Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles Mbuge akifungua Kikao kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabiliana na Maafa Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika Jijini Dodoma.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Wataalam ya Usimamizi wa Maafa kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wakifuatilia kikao hicho.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Wataalam ya Usimamizi wa Maafa kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wakifuatilia kikao hicho.
Mkurugenzi
Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa (Utafiti)
Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Charles Msangi akiwasilisha Sera, Sheria na Mfumo wa
Usimamizi wa Maafa wakati wa kikao kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya
Wataalam ya Kukabilianana Maafa Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency
Response Team – DoMAERT) kilichofanyika Jijini
Dodoma.Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa (Utafiti) Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Charles Msangi akiwasilisha Sera, Sheria na Mfumo wa Usimamizi wa Maafa wakati wa kikao kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabilianana Maafa Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mtaalam Mshauri kutoka DarMAERT Dkt. Christopher Mnzava (aliyesimama) akiwasilisha Muundo wa Timu Mtambuka ya Wataalam ya kukabiliana na Maafa pamoja na Taratibu, Majukumu ya Kiutendaji wakati wa kukabiliana na Maafa katika kikao hicho.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Mkurugenzi
wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles
Mbuge (wa tano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Wataalam ya Usimamizi wa Maafa
baada ya Kikao kazi cha Kuweka Mkakati
wa Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabiliana
na Maafa Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult
Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika Jijini Dodoma.Na Mwandishi wetu- Dodoma
Mkurugenzi
wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles
Mbuge amewataka Wataalam kuanzisha Timu Mtambuka ya Wataalam ya
Kukabiliana wa Maafa kila Mkoa ambayo itarahisisha mawasiliano ndani ya Mkoa wakati wa
kukabiliana na dhahrura.
Meja
Jenerali Mbuge ameyasema hayo wakati akifungua Kikao Kazi cha Kuweka Mkakati wa
Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabilianana Maafa Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency
Response Team – DoMAERT) kilichofanyika Jijini Dodoma.
Amesema
uwepo wa timu hiyo pia itasaidia kuunganisha nguvu kwa wadau waliopo ndani ya
Mkoa na kuweza kutumia rasilimali zilizopo kuhakikisha maafa yanakabiliwa na
wananchi kuwa katika mazingira salama.
“Nchi
yetu imekuwa ikipata maafa mara kwa mara ambayo uratibu wake unahitaji kila
Mkoa kuwa na Timu Mtambuka ya Wataalam ya Kukabiliana wa Maafa kwa mujibu wa
Sheria ya Usimamizi ya Maafa Na. 6 ya mwaka 2022 na kanuni zake hivyo uundwaji
wa timu hizo ni muhimu kwa usalama wa wananchi na mali zao,” Amesema Meja
Jenerali Mbuge.
Pia
Mkurugenzi huyo amewasisitiza washiriki kupitia kikao kazi hicho kuhakikisha
kila mmoja kwa nafasi yake anafahamu
jukumu lake na kulitekeleza kikamilifu pamoja
na tayari kwa ajili ya kukabiliana na
maafa ndani ya Mkoa.
Katika
hatua nyingine ameeleza Meja Jenerali Mbuge kwamba Idara ya Menejimeti ya Maafa
Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kuchukua
hatua za kupunguza madhara kwa kuhakikisha usimamizi na uratibu wa maafa na
huduma za dharura zinatolewa kwa wakati kwa kuzingatia mipango, miongozo na
mikakati ya kitaifa na kisekta.
“Idara
ya Menejimenti ya Maafa kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya
Mwaka 2004 na Sheria ya Usimamizi wa Maafa, Na. 6 ya mwaka 2022 inaratibu na
kusimamia masuala ya maafa nchini,”Amebainisha Mkurugenzi huyo.
Aidha
Mkurugenzi huyo akawahimiza wananchi kushirikiana na Serikali pamoja na wadau
wa maendeleo ili kuhakikisha malengo ya mapambano dhidi ya maafa yanafaikiwa
kama iliyokusudiwa.