GEF KUPITIA UNDP YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 4 KWA CSOs 44 NCHINI KUTEKELEZA MIRADI NGAZI YA JAMII

April 05, 2024

 


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia Programu ya Ruzuku ndogo inayotekelezwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) limesaini makubaliano ya kutoa sh 4.04 bilioni kwa mashirika yasiyo ya kiserikali 44 nchini ili kutekeleza miradi ya Uhifadhi wa Mazingira, Misitu, kuendeleza ufugaji nyuki, kutunza vyanzo vya Maji na uwezeshaji Jamii kiuchumi.

Utiaji saini wa Makubaliano hayo umefanyika leo April 4, 2024 katika Makao Makuu ya Jengo la Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na kuongozwa na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP, Bw. Shigeki Komatsubara.

Miongoni mwa mashirika yaliyosaini mkataba wa kupatiwa fedha hizo ni Shirika la Connecting Youth Connecting Tanzania (CYCT) ambalo limekuwa likihamasisha uhifadhi wa mazingira, Misitu na Mabadiliko ya tabia nchi kuhusisha vijana, Wanawake na Wanafunzi na Kundi la watu Maalum

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Komatsubara amesema kuwa mashirika zaidi ya 400 yalituma maombi kuomba fedha za kutekeleza miradi midogo midogo nchini Tanzania bara na Zanzibar lakini ni mashirika 44 tu ndio yamefanikiwa.

“Hongereni sana leo kuwa miongoni mwa mashirika na asasi ambazo zimepata fursa kutekeleza miradi midogo Tanzania.

Bw. Komatsubara amesema anaimani kubwa mashirika ambayo yanapewa fedha hizo yatakwenda kutekeleza vyema miradi ambayo itagusa jamii hasa wanawake, vijana, Walemavu na Jamii za pembezoni.

“Tunatarajia miradi yetu itakwenda kuchochea maendeleo katika jamii ikiwepo pia kukabiliana na vichocheo vya uharibifu wa mazingira” amesema.

Naye Mwakilishi kwa niaba ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Bi. Lilian Lukambuzi akizungumza katika hafla hiyo alitaka mashirika yaliyopewa fedha hizo kuzitumia kama ilivyokusudia.

Amesema serikali itafuatilia miradi ambayo inakwenda kutekelezwa ili kuhakikisha inakuwa na tija.

Awali, mratibu wa programu ya ruzuku ndogo za GEF nchini, Bw. Faustine Ninga amesema haikuwa kazi rahisi kupitisha mashirika hayo machache kupata ruzuku kutokana na uhitaji mkubwa kutoka katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kamati ya Uendeshaji ya programu hiyo ya Ruzuku Ndogo za GEF ambayo inaundwa na wataalam kutoka sekta mbalimbali na taasis zisizo za Kiserikali kwa kushirikia na UNDP ilifanya kazi kubwa ya kuchambua maandiko ya miradi zaidi ya 400.

Hata hivyo, amesema kutokana na uhitaji kuwa mkubwa ni mashirika 44 tu ndio yalipitishwa, ijapokuwa mashirika mengine yalikuwa na madokezo mazuri ya miradi.

Hata hivyo ameyataka mashirika haya kufuata kanuni na taratibu za nchi na miongozi ya uendeshaji wa taasisi zisizo za kiserikali katika utekelezaji wa miradi yao ili miradi iwe na matokeo mazuri.

Amesema kamati ya ufuatiliaji miradi hiyo itakagua na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi yote ili kuhakikisha kuwa jamii zinanufaika.

Wakizungumza baada ya kusaini mikataba baadhi ya watendaji wa mashirika hayo walipongeza UNDP kwa kuendelea kutoa fedha za kutekeleza miradi midogo katika jamii.
Mratibu wa Shirika la CYCT, Bw. Mensieur Elly amesema hii ni mara ya kwanza shirika hilo kupata fedha kutoka kwa wahisani hao.

“Tunatarajia kushirikiana na wadau mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kutunza Ikolojia ya mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya “Go green, serve Nature “ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Siha, Mkurugenzi Siha, TFS West na North Kilimanjaro, Afisa mipango na maendeleo jamii, Afisa elimu, mwenyekiti wa Halmashauri, afisa Tarafa, afisa Mtendaji, madiwani na vikundi vya vijana na wanawake West Kilimanjaro katika kutekeleza na kupata matokeo chanya na yanayoshikika.

Nae mratibu miradi wa Shirika la WODSTA, Bi. Clara Chuwa amesema wanakwenda kutekeleza mradi kwa ajili kuwezesha kutunza mazingira na matumizi endelevu ya msitu na chanzo cha maji kijiji Cha lemanda, Kata ya Oldonyosambu, Wilaya ya Arumeru.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la SECCA, Bw. Esaya Yusufu amesema wanakwenda kutekeleza mradi wa upandaji miti na kuchimba kisima katika eneo la ikolojia ya Serengeti.

Mfuko wa mazingira Duniani (GEF) ulianzishwa mwaka 1992 na umekuwa na miradi katika nchi 136 Duniani.

MPANGO WA SERIKALI KUHAKIKISHA IFIKAPO MWAKA 2034 ASILIMIA 80 YA WATANZANIA WATATUMIA NISHATI SAFI

April 05, 2024
MKUU wa Mkoa wa Tanga Batilda Burian akizungumza wakati akifungua mkutano wa kwanza wa bajeti wa mwaka 2024 kati ya wabia wa maendeleo ya nishati pamoja na wakala wa nishati vijijini (REA) ambapo alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha watanzania wanapata nishati ya umeme kwenye maeneo yao na wakala huo umekuwa ukifanya kazi nzuri ya kusambaza umeme.
NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Dkt James Mataragio akifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Batilda Burian leo
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya REA Balozi ,Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu akiwa kwenye kikao hicho




NAIBU KATIBU Mkuu wa Wizara ya Niashati James Mataragio amesema mpango wa Serikali ni kuhakikisha Tanzania ifikapo mwaka 2034 watanzania asilimia 80 watakuwa wanatumia matumizi ya nishati safi.

Mataragio aliyasema hayo leo mjini Tanga wakati wa uzinduzi wa mkutano wa kwanza wa bajeti wa mwaka 2024 kati ya wabia wa maendeleo ya nishati pamoja na wakala wa nishati vijijini (REA) ambapo alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha watanzania wanapata nishati ya umeme kwenye maeneo yao na wakala huo umekuwa ukifanya kazi nzuri ya kusambaza umeme.

Alisema kwamba kazi hiyo wamekuwa wakifanya kwa kushirikiana na wenzao wabia wa maendeleo wamekuwa msaada mkubwa wakisapoti huo mpango na wametoa fedha nyingi kuhakikisha rea wanasambaza umeme maeneo mengi.

Alisema kwamba sio umeme tu bali hivi karibu kwa kushirikiana n area wamekuwa wakigawa majiko ya nishati safi ya kupikia na wanajua Rais Dkt Samia Suluhu amekuwa kinara wa mpango huo kuhakikisha kwamba Tanzania ifikapo mwaka 2034 watanzania asililia 80 wanakuwa na matumizi ya nishati safi kwa hiyo.

Alisema wanawashukuru wenzao kwa kusapoti jitihada za Rais hivyo sisi kama Serikali tutaendeleza mashirikiano nao kwenye miradi mengine jadidifu ikiwemo joto ardhi kwenye mradi huo na ni miradni inayolenga kupunguza hewa ya ukaa ifikapo mwaka 2034.

Aidha Dkt Mataragio alisema kwa sasa kuna maendeleo makubwa sana ya uhakika wa umeme hapa nchini kwani hata hivi karibuni Naibu Waziri Mkuu hivi karibu Naibu Waziri Mkuu alizindua mtambo wa kuzalisha umeme Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere (JNNH) na sasa hawana mgawo kutokana na uwepo wa uzalishaji wa umeme wa kutosha.

“Kuna matatizo kwenye gridi ambayo Tanesco na Wizara ya nishati tunahakikisha yanatatuliwa tunaendelea kuboresha muindombinu ya kusambaza umeme na kuongeza uzalishaji wa mashine za JNHP zipo 9 moja imekamilika na inazalisha umeme na nyengine imefikia asilimia 99 muda sio mrefu itazinduliwa na itakapokamilika watazindua na wanategemea kutakuwa na umeme wa kutosha “Alisema Dkt Mataragio.

Hata hivyo alisema kwa sasa wana vyanzo vya gesi vinazalisha gesi kama nchi wana umeme wa kutosha maana wana gesi na maji na wanaangalia nishanti nyengine.

Naibu Katibu Mkuu huyo aliwataka watanzania kuchangamkia fursa ya uwepo wa nishati ya umeme kwenye maeneo yao ili kuweza kujikwamua kiuchumi hususani maeneo ye vijijini kutokana na kwamba wakiitumia vizuri inaweza kuwa na manufaa kwao ambayo yatawezesha kuwaongeza kipato huku akiwahimiza wananchi maeneo umeme ulipopita watumie fursa ya kujiunganisha kwenye majumba yao.

Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Tanga Batilda Burian alimpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa jinsi alivyoendelea kuhakikisha sekta zote zinakuwa na maendeleo makubwa hususani nishati kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Tanzania nzima imepata umeme na Tanga kwenye vijiji 772 vyote vimepata umepata umeme kasoro 30 na kazi inayoendelea ni kupeleka kwenye vitongoji na wana asilimia 80 imekwenda kwenye vitongoji.

Alisema kupitia kikao hicho cha Wakala huo na wadau wa maendeleo wa nishati kupitia bajeti na kupata fedha za kuongeza ili kuweza kukamilisha vitongoji vilivyosalia kutokana na umuhimu wa umeme katika kuchochea kasi ya ukuaji wa maendeleo kwa wananchi kwenye maeneo mbalimbali.

“Umeme ukipatikana unasaidia kuchochea maendeleo na uchumi unakuwa lakini hata vituo vya afya vitafanya kazi,shuleni watoto watasoma tunawashukuru REA wamekuwa wakipeleka Umeme na kuunganisha na mlipokuja Tanga mmeweza kutembelea kituo cha Afya Pangani na mmetoa majiko ya gesi na banifu kwa shule ili kuhakikisha Sera na azma ya Rais Dkt Samia Suluhu ifikapo mwaka 2030 nishati hiyo inatumika tunawashukuru wadau wetu Benki ya Dunia,Benki ya Afrika na wadau wengine wa maendeleo walioshiriki kwenye mpango huu”Alisema

Naye kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassani Saidy alisema hicho ni kikao cha kwanza cha kuandaa mpango kazi na bajeti kwa mwaka ujao wa fedha na serikali imekuwa ikifanya kazi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye sekta hasa upande wa nishati ya Umeme Vijijini.

“Tunawashukuru wadau tunaoshirikiana nao wakiwemo Benki ya Dunia,Benki ya Afrika,Umoja wa Ulaya,Norway ,Swedeni na MG ya Ufarasa hawa wanachangia kwenye gharama za utekelezaji wa miradi yetu kwa hiyo wananchi wanapoona miradi inaendelea wajue fedha nyingi zinatoka serikali na wadau wanawashirikisha ili kuwaongezea imani yao kuweza kutoa ushirikiano kwemye miradi yao”Alisema Mhandisi Hassani

Mwisho.