MBUNGE WA JIMBO LA MAFINGA MJINI COSATO CHUMI AMESAINI MKATABA WA USHIRIKIANO NA NGO YA WORLD SHARE YA NCHINI KOREA

July 31, 2016

Afisa wa NGO ya world share ya nchini korea Nara Kim na mbunge wa jimbo mafinga mjini Cosato Chumi wakisaini mkataba wa makubaliano ya kazi
NAIBU WAZIRI MPINA AZITAKA RADIO ZA JAMII KUHAMASISHA USAFI WA MAZINGIRA

NAIBU WAZIRI MPINA AZITAKA RADIO ZA JAMII KUHAMASISHA USAFI WA MAZINGIRA

July 31, 2016

hag1 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina (katikati) akiangalia samaki katika soko ya wilaya ya Masasi akiwa katika ziara yake ya usafi na ukaguzi wa mazingira mjini Masasi, (kilia) ni Mkuu wa Wilaya ya Masasi Bw. Selemani Mzee.
hag2 
Aliyeinama katikati akikusanya uchafu ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akishiriki katika zoezi la usafi wa mazingira Wilayani Masasi mwishoni mwa wiki.
hag4 
Bw. Benjamini Elias (kulia) Afisa Afya wa Halmashauri ya Mji wa Masasi akitoa taarifa na maelezo ya hali ya usafi  wa soko la mji wa Masasi kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina (kushoto), wakati wa ukaguzi wa usafi wa mazingira  mjini Masasi. (PICHA NA EVELYN MKOKOI)
……………………………………………………………………………………………
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb) amezitaka Radio za jamii kuhamasisha usafiri wa mazingira nchini. Naibu  Waziri Mpina ametoa kauli hiyo alipokuwa akishiriki siku ya usafi kitaifa,  mwishoni mwa wiki wilayani Masasi Mkoani Mtwara.
Akitolea Mfano wa Radio Pride FM ya Mjini Mtwara yenye kupatikana katika frequencies 87.8 mjini Mtwara, ambayo imeanzisha kampeni ya usafi katika mkoa wa mtwara na wilaya zake kwa kufanya vipindi vya moja kwa moja na kutembelea wilaya za mkoa huo kufanya usafi wa mazingira kwa vitendo.
Kwa Upande wake Bw. JUma Andrea Manager uzalishaji wa kituo hicho cha Radio, alisema kuwa lengo kubwa la kituo hicho kuhamasiha usafi ni kuunga mkono agizo la Mhe. Rais kwa kuwaweka pamoja wananchi, kuweka muamko na hamasa ili kujenga tabia ya kupenda usafi na kuepukana na magonjwa yatokanayo na uchafu akitolea mfano ugonjwa wa homa ya matumbo na kipindipindu.
Akiongea na Uongozi wa Mkoa wa Mtwara katika majumuisho ya ziara yake Wilayani Masasi, Naibu Waziri Mpina aliwataka viongozi wa mkoa huo kuunda sheria ndogondogo za mazingira zitakazo watoza faini wananchi waharibifu wa mazingira mkoani humo, na kuwachukulia hatua za kisheria kulingana na hali ya wananchi ili waweze kujifunza na kujijengea tabia ya usafi.
“Nimeona kuwa uchomaji moto misitu ovyo hapa kwenu umekithiri, uchomaji moto taka nao siyo njia nzuri ya uondoshwaji wa taka,hiyo kuwe na miondombinu rafiki kwa uondoshwaji wa taka, na kiongozi wa mkoa ambae hatakuwa tayari kushughulikia usafi wa mazingira na yeye awe tayari kushughulikiwa alisisitiza.”
Ziara ya Naibu Waziri Mpina Mkoani Mtwara ni muendelezo wa Ziara zake nchini za ukaguzi wa viwanda na usafi wa mazingira iliyohusisha pia ukaguzi wa machinjio ya mji wa Masasi.
Radio Maria waiomba Serikali kurekebisha Sheria ya leseni ya redio za jamii

Radio Maria waiomba Serikali kurekebisha Sheria ya leseni ya redio za jamii

July 31, 2016

maki1Mwashamu Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara akikata keki wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda, katikati ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania (RMTZ) Padre John Maendeleo.
maki2 
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akikata keki wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam yaliyoanza rasmi tangu April 26 mwaka huu. Katikati ni Mwashamu Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara Titus Mdoe,kutoka kulia ni Mhamasishaji Mkuu wa Redio Maria Tanzania Bi. Veronica Mwita na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania (RMTZ) Padre John Maendeleo.
maki3 
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa akisalimiana na Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara Mwashamu Askofu Titus Mdoe wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania Padre. John Maendeleo.
maki4 
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Saalam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizungumza na wadau na marafiki wa Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo
maki5Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania Padre John Maendeleo akizungumza na wadau na marafiki wa Radio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo.
maki6 
Rais wa Redio Maria Tanzania Humphrey Julius Kira akizungumza na wadau na marafiki wa Radio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo.
maki7 
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akipokea risala kutoka kwa Rais wa Redio Maria Tanzania Humphrey Julius Kira(Kulia) wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam.
maki8 
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akipeana mkono na baadhi ya marafiki wa Redio Maria Tanzania waliofika kuchangia Redio hiyo katika harambee iliyofanyika ikiambatana na sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais wa Redio Maria Tanzania Bw. Humphrey Julius Kira.
maki9 
Baadhi ya waumini wa Roman Katoliki wakifurahi wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania (RMTZ).
Picha zote na Frank Shija, MAELEZO.
………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Rais wa Redio Maria Tanzania, Humphrey Kira ameiomba Serikali kurekebisha Sheria ya leseni ya redio za jamii ili ziweze kuwa na vituo vingi vya kurushia matangazo yake.
Hayo yamesemwa leo na Rais huyo wakati alipokuwa akisoma risala kwenye sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya redio hiyo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Msimbazi Centre, Jijini Dar es Salaam.
Kira amefafanua kuwa redio za kijamii hasa zilizojikita katika nyanja za kiimani zinasaidia kufundisha maadili na kufanya wananchi wakomae kiimani, hivyo angefurahi sana kuona redio za aina hiyo zinapewa leseni za kurusha matangazo yake nchi nzima.
“Ndugu mgeni rasmi, redio yetu inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ufinyu wa sehemu za usikivu (coverage areas) ambapo tatizo hili linatokana na sheria ya leseni za redio ambayo hairuhusu redio za aina hiyo kuwa na vituo zaidi ya kumi nchini nzima, tunaomba serikali itusaidie kuiboresha sheria hii ili tuongeze vituo vya matangazo ya dini”, alisema Kira.
Rais huyo ameongeza kuwa majimbo yote yanahitaji kufikiwa na huduma za maombi, hivyo anawashauri wasikilizaji wote kuendelea kuisikiliza redio hiyo kwa njia ya mitandao ikiwemo simu za mkononi kwani hivi sasa huduma hiyo inapatika nchi nzima.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ametoa rai kwa uongozi wa redio hiyo kutobadilisha maudhui wala kuweka vipindi visivyokuwa vya dini ili iendelee kuunganisha familia na sio kuzigawa familia.
“Tunasema kuwa redio Maria ni sauti ya kikristu nyumbani mwako lakini mimi nasema ni sauti ya Mungu ndani ya familia kwa kuwa inafanya kazi ya kuunganisha familia, vyombo vingine vya habari vinafanya kazi kubwa ya kuigawa familia lakini Redio Maria ni tofauti”, alisema  Pengo.
Askofu Pengo amewashukuru wananchi wote waliohudhuria kwenye maadhimisho hayo kwa kuwa kufanya hivyo ni njia moja wapo ya kumuenzi na kumpa heshima Mama Bikira Maria.
Nchini Tanzania, Redio Maria ilianzishwa Aprili 26 mwaka 1996 katika Jimbo Kuu Katoliki la Songea ikiwa na lengo la kumsaidia Mama Bikira Maria katika kazi yake ya kumtangaza Yesu Kristo kwa watu wote. Mpaka sasa ina vituo 10 Tanzania Bara na viwili Zanzibar.

BOHARI LATEKETEA KWA MOTO SINZA LEGO JIJINI DAR JIONI HII

July 31, 2016
Bohari likiwa linateketea kwa moto jioni hii Sinza Lego
Mmoja wa kijana ambaye alifika kushuhudia tukio hilo akipanda juu ya Ghorofa baada ya kunusurika kudondokea katika moto huo
Moto ukiendelea kuwaka huku juhudi za kuzima zikiendelea
Mbele ni Gari la zima moto likiwa limefanya juhudi za kuzima moto ,  hapa wakiondoka kufuata maji mengine ili kuendelea na zoezi la kuzima moto huo
Moto ukiendelea kuwaka katika Bohari hilo
Baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia tukio hilo la kuwaka kwa Bohari
Magari yakiwa yameruhusiwa kuendelea na safari baada ya moto huo na moshi mkubwa kupungua 

Picha na Fredy Njeje/Blogs za mikoa
Bohari moja ambalo lilikuwa la kuhifadhia mataili pamoja na vifaa vyenginevyo vya magari lililopo Sinza Lego ambalo mmiriki wake hakufahamika kwa mara moja limeteketea kwa moto ambapo kwa mujibu ya wenyeji wa eneo hilo wamedai kuwa chanzo cha moto huo ni mataili.  Pia katika eneo hilo kuna Gereji ambayo haikuathirika na moto huo mkubwa, mpaka jioni hii kikosi cha kuzima moto kilikuwa eneo la tukio kuendelea kusaidiana na wananchi kuhakikisha moto huo unazimika. Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi.
Regards Tone Multimedia Company Limited Plot No.223/225 Block 46, Umoja Street Kijitonyama P.O Box 32529 Dar es salaam Tanzania Tel +255 22 2772919 Fax +255 22 2772892 Mob +255 654221465 E-Mail blogszamikoa@live.com Facebook: www.facebook.com/blogszamikoa Web: www.blogszamikoa.com 1458109219454_logo_blog_za_mikoi.png

JPM AKOSHWA NA DC WA IGUNGA JOHN MWAIPOPO, AAMURU STENDI YA BASI NA SOKO VIANZE KAZI JUMATATU

July 31, 2016
 Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo akielezea changamoto za Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabiri wilaya hiyo wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016. Mkuu huyo wa wilaya ambaye ana mwezi mmoja toka aanze kazi alimweleza Rais kwamba kuanza kwa stendi ya basi kunasubiri kibali kutoka SUMATRA na kwamba soko jipya ambalo limeshamalizika kujengwa halitumiki kwa sababu ya mkanganyiko unaohusu badhi ya wafanyabishara kuhodhi sehemu kubwa ya soko jipya na kutolitumia huku wakiendelea kufanya bishara kwenye soko la zamani ambako nako pia wana sehemu za Biashara.
  Rais  Dkt Magufuli akiendelea kumsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo wakati akielezea changamoto za Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabili wilaya hiyo wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016
  Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo akiandika maagizo ya Rais Dkt. Magufuli kuhusiana na  Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko ambapo ameamuru huduma hizo zifunguliwe Jumatatu bila kukosa. Rais ameitaka SUMATRA ihakikishe stendi hiyo inaanza kufanya kazi Jumatatu. Pia ameiagiza halmashauri ya wilaya hiyo kuhakikisha wafanyabishara waliohodhi sehemu za biashara bila kuzitumia katika soko jipya wathibitiwe mara moja.
 Wananchi wa Igunga wanalipuka kwa furaha na Mzee huyu anatoa  noti ya shilingi 10,000/- akitaka kumtuza  Rais Dkt Magufuli kwa kuweza kutatua changamoto za Stendi ya mabasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabiri wilaya ya Igunga wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016
Rais Dkt Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipokea zawadi ya mchele wa grade One kutoka uongozi wa wilaya ya Igunga  wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016