Na Oscar Assenga,Tanga.
Watanzania wameshauriwa kuacha tamaa zakupenda kujilimbikizia mali pamoja na kung’ang’ania madaraka kwani kwa kufanya hivyo kunachangia kasi ya uvunjifu wa amani pamoja na nchi kukosa Baraka za Mungu.
Hayo yameeleza na Askari mstaafu aliyepigana vita ya pili ya dunia Francis Bernado wakati akiongea na waandishi wa habari katika sherehe za kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa zilizofanyika kimkoa katika bustani za uhuru park Jijini Tanga na kuhudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego pamoja na viongozi wengine wa serikali.
Alisema machafuko yalianza kujitokeza kwa sasa ni matokeo ya baadhi ya viongozi kutaka madaraka au kung’ang’ania nafasi Fulani badala ya kuwa na uzalendo wa kuwatumikia wananchi pamoja na taifa kwa ujumla ili kuharakisha maendeleo.
“Tamaa ya kutaka kumiliki vitu vikubwa peke yako ndio inayosababisha nchi kwa sasa kusikia sehemu Fulani kuna machafuko ,watu wamemsahau Mungu na kujifanyia maamuzi bila kufikiri kama anachokifanya kitaleta manufaa gani kwa jamii”alisema Bernado.
Hata hivyo aliiomba serikali kuwa kumbuka askari wastaafu kwa kuwaongezea mafao yao kwani wengi wao wanaishi maisha magumu baada ya kustaafu huku wakiwa wamelitumikia taifa kwa moyo wa upendo na kujituma .
“Naomba serikali ituangalie sisi askari tulioiletea heshima nchi hii kwani kwa sasa inaonekana kama thamani yetu ni ndogo kwa serikali kutoka na kututelekeza na msaada pekee tunapata kwa familia zetu tu”alisema Askari huyo mstaafu.
Watanzania wameshauriwa kuacha tamaa zakupenda kujilimbikizia mali pamoja na kung’ang’ania madaraka kwani kwa kufanya hivyo kunachangia kasi ya uvunjifu wa amani pamoja na nchi kukosa Baraka za Mungu.
Hayo yameeleza na Askari mstaafu aliyepigana vita ya pili ya dunia Francis Bernado wakati akiongea na waandishi wa habari katika sherehe za kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa zilizofanyika kimkoa katika bustani za uhuru park Jijini Tanga na kuhudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego pamoja na viongozi wengine wa serikali.
Alisema machafuko yalianza kujitokeza kwa sasa ni matokeo ya baadhi ya viongozi kutaka madaraka au kung’ang’ania nafasi Fulani badala ya kuwa na uzalendo wa kuwatumikia wananchi pamoja na taifa kwa ujumla ili kuharakisha maendeleo.
“Tamaa ya kutaka kumiliki vitu vikubwa peke yako ndio inayosababisha nchi kwa sasa kusikia sehemu Fulani kuna machafuko ,watu wamemsahau Mungu na kujifanyia maamuzi bila kufikiri kama anachokifanya kitaleta manufaa gani kwa jamii”alisema Bernado.
Hata hivyo aliiomba serikali kuwa kumbuka askari wastaafu kwa kuwaongezea mafao yao kwani wengi wao wanaishi maisha magumu baada ya kustaafu huku wakiwa wamelitumikia taifa kwa moyo wa upendo na kujituma .
“Naomba serikali ituangalie sisi askari tulioiletea heshima nchi hii kwani kwa sasa inaonekana kama thamani yetu ni ndogo kwa serikali kutoka na kututelekeza na msaada pekee tunapata kwa familia zetu tu”alisema Askari huyo mstaafu.
MKUU wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego akikabidhiwa ngao na sime na askari wa JWT kwenye sherehe za siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa zilizofanyika Jijini Tanga. |
DC Dendego akiweka Sime kwenye mnara wa kijiji cha Miaka 21 ikiwa ni kumbukumbu ya siku ya Mashujaa. |
Askari wa Mgambo wakiwa wakijiandaa na gwaride leo. |
Askari Mgambo wakiwa wamejipanga tayari kwa ajili ya kukaguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego. |
VIONGOZI mbalimbali wakifuatilia maadhimisho hayo wa kwanza mebel kwenye shati la kijani na koti jeusi ni Meya wa Jiji la Tanga,Omari Guledi wanaofuatia kwa nyuma wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tanga,Abdi Makange,anayefuatia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga,Lucia Mwiru na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tanga,Kassim Mbuguni.