JIJI LA TANGA LAZIZIMA KWA MSIMU WA TIGO FIESTA 2017 USIKU WA IJUMAA HII

October 28, 2017
Msanii Aslay akitumbuiza mashabiki waliofurika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga kwenye Tamasha kubwa la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jumamosi.

TASNIA HALISI WHATSAAP GROUP YAZINDULIWA KWA KISHINDO JIJINI DAR ES SALAAM

October 28, 2017

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAANDISHI wa habari ambao ni wanachama wa kundi la Whatsaap lijulikanalo kama TASNIA HALISI wamezindua kundi hilo leo Oktoba 28, 2017 kwa sherehe kabambe ya kukata na shoka iliyohanikizwa na nyama choma, vinywaji vya kila aina na muziki.
Mratibu wa shughuli hiyo, Bi. Angela Msangi amesema, kundi hilo ni mukusanyiko wa wanataaluma na wadau wa habari na linalenga kuwaleta pamoja wana tasnia kwa nia ya kubadilishana taarifa na kusaidiana kitaaluma na kijamii.
Katika uzinduzi huo uliosindikizwa na burudani ya muziki umeshuhudia waandishi kutoka sehemu mbalimbali nchini wakishiriki.
Katika sherehe hiyo, shampeni mbili zilifunguliwa ikiwa ni pamoja na kukata keki.







Tigo yachangia katika ukuaji wa teknolojia na huduma za kifedha kwa njia ya mtandao nchini

October 28, 2017
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Simon Karikari (Kulia) akichangia mada wakati wa mkutano wa kutangaza matokeo yamakampuni 100 yanayoibukia katika uwekezaji nchini, ambapo zawadi kwa washindi zilitolewa mwishoni wa wiki hii  jijini Dar es Salaam, kushoto ni mkurugenzi wa 361 Degrees Mustafa Hassanali.
washiriki wa  mkutano wa kutangaza matokeo yamakampuni 100 yanayoibukia katika uwekezaji nchini wakifurahia jambo , ambapo zawadi kwa washindi zilitolewa mwishoni wa wiki hii  jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Simon Karikari (Kulia) akichangia mada wakati wa mkutano wa kutangaza matokeo yamakampuni 100 yanayoibukia katika uwekezaji nchini, ambapo zawadi kwa washindi zilitolewa mwishoni wa wiki hii  jijini Dar es Salaam, kushoto ni mkurugenzi wa 361 Degrees Mustafa Hassanali.

Mafunzo kwa wafanyakazi wa nyumbani, waajiri pamoja na watendaji Jijini Mwanza

October 28, 2017
Binagi Media Group
Utafiti uliofanywa na Shirika la hutetea haki za watoto wafanyakazi wanyumbani WOTESAWA Jijini Mwanza, unaonyesha kwamba watoto hao bado wanakumbana na aina mbalimbali za ukatili ikiwemo utumikishwaji.

Utafiti huo uliofanyika mwaka jana ulibaini kwamba asilimia 91.9 ya watoto wafanyakazi wa nyumbani katika Kata nne za Jiji hilo hawana mikataba ama makubaliano baina ya wazazi na waajiri wao, asilimia 5.4 wana mikataba huku asilimia 80 ikionyesha wapo wanaofanya kazi bila malipo huku wanaolipwa mshahara chini ya shilingi 20,000 wakiwa ni asilimia 20.

Utafiti huo ulifanyika katika Kata za Igogo ambapo watoto wafanyakazi wa nyumbani 43 walifikiwa, Mkuyuni 42, Nyamagana 32 pamoja na Butimba 37 na hivyo kufanya idadi ya watoto wafanyakazi wa nyumbani waliofikiwa kuwa 154, wavula wakiwa ni 16 na wasichana 138.


Hali hii inaongeza chachu kwa shirika la WOTESAWA kuwajengea uwezo watoto wafanyakazi wa nyumbani, waajiri wao pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani, Watendaji, Wenyeviti wa Mitaa, Maafisa Ustawi wa Jamii, pamoja na maofisa wa dawati la jinsia kutoka jeshi la polisi kama anavyoeleza Mkurugenzi wa shirika hilo, Angel Benedicto.
Washiriki wa semina hiyo wakimsikiliza Mkurugenzi wa WOTESAWA, Angel Benedicto
Mkurugenzi wa WOTESAWA, Angel Benedicto akizungumza kwenye semina hiyo
Washiriki wa semina hiyo wakimsikiliza Mratibu wa Shirika la WOTESAWA
Mratibu wa Shirika la WOTESAWA, Elisha Daud akiwasilisha mada kwenye semina hiyo
Mratibu wa Shirika la WOTESAWA, Elisha Daud akiwasilisha mada kwenye semina hiyo

MAFUNDI WA TANESCO WAWEKA KAMBI MBEZI KWA MALECELA KUREJESHA MIUNDOMBINU ILIYOSOMBWA NA MAFURIKO YA MVUA ZA VULI

October 28, 2017

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
JUHUDI kubwa zimekuwa zikifanywa na wahandisi na mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), kurejesha miundombinu iliyoathiriwa na mvua za vuli zilizonyesha kwa siku mbili mfululizo jijini Dar es Salaam na hivyo kusababisha maeneo kadhaa ya jiji kukosa umeme.
Eneo la Mbezi chini ni moja ya maeneo yaliyoathirika vibaya ambapo kwa uchache nguzo nne zimesombwa na maji na kupelekea nyaya za kuafirisha umeme kukatika.
Leo Oktoba 28, Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO bi Leila Muhaji, alifanya ziara kutembelea maeneo hayo yaliyoathirika ili kujionea mwenyewe na hivyo kuwa na majibu sahihi kwa wateja abao wamekuwa wakiulizia juu ya tatizo hilo lakukosa umeme.
Akiwa katika eneo la Mbezi chini eneo la daraja la “Kwa Malecela” ambako nguzo hizo zinakatisha kwenye daraja hilo na kukuta mafundi wakienendelea na kazi ya kusimika nguzo na kufunga nyaya.
Kwa mujibu wa Muhandisi Mkuu wa TANESCO Kinondoni Kaskazini Mhandisi Godlove Mathayo, amesema mafundi wanafanya jitihada kusimika nguzo na kushughulikia tranforma mbili moja iliyoko eneo la Victor5ia na nyingine hapo kwa Malecela, na kazi hiyo ikikamilika basi umeme utarejea usiku huu.
:Kuna baadhi ya transoma zimezingirwa na madimbwi ya maji na tunashindwa kuzifikia kwa sasa na pindi maji yatakapopungua kazi ya kuzirekebisha tranforma hizo tutafanya marejkebisho ili umeme uweze kurejea katika hali yake ya kawaida.
“Amesema baada ya matengenezo hayo yanayoendelea sasa, wakazi ambao wanategemea kupata umeme ni wote wa maeneo ya Kwa Malecela, Victoria na Kawe kwa maana ya eneo la Mbezi Chini.” Alisema.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Uhusioano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, amewaomba radhi wateja waloathirika kutokana na hitilafu hiyo na kuwasihi kuwa wavumilivu kwani mafundi wanafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha umeme unarejea katika hali yake ya kawaida.
“Lakini niwaombe tu wananchi watoe taarifa pale wanapoona maeneo yao hayana umeme, watufahamishe ili mafundi wafike kwa haraka na kufanya marekebisho, wanaweza kufanya hivyo kupitia anuani zetu na mitandao ya kijamii ya Shirika.” Alisema.
Miundombinu imeathirika kutokana na mvua hizi za vuli lakini nitoe tahadhari umeme na maji haviendani, wananchi wasisogelee miundombinu ya umeme wanapoona nguzo imelala au waya umelala wasiguse watoe taarifa na mafundi wetu ambao wana vifaa maalum watafika mara moja na kuondoa hatari hiyo. Alifafanua Bi. Leila.

 Winchi ikinyanyua nguzo wakati wa urejeshaji miundombinu ya TANESCO eneo la Kwa Malecela Mbezi chini jijini Dar es Salaam leo Oktoba 28, 2017.
 Fundi wa TANESCO akiwa amebeba vipuri wakati wa zoezi la kurejesha miundombinu ya umeme iliyoathirika na mafuriko ya mvua za vuli enel la Mbezi chini jijini Dar es Salaam Oktoba 28, 2017.
 Mhandisi Mkuu wa TANESCO Kinondoni Kaskazini, Mhandisi Godlove Mathayo, (kulia), akimuoneyesha Kaimu Meneja Uhusiano, TANESCO, Bi Leila Muhaji, jinsi kazi inavyoendelea eneo la Mbezi Kwa Maalecela jijini Dar es Salaam Jumamosi Oktoba 28, 29017.

MBEGU BORA ZA MIGOMBA, VIAZI LISHE NA MIHOGO KUWAKOMBOA WAKULIMA MKOANI KAGERA

October 28, 2017
Kaimu Ofisa Kilimo Wilaya ya Muleba,  Kokushubila Pesha akipanda mbegu ya muhogo katika shamba darasa la kikundi cha Ujamaa  lililopo Kata ya Magata Karutanga wilayani humo. 


Ofisa Mtendaji wa kata ya Magata Karutanga Joyce Rassia akizungumza na wakulima wakati wa uzinduzi wa upandaji wa shamba darasa la kikundi hicho.

Dkt. Kigwangalla atembelea pori tengefu la Loliondo ashuhudia uhalisia wa mgogoro

October 28, 2017
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla mapema jana Oktoba 27,2017 ameweza kutembelea eneo la pori tengefu la Loliondo lililopo Wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha na kujionea mambo mbalimbali juu ya mgogoro wa muda mrefu maarufu Loliondo.
Waziri Dk. Kigwangalla ameweza kutembelea katika eneo hilo katika kushuhudia kiini hicho cha mgogoro uliozidi zaidi ya miaka 20, ambapo anatarajia kurejesha majibu kwa Waziri Mkuu pamoja na Rais mara tu baada ya kumaliza ziara yake hiyo pamoja  na kukutana na watalaam wake wa Wizara.
Waziri Dkt. Kigwangalla  ameweza kuoneshwa eneo lenye mgogoro  baina ya mwekezaji pamoja na wananchi wa jamii ya wafugaji kwenye eneo hilo sambamba na kufuatilia mipaka baina ya maeneo mbalimbali yanayozunguka mipaka ya pori hilo tengefu pamoja na hifadhi ya Serengeti.
Awali Waziri Dk.Kigwangalla akiwa katika mkutano wa wazi kwenye Mji wa Wasso aliweza kusitisha operesheni zilizokuwa zinaendelea katika pori hilo tengefu la Loliondo na huku akiagiza mifugo yote iliyoshikiriwa na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo haijafikishwa mahakamani kuachiwa huru huku ile mingine iliyofunguliwa kesi kuendelea kushikiriwa mpaka shahuri la msingi litakapotatuliwa.
Aidha, Waziri Dkt. Kigwangalla amewataka wananchi hao jamii ya wafugaji katika mgogoro huo kuacha mara moja kuingiza mifugo ndani ya hifadhi licha ya kusitisha Operesheni iliyokuwa ikifanyika na kuwataka wakae meza moja ya majadiriano kupata ufumbuzi.
Akiwa ndani ya pori hilo pia alishuhudia kundi kubwa la wanyama mbalimbali kwenye maeneo hayo ambapo imeelezwa awali hawakuwapo kutokana na kukimbia mifugo iliyokuwa imeingizwa na wafugaji hao.
Waziri wa Maliasili Dkt.Kigwangalla akiwasili eneo la Loliondo kushuhudia kiini cha mgogoro huo
Dkt.Kigwangalla akiwa pamoja na Mbunge wa jimbo hilo la Ngorongoro ambaye pia ni Naibu Waziri wa Elimu Mh.Ole Nasha wakati alipofika kukagua kiini cha mgogoro huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla akitazama wanyama eneo lenye mgogoro ambalo ni pori tengefu la Loliondo ambalo awali lilikuwa limevamiwa pamoja na mifugo ya wananchi.
 
Dkt. Kigwangalla akifuatilia ramani yenye kuonesha eneo la pori tengefu la Loliondo
Baadhi ya wanyama walioonekana wakati Waziri Dkt.Kigwangalla alipotembelea pori hilo ambapo awali wanyama hao walitoweka kutokana na kuingizwa kwamifugo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya  ya Ngorongoro Mh.Rashid Taka (kulia) pamoja na Mhifadhi Mkuu wa Serengeti William Mwakilema  wakati wakikagua maeneo hayo yenye mgogoro huo wa Loliondo.
Dkt.Kigwangalla wakikatisha katika maeneo hayo ya Loliondo wakati akikagua maeneo yenye migogoro.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla akimsikiliza mmoja wa wananchi waliokuwa wakitoa kilio chao kuhusiana na mgogoro huo wa Loliondo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla akizungumza na wananchi jamii ya wafugaji (Hawapo pichaani) wakati alipotembelea  eneo la Loliondo ili kubaini kiini cha mgogoro huo.

NAIBU WAZIRI AWESO AWATAKA WAKAZI WA PANGANI KUWA NA MSHIKAMANO ILI KUPATA MAENDELEO.

October 28, 2017
 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso akiwahutubia wananchi wa wilaya ya Pangani kwenye mkutano wa hadhara uliyofanyika uwanja wa sokoni ambapo alisisitiza umoja na mshikamano kwa wananchi ili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo 
 Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani akizungumza katika mkutano huo
 Mkuu wa wilaya ya Pangani.Zainabu Issa akizungumza katika mkutano huo ambapo alimuomba Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo kuiwekea msukumo barabara ya Tanga-Pangani ili kufungua fursa za kiuchumi kwa wilaya hiyo
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya PanganiSeif Saidi akizungumza katika mkutano huo
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Sabas Chamnbasi akizungumza katika mkutano huo
 Diwani wa Kata ya Pangani Magharibi (CCM) John Semkande akizungumza katika mkutano huo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso akilakiwa na wananchi wa Jimbo la Pangani wakati alipokwenda kuhutubia wananchi wa wilaya ya Pangani kwenye mkutano wa hadhara uliyofanyika uwanja wa sokoni ambapo alisisitiza umoja na mshikamano kwa wananchi ili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso akilakiwa na wananchi wa Jimbo la Pangani wakati alipokwenda kuhutubia wananchi wa wilaya ya Pangani kwenye mkutano wa hadhara uliyofanyika uwanja wa sokoni ambapo alisisitiza umoja na mshikamano kwa wananchi ili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso akiingia eneo la mkutano kushoto ni Katibu wa CCM wilaya ya Pangani
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso akiwapungia mkono wananchi wa Jimbo hilo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso akisalimiana na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano huo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso katikati akifuatilia matukio mbalimbali kwenye mkutano huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani,Zainabu Issa kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani.

 Kikundi cha Burudani kikitoa burudani kwenye mkutano huo wa hadhara.
 Mganga Mkuu wa wilaya ya Pangani,Dkt Juma Mfanga akifuatilia mkutano huo
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mji wa Pangani wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Jumaa Aweso