KIKOSI CHA LIPULI FC YA IRINGA KILICHOCHEZA NA AFRICAN SPORTS LEO LIGI DARAJA LA KWANZA |
KIKOSI CHA AFRICAN SPORTS KILICHOLAZIMISHWA SARE NA LIPULI FC YA IRINGA LEO MKWAWANI. |
HAPA WACHEZAJI WAKISALIMIANA KABLA YA KUANZA MECHI HIYO |
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
TIMU za soka African Sports na Lipuli FC ya Iringa leo zimeshindwa kutambiana baada ya kulazimishana sare ya kufungana bao 1-1 ikiwa ni muendelezo wa Michuano ya Ligi daraja la kwanza ngazi ya Taifa mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani.
katika mechi hiyo ambayo ilikuwa ya ushindani mkubwa kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu ,African Sports ndio ilikuwa ya kwanza kuweza kupata bao lake dakika ya 44 Ally Ramadhani kwa njia ya Penati iliyotokana na shambuliaji wao Hassani Materema kuangushwa eneno la Hatari.
Baada ya tukio hilo mwamuzi wa mechi hiyo Klina Kabala kutoka Dar es Salaam kuamuru ipigwe peneti iliyopigwa kuifundi na mshambuliaji huyo na kuzama wavuni.
Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa kila timu.
Wakionekana kujipanga na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye kipindi cha kwanza,Lipuli FC waliweza kufanya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa African Sports na kufanikiwa kuandika bao la kusawadhisha kwenye dakika ya 54 kupitia Abdallh Mussa.
Katika mechi nyengine iliyochezwe kwenye dimba la soka Mafinga timu za Kurugenzi FC na Polisi Dar zimegawana pointi moja moja baada ya kulazimishana sare ya kutokufungana.
Katika mechi nyengine iliyochezwe kwenye dimba la soka Mafinga timu za Kurugenzi FC na Polisi Dar zimegawana pointi moja moja baada ya kulazimishana sare ya kutokufungana.