Wakati akiwasilisha taarifa ya Kamati
ndogo ya Uchunguzi ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kuhusu
Operesheni Tokomeza Ujangili, Mwenyekiti wake, James Lembeli alisema
baadhi ya wabunge walitajwa kujihusisha na ujangili.
MAJANGILI WAIBUKA UPYA , MMOJA AKAMATWA NA NYAMA YA SWALA KARIBU NA HIFADHI YA RUAHA IRINGA
Swala wakiwa katika hifadhi |
WAKATI
taarifa ya wizara ya maliasili na utalii iliyotolewa na naibu waziri
mwenye dhamana na wizara hiyo Lazaro Nyalandu kudai kuwa
kumekuwepo na ongezeko kubwa la ujangili wa wanyama katika hifadhi za
Taifa baada ya oparesheni ya tokemeza ujangili kusimama ,jeshi la
polisi mkoani Iringa
linamshikilia mkazi mmoja wa kijiji cha Idodi wilaya ya Iringa
vijijini Bw Kegete Makoga (56) kwa tuhuma za kukutwa na nyara za
serikali ambazo ni nyama ya swala kilo 8 .
Kamanda
wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi ameueleza mtandao huu leo kuwa tukio hilo lilitokea Desemba
29 majira ya saa
3 usiku katika tarafa ya Idodi karibu na maeneo ya hifadhi ya Taifa
ya Ruaha .
Alisema
kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na askari wa hifadhi ya Taifa ya
Ruaha Iringa ambao walikuwa katika doria katika hifadhi hiyo.
Kamanda
Mungi aliasema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na nyama hiyo ya
Swala baada ya doria ya askari hao na kwa sasa anashikiliwa na jeshi
la polisi kwa uchunguzi zaidi kabla ya kufikishwa mahakamani kwa
kosa la kukutwa na nyara za serikali kinyume na utaratibu.
CHANZO:FRANCIS GODWINBLOG
CHANZO:FRANCIS GODWINBLOG
HAFLA YA KUKABIDHI RASIMU YA PILI YA KATIBA
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba Mhe. Joseph S. Warioba mara baaada ya kuwasili katika viwanja vya
Karimjee Hall kupokea Rasimu ya Pili ya Katiba. Kulia ni Mhe. Assaa Rashid, Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,
Rais Kikwete akisalimiana na Mhe Assaa Rashid, Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,
Rais
Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu
huku Jaji Mkuu wa Tanzania Bara Mhe Mohamed Chande Othman, Spika wa
Bunge la Muungano Mhe Anne Makinda na Spika wa Zanzibar Mhe Pandu Ameir
Kificho wakisubiri zamu zao
Rais Kikwete akimuamkia na Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi
Rais Kikwete akimuamkia Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Cleopa David Msuya
MBUNGE MSINGWA AMCHARUKIA ZITTO KABWE KUWA SI MAARUFU KULIKO CHADEMA ,AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA RASMI YA KATIBA MPYA
Wananchi wa jimbo la Iringa mjini wakiwa katika mkutano wa mbunge Peter Msigwa leo |
WATAKA KAMATI IWATAJE WABUNGE WANAOHUSIKA NA UJANGILI:IMEWEKWA DESEMBA 31.
Wananchi mbalimbali wakiwamo wasomi na
wabunge, wamelitaka Bunge kuweka wazi majina ya wabunge waliotajwa
kuhusika na vitendo vya ujangili wa wanyamapori. (HM)
TFF KUTOA ELIMU KWA MASHABIKI JUU YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), kwa kushirikiana na Benki
ya CRDB, wamejipanga kutoa elimu kwa mashabiki wa soka nchini juu ya mfumo mpya
matumizi ya tiketi za Kielektroniki zinazotarajiwa kuanza kutumika rasmi katika
raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
CRDB ndio wazabuni walioshinda tenda ya kuuza aina hiyo ya
tiketi, ambazo mpaka sasa zimeanza kufanyawiwa majaribio ya mauzo katika mechi
ya Azam FC, dhidi ya RuvuShooting kwenye Uwanja wa Chamazi wiki iliyopita.
Maajabu, jamaa apanda juu ya mnara akishinikiza kuonana na Rais Kikwete
Askari
wa Kikosi cha Zima moto na Uokoaji Wakiwa wamepanda juu ya Mnara wa
Simu Uliopo Ubungo Jijini Dar Es Salaam Muda mfupi uliopita kwaajili ya
kumuokoa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Hassan Ambaye
alipanda juu ya mnara huo kwa lengo la kufikisha Ujumbe wa kutaka
kuonana na Raisi Kikwete ili aweze kumwelezea kwa kile anachodai kuwa
jeshi la polisi lilimbambikia kesi na hatimaye kuhukumiwa kifungo cha
Miaka 6 kwenda jela
Askari
wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wakiendelea na zoezi la kumuokoa
Kijana Hassan kwaajili ya kutojirusha kutoka Juu ya Mnara wa Simu Muda
mfupi uliopita Ubungo Jijini Dar Es Salaam Leo
MISS TANZANIA 2013 KULA MWAKA MPYA 2014 NA YATIMA WA NIRA MBAGALA
Kama tulivyotoa taarifa kwa vyombo vya habari hapo
awali wakati wa Sikukuu ya Noel [Christmass ] Redds
Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa, baada ya kujumuika na watoto waishio
katika mazingira magumu kule Bigwa Morogoro katika Kituo cha Mgolole,
Mrembo huyo ataungana na warembo wengine watatu, akiwemo
Miss Tanzania mshindi wa pili Latifa Mohamed, Miss Tanzania mshindi wa tatu Clara Bayo, kukabidhi misaada ya kijamii
pamoja na kushereheka nao pamoja wakati wa Sikukuu ya Mwaka mpya tarehe 1
Januari 2014, katika kituo kiitwacho Nira Children and Youth Orphans Foundation
kilichopo eneo la Mbagala Nzasa A, kwa mzungu kaburi moja, Kata ya Charambe,
Wilaya ya Temeke.
Miss Tanzania pamoja na warembo wenzake, watakabidhi misaada
hiyo ya vyakula, ikiwa ni pamoja na vifaa vya shule, kama vile Madaftari,
kalamu, vitabu n.k.
Wakati huo huo Mrembo wa Kanda ya Mashariki Diana Laizer, kutoka Mkoa wa Morogoro, nae
atakabidhi misaada kama hiyo katika Kituo cha Amani kilichopo Manispaa ya
Morogoro, pamaja na kushereheka nao katika Sikukuu hii ya Mwaka mpya 2014.
KIKWETE AMWAPISHA IGP MPYA PAMOJA NA NAIBU WAKE LEO
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Inspekta Generali wa Polisi (IGP)
mpya Afande Ernest Mangu katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam
jioni hii
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpatia nyenzo za kazi baada ya kumuapisha
Naibu Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Abdulrahman Kaniki
katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali na
Katibu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Inspekta
Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu na naibu wake Naibu
IGP Afande Abdulrahman Kanini katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es
salaam jioni hii
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali
Mawaziri na Katibu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja
na Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu na naibu
wake Naibu IGP Afande Abdulrahman Kanini katika viwanja vya Ikulu jijini
Dar es salaam jioni hii
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na IGP mpya Afande
Ernest Mangu, Naibu Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande
Abdulrahman Kaniki pamoja na IGP mstaafu Afande Saidi Mwema katika
viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na IGP mpya Afande
Ernest Mangu, Naibu Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande
Abdulrahman Kaniki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni
hii. PICHA NA IKULU
SIMBA SC WAKIWA SAFARINI ZANZIBAR KUFUATA 'NDOO' YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI
Kulia Said Ndemla 'Ozil', kushoto Nassor Masoud 'Chollo' na katikati Ramadhani Chombo 'Redondo'. Michuano ya mwaka huu itakwenda sambamba na sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. |
Supa staa; Ramadhani Sngano 'Messi' hakuwa na sare ya timu kama wenzake |
Nahodha Chollo kushoto akimpa tiketi yake beki Mganda, Joseph Owino. Wengine kulia ni Daktari, Yaasin Gembe na Kocha Msaidizi, Suleiman Matola kushoto |
Chollo akimpa tiketi Amri Kiemba |
Kulia Redondo, katikati kocha wa makipa Iddi Pazi 'Father' na kushoto mshambuliaji Ali Badru |
Kipa Yaw Berko akiikagua tiketi yake baada ya kukabidhiwa na Nahodha Msaidizi, Haruna Shamte kushoto |
SIMU ZAO HAZIPATIKANI TANGU ASUBUHI
Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
RASMI. Yanga SC imejitoa katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, kwa sababu timu yao haina benchi la Ufundi, baada ya kufukuzwa kwa Kocha Mkuu, Ernie Brandts.
Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto ameiambia BIN ZUBEIRY muda huu kwamba, uongozi umefikia hatua hiyo kwa sababu bado hawajapata benchi jipya la Ufundi.
RASMI. Yanga SC imejitoa katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, kwa sababu timu yao haina benchi la Ufundi, baada ya kufukuzwa kwa Kocha Mkuu, Ernie Brandts.
Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto ameiambia BIN ZUBEIRY muda huu kwamba, uongozi umefikia hatua hiyo kwa sababu bado hawajapata benchi jipya la Ufundi.
Kikosi cha Yanga kilichofungwa 3-1 Kombe la Mapinduzi |
Yanga
SC ilikuwa imepangwa Kundi C la michuano hiyo inayoanza kesho pamoja na
Spice Star, Azam FC na Tusker ya Kenya- maana yake kwa kujitoa kwao,
Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kitalazimika kupanga upya Ratiba yake au
kuiingiza timu nyingine katika nafasi ya mabingwa hao wa Bara.
Mapema jana, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC, Mussa Katabaro aliiambia TANGA RAHA kwamba wanachelewa kwenda Zanzibar kwa sababu hawajapata mwaliko na waliwaandikia barua ZFA juu ya hilo, lakini hadi sasa hawajapata majibu.
Mapema jana, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC, Mussa Katabaro aliiambia TANGA RAHA kwamba wanachelewa kwenda Zanzibar kwa sababu hawajapata mwaliko na waliwaandikia barua ZFA juu ya hilo, lakini hadi sasa hawajapata majibu.
SSRA YAJADILIANA NA JUKWAA LA WAHARIRI KUHUSU MPANGO MKAKATI WA KUPANUA WIGO WA HIFADHI YA JAMII KUPITIA ELIMU KWA UMMA
Mkurugenzi
Mkuu wa SSRA Bi. Irene Isaka akiwasilisha mada kuhusu hali halisi ya sekta ya
hifadhi ya jamii nchini changamoto na mafanikio
Baadhi
ya wahariri wakuu wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakisiliza mada
ikiwasilishwa na mkurugenzi mkuu wa SSRA (hayupo pichani)
Mhariri
mkuu wa gazeti la Nipashe Bwana Jesse Kwayu akiuliza swali mara baada ya
uwasilishwaji mada
Bi.Irene Isaka Mkurugenzi
mkuu wa SSRA akijibu swali lililoulizwa
na mmoja wa Wahariri,kulia kwake Mkuu wa mawasiliano na uhamashishaji wa
SSRA Bi. Sarah Kibonde – Msika
Bi Irene Isaka Mkurugenzi
Mkuu wa SSRA akisisitiza juu ya umuhimu wa vyombo vya habari katika kutoa elimu
ya hifadhi ya jamii kwa wananchi,kushoto kwake Bwana Absalom Kibanda ambaye ni
mkuu wa Jukwaa la Wahariri nchini na kushoto kwake ni Mkuu wa mawasilianao na
uhamashishaji wa SSRA Bi. Sarah Kibonde –Msika .
Subscribe to:
Posts (Atom)