KINANA AMALIZA ZIARA YAKE SAME MAGHARIBI, KESHO KUENDELEA SAME MASHARIKI

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE SAME MAGHARIBI, KESHO KUENDELEA SAME MASHARIKI

March 26, 2015

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mbunge wa jimbo la Same Magharibi mkoani Kilimanjaro Mh. David Mathayo David wakishiriki katika ujenzi wa madarasa ya shule ya sekondari ya Njoro wilayani Same, wakati Katibu Mkuu huyo alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-SAME) 2 
Mbunge wa jimbo la Same Magharibi Mh. David Mathayo David akipanda mti wa kumbukumbu katika shule ya sekondari ya Njoro wilayani Same.
3 
Wananchi wakinyanyua mikono yao juu huku wakimsalimia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipowasili katika kijiji cha Suji. 7 
Wana CCM wakiimba nyinbo za kumpokea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani pamoja na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha kabla ya kuahirishwa kwa mkutano huo mjini Same.

RAIS KIKWETE ATEUA WABUNGE WAWILI WAPYA

March 26, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili (2) wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba.
Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10.

Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba.
Wabunge ambao wameshateuliwa ni:
- Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa
- Mhe. Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo
- Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro
- Mhe. Janet Zebedayo Mbene
- Mhe. Saada Salum Mkuya
- Mhe. Zakhia Hamdani Meghji
- Mhe. Shamsi Vuai Nahodha
- Mhe. James Fransis Mbatia
Uteuzi huu umeanza tarehe 20 Machi, 2015.
NDEGE YA UJERUMANI: ZOEZI LA UTAFUTAJI MIILI LAENDELEA, KINASA SAUTI CHAPATIKANA KIKIWA KIMEHARIBIKA

NDEGE YA UJERUMANI: ZOEZI LA UTAFUTAJI MIILI LAENDELEA, KINASA SAUTI CHAPATIKANA KIKIWA KIMEHARIBIKA

March 26, 2015
Baadhi ya mabaki ya ndege ya Ujerumani aina ya Airbus A320 baada ya ajali.
Helkopta ikielekea eneo la tukio kuendelea na uchunguzi.
Kinasa sauti cha ndege hiyo kilichopatikana kikiwa kimeharibika.
ZOEZI la utafutaji miili ya watu 150 waliopoteza maisha katika ajali ya ndege ya Ujerumani aina ya Airbus A320 yenye namba za usafiri 4U 9525 iliyoanguka jana katika Milima ya Alps, Ufaransa limeendelea leo huku kifaa cha kunasia sauti kikipatikana huku kikiwa kimeharibika.
Vikosi vya uokoaji vikiwa eneo la tukio.
Waziri wa maswala ya ndani nchini Ufaransa, Bernard Cazeneuve, amesema kuwa kifaa hicho cha kunasa sauti kwenye ndege kilipatikana jana Jumanne baada ya kuanguka kwa ndege hiyo iliyokuwa ikielekea Ujerumani ikitokea Hispania.
Mabaki ya ndege hiyo yaliyokutwa eneo la ajali.Mbali na kuharibika, Waziri Cazeneuve amesema kuwa kifaa hicho bado kitatoa taarifa kwa wataalam wanaojaribu kubaini kilichosababisha kuanguka kwa ndege hiyo, ambayo iliwauwa abiria na wahudumu waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Helikopta zimeonekana zikipaa katika eneo la tukio huku maofisa wa polisi wakiendelea kuchunguza mabaki ya ndege hiyo.
Sehemu ya kinasa sauti cha ndege hiyo.Maofisa wakuu wanaonya kuwa kupata mabaki ya miili ya abiria itachukua muda mrefu kutokana na hali mbaya ya anga katika eneo hilo.
Kansela wa Ujerumani pamoja na Rais wa Hispania na waziri wake mkuu, wanatarajiwa kuzuru eneo la ajali hiyo leo Jumatano.

Rais Kagame ahudhuria mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati jijini Dar es salaam leo

March 26, 2015

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Paul Kagame wa Rwanda kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na wageni wake Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Pierre Nkurunzinza kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakiwa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda katika picha ya pamoja na mawaziri wa Tanzania, kenya, DRC na Uganda kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakisiliza maelezo toka kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Rished Bade walipotembelea kituo cha kulipia ushuru wa aina zote chini ya paa moja katika bandari ya Dar es salaam leo Machi 26, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakisiliza maelezo toka kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Rished Bade walipotembelea kituo cha kulipia ushuru wa aina zote chini ya paa moja katika bandari ya Dar es salaam leo Machi 26, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakiteta jambo walipotembelea bandari ya Dar es salaam leo Machi 26, 2015.
Rais Paul Kagame wa Rwanda akipeperusha bendera kuashiria kuzinduliwa kwa safari za treni za mizigo kuelekea Rwanda katika stesheni ya reli ya Dar es salaam akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho kikwete leo Machi 26, 2015.PICHA NA IKULU

Kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni

March 26, 2015
Habari, nimeandika kitabu changu kinachoelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na changamoto na namna ya kuzitatua za wilaya ya Handeni, mkoani Tanga. Naomba unisaidie ndugu mwanahabari ili kuhabarisha umma. Nakushukuru sana, tena sana kwa sapoti yako. By Kambi Mbwana
Picha juu na chini ni mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Bingwa, Dimba na Mtanzania kutoka Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Sharifa Mmasi pichani akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichoandikwa na Kambi Mbwana, ambaye ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu linalofanyika kila mwisho wa mwaka wilayani Handeni, mkoani Tanga. Picha na Mpigapicha wetu.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWANDISHI wa Habari za Michezo ambaye pia ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Utamaduni la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, ameandika kitabu chake kinachojulikana kama ‘Dira na Tumaini Jipya Handeni’, kilichoanza kupatikana mapema wiki hii jijini Dar es Salaam na wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Kitabu hicho kimeelezea kero na changamoto mbalimbali za wananchi wa Handeni, kama vile shida ya maji, elimu na migogoro ya ardhi kwa ajili ya kushirikisha mawazo ya viongozi wa serikali, wadau na wananchi ili kukabiliana na tatizo hilo wilayani humo na mikoa ya jirani ambapo changamoto hizo zinashabihiana kwa kiasi kikubwa.
Sharifa Mmasi akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni, kilichoandikwa na Kambi Mbwana.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mbwana alisema kwamba kuandika kitabu hicho kuna lengo kubwa la kuelimisha jamii kwa ajili ya kutafuta fursa ya kimaendeleo katika wakati huu ambao wananchi wengi wamekuwa wakilia bila kupata msaada wowote.

“Naijua vizuri wilaya yangu ya Handeni na mkoa wa Tanga kwa ujumla, hivyo nimeamua nitumie kipaji change katika kuandika kitabu hiki ambacho kimeweza kuanika mambo mengi yenye tija kwa serikali na wananchi kwa ujumla, hivyo naomba waniunge mkono kwa kuhakikisha kwamba wanapata kitabu hiki popote kitakapokuwapo.

Kinapatikana kwa bei ndogo mno ya Sh 3500 kwa kuwa sikuwa na lengo la kutajirika kwa kupitia kitabu hiki bali kutoa mawazo yangu na kuelimisha jamii yangu inayonizunguuka, hivyo ni wakatai wa Watanzania wote, bila kusahau wakazi na wananchi wa Handeni kupata nafasi ya kusoma mawazo yangu kwa ajili ya kutafuta namna ya kufika mbali kiuchumi na kiutamaduni, ukizingatia kuwa kitabu kimegusia mambo kadhaa ambayo ni muhimu,” alisema Mbwana.

Kwa mujibu wa Mbwana, maeneo yanapopatikana kitabu hicho kwa jijini Dar es Salaam ni pamoja na ambapo ni Kinondoni Kwa Manyanya, kwenye kituo cha basi kwa muuza magazeti aliyekuwa pembeni ya ghorofa la Mwaulanga, Sinza Kijiweni kwenye studio inayoangaliana na lango la New Habari 2006 Ltd, upande wa wanaokwenda mjini, huku studio hiyo ikiwa karibu na duka la vifaa vya ujenzi. Maeneo mengine ni muuza magazeti wa Kimara Mwisho kwenye kituo cha basi cha wanaokwenda mjini, huku Buguruni kikipatikana katika studio ya upigaji wa picha karibu na Hoteli ya New Popex, Buguruni, jijini Dar es Salaam.

Aidha Mbwana alisema kwa wanaotaka kuwasiliana naye juu ya kitabu hicho cha Dira na Tumaini Jipya Handeni wanaweza kumpata kwa +255 712053949 au barua pepe; kambimbwana@yahoo.com.

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda AKUTANA NA UONGOZI WA KAMPUNI YA CHINA MERCHANT GROUP

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda AKUTANA NA UONGOZI WA KAMPUNI YA CHINA MERCHANT GROUP

March 26, 2015

2
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimwonyesha Mwenyekiti wa Kampuni ya China Merchants, Group, Bw. Li Xiaopeng jarida linaloonyesha fursa za uwekezaji nchi lililotolewa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Wazri Mkuu jijini Dar es salaam Machi  2015. Kampuni hiyo Inatarajiwa kuanza ujenzi wa bandari ya Bagamoyo hivi karibuni.
3
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana   na Mwenyekiti wa Kampuni ya China Merchant Group, Bw. Li Xiaopeng (kulia)  na balozi wa China nchini, Lu Youqing baada ya mazungumzo yake na uongozi wa kampuni hiyo  Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dare s salam Machi 26, 2015 . Kampuni hiyo inatarajiwa kuanza ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo hivi karibuni.
4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na  Mwenyekiti wa Kampuni ya China Merchants, Group, Bw. Li Xiaopeng , Ofisini kwa Wazri Mkuu jijini Dar es salaam Machi 26,  2015. Kampuni hiyo Inatarajiwa kuanza ujenzi wa bandari ya Bagamoyo hivi karibuni.
5
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akiwa katika picha ya pamoja    na Mwenyekiti wa Kampuni ya China Merchant Group, Bw. Li Xiaopeng (kulia kwake ) pamoja na ujumbe wake  na balozi wa China nchini, Lu Youqing (kushoto kwake ,baada ya mazungumzo yake na uongozi wa kampuni hiyo  Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dare s salam Machi 26, 2015 . Kampuni hiyo inatarajiwa kuanza ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo hivi karibuni.
6
Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda akizungungumza na Mwenyekiti wa Kampuni ya China Merchant Group, Bw. Li Xiaopeng (watatu kushoto ) pamoja na ujumbe wake  na balozi wa China nchini, Lu Youqing ( kushoto kwake) ,baada ya mazungumzo yake na uongozi wa kampuni hiyo  Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dare s salam Machi 26, 2015 . Kampuni hiyo inatarajiwa kuanza ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo hivi karibuni.
1
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Rais wa Burundi Pierr Nkurunzinza katika chakula cha jioni kilichoandaliwa na Rais jakaya Kikwete , Ikulu jiji Dar es salaam Machi 25, 2015 kwa viongozi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
(picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
DK,SHEIN ATEMBELEA UJENZI WA BARABARA MATEMWE MKOA WA KASKAZINI UNGUJA

DK,SHEIN ATEMBELEA UJENZI WA BARABARA MATEMWE MKOA WA KASKAZINI UNGUJA

March 26, 2015

1
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiangalia ramani ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja inayojengwa na Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd ambayo inasimamia mradi wa (Amber Golf&Beach Resort) wakati alipotembelea ujenzi wa barabara leo (wa tatu kushoto) Mkurugenzi na Mmiliki wa Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd Bw.Brian Thomson na (wapili kulia) Bi Naila Jidawi msemaji Mkuu wa Kampuni hiyo,
[Picha na Ikulu.]
2
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji wakati alipofika kutembelea maendeleo  ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja leo inayojengwa na Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd,
3
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Bi Naila Jidawi msemaji Mkuu wa Kampuni Pennyroyal Gibraltar Ltd ya Mradi wa (Amber Golf&Beach Resort) wakati alipotembelea maendeleo  ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja leo inayojengwa na Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd,
4
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Wananchi wakati alipotembelea maendeleo  ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja leo  inayojengwa na Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd,
5
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kutoka kwa  Mkurugenzi na Mmiliki wa Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd Bw.Brian Thomson leo alipokuwa akiangalia ramani ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja inayojengwa na Kampuni hiyo ambayo inasimamia mradi wa (Amber Golf&Beach Resort),
6
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa  Mkurugenzi na Mmiliki wa Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd Bw.Brian Thomson alipokuwa akiangalia ramani ya ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja  leo inayojengwa na Kampuni hiyo ambayo inasimamia mradi wa  Amber Golf&Beach Resort  (kulia) Bi Naila Jidawi msemaji Mkuu wa Kampuni Pennyroyal Gibraltar Ltd (wa pili kushoto) Katibu Mkuu wa Wizara ya  Miundombinu na Mawasiliano Dk.Juma Malik Akili.
7
Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein   akizungumza na Wananchi wakati alipotembelea ujenzi wa Barabara za Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja inayojengwa na Kampuni  ya Pennyroyal Gibraltar Ltd, ambayo inasimamia mradi wa  Amber Golf&Beach Resort.
8
Katapila ya Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar Ltd likifanya kazi ya kutawanya mlima wa mawe wakati wa ujenzi wa Barabara ya Kiashange -Kijini-Mbuyutende na Matemwe-Muyuni Mkoa wa Kaskazini Unguja inayojengwa na Kampuni hiyo ambayo inasimamia mradi wa  Amber Golf&Beach Resort Mkoani humo wakati Rais  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipofanya ziara fupi kutembelea barabara hiyo leo.