DKT KARATA AIPONGEZA SERIKALI KWA KUWEKA MPANGO MZURI WA UTOAJI WA DAWA ZA KUPUNGUZA MAKALI KWA WARAIBU WA DAWA ZA KULEVYA

January 14, 2024


Na Mwandishi Wetu,Tanga

DAKTARI wa Afya ya Akili katika kituo cha Methadone (MAT) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Dkt Wallace Karata ameipongeza Serikali kuweka mpango mzuri wa utoaji wa dawa za kupunguza makali kwa waraibu wa dawa za kulevya na matokeo yake yamekuwa mazuri.

Matokeo hayo yameweza kuleta mabadiliko na wapo ambao wamekamilisha matibabu yao wapatao 28 na wanaendelea vizuri katika jamii kutokana ikiwemo kubadilika na kuachana na matumizi.

Dkt Karata aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na mtandao huu ambapo alisema mpango huo wa Serikali kupitia Wizara ya Afya washirikiana na wadau wa Maendeleo umesaidia kuwezesha kupatikana vifaa kazi ambavyo vitawasaidia waweza kujikwamua kiuchumi.

Alisema katika mpango huo watakuwa na mashine za kufyetulia Tofali,Mashine za kuosha Magari (Car wash),Mashine za Salooni,Mashine za Kushonea nguo na watakuwa wanawaandaa vijana na shughuli za uzalishaji mali katika Jiji la Tanga baada ya kupata nafuu.

“Jambo hili ni hatua kubwa sana na yakupongezwa kwani changamoto iliyopo kwenye jamii ni ukosefu wa shughuli za kufanya baada ya kupata nafuu lakini mpango huo utakuwa chachu yao kushiriki shughuli za kiuchumi na hatimaye kupata maendeleo”Alisema

“Katika kituo chetu hapa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo tunatoa huduma kwa waraibu wa dawa za kulevya aina ya hereion na mchanganyiko wa dawa mbalimbali ikiwemo Ugoro,Pombe,Mirungi na mwamko upo kwenye jamii kutokana na kufanya kazi na asasi za kiraia ambao wamekuwa wakiwaibua watumiaji wa dawa za kulevya kwenye mitaa mbalimbali”Alisema

Dkt Karata alisema Asasi hizo zimekuwa zikiwaandaa na kuwapelekea ili kuweza kuendelea nao kwenye tiba ambayo ni kuwasaidia kuwaondolea maamivu ya arosto kwa kutumia dawa ya methadone na kuweza kuwapa tiba za kisaikolojia.

“Kwa sasa kila siku tunasajili waraibu wawili mpaka watatu kwa siku ambapo kwa wiki idadi inafikia 12 mpaka 13 hii inatokana na uwepo wa Asasi za Kiraia ambazo zimekuwa zikiwaibua waraibu wa dawa za kulevya kutoka kwenye vijiwe na fukwe na maeneo wanayopatikana wakiwa wanafanya matumizi ya dawa hizo”Alisema

Hata hivyo Dkt Karata alitoa wito kwa jamii kupeleka elimu kinga kwa wale ambao hawajaanza kuingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya ili kuweza kudhibiti matumizi mapya

“Lakini pia niwaombe viongozi wa dini wakiwemo Mashehe, wachungaji na Maaskofu wachukulie uraibu kama ugonjwa tena sugu wa akili na waone huo ni mpango mbaya wa shetani kuharibu vizazi vyetu hivyo watumie nafasi zao kuhakikisha wanakemea “Alisema

WAZIRI WA BIASHARA ZNZ AFUNGA MKUTANO WA WAKUU WA TAASISI ZA SMZ NA SMT NYAMAZI

January 14, 2024

Waziri wa Biashara na maendeleo ya Viwanda Zanzibar Mhe Omar Said Shaaban akizungumza wakati akifunga mkutano wa wakuu wa Taasisi za SMZ na SMT katika kusherehekea miaka 60 ya Mapinduzi huko kituo cha maonesho ya biashara nyamazi Zanzibar.






Mwenyekiti wa jukwaa la Taasisi za SMZ na SMT (CEOs) Latifa M.Khamis akisoma maazimio wakati wa kufunga mkutano wa wakuu wa Taasisi hizo uliofanyika katika Ukumbi wa Dkt Hussein Mwinyi Nyamanzi katika kusherehekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.


PICHA NA FAUZIA MUSSA MAELEZO ZANZIBAR

Na Rahma Khamis Maelezo

Waziri wa Biashara na maendeleo ya Viwanda Zanzibar Mhe Omar Said Shaaban amesema Wizara ipo tayari kutoa mashirikiano kwa wafanya biashara ili kukuza pato la taifa.

Akizungumza wakati akifunga mkutano wa watendaji wakuu wa SMT na SMZ katika Ukumbi wa Dkt Mwinyi Nyamanzi amesema utayari huo unahusisha na utoaji wa vibali kwa wafanya biashara ili kuendeleza biashara zao.

Mhe Shaaban pia amewaomba watendaji wa Taasisi za SMZ na SMT kuzingatia mipango madhubuti waliyojiwekea ili kufikia malengo waliyoyakusudiwa.

Aidha amezishukuru Taasisi, Mashirika na Wadau mbalimbali kwa kuwaunga mkono na kufanikisha kufanyika mkutano huo.

Aidha aliendelea kusisistiza taasisi za Serikali kuutumia Ukumbi wa mikutano wa Dkt Hussein Mwinyi uliopo katika kituo cha Manyesho ya Biashara Nyamazi kwa kufanya shughuli zao mbalimbali ili kuongeza pato la taifa.

Akiwasilisha maazimio ya mkutano huo Mwenyekiti wa Jukwaa la Taasisi hizo Latifa Khamis amesema Jukwaa la viongozi wa Mashirika na Taasisi za Umma kutoka SMZ kudhamiria kukamilisha usajili rasmi ifikapo robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Ameongeza kuwa Jukwaa hilo limedhamiria kutoa ushirikiano wa kiutendaji kwa Jukwaa tarajiwa la Watendaji Wakuu la SMZ katika zoezi la kurasimisha Jukwaa hilo kupitia usajili rasmi.

Aidha amefahamisha kuwa Wakurugenzi Wakuu wote kwa umoja wao na kwaniaba ya Mashirika wanayoyaongoza wanaahidi kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza malengo ya Taasisi na dhamira ya waheshimiwa ,Marais na Serikali zote mbili kuchochea utoaji wa huduma katika Taasisi hizo.

Mkutano wa Wakuu wa Taasisi za SMZ na SMT ulifunguliwa January 13 na Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda Axaud Kigahe Katika kuseherehekea miaka 60 ya Mapinduzi


MAVUNDE AWAKOSHA MAMA, BABA LISHE DODOMA, AWAPA MAJIKO YA GESI 500

January 14, 2024
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde akiwa amekumbatiwa na mmoja wa mama lishe waliobahatika kupata fursa ya jiko la gesi kama ishara ya kushukuru. 

Na Dotto Kwilasa, Malunde 1 Blog, Dodoma

MBUNGE wa Jimbo la Dodoma Mjini na Waziri wa Madini Anthony Mavunde amegawa majiko ya  gesi 500 kwa Mama Lishe na Baba Lishe wa Jijini Dodoma ikiwa ni hatua yake ya kuchochea uchumi kwa Wajasiriamali ili kuboresha shughuli zao na kuinua kipato chao. 

Akizungumza kwenye zoezi hilo jijini hapa amesema anaamini majiko hayo yatachochea zaidi shughuli za kiuchumi kwa Wajasiriamali hao na hivyo kuboresha shughuli zao za kipato cha kila siku.

Pamoja na hayo ameeleza kuwa juhudi zake hazitaishia hapo na badala yake yeye kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  ataandaa utaratibu wa upatikanaji wa mitambo ya kutengeneza mkaa mbadala(briquette) na kugawa kwa vikundi vya wakina Mama na vijana. 

"Naamini hatua hii itasaidia kuboresha maisha ya watanzania wa kipato cha chini ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira yetu ambayo yapo hatarini kutokana na uharibifu wa ukataji miti hovyo kwa ajili ya mkaa, " Amesema
Mavunde pia ametumia nafasi hiyo kuwataka wajasiriamali wa Jiji la Dodoma kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo Dodoma na hasa kuzingatia ukuaji wa kasi wa Jiji baada ya maamuzi ya Serikali kuhamishia shughuli zake zote Dodoma.

Mbunge huyo amesema nafasi hiyo ni yakipekee ambayo wanadodoma wanapaswa kuichangamkia badala ya kuwa watazamaji wa fursa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri amepongeza zoezi la ugawaji majiko hayo kwa wajasiriamali huku akitoa elimu ya matumizi ya majiko hayo ili yasilete athari baadaye.

"Kuna watu hawataki kutumia majiko ya gesi kwa kudhani kuwa yana madhara,inatakiwa kuwa waangalifu wakati wa matumizi yake, ukisikia harufu kama ya yai viza hakikisha unafungua madirisha yote ya nyumba na kufunga vizuri jiko lako kabla ya kuliwasha, " Amesema

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ORYX Benoit Araman amesema Kampuni yake inaunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu  Hassan za matumizi ya nishati safi kwa wananchi ili kuokoa mazingira. 

 "Tunatambua umuhimu wa kutunza mazingira hivyo tutaendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kutimiza lengo la 80% ya matumizi ya nishati safi kwa wananchi ifikapo mwaka 2032," Amesisitiza Mkurugenzi huyo . 

KILIMO CHA PAMBA KULIMWA RUFIJI MKOANI PWANI-RC KUNENGE

January 14, 2024

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani,Abubakar Kunenge amezindua mradi wa kilimo cha Pamba Wilayani Rufiji utakaotekelezwa na Kampuni ya Rufiji Cotton Ltd ambapo pia amepokea matrekta na pikipiki zitazotumika kwenye mradi huo.

Akizungumza na wananchi wa Chumbi kwenye uzinduzi huo, aliwapongeza wawekezaji hao kutoka India kwa uwekezaji huo.

Ameeleza kuwa kwenye historia ya Pamba ilianza kulimwa nchini kwa mara ya kwanza wilayani Rufiji mwaka 1964 hivyo Serikali ipo tayari kuumpa ushirikiano mwekezaji huyo.

"Kwenye kipaumbele changu kwa Mkoa Kilimo ni kipaumbele na bado hakijafanya vizuri, "wilaya ya Rufiji kwa kuendelea kuwapokea wawekezaji kwa sasa wilaya hii ina wawekezaji wakubwa wa Kilimo cha Sukari, na Kilimo cha Pamba, niwaombe wakazi wa Rufiji kutumia fursa hizi mnazopata"alieleza Kunenge.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Wille Mtunga alieleza kuwa ,ziara ya India ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imezaa matunda na tunazindua mradi wa Pamba Rufiji.

Anaeleza kwa historia Pamba ilianza kupandwa Wilaya ya Rufiji, wamepita vijiji 24 wilayani Rufiji kufundisha juu ya kilimo bora cha pamba.

Alisema, ili kuwa na kilimo bora wameleta timu ya ushindi ambao ni maafisa ugani 24 watakao hudumu kwenye vijiji hivyo 24.

"Mpaka sasa tumesajili wakulima wenye jumla ya ekari 3012 wilayani Rufiji, ifikapo wiki ijayo tutaaleta mbegu za pamba, viutilifu, mabomba ya kupulizia mazao na vyote vitagawiwa kwa wakulima bure."

Balozi wa zao la Pamba Nchini ,Aggrey Mwanri, ametuma Salaam kwa Rais Dkt Samia za pongezi kwa kuvutia uwekezaji katika sekta ya Pamba.


Alieleza kuwa kilo zinazozalishwa wilayani Rufiji ni laki moja na kiwanda kitakacho jengwa kitahitaji kilo laki tano.


Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Rufiji Cotton Ltd ,Hassan Kinje alieleza , wamekuja kuwekeza Rufiji kwa sababu ya mazingira mazuri ya uwekezaji, kampuni itatoa uwezeshaji wa huduma bure ya matrekta kwa ajili ya kilimo.


Vilevile wameajiri maafisa ugani 24 na kutoa pikipiki ambazo zitatumika kutoa elimu kwa wakulima na wanategemea kujenga kiwanda cha kuchambua Pamba, kiwanda vya nguo.


Kwa upande wake, Ally Athuman Nguyu Diwani kata ya Chumbi alipongeza Wananchi kujitolea ekari 6000 kwa ajili kilimo cha Pamba na ujenzi wa kiwanda cha kuchakata pamba.




VODACOM YAKABIDHI BIMA ZA AFYA 200 KWA AKINA MAMA NA WATOTO PAMOJA NA ZAWADI MBALIMBALI KUPITIA KAMPENI YA ‘SAMBAZA SHANGWE, GUSA MAISHA’ MKOANI IRINGA.

January 14, 2024

  

Mshindi wa pesa taslimu shilingi milioni 10 kupitia kampeni ya Vodacom Tanzania PLC ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, Bw. Kennedy Ntenje (wa tatu kulia) akiwa ameshikilia mfano wa hundi pamoja na Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) na wafanyakazi wa kampuni hiyo katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia tamati wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
 

Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na Mkuu wa Kanda Nyanda za Juu Kusini - Vodacom Tanzania, Abednego Mhagama (wa kwanza kushoto) wakikabidhi mfano wa kadi ya bima kwa Kaimu Mganga Mfawidhi, Dkt. Scholastica Malangalila na mmojawapo wa akina mama walionufaika, Bi. Grace John (katikati) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia tamati ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
 

Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) akifurahia pamoja na mmojawapo wa akina mama na mtoto wake walionufaika na bima ya bure ya afya kutoka Vodacom Tanzania, Bi. Grace John katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
 

 Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) akifurahia pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC mara baada ya kukabidhi bima kubwa za bure kwa akina mama na mtoto wao kwa mwaka mzima katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
 

Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa luninga kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
 

Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa pikipiki kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
 

Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa simujanja kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
 

Msanii wa Bongo Flava maarufu kama ‘Dogo Janja’ akijumuika pamoja na wakazi wa Iringa kutoa burudano kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’ ya Vodacom Tanzania PLC, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani humo mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.

'KALAMU' YA KIBOSHO ILIVYOZALISHA WASOMI HADI MAPROFESA

January 14, 2024

 

 

Na Deogratius Temba - Moshi

KALAMU sio kitu kipya kwa watu wote, unaposikia neno ‘Kalamu’ kinachokujia kichwani ni ile inayotumika kuandikia kwenye karatasi au sehemu nyingine.

Huko Kibosho Moshi,mkoani Kilimanjaro, wanawake wafanyabiashara wadogo wa ndizi mbivu, wanaotokea maeneo ya Kibosho Kirima , kwao kalamu ni aina ya Kibox ambacho hutumika kubeba ndizi mbivu, kilichotengenezwa kwa ustadi mkubwa na fundi seremala kwaajili ya kumwezesha kujitwisha kichwani na kusafiri nachO hadi Moshi mjini kwaajili ya kuuza ndizi. Kalamu hutumika kutunza usalama wa mikungu ya ndizi zisiharibike.

Hivi karibuni, wakati wa mapumziko ya sikukuu za Noeli (Krismas), nikakutana na Mama anayeitwa Maria Modest, ambaye ni mwenyeji wa Kibosho - Kirima masoka ambaye anaitumia ‘kalamu’ kuuzia ndizi zake.

Nilimuuliza, ni kwanini hii inaitwa ‘kalamu’? akasema “kwani hujui? Hii ilitumika tangu zamani sana, Bibi zetu ndio walikibatiza hiki kibox jina hilo” akasema Maria akifikiri kwamba mwandishi ni mgeni sana eneo hilo.

Mwandishi: kwanini hao kina Bibi wa zamani, wajasiriamali walikiita jina hilo? 

Maria akajibu: “Ahaaaa, sasa ni kuambie, hao kina Bibi, walitusimulia kwamba walikiita hivyo kwa sababu walifanya biashara hii ya ndizi kwa kubeba kichwani na wakafanikiwa kuwasomesha watoto wao hadi wakafika vyuo vikuu”

Mwandishi: Ehheee! Hadi Vyuo vikuu kabisa? Ada inapatikana kwa hii biashara?

Maria: “ Mhhhh, yaani mwanangu nikuambie, hata mimi ni shahidi, nimesomesha watoto wangu shule nzuri, wapo wawili, mmoja ameshamaliza Chuo Kikuu, na sasa amepata kazi, huyo mdogo wake yupo Chuo kikuu kingine, ninalipa ada shilingi 1,600,000 kwa biashara yangu hii, na mimi nina pata mahitaji yangu yote na matibabu” anaeleza maria kwa kujiamini.

Lakini maria anaeleza kwamba, wanawake wengi hapo awali hawakuamini kwamba biashara ile ya kubeba ndizi kichwani itawakomboa, lakini kwa kuona wanawake wa Kibosho –Kirima Boro waliofanikiwa waliamua kuiga na sehemu nyingine.

Anaeleza kwamba, wakiwa wanashangaa wale wanaotokea maeneo ya Boro wanavyofanikiwa, wale wanaotokea maeneo ya Kirima Masoka, walikuja kuiga biashara hiyo na sasa wamefanikiwa sana.

“Mimi ninazaliwa kule Boro, lakini nimeolewa Masoka, kule Boro biashara hii ipo sana, wanawake karibia wote wenye afya nzuri wanafanya biashara hizi, upatikanaji wa ndizi mbichi kwaajili ya kufundika ni wa shida, lakini huku masoka ndizi zipo maana awali hakukuwa na ushindani mkubwa wa wanawake anaozifundika”, anasema Maria.

Jitihada za wanawake wengi kufanya biashara kwa lengo la kujikombia kiuchumi zinafanikiwa kwa jinsi wao wenyewe wanavyoweka mtazamo chanya juu ya kile wanachokifanya wakiamini kwamba kitaleta tija. Suala muhimu ni serikali kuweka mifumo rafiki ya kuwawezesha kufanya biashara na kukutana na wateja wao bila kusukumwa, kunyang’anywa biashara zao na mgambo, au maafisa wengine.


WMA NA ZAWEMA ZAKUBALIANA KUSHIRIKIANA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA VIPIMO

January 14, 2024

 


Taasisi za Wakala wa vipimo za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (WMA) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (ZAWEMA) zimetiliana saini hati ya makubaliano ya ushirikiano (MoU) ili kuimarisha utendaji kazi wao katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kubadilishana utaalamu na vitendea kazi ili kuendelea kutoa huduma bora kwa Wananchi wanao hudumiwa kwa upande wa Bara na Visiwani Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini huo katika Ukumbi wa Dokt Mwinyi kituo cha maonesho ya biashara Nyamanzi Fumba Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Hashil Abdallah amesema ni vyema kuimarisha mashirikiano kati ya taasisi hizo ili kuhakikisha vipimo vyote vinakuwa sahihi na mnunuzi wa bidhaa anapata kulingana na thamani ya fedha anayotoa.

Dkt. Hashil amesema, kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo Wakala wa Vipimo ndio taasisi pekee inayopaswa kusimamia matumizi sahihi ya vipimo kwa kuhakikisha kuwa vipimo vinavyotumika katika biashara viko sahihi, na kuzingatia matumizi sahihi ya vipimo ili kuepusha madhara yatokanayo na vipimo batili na kulinda walaji na watumiaji.

Aidha, amesema makubaliano hayo yatasaidia kuimarisha utendaji wa kazi na kuongeza ufanisi utakaopelekea kufikia malengo ya Taasisi hizo kwakuwa taasisi ya Wakala wa Vipimo Bara (WMA) ilianzishwa muda mrefu na inauzoefu wa muda mrefu na vifaa vingi vya kisasa kwa mashirikiano haya itaiwezesha zaidi taasisi ya ZAWEMA kutumia pia vifaa hivyo na wataalamu ili kusimamia matumizi sahihi ya vipimo katika sekta nyingi zaidi.

Kadhalika, Katibu Mkuu Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Ndugu. Ali Khamis Juma ameeleza kuwa mashirikiano baina ya taasisi za WMA na ZAWEMA ni mashirikiano ya kudumu kwa muda mrefu sio ya kipindi cha muda mfupi kwani hivyo itaiwezesha taasisi ya ZAWEMA kukua zaidi na kuingia katika maeneo mengi ya kiutendaji kama ilivyo upande wa WMA Tanzania Bara.

Akizungumza na waandishi Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo Bara (WMA) Bi. Stella Kahwa ameeleza kuwa mashirikiano baina ya WMA na ZAWEMA yamekuwepo kwa muda japo hayakuwa rasmi kimaandishi na sasa yamekuwa rasmi taasisi hizi zitazidi kuimarisha zaidi mashirikiano hayo na mara nyingi WMA na ZAWEMA hushirikiana hata katika kuendesha kaguzi mbalimbali visiwani Zanzibar kwa wauzaji wa vito na madini, mafuta na hata katika sekta ya gesi ili kuhakikisha vipimo vinakuwa sahihi wateja hawapunjiki.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa wakala wa Vipimo Zanzibar (ZAWEMA) Bw. Mohammed Simai Mwalim ameeleza kuwa endapo vipimo vitasimamiwa kwa usahihi katika bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini na bidhaa zinazoingizwa kutoka nje ya nchi itasaidia Serikali kukusanya kodi kwa usahihi.

Hata hivyo alisema endapo vipimo hivyo havitasimamiwa vyema itasababisha wananchi kupata huduma au bidhaa ambazo haziendani na thamani ya fedha wanayotumia.

Mkurugenzi Mohammed ametoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara wote wa Tanzania bara na Zanzibar kuhakikisha wanatumia vipimo sahihi na endapo watakutana na changamoto yoyote inayohusu vipimo wafike kwenye ofisi za Wakala wa Vipimo kwa ajili ya kupata msaada wa kitaalamu.

Hata hivyo aliwaonya Wamiliki wa vipimo kutochezea vipimo kwa lengo la kuwaibia wananchi, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kufanya vitendo hivyo ambavyo vinakatazwa hata kwenye maandiko matakatifu.

Nao Washiriki walioshuhudia utiaji wa saini huo walisema kuwa makubaliano hayo yametiwa saini katika kipindi muafaka cha kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi na yataongeza mashirikiano zaidi ili kuyaenzi na kuyalinda Mapinduzi hayo.

Hati hiyo ya makubaliano ya kiutendaji yalisainiwa na Mtendaji Mkuu wakala wa vipimo Bara (WMA) Stela Kahwa na kwa upande wa Zanzibar Mkurugenzi wakala wa vipimo Zanzibar (ZAWEMA) Mohammed Mwalim Simai.
TPA IPO KATIKA HATUA NZURI UJENZI WA KITUO JUMUISHI CHA KUPOKEA MAFUTA

TPA IPO KATIKA HATUA NZURI UJENZI WA KITUO JUMUISHI CHA KUPOKEA MAFUTA

January 14, 2024






Na Sophia Kingimali

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imesema ipo kwenye hatua nzuri ya utekelezaji wa ujenzi wa kituo jumuishi cha kupokea mafuta eneo la Kigamboni na Kurasini,ili kutatua changamoto ya meli za mafuta zinazoingia katika bandari hiyo kukaa kusubiri muda mrefu kwa ajli ya kushusha shehena ya mafuta.

Hayo ameyasema leo Januari 14,2024 jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho wakati wa ziara yake na waandishi wa habari katika bandari hiyo ili kujionea maboresho mbalimbali yanayofanyika katika bandari hiyo ikiwemo upanuzi wa lango la kuingilia meli.

Amesema ujenzi wa kituo hicho cha kuhifadhia mafuta kitapunguza gharama na kurahisisha utendaji kazi ambapo watu wote watakua wanaenda kuchukulia mafuta hapo na si kama ilivyo sasa ambapo mafuta yanapelekwa katika kampuni binafsi.
- Advertisement -

Ameongeza kuwa uongezaji wa kina kwenye bandari hiyo kutoka mita tisa hadi kufikia mita 14 umeendelea kuchagiza uingiaji wa meli kubwa zenye urefu wa mita hadi 200 tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Pamoja mambo mengine Mrisho ameweka bayana kuwa bandari hiyo imedhamiria kuvuka malengo yaliyowekwa na serikali katika mwaka wa fedha 2023/24 ya utoaji wa huduma ya mizigo kutoka tani milioni 22 hadi milioni 24 kutokana na maboresho makubwa yanayoendelea kufanyika.

Akizungumzia eneo la kuhudumia magari amesema eneo hilo la mita 320 linahudumia magari 6000 kwa mwezi huku kwa mwaka yakiwa magari 250,000 mpka 300,000.

“Eneo hili la magari linamifumo ya ulinzi na usalama na hii imesaidia kuondoa changamoto ya wizi wa vifaa vya magari iliyokuwepo awali”amesema Mrisho.

Aidha Mrisho amesema pamoja na kuwa na ufanisi mkubwa unaofanyika kwenye bandari hiyo lakini pia kunachangamoto kwenye upakuaji wa baadhi ya mizigo hasa kwenye kipindi cha mvua.

Amesema kuna baadhi ya mizigo kama mbolea,ngano zinaathiliwa na mvua hivyo katika kipindi hiko huduma zinakuwa zinathitishwa ili kuepuka uharibifu.

“Hizi product hazihitaji maji ukilazimisha unakua unaharibu meli kama hii ya baric yenye tani 49,000 mpka 50,000 kama utaweka tageti ya huihudumia kwa siku saba au tano siku lazima zitaongezeka hivyo mvua zinazonyeesha zinaathiri utendaji kazi”amesema.

Aidha ameongeza kuwa ongezeko la meli bandarini ni ufanisi mkubwa wa bandari hiyo hivyo ongezeko hilo linasaidia kuongeza mapato kwa nchi na kuinua uchumi.

Amesema kwa kuanzia ijumaa januari 12,2024 mpka jumatatu januari 15 wanatarajia kupokea meli mpya 16 zitakazoingia nchini ili kupata huduma ambapo amesema wajibu wa bandari ni kuongeza spidi ya kuzihudumia.

MIAKA 60 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR,TANESCO INAHISTORIA NAYO

January 14, 2024

 






Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme la Tanzania,TANESCO Mha.Gissima Nyamo-hanga, ameelezea maendeleo ya TANESCO ndani ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar ,katika jukwaa la wakuu wa Taasisi lililofanyika Januari 13,2024 Unguja, Zanzibar

Katika jukwaa hilo Mha. Nyamo-hanga amesema kuwa kwa mara ya kwanza mwaka 1980 TANESCO ilijenga njia ya kusafirisha Umeme za ardhini zenye ukubwa wa kilometa 37.14 kutoka Rati kilomoni , Tegeta -Dar es salaam mpaka eneo la Rati Fumba - Zanzibar, kiasi cha Umeme wa Megawati 45.


“Miaka 43 iliyopita ambayo inakaribia na miaka 60 ya muungano wa Tanzania Bara na visiwani, Kwa mara ya kwanza tulijenga underground cable ya kusafirisha umeme kutoka Dar es salaam kuja zanzibar” alisema Mha. Nyamohanga

Aliongeza kwa kusema kuwa mwaka 2013 baada ya kuongezeka kwa matumizi ya umeme zanzibar, TANESCO ilijenga njia nyingine ya kusafirisha Umeme ya ardhini ya kuleta umeme Zanzibar iliyobeba umeme wa Megawati 100, njia hizo mbili ndizo zinazoendelea kutumika kuleta Umeme zanzibar hadi Sasa.

Akizungumzia Pemba,Mha.Nyamo-hanga amesema kuwa mwaka 2010 , Pemba iliunganishwa na Tanzania Bara kupitia Eneo la majani mapana Tanga, ambapo ilijengwa njia ya Umeme ya megawati 20, umbali wa kilometa78 chini ya bahari kufikisha Umeme Pemba, njia ambayo bado inaendelea kutumika kufikisha Umeme Pemba.

Aliongeza kwa kusema kuwa matumizi ya Zanzibar yanaongezeka siku hadi siku hivyo mpango uliowekwa na Shirika ni kujenga njia kubwa za Umeme zitakazokuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kusafirisha Umeme Zanzibar ili kuendana na mahitaji ya Umeme kwa Wananchi wa Unguja na Pemba.

KAMISHNA MABULA AFANYA UKAGUZI WA KARAKANA YA KISASA MANYONI, ATOA MAELEKEZO MAHSUSI

January 14, 2024


Na. Beatus Maganja

Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda ameeleza kufurahishwa kwake na ubora wa viwango vya ujenzi wa karakana ya matengenezo ya magari na mitambo iliyojengwa Kanda ya Kati ya TAWA wilayani Manyoni, karakana inayotajwa kuwa ni kubwa kuliko karakana zote zilizojengwa na taasisi hiyo.

Ameyasema hayo Januari 14, 2024 akiwa katika ziara yake Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya TAWA wilayani Manyoni, ziara yenye lengo la kukagua shughuli za uhifadhi na utalii zinazotekelezwa na TAWA wilayani humo.

"Nimetembelea na kukagua karakana, kimsingi nimeona imejengwa vizuri na pia nimeona ina uwekezaji mkubwa wa vifaa vitavyotumika na nina imani hii karakana itatusaidia sana" amesema

Akibainisha sababu za kuifanya karakana hiyo kuwa kubwa wilayani humo, Kamishna Mabula amesema Manyoni ni katikati ya nchi na ni sehemu inayofikika kwa urahisi, hivyo kutokana na ukubwa wake itatumika kutengeneza magari si tu ya Kanda ya Kati bali ya taasisi nzima.

Aidha, Kamishna Mabula ameuelekeza uongozi wa Kanda hiyo kuweka mfumo madhubuti wa usimamizi wa karakana ikiwa ni pamoja na kuwapeleka wataalamu wa vifaa hivyo ili iweze kusimamiwa na kuendeshwa Kisasa.

Vilevile Kamishna Mabula ametumia ziara hiyo kuwahimiza Maafisa na Askari wote wa TAWA kurejea mpango mkakati wa taasisi hiyo ambao unafikia kikomo Mwaka 2026 ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Amefafanua kuwa mpango mkakati wa TAWA una malengo makuu matatu ambayo ni kuhakikisha rasilimali ambayo TAWA imepewa kusimamia inakuwa salama, pia kuhakikisha wateja wote wa taasisi wakiwemo wawekezaji wanapata huduma na kuridhika na huduma inayotolewa na lengo la tatu ni kuhakikisha TAWA inafanya kazi kwa ufanisi na tija.

Kamishna huyo amesisitiza kuwa malengo hayo hayataweza kutimia bila kuishi katika tunu za taasisi hiyo ambazo ni uadilifu, kufanya kazi kwa ushirikiano, kutenda kazi kwa ubunifu pamoja na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.

Naye Kamishna Msaidizi Ulinzi wa Rasilimali za Wanyamapori Hadija Malongo akimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa Kanda ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia TAWA kwa kuwezesha ujenzi wa karakana hiyo ambayo kukamilika kwake kutasaidia kupunguza gharama za matengenezo ya magari ambayo ilikuwa changamoto kubwa

Mradi wa ujenzi wa karakana hiyo umegharimu zaidi ya TZS Million 217.