza ikiwa ni Ethiopia (tani 45,000 kwa mwaka).
 “Inakadiriwa kuwa Tanzania ina uwezo wa kuzalisha tani 140,000 za asali na tani 10,000 za nta kwa mwaka. Lakini ni asilimia saba tu ya uwezo huo ndio huzalishwa. Hii ni kwa sababu zao hilo limepuuzwa tangu siku nyingi na halijapewa msukumo unaostahili.”
 Alisema sekta ya ufugaji nyuki ina mchango mkubwa katika maisha ya mwanadamu kwa kumpatia chakula, ajira na kipato. “Wananchi hunufaika kutokana na mauzo ya asali, nta na mazao mengine ya nyuki, utengenezaji wa vifaa vya ufugaji nyuki, kusambaza malighafi za viwandani na huduma ya uchavushaji,” aliongeza.
“Wafugaji wa nyuki katika nchi zilizoendelea wanatumia teknolojia ya kuvuna sumu ya nyuki (bee venom), gundi ya nyuki (propolis), maziwa ya nyuki (royal jely) na chavua (pollen) ambavyo hutumiwa kama virutubisho na dawa. Tafiti zimethibitisha kuwa gundi ya nyuki hutibu maumivu ya meno, malaria na homa ya mifupa(arthritis) na kuongeza kinga mwilini. Sumu ya nyuki imekuwa ikitumiwa kuongeza nguvu za uzazi, kutibu uvimbe na homa ya mifupa,” alisema huku akishangiliwa.
 Waziri Mkuu aliitaka sekta  binafsi  na  taasisi  za utafiti barani Afrika zifanye tafiti zaidi katika eneo hili na kuwekeza katika teknolojia ambayo inaweza kuvuna na kuchakata mazao hayo ambayo yana soko kubwa katika viwanda vya kutengeneza madawa, virutubisho na vipodozi.
 Mapema, akielezea kuhusu kongamano hilo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Bw. Lazaro Nyalandu alisema Juni mwaka jana, Wizara hiyo ilisaini makubaliano na Shirikisho la Ufugaji Nyuki Duniani (Apimondia) ili waweze kuandaa kongamano la ufugaji nyuki barani Afrika mwaka 2014.
 Alisema kongamano hilo ambalo kaulimbiu yake ni: “Kufuga nyuki kwa kuzingatia hifadhi ya mazingira na kukuza uchumi” yaani “African Bees for a Green and Golden Economy”  litahusisha mada 88 ambazo kati yake, 45 zitawasilishwa na watafiti wa kisayansi, 26 zitakuwa za majadiliano (roundtable) na 17 zitawasilishwa katika semina.
 Alisema kongamano hilo ni kwanza kwa sababu ni mara ya kwanza kwa kongamano kama kuandaliwa barani Afrika kwa kushirikiana na Apimondia kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu species za nyuki zilizopo Afrika na mazingira ya ufugaji nyuko barani humu.
Injinia Dkt Binilith Mahenge awataka watanzania kutumia teknolojia ya kisasa kuzalisha mazao

Injinia Dkt Binilith Mahenge awataka watanzania kutumia teknolojia ya kisasa kuzalisha mazao

November 11, 2014

0 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt Injinia Binilith Satano Mahenge akifungua rasmi Kongamano la ukuaji wa uchumi unaohimili mabadiliko ya Tabia Nchi  kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mohammed Gharib Bilal,itakayofanyika kwa muda wa  siku mbili katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam leo.
1 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Ndg. Sazi Salula (katikati), akibadilishana mawazo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt Injinia Binilith Satano Mahenge (kulia), pamoja na Mkurugenzi Msaidizi – Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt.Richard Muyungi katika Kongamano la ukuaji wa uchumi unaohimili mabadiliko ya Tabia Nchi  iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam leo.
Sehemu ya Washiriki kutoka Nje na ndani ya Nchi wakisikiliza kwa makini hotuba inayotolewa na mgeni rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt Injinia Binilith Satano Mahenge (hayupo pichani). unnamed 
Mgeni Rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt Injinia Binilith Satano Mahenge (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki kutoka Ndani  na Nje ya Nchi waliohudhuria katika Kongamano la ukuaji wa uchumi unaohimili mabadiliko ya Tabia Nch4Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt Injinia Binilith Satano Mahenge (wa pili kushoto), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ,kuhusu umuhimu wa Kongamano hilo lililoandaliwa na Benki Kuu ya Dunia kwa ushirikianao na Ofisi ya Makamu wa Rais. Anayefuatia wa pili kulia Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,maliasili na Mazingira  Mhe. James Lembeli, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Bw. Philippe Dongier (kulia) pamoja na Bw.Vel Gnanendran Mkuu wa Ofisi ya DFID nchini Tanzania.
………………………………………………………………………….
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais –Mazingira Injinia Dkt Binilith Mahenge amewasihi Watanzania kutumia teknolojia mpya  na za kisasa katika kuzalisha mazao na sekta nzima ya kilimo kwa ujumla ili kuzuia uharibifu wa mazingira ikiwemo misitu. Aliyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Ukuaji wa Uchumi unaohimili mabadiliko ya Tabia Nchi. Lililofanyika jijini Dar Es Salaam. Alifungua Kongamano hilo kwa Niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Gharib Bilal.
Aliongeza kuwa Mikoa na Wilaya zote Tanzania  zinatakiwa kuweka sera endelevu ambazo zitaweza kuhakikisha kukabiliana na uharibifu wa Mazingira. Aidha alisema kuwa zipo juhudi ambazo Serikali imezichukua katika  kuhakikisha utunzaji wa  mazingira unatekelezwa na pia  kuzuia uharibifu wa mazingira kwa njia moja au nyingine.
Akiongea katika Kongamano hilo Mkurugenzi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Philippe Dongier alisema Kongamano hilo ni fursa adhimu kwa ajili ya majadiliano kuhusu program za maendeleo ya Tanzania zinavyoweza kustawi licha ya kuwepo kwa mabadiliko ya tabia Nchi. Hivyo basi Watanzania hawana budi kuwa waangalifu sababu mabadiliko ya Tabia Nchi yana athari kubwa.
Mwisho Waziri Mahenge aliwashukuru Wadau mbalimbali ambao wamehudhuria kongamano hilo kutoka ndani na nje ya Nchi. Akiwasihi sana kuendelea kutunza mazingira na pia aliwaomba watembelee vyanzo mbalimbali vya Utalii vilivyopo Nchini Tanzania ili kukuza uchumi .
Kongamano hilo ni muendelezo ya Mkutano wa New York kuhusu mabadiliko ya tabia nchi uliofanyika mwezi Septemba mwaka huu na limehudhuriwa na washiriki kutoka Ndani na Nje ya Nchi ya Tanzania.
PROFESA JOHN NKOMA AWAFUNDA MABLOGGER JINSI YA KUANDIKA KWA USAWA HABARI ZA UCHAGUZI

PROFESA JOHN NKOMA AWAFUNDA MABLOGGER JINSI YA KUANDIKA KWA USAWA HABARI ZA UCHAGUZI

November 11, 2014

1Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini Tanzania TCRA Profesa John Nkoma akizungumza katika mkutano na Mablogger wakati alipofungua mkutano huo uliojadili jinsi ya kuripoti kwa usawa habari za uchaguzi wa serikali za mitaa, Ubunge na Rais kuanzia mwaka huu mpaka mwakani, Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam ambapo pia viongozi wa Muda wa kuratibu uanzishwaji wa  Chama cha Mablogger wamechaguliwa ambao ni Joachim Mushi, Aron Msigwa mwakilishi kutoka serikalini, Shamimu Mwasha Blog za Biashara, Francis Godwin mablogger wa mikoani, Othman Maulid mwakilishi kutoka Zanzibar, Khadija Khalili, William Malecela na Henry Mdimu ambao wataongoza kwa muda wakati wa mchakato huo mkutano huo umesimamiwa na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE)DSC_5572Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Assah Mwambene akifunga rasmi mkutano huo uliofanyika Mlimani City jijini Dar es salaam.10 
Baadhi ya Malogger wakiwa katika mkutano huo. 9 
Kutoka kushoto ni Josephat Lukaza wa Lukaza Blog, Shamimu Mwasha wa 8020Fashion na Geofrey Wapamoja Blog wakiwa katika mkutano huo 8 
Baadhi ya maofisa kutoka TCRA wakiwa katika mkutano huo.  6 
John Bukuku Mkurugenzi wa Fullshangweblog.com akiwa katika mkutano huo. 5 
Baadhi maofisa wa TCRAwakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo. 4 
Andrew Kisaka Ofisa Mwanamizi wa Utangazaji TCRA akitoa mada katikamkutano huo.
TAARIFA ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TFF

TAARIFA ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TFF

November 11, 2014

index17
TAIFA STARS YAWASILI JOHANNESBURG
Kikosi cha wachezaji 23 wa Taifa Stars tayari kimewasili Johannesburg, Afrika Kusini tayari kwa maandalizi ya mechi dhidi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Swaziland.
 Mechi hiyo itafanyika Jumapili (Novemba 16 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa wa Somhlolo jijini Swaziland. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwepo Johannesburg hadi Ijumaa itakapoondoka kwenda Mbabane.
 Wachezaji wote walioitwa na Kocha Mart Nooij wapo kwenye msafara huo isipokuwa kiungo mshambuliaji Mrisho Ngasa ambaye amebaki Dar es Salaam kutokana na matatizo ya kifamilia.
 Taifa Stars inatarajia kurejea nyumbani Jumatatu (Novemba 17 mwaka huu) saa 12.45 jioni kwa ndege ya South Africa Airways.
 Wakati huo huo, kikosi cha maboresho cha Taifa Stars kitacheza mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya Rwanda kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 23. Mechi hiyo itachezwa Desemba 9 mwaka huu nchini Tanzania.
 Kikosi cha maboresho cha Taifa Stars kinachoundwa na wachezaji wenye umri chini ya miaka 23 kitakuwa kinakutana mara moja kila mwezi hadi Mei mwakani kwa ajili ya mazoezi na kucheza mechi moja ya kirafiki.
 Kocha Mart Nooij atatangaza kikosi kwa ajili ya mechi hiyo na programu nzima mara atakaporejea kutoka Swaziland.
 WAAMUZI 23 KUSHIRIKI SEMINA DAR
Waamuzi 23 wa daraja la kwanza wakiwemo wenye beji la Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameteuliwa kushiriki semina itakayofanyika Novemba 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
 Washiriki wa semina hiyo ambayo pia itakuwa na mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) wanatakiwa kuripoti Novemba 15 mwaka huu kwenye hosteli ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.
 Wakufunzi wa semina hiyo wanaotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ni Riziki Majala na Soud Abdi.
 Waamuzi watakaoshiriki semina hiyo ni Ahmed Juma Simba (Kagera), Arnold Bugado (Singida), Charles Peter Simon (Dodoma), Dalila Jafari Mtwana (Zanzibar), Ferdinand Chacha Baringenge (Mwanza), Florentina Zabron (Dodoma) na Frank John Komba (Pwani).
 Grace Wamara (Kagera), Hellen Joseph Mduma (Dar es Salaam), Israel Mujuni Nkongo (Dar es Salaam), Issa Bilali Ali (Zanzibar), Issa Haji Vuai (Zanzibar), John Longido Kanyenye (Mbeya), Jonesia Rukyaa Kabakama (Kagera) na Josephat Deu Bulali (Tanga).
 Kudra Omary (Tanga), Martin Eliphas Saanya (Morogoro), Mary Kapinga (Ruvuma), Mfaume Ali Nassoro (Zanzibar), Mgaza Ali Kinduli (Zanzibar), Samwel Hudson Mpenzu (Arusha), Soud Iddi Lila (Dar es Salaam) na Waziri Sheha Waziri (Zanzibar).