Watanzania watakiwa kutumia mobile banking kukuza uchumi wao

Watanzania watakiwa kutumia mobile banking kukuza uchumi wao

April 13, 2016

DSC_0093
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Kutokana na kukua kwa huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking), Watanzania wametakiwa kutumia nafasi hiyo vizuri ili iweze kuwasaidia kukuza uchumi wao.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa siku mbili unaozungumzia maendeleo ya sekta za fedha kwa kutumia mifumo ya huduma za kibenki kwa kutumia mitandao ya simu (Africa Digital Banking Summit), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji amesema ni muda muafaka kwa Watanzania kutumia huduma hizo kwa ajili ya kujiongezea kipato.
Alisema kupitia huduma hizo, Watanzania wanaweza kutuma nakupokea pesa kutoka maeneo mbalimbali hata ambayo yapo mbali na matawi ya benki hivyo wanaweza kufanya shughuli mbalimbali ikiwepo kufanya biashara kwa kutumia huduma hizo.
“Serikali imeunganisha nchi nzima na mkongo wa taifa na hii inawapa fursa watanzania kutuma pesa sehemu yoyote hivyo niwasihi watanzania kutumia kikamilifu nafasi hiyo ili kuboresha uchumi wao,” amesema Dkt. Kijaji.
DSC_0032
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji akitoa hotuba katika mkutano huo. (Picha zote na Rabi Hume, Modewjiblog)
Nae Mkurugenzi Mkuu wa NMB nchini, Ineke Bussemaker amesema kuwepo kwa huduma za kibenki kupitia mitandao ya simu kumewezesha wateja wao kupata huduma kirahisi tofauti na miaka ya nyuma kabla ya kuanza kwa huduma ya mobile banking.
Alisema kupitia huduma hiyo kwa sasa wateja wao wanauwezo wa kutoa fedha, kulipia huduma mbalimbali kama kodi, kununua umeme, tiketi za ndege na hata kuangalia salio lililo katika akaunti zao za benki na wanachokifanya kwa sasa ni kuangalia jinsi gani wanaboresha zaidi huduma hizo kwa wateja hasa walio maeneo ya vijijini.
“Miaka ya nyuma kama mteja yupo kijijini anatumia muda mwingi kwenda sehemu iliyo na huduma ya benki lakini kwa sasa huduma za kibenki katika mitandao ya simu imerahisisha hata wateja wetu walio vijijini kupata huduma zetu kiurahisi,” amesema Bi. Bussemaker.
DSC_0061
Mkurugenzi Mkuu wa NMB nchini, Ineke Bussemaker akizungumza katika mkutano huo.
Nae Meneja wa Mifumo wa Malipo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Dadi amesema huduma za kibenki kwa kutumia mitandao ya simu imekuwa ikizidi kukua siku baada ya siku tangu ilipoanza nchini mwaka 2008 na mpaka sasa kuna benki 30 ambazo zimejiunga katika mfumo huo ili kuwasogezea huduma wateja wake.
DSC_0043
Meneja Mifumo ya Malipo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Dadi akitoa taarifa kuhusu matumizi ya mobile banking nchini.
DSC_0015
Mwongozaji wa mkutano huo, Chris Mauki.
DSC_0026
Mwenyekiti wa mkutano wa Africa Digital Banking Summit, Baraka Mtavangu akizungumza kuhusu mkutano huo.
DSC_0029
Baadhi ya washiriki walioshiriki mkutano huo unaofanyika kwa siku mbili.
DSC_0051
Pia Mkurugenzi Mkakati wa Jackson Group Ltd, Kelvin Twissa ni mmoja wa washirikia waliohudhuria mkutano huo (wa kwanza kulia).
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA KATI YA TANZANIA NA OMAN

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA KATI YA TANZANIA NA OMAN

April 13, 2016

2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Kongamano la Uwekazaji kwa Wafanyabiashara baina ya Tanzania na Oman kuhusu kuangalia fursa za uwekezaji katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi kati ya Nchi mbili hizo, Kongamano hilo limefunguliwa leo April 13,2016 katika Hoteli ya Hyatt Regence Dar es salaam.
3 4 
Washiriki wa Kongamano la Uwekezaji kiuchumi kati ya Tanzania na Oman wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokua akifungua Kongamano hilo kuhusu kuangalia fursa za uwekezaji katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi baina ya Nchi mbili hizo, Kongamano hilo limefunguliwa leo April 13,2016 katika Hoteli ya Hyatt Regence Dar es salaam.
5 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Uwekazaji kwa Wafanyabiashara baina ya Tanzania na Oman kuhusu kuangalia fursa za uwekezaji katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi kati ya Nchi mbili hizo  baada ya kufungua Kongamano hilo leo April 13,2016 katika Hoteli ya Hyatt Regence Dar es salaam.Picha na OMR

WAGOMBEA NASAFI YA KATIBU MKUU UMOJA WA MATAIFA WAANZA KUHOJIWA

April 13, 2016


  Mgombea wa Nafasi ya  Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa, Bw. Igor Luksic ( Montenegro), akimwaga sera zake mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  wakati wa majadiliano/mhadalo  usio rasmi ulioandaliwa na  Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa lengo  kutoa fursa kwa wanaowania nafasi ya  Katibu mkuu kueleza sera zao na kisha kuulizwa maswali  
 Bi. Irina Bokova ( Burgalia) mmoja wa wanawake wanne waliojitokeza hadi sasa  kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naye akijieleza mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 
Bw. Antonio Guterres ( Portugal) mmoja wa wagombea waliohojiwa  katika siku ya kwanza ya mdahalo  usio rasmi wa kuwasikiliza wagombea waliojitokeza kuwaania nafasi itakayoachwa wazi na Ban Ki Moon, mwishoni mwa mwaka  huu. jumla ya wagombe tisa wamekwisha jitokeza mpaka jana ( jumanne).
  Taswira ya  Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa,  katika siku ya kwanza ya mdahalo wa kihistoria ya wagombea  nafasi ya  Ukatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mdahalo/majadiliano ya kwanza ya aina yake kufanyika katika   nafasi ya kumtafuta Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa .
Na Mwandishi Maalum, New York
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  jana ( Jumanne) limeandika historia kwa mara nyingine, kwa kuanza   mchakato usio  rasmi wa  kuwasikiliza na kuwauliza maswali  wagombea  watarajiwa waliojitokeza kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Mchakato huo ulianza kwa kuwasikiliza wagombea watatu kati ya tisa wakiwamo wanawake wake wanne  ambao hadi siku ya jumanne walikuwa wametangazwa rasmi kuwania nafasi hiyo itakayo achwa wazi na Katibu Mkuu wa  sasa   Ban Ki Moon anayemaliza muda  wake mwishoni mwa mwaka huu.
Katika awamu ya hiyo ya kwanza, kila  mgombea mtarajiwa  alipewa fursa ya kujieleza na kuelezea visheni yake,  sera, mipango, vipaumbele vyake  na nini anatarajia kukifanya  endapo  atachaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa  Mataifa  , Umoja  wenye wanachama 193.
Walioshiriki mdahalo huo katika siku ya kwanza  walikuwa ni  Dr. Igor Luksic ( Motenegro), Bi. Irina Bokova ( Bulgaria) na  Bw. Antonio Guterres ( Portugal)
Wengine ambao wamejitokea kuwania nafasi hiyo ni  Dr. Damilo Turk ( Slovenia) Prof.Dr. Vesna Pusic ( Crotia), Bi. Natalia Gherman ( Moldova), Dr. Srgian Kerim ( Macedonia),  Bi. Helen Clark ( New Zeland) na   Bw. Vuk Jeremic ( Serbia)
Ulikuwa ni mdahalo wa aina yake wa kwanza kutokea tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa miaka karibu  70  iliyopita, mdahalo  ulioendedeshwa katika  mazingira ya uwazi, na ambao kwayo umebadilisha kabisa utaratibu wa kumpata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
 Mdahalo huo ambao  umeratibiwa na kusimamiwa na  Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa Bw. Monges Lykketoft, umetokana na makubaliano ya  pamoja kati ya  Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, na Rais wa Baraza la Usalama wakati huo ( mwezi  desemba) Mwakilishi wa Kudumu wa Marekani. Na pia azimio  namba 69/321 la Baraza  Kuu la  Umoja wa Mataifa.
Katika  barua yao kwa wawakilishi wa kudumu wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa,  Bw.  Lykketoft na Balozi Samantha Power ( USA) walieleza juu ya kuwapo kwa  majadiliano au mdahalo wa wazi  na usio  rasmi  lakini muhimu   ambapo    makundi yote  yanayowakilisha nchi wanachama wa UN  yatapata fursa  ya kuwauliza maswali wagombea, maswali ambayo yamejielekeza  zaidi kwa maslahi ya makundi hayo, vipa umbele vyao na namna wanavyouona  Umoja wa Mataifa katika sura yake ya sasa.
Kama ilivyoelezwa hapo awali, hii ni mara ya kwanza kwa historia ya  Umoja wa Mataifa,   kwanza, kutoa fursa kwa wagombea wengi kujitokeza kuwania nafasi hiyo na kupewa nafasi ya kujieleza,  pili  nchi wanachama  wa Umoja wa Mataifa kupewa fursa ya kuwafahamu, kuwasikiliza na kisha kuwauliza na  maswali, na tatu  Asasi zisizo za kiserikali nazo kushirikishwa  katika mchakao huu. 
Vile vile ni historia ya   aina yake ambapo   kipaumbele kimetolewa kwa wagombea wanawake nao kujitokeza kuwania  nafasi hiyo ya juu kabisa katika Umoja wa Mataifa. Kwa takribani  mwaka mmoja sasa kumekuwapo  na kundi maalum ambalo lenye limejipambanua kama  marafiki wa mgombea mwanamke 
Mfumo wa uulizwaji wa maswali kwa wagombea hao ulikuwa ni ule  ambao Wenyeviti wa Makundi ya  Nchi wa wanachama wa Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa Nne  (April ) ndio waliouliza maswali kwa  niaba ya makundi hayo. Aidha  hata  zile nchi ambazo  ni za visiwa au ambazo kwa lugha nyepezi  zimezungukwa na  mataifa  mengine (  land Locked countries) nazo zilipata  fursa ya kuuliza maswali yenye maslahi kwa  nchi zao.Kwa mfano  maswali ya  nchi za Afrika yaliulizwa na  Mwakilishi wa  Kudumu wa Uganda ambaye ni   Mwenyekiti wa Kundi la Nchi za Afrika kwa mwezi huu wa Nne.
Maswali  mengi waliyoulizwa wagombea,  yamejikita katika maeneo  mtambuka  kama vile  haki za binadamu,   operesheni za ulinzi wa Amani na utafutaji  suluhu  na  ufumbuzi wa migogoro, unyanyasaji wa kijisia unaofanywa na walinda Amani,   kuimbuka kwa  tatizo la ugaidi,  tatizo la wakimbizi, utekelezaji wa  malengo ya  maendeleo endelevu ( Agenda 2030), nafasi za  uteuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijiografia na kikanda  katika ngazi za juu  za watendaji  katika sekretarieti ya Umoja wa Mataifa.
Maswali mengine yalihusu umalizwaji wa ukoloni,  utegemezi kwa wafadhili wachache katika uendeshaji wa Umoja wa Mataifa,  marekebisho ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yakiwamo kuongezwa kwa idadi ya  wajumbe wa kudumu wa baraza hilo,  weledi na sifa za uongozi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  na nini kifanyike ili kuufanya  Umoja wa Mataifa  kutekeleza  majukumu  yake ipasavyo kwa kuzingatia   mazingira   na hali  ya sasa na hususani kile kinachoelezwa kupoteza  mweleko wa  chombo  hicho  kikiuu cha kimataifa. 
Utaratibu uliozoeleka wa uchaguzi au uteuzi wa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  ulibebwa zaidi na matakwa ya  Baraza  la Usalama na hasa kundi la   P5 ambao ni wajumbe wa kudumu wa Baraza hilo katika kupitisha  jina la waliyemtaka kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Baada ya Baraza   la Usalama, kupitisha jina la mteule waliyemtaka  jina hilo baadaye lilipelekwa  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambalo lilipitisha na halikuwa na uwezo wa kulikataa kwa kuwa limeshapitishwa na  Baraza la Usalama.
Utaratibu huu  umekuwa ukilalamikiwa na  Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa lenye wajumbe  193 kwamba  lilikuwa likitumikia kutia muhuli jina  ambalo limependekewa na wajumbe wachache ( Baraza la Usalama lenye wajumbe  15 wakiwamo watano wa kudumu).

Ni kwa sababu hiyo safari hii  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeamua kuchukua hatamu  na baada ya majadiliano ya kina baina ya nchi wanachama kuhakikisha kwamba  Baraza  hilo linakuwa na kauli au fursa    katika uteuzi wa Katibu Mkuu  badala ya kuwa watiaji  muhuri ( rubber stamp).
Leo  (jumatano) itakuwa ni zamu ya  Dr. Danilo Turk,   Prof.Dr. Vesna Pusic na Bi. Natalia Gherman.

METTE-MARIT AITAKA JAMII KUWA NA MTAZAMO TOFAUTI KWA WATU WANAOISHI NA UKIMWI

April 13, 2016
DSC_0016
Balozi wa Kimataifa wa UNAIDS, Mette-Marit akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kazi anazofanya kama balozi wa UNAIDS kwa kipindi cha miaka 10 tangu aanze kazi hiyo. (Picha na Rabi Hume wa Modewjiblog)
Katika kuhakikisha watu wanaoishi na UKIMWI wanaishi kwa furaha bila kunyanyapaliwa na watu wanaowazunguka, jamii imetakiwa kuwa na mtazamo tofauti kwa watu wanaoishi na ugonjwa huo.
Hayo yalisemwa na mke wa mtoto wa mfalme wa Norway, Mette-Marit ambaye pia ni balozi kimataifa wa Shirika la Umoja la kupambana na HIV na UKIMWI (UNAIDS) wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kazi anazozifanya kwa UNAIDS kama balozi ambaye anazunguka maeneo mbalimbali duniani ili kuelimisha jamii kuhusu UKIMWI.
Mette-Marrit alisema kuwa watu wenye UKIMWI ni kama watu wengine hivyo wana haki ya kupata huduma bila kunyanyapaliwa ili waweze kuishi kwa uhuru kama watu wengine na ili kufanikisha hilo ni wajibu wa kila mtu kuwasaidia waathirika.
“Watu kuwa na UKIMWI sio mwisho wa maisha inatakiwa kwanza jami kuwa na mtazamo tofauti na inatakiwa kila mtu kusaidia mapambano ya UKIMWI sio jambo la mtu mmoja mmoja,” alisema Mette-Marit.
DSC_0021
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho akizungumzia kuhusu juhudi zinazofanywa na serikali katika mapambano ya UKIMWI.
Nae Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho alisema Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ili kupambana na UKIMWI lakini pia ili kufanikisha mapambano hayo wanahitaji kushirikiana na taasisi ambazo zitawasaidia katika mapambano hayo.
Lakini pia Dkt. Mrisho amezitaka serikali za mitaa kuacha kusubiri mpaka serikali imepeleke pesa ndiyo wawasaidie watu wanaoishi na UKIMWI na hivyo waweke utaratibu wa kutumia sehemu ya mapato yao ili kusaidia mapambano hayo.
“Serikali haijalala katika mapambano tunahitaji kushirikiana na taasisi ambazo zinatusaidia kupunguza maambukizi mapya na tunaona Mette-Marit amekuwa akifanya jambo zuri anazunguka sehemu nyingi ili kusaidia kupunguza maamukizi mapya ya UKIMWI,” alisema Dkt. Mrisho.
DSC_0009
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na Ukimwi, UNAIDS nchini Tanzania, Warren Naamara akizungumzia ugonjwa wa UKIMWI.

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA KUMBUKUMBU YA MIAKA 32 YA KIFO CHA SOKOINE

April 13, 2016
 Rais Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa akimaliza kuweka saini katika kitabu cha Kumbukumbu ya miaka 32 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya Ibada maalumu ya Kumbukumbu ya kifo hicho katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda alipowasili kuhudhuria Ibada maalumu ya Kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine  katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Katibu Mkuu wa TEC Fr. Raymond Saba  alipowasili kuhudhuria Ibada maalumu ya Kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine  katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na mtoto Balozi Joseph Moringe Sokoine  alipowasili kuhudhuria Ibada maalumu ya Kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine  katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Wajane na binti wa   aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine  wakiwa katika Ibada Maalumu ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya kifo chake katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Ibada Maalumu ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya kifo chake katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Rais Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa wakishiriki katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Sehemu ya waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
  Sehemu ya waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
  Viongozoi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Viongozoi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Balozi Joseph Sokoine na viongozoi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Sehemu ya watu waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Sehemu ya watu waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Sehemu ya kinamama na watoto wao waliohudhuria katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
   Wanakwaya katika Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Rais Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa akiongea  machache wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
  Msemaaji wa familia akiongea  wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea  machache wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Balozi Joseph Sokoine na wageni wengine wakisiliza hotuba  wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Wageni wakisikiliza hotuba mbalimbali  wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Wageni wakisikiliza hotuba mbalimbali  wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Wageni wakisikiliza hotuba mbalimbali  wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na mkewe na wageni wengine wakifuatilia yaliyojiri 
Wageni wakisikilizawakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Katibu Mkuu wa TEC Fr. Raymond Saba  akiongea wakati wa  Ibada maalumu ya Kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine  katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akiongea wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Rais Mstafu Mzee Benjamin William Mkapa wakifurahia jambo wakati wa hotuba ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo na Katibu Mkuu wa TEC Fr. Raymond Saba wakiwapa mikono familia ya Marehemu wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwapa mikono familia ya Marehemu wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwapa mikono wajane wa  Marehemu wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Rais Mstafu Mzee Benjamin William Mkapa  wakiwapa mikono wajane wa  Marehemu wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisi dikizwa na Balozi Joseph Moringe Sokoine baada ya Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam Jumanne April 12, 2016.
PICHA NA IKULU