Madaktari Mkoani Tanga Wapania Kutokomeza Vifo Vitokanavyo Na Uzazi

July 23, 2014


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt Asha Mahita akieleza mkakati wa kukabiliana na upungufu wa damu kwa wajumbe 
Mratibu wa afya ya mama na mtoto Mkoa wa Tanga Dorothy Lema akionesha hali ya vifo vya kina mama tangu mwaka 2010 -2013
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Pangani Dkt Dennis Ngaromba akichangia mjadala jinsi ya kukabiliana na vifo vitokanavyo na uzazi .Habari & picha na Fatna Mfalingundi- Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe.
Madaktari Mkoani Tanga kwa pamoja wameazimia kuchukua hatua za tahadhari  ikiwemo kubuni njia mbadala  zitakazowezesha kuokoa maisha ya mama na mtoto  pindi wanakapokumbana na vikwazo vya dharura wakati wa mama kujifungua ili kufikia lengo la nne la dunia  la kukabiliana na vifo vya uzazi,watoto wachanga na walio chini ya umri wa miaka mitano.
Madaktari hao walifikia hatua hiyo mwishoni mwa wiki wakati wa kikao  cha pamoja cha Sekta ya Afya kilichofanyika Wilayani Lushoto na kuwajumuisha ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa, Waganga Wakuu wa Wilaya ,Wenyeviti wa Bodi za Afya, Wadau wa Sekta ya Afya wakiwemo MSD,NHIF,WHO,kfw,WEI na GIZ kwa lengo la kujadili changamoto na mikakati ya kuboresha Sekta ya Afya kwa mwaka 2014/2015.
Akitoa maelezo kuhusu kukabiliana na changamoto ya upungufu wa damu salama katika benki za damu ambayo ilitajwa kuwa ni miongoni mwa sababu kubwa zinazopelekea vifo vingi vya wajawazito, Mganga Mkuu wa Mkoa wa  Tanga Dkt Asha Mahita, alisema kuwa miongoni mwa mikakati waliyojiwekea ni pamoja na kuifanya hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo kuwa kituo cha kusambaza damu kwa hospitali za Wilaya badala ya kila wilaya kuomba na  kusubiri damu kutoka hospitali ya rufaa ya KCMC.
“Tumeshaiandikia  Wizara kuiombea hospitali ya Mkoa ya Bombo kuwa kituo cha kusambaza damu kwa Halmashauri zake, tunaamini kwa kufanya hivyo tunaweza kupunguza tatizo la upungufu wa damu na vifo vya kinamama”.Alisema Dkt Mahita.
Akichangia mjadala  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Pangani Dkt Dennis Ngaromba, aliwashauri madaktari wenzake kuachana na rufaa za ghafla na kuwataka  kuwafuatilia wajawazito wanaowapatia rufaa ya kwenda kujifungulia mahali kwingine kwa kuanzisha utaratibu wa kujaza fomu tatu ambayo moja itabaki mahali alipofungulia kadi,nyingine itakwenda alikopewa rufaa na nyingine kubaki katika ofisi za kijiji au mtaa ambapo utaratibu huo utakwenda sambamba na mawasiliano ya simu lengo likiwa ni kutoa historia ya Mjamzito ili hatua stahiki za haraka zichukuliwe.
“Pangani tumeweza kupunguza  vifo vya uzazi  kwa kuachana na rufaa za fumanizi na tumeweka utaratibu wa kuwatambua wanaofariki kutokana na uzazi kwa kuzishirikisha vyema ofisi za Serikali za vijiji”.Aliongeza Dkt Ngaromba.
 
Awali akiwasilisha mada Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto Mkoa wa Tanga Dorothy Lema, alisema kuwa hali ya vifo vya uzazi pamoja na watoto wachanga nchini Tanzania bado siyo nzuri,kwani inakadiriwa kuwa wanawake 8000 hupoteza maisha kila mwaka hapa nchini,huku Tanga peke yake wanawake 225 walipoteza maisha mwaka 2013. 

WAZIRI MGIMWA AKUTANA NA RC GALLAWA KUHUSU MGOGORO WA ARDHI HIFADHI YA TAIFA YA MKOMAZI.

July 23, 2014
Naibu Waziri wa Wizara ya Mali Asili na Utalii Mhe. Mahmood Mgimwa na ujumbe wake wakiwa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Chiku Gallawa kwa Ziara ya kutembelea kijiji cha Kimuni Kata ya Mwakijembe Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga kusikiliza  wananchi utatuzi wa Mgogoro wa ardhi Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.
  Katibu Tawala Msaidizi  Mkoa wa Tanga Miundi mbinu, Bi Monica Kinara akitoa taarifa ya Mgogoro wa ardhi kijiji cha Kimuni Wilayani Mkinga
  Mkuu wa Mkoa Mhe. Chiku Gallawa akisisitiza jambo
Ujumbe wa Naibu waziri, Viongozi wa Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Mkinga
WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AFUNGUA MKUTANO WA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA BRN

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AFUNGUA MKUTANO WA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA BRN

July 23, 2014


1 
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu akichangia hoja wakati wa mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN) uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Bashir Mrindoko
2.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akichangia hoja wakati mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Asha- Rose Migiro na (katikati) Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais- Usimamizi wa Utekelezaji wa Miradi (PDB), Bw. Omari Issa.
3.
4.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Angellah Kairuki (katikati) akichangia hoja wakati mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
5.
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (kulia) akichangia akichangia hoja wakati mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Shukuru Kawambwa, Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mhe. Mwigulu Nchemba, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi.
(PICHA NA ISMAIL NGAYONGA- MAELEZO)
PINDA AKUTANA NA VIONGOZI WA MAKAMPUNI UA SOMITO NA CITI BANK

PINDA AKUTANA NA VIONGOZI WA MAKAMPUNI UA SOMITO NA CITI BANK

July 23, 2014

PG4A5925
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na   viongozi wa  Citi Bank  ofisini kwake  jijini Dar es salaam Julai 23, 2014. Kulia kwake ni Waziri wa Uchukuzi , Dr. Harrison Mwakyembe. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PG4A5939
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Citi Bank baada ya kuzungumza nao , Ofisini kwake jijini  Dar es salaam julai 23, 2014. kushoto ni Waziri wa Uchukuzi aliyemabatana na ujumbe huo na kushoto kwa Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dr. Mary Nagu.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PG4A5978
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na  viongozi wa kampuni ya  Sumitomo Chemicals ya Japan wanaokusudia kuwekeza  kiwanda cha mbolea nchini na katika kilimo  cha mpunga. Wapili kushoto  ni Waziri wa  Kilimo , Chakula na  Ushirika, Mhandishi Christopher Chiza. (Picha na Ofisi  ya Waziri Mkuu)

TBL YATOA MSAADA WA SH. MIL. 45 ZA KISIMA KIJIJI CHA KAMBI YA SIMBA KARATU

July 23, 2014

 Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Doris Malulu akipeana mkono na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kambi ya Simba, Damian John wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi ya Sh. Milioni 45 zilizotolewa kwa ajili ya kuchimba kisima cha maji kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Wengine ni Meneja Mauzo TBL Mkoa wa Arusha Richard Temba (mwenye miwani) na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Karatu Moses Mabula.
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Doris Malulu akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kambi ya Simba, Kata ya Mbulumbulu wilayani Karatu, Arusha, wakati wa hafla ya kuwakabidhi mfano wa hundi ya sh. mil. 45 za kugharamia uchimbaji wa kisima cha maji kijijini hapo, mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Mauzo TBL Mkoa wa Arusha Richard Temba na aliyekaa ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Karatu, Moses Mabula.
Wananchi wa kijiji hicho wakishuhudia makabidhiano ya hundi hiyo
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Karatu, mkoani Arusha, Moses Mabula na Meneja Mauzo TBL Mkoa wa Arusha Richard Temba wakiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Maji ya Kijiji cha Kambi ya Simba pamoja na watalaamu watakaochimba kisima hicho cha maji, baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya Sh. Milioni 45 na TBL.
MAAMUZI YA PATRICK VIEIRA KUITOA MAN CITY UWANJANI BAADA YA FOFANA KUBAGULIWA, YAUNGWA MKONO NA MANUEL PELLEGRINI

MAAMUZI YA PATRICK VIEIRA KUITOA MAN CITY UWANJANI BAADA YA FOFANA KUBAGULIWA, YAUNGWA MKONO NA MANUEL PELLEGRINI

July 23, 2014


Flashpoint: Seko Fofana (No 8) kicked out at a NHK Rijeka player after being allegedly racially abused
Seko Fofana (Jezi namba 8) alimpiga mchezaji wa kNHK Rijeka baada ya kubaguliwa.

Imechapishwa Julai 23, 2014, saa 6:32 mchana

Patrick Vieira alikuwa sahihi kukitoa nje ya uwanja kikosi cha wachezaji wa timu ya vijana ya Manchester City  baada ya wanandinga wake kuoneshwa vitendo vya ubaguzi wa rangi, amesema kocha Manuel Pellegrini.
Vieira alisimamisha mechi dhidi ya NHK Rijeka katika ziara yao nchini Croatia kujiandaa na msimu mpya baada ya kinda mwenye miaka 19, Mfaransa, Seko Fofana kubaguliwa.  
Pellegrini alisema: 'Sijui sana kuhusu hilo, lakini kama Patrick aliona ni sahihi kuwatoa uwanjani wachezaji, basi itakuwa kitu sahihi'.
Seeing red: Fofana was sent off for kicking out at his opponent as the players come together
Kadi nyekundu: Fofana alioneshwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mpinzani wake
Taking a stand: Patrick Vieira (third left) walked onto the pitch after hearing what may have happened
Alionesha msimamo: Patrick Vieira (wa tatu kushoto) akiingia uwanjani baada ya kusikia kilichotokea.
Stopped: The match is abandoned as Vieira leads his team off the pitch in Croatia
Ngoma imeisha: Mechi iliahirishwa baada ya  Vieira kuwaongoza wachezaji wake kutoka nje ya uwanja nchini   Croatia
'Alitathimini hali halisi na alifanya kitu sahihi. Haiwezekani kuendelea kucheza wakati kitu kama hiki kimetokea'.
Fofana alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mpinzani wake, lakini klabu imeeleza imani yake kuwa Fofana, kijana mwenye kipaji kikubwa, alibaguliwa kabla ya kutokea kwa tukio hilo. Tukio hilo lilitokea kabla ya mapumziko.
Maamuzi ya kuahirisha mechi yalichukuliwa na viongozi waliokuwa na kikosi hicho  na Vieira aliamua kumuunga mkono kinda huyo kwasababu alikuwa na mawazo mengi kutokana na tukio hilo.
Taarifa ya klabu jana jioni ilisomeka: 'Kikosi cha vijana chini ya miaka 20 cha Manchester City kilikuwa na mchezo dhidi ya  HNK Rijeka leo (jumanne) na imeahirishwa kutokana na tukio la kiungo kijana,  Seko Fofana  kubaguliwa na mchezaji wa timu pinzani'.
Youngster: Fofana in action during an Under-21 match against Chelsea last season
Kinda: Fofana akiwa akionesha vitu vyake katika mechi dhidi ya  Chelsea ya vijana chini ya miaka 21 msimu uliopita.
Rais Kikwete afungua nyumba za Watumishi wa Afya Matemanga – Tunduru

Rais Kikwete afungua nyumba za Watumishi wa Afya Matemanga – Tunduru

July 23, 2014
haadara 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi wa kijiji cha Matemanga wakati wa hafla ya uzinduzi nyumba 480 za watumishi wa umma zilizojengwa na Taaasisi ya Benjamin W.Mkapa kwa ushirikiano na Wizara ya Afya(picha na Freddy Maro).
r
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamin w.Mkapa Dkt  Ellen Mkondya Senkoro(kushoto) akimuonesha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete michoro na ramani za nyumba za watumishi wa afya zilizojengwa na taasisi hiyo wkati hafla ya uzinduzi wa nyumba hizo uliofanyika katika kijiji cha Matemanga wilayani Tunduru leo.Watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Afya Dkt. Kebwe Stephen Kebwe na wane kushoto ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka.
utepe
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua mradi wa nyumba za watumishi wa afya zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa Foundation katika hafla iiyofanyika katika kijiji cha Matemanga wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma leo.Jumla ya nyumba 480 zinajengwa katika halmashauri 48 nchini na miongoni mwa nyumba hizo 40 zipo katika mkoa wa Ruvuma.Taasisi ya Benjamin Mkapa iliingia mkataba na Wizara ya Afya kutekeleza mradi wa miaka mitano(2011-2016) wa uimarishaji wa mifumo ya Huduma za afya chini ya ufadhili wa mfuko wa Dunia wa kupambana na ukimwi,kifua kikuu na Malaria(Global Fund).Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamin W.Mkapa Dkt.Ellen Senkoro, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Mhandisi Ramo Makani, Meneja wa Portfolio, Mfuko wa Dunia wa Kupambana na ukimwi,kifua kikuu na Malaria Bi. Tatajana Peterson, Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof.Anna Tibaijuka, Naibu Waziri wa TAMISEMI Aggrey Mwanri, Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Kebwe Stephen  Kebwe, na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Saidi Mwambungu.
KILEMA
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kiwete akiteta jambo na mkazi wa kijiji cha Ligela wilayani Namtumbo Bwana Edwin Ngonyani wakati alipokuwa anahitimisha ziara yake wilayani humo.Bwana Ngonyani ambaye alipata ulemavu baada ya kupoteza miguu yote miwili katika ajali ya moto alimweleza Rais kuwa anapata taabu ya kutafuta riziki kwakuwa anatambaa kwa taabu.Rais Kikwete alitoa ahadi ya kumsaidia mlemavu huyo ili aweze kujikimu kimaisha.
Benki ya Exim Tanzania yaandaa futari kwa wateja wake wa mkoani Tanga

Benki ya Exim Tanzania yaandaa futari kwa wateja wake wa mkoani Tanga

July 23, 2014

PIX 1
Baadhi ya wateja wa Benki ya Exim Tanzania na wafanyakazi wakifuatilia yaliyokuwa yakizungumzwa wakati wa futari iliyoandaliwa na benki hiyo mkoani Tanga kwa ajili ya wateja wake. Picha na mpiga picha wetu.
PIX 2
Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Omary Uledi, ambaye pia ni mgeni rasmi (wapili kulia)  akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya Exim Tanzania kwa wateja wake wa mkoani Tanga hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Deogratius Makwaia, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Suleiman Lighuchu (watatu kushoto)na Katibu wa Bakwata wa Mkoa, Bw. Mohamed Riami (wa kwanza kulia). Picha na mpiga picha wetu.
PIX 3
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Suleiman Lighuchu akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya Exim Tanzania kwa wateja wake wa mkoani Tanga hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Deogratius Makwaia, Mgeni Rasmi Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Omary Uledi (Wa pili kulia)na Katibu wa Bakwata wa Mkoa, Bw. Mohamed Riami (wa kwanza kulia). Picha na mpiga picha wetu.
PIX 4
Baadhi ya wateja wa Benki ya Exim Tanzania na wafanyakazi wakichukua vyakula mbali mbali vilivyoandaliwa malum kwa ajili ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo mkoani Tanga kwa ajili ya wateja wake. Picha na mpiga picha wetu.
Rais Kikwete azindua ujenzi wa Barabara ya Matemanga Tunduru Mangaka

Rais Kikwete azindua ujenzi wa Barabara ya Matemanga Tunduru Mangaka

July 23, 2014


D92A9730
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Mbunge wa Tunduru mhandisi Ramo Makani, Balozi mdogo wa Japan Kazuyoshi Matsunaga na mwakilishi Mkazi wa Benki ya maendeleo ya Afrika(ADB) Bibi Tonia Kandiero wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuzindua ujenzi Barabara ya kilometa 195.7 ya Matemanga Tunduru-Mangaka uliofanyika Tunduru mjini.Barabara hiyo imejengwa na serikali ya Tanzania kupitia wakala wa Barabara TANROADS ikisaidiwa na Benki ya mendeleo ya Afrika ADB na shirika la maendeleo la Japan JICA.Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika mjini Tunduru jana.
D92A9760
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Matemanga-Tunduru hadi Mangaka yenye urefu wa kilometa 195.7 wakati wa hafla iliyofanyika mjini Tunduru leo.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mbunge wa Tunduru Mhandisi Ramo Makani, Balozi mdogo wa Japan Kazuyoshi Matsunaga, Mwakilishi Mkazi wa ADB Bi.Tonia Kandiero na waairi wa Ujenzi John Pombe Magufuli. Barabara hiyo imejengwa na serikali ya Tanzania kupitia wakala wa Barabara TANROADS ikisaidiwa na Benki ya mendeleo ya Afrika ADB na shirika la maendeleo la Japan JICA.(picha na Freddy Maro)

MUDA WA USAJILI WAONGEZWA KWA WIKI MBILI

July 23, 2014

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeongeza muda wa usajili kwa wiki mbili ili kuzipa klabu nafasi ya kukamilisha taratibu zinazotakiwa. Hivyo hatua ya kwanza ya usajili inakamilika Agosti 17 mwaka huu badala ya Agosti 3 ya awali.

Kutokana na marekebisho hayo, kipindi cha uhamisho kinakamilika Agosti 17 mwaka huu wakati pingamizi itakuwa kati ya Agosti 19 hadi 26 mwaka huu.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itathibitisha usajili kati ya Septemba 1 na 2 mwaka huu.

Uhamisho wa kimataifa, usajili wa wachezaji huru, na utatuzi wa dosari za usajili unatakiwa uwe umekamilika kufikia Septemba 7 mwaka huu. Uthibitisho wa hatua ya mwisho ya usajili utafanywa Septemba 15 mwaka huu.

Kwa upande wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2014/2015 itaanza Septemba 20 mwaka huu, na ratiba itatolewa mwezi mmoja kabla ya kuanza ligi hiyo.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF

MBUNGE WA JIMBO LA KOROGWE MJINI AFUNGUA LIGI YA IDDI CUP ,AWATAKA VIJANA KUPENDA MICHEZO.

July 23, 2014


MBUNGE WA JIMBO LA KOROGWE MJINI,NASRI YUSUPH AKIUZNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI WAKATI WA UFUNGUZI WA LIGI YA IDDI CUP INAYOCHEZWA KWENYE UWANJA WA SOKONI WILAYANI KOROGWE,MBUGE HUYO AMEFADHILI MASHINDANO HAYO KWA KUTOA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU ZOTE ZINAZOSHIRIKI MASHINDANO HAYOO.



WACHEZAJI WA TIMU ZA KILOLE UNITED NA KOROGWE CITY WAKIWANIA MPIRA KWENYE MCHEZO WA UFUNGUZI WA MASHINDANO HAYO YANAYOCHEZWA KWA MTINDO WA MTOANO AMBAPO KILOLE UNITED WALIIBUKA NA USHINDI WA MABAO 4-1 DHIID YA KOROGWE CITY.
KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA KOROGWE MJINI,ROBERTY BAGO AKIZUNGUMZIA MASHINDANO HAYO AMBAPO ALISIFU JUHUDI ZINAZOFANYWA NA MBUNGE HUYO ZA KUINUA MICHEZO KWENYE JIMBO HILO. WA KWANZA KULIA NI MBUNGE WA JIMBO LA KOROGWE MJINI,YUSUPH NASIR, KATIKATI KULIA MWENYEKITI WA CHAMA CHA SOKA WILAYA YA KOROGWE,PETER JUMA NA KATIBU WA CHAMA CHA SOKA WILAYA YA KOROGWE,ZAINA HASSANI.
BAADA YA KUFUNGWA BAO 4-1 HALI ILIKUWA HIVI JAMANI KWANINI MMEKUBALI KUFUNGWA ONA SASA TUNATOKA.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA CHUO CHA UFUNDI GONJA MHEZA WILAYANI SAME.

July 23, 2014

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akiondoa kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha Ufundi Gonja-Mheza wilayani Same.
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria kufungua jengo moja wapo katika chuo cha Ufundi Gonja-Mheza wilayani Same.
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akitoka katika moja ya jengo katika chuo cha Ufundi Gonja-Mheza muda mfupi baada ya kuweka jiwe la msingi na kukata utepe kuaashiria kuanza kwa  ujenzi wa chuo cha Ufundi Gonja-Mheza wilayani Same.
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akiotesha mti katika eneo la ujenzi wa chuo cha Ufundi Gonja-Mheza wilayani Same.
Mke wa Waziri mkuu,Mama Tunu Pinda akiotesha mti katika eneo la ujenzi wa Chuo cha Ufundi cha Gonja-Mheza wilayani Same.
Mke wa Waziri mkuu Mama Tunu Pinda akizungumza na wakazi wa Gonja Maore ,wakati waziri mkuu Mizengo Pinda alipofanya ziara ya siku moja kuweka jiwe la msingi katika chuo cha ufundi Gonja Mheza wilayani Same.
Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Ibrahim Msengi akimtambulisha mbunge wa jimbo la Same Mashariki ,Anne Kilango kwa wageni waliofika katika uwekaji wa jiwe la Msingi katika chuo cha Ufundi Gonja Mheza wilayani Same.
Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania ,Mizengo Pinda akizungumza muda mfupi baada ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha Ufundi Gonja Mheza wialayani Same.
Mbunge wa jimbo la Same Mashariki ,Anne Kilango akizungumza muda mfupi baada ya waziri mkuu Mizengo Pinda kuweka jiwe la Msingi katika Chuo cha ufundi cha Gonja Mheza.
Wakazi wa kijiji Cha Maore walitoa zawadi ya Upinde na Mishale kwa Waziri mkuu Mizengo Pinda.
Mke wa Waziri mkuu pia alipataiwa zawadi ya kitenge na Vyakula.
Baaadhi ya wananchi waliofika katika shughuli hiyo.
Sehemu ya ujenzi wa Chuo cha ufundi cha Gonja Mheza.