WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU WILAYANI ILEMELA WANUFAIKA NA KITUO CHA SHALOOM CARE HOUSE.

January 08, 2016
Na:Binagi Media Group
Zaidi wa Wanafunzi 400 wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, wamenufaika na msaada wa vifaa vya elimu vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni Kumi ili kuwawezesha hao kupata elimu.

Msaada huo umetolewa na Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika Mazingira Magumu na hatarishi cha Shaloom Care House kilichopo katika Manispaa hiyo.

Mratibu wa Kituo hicho Msafiri Wana amebainisha kwamba wanafunzi 221 wa shule za Msingi na wanafunzi 187 wa shule za Sekondari, wamenufaika na msaada huo ambao ni pamoja na madaftari, kalamu na sare za shule ambapo thamani yake ni shilingi Milioni Kumi na Laki Tano.

Baadhi ya wanafunzi waliopokea msaada huo wametoa shukrani zao kwa Kituo hicho ambapo pia wamewasihi wanafunzi wengine ambao wazazi ama walezi wao hawana uwezo wa kuwahudumia mahitaji ya kielimu, kufika katika kituo hicho ili wapate usaidizi huo.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo amewataka Wakuu wa Shule za Msingi, Sekondari pamoja na Maafisa Elimu kusimamia vema matumizi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni Mia Tisa Tisini na Tisa, Laki Tatu na Elfu sabini na Sita zilizotolewa na serikali katika Mkoa wa Mwanza kwa mwezi huu ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake ya kutoa elimu bure nchini.
Bonyeza PLAY Hapa Chini Kusikiliza
TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MOROCCO

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MOROCCO

January 08, 2016
Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa kocha msaidizi wa Taifa Stars Hemed Suleiman “Morocco” kufutia kifo cha baba yake mzazi Suleiman Ally Hemed kilichotokea juzi kisiwani Zanzibar.

Katika salamu hizo za rambirambi, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wapo pamoja na familia ya marheemu katika kipindi hiki kigumu cha maombeloezo.

Aidha pia TFF imetuma rambirambi (ubani) wa shilingi laki mbili (200,000) kwa familia ya kocha Hemed Moroco kufuatia kifo cha baba yake Suleiman Ally.

Mazishi ya marehmu Suleiman Ally Hemed mefanyika jana jioni mjini Zanzibar
HONGERA KWA TUZO SAMATTA.

HONGERA KWA TUZO SAMATTA.

January 08, 2016

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Jamal Malinzi amempongeza mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe ya Congo DR kwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani.
Samatta ameshinda tuzo ya mchezaji bora kwa wachezaji wanaocheza Afrika baada ya kwashinda Robert Kidiaba (Congo DR) alieshika nafasi ya pili na Bounedjah Baghdad (Algeria) aliyeshika nafasi ya tatu.
Kwa kushinda tuzo hiyo, Samatta amekua mchezaji wa kwanza kwa ukanda wa Afrika Mashariki kushinda tuzo kubwa barani Afrika.
Pamoja na kushinda tuzo hiyo, Samatta pia amejumuishwa katika kikosi bora cha wachezaji wa Afrika kwa mwaka 2015 sambamba na Robert Kidiaba (Congo DR), Sergie Aurier (Ivory Coast), Aymen Abdenmor (Tunisia), Mohamed Meftah (Algeria), Sadio Mane (Senegal), Yaya Toure (Ivory Coast), Yacine Ibrahim (Algeria), Andrew Ayew (Ghana), Mbwana Samatta (Tanzania), Pierre-Emercik Aubameyang (Gabon) na Baghdad Bounedjah (Algeria).
Mshambuliaji Mbwana Samatta alieyambatana na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine wanatarajia kuwasili nchini leo saa 8 usiku kwa shirika la ndege la Ethiopia.

MBUNGE WA JIMBO LA NYAMAGANA KUKOMALIA UJENZI WA MAEGESHO JJINI MWANZA.

January 08, 2016
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza Stanslaus Mabula (CCM, ameahidi kushughulikia suala la ujenzi wa maegesho ya magari makubwa ya mizigo nje ya jiji la Mwanza ili kuzuia magari hayo kuingia katikati ya jiji.

Akizungumza ofisini kwake hii leo, Mabula amebainisha kuwa upo mpango wa kujenga maegesho hayo katika maeneo yaliyo nje ya Jiji la Mwanza, hatua ambayo itasaidia magari hayo kutoingia katikati ya Jiji na hivyo kuondoa malalamiko yaliyopo kutoka kwa madereva wa magari madogo ya mizigo wanaolalamikia uingiaji wa magari makubwa ya mizigo katikati ya jiji.

Ameyataja maeneo yanayotarajiwa kujengwa maegesho hao kuwa ni Buhongwa pamoja na Igoma na kwamba baada ya ujenzi wake kukamilika, magari yote makubwa ya mizigo hayataruhusiwa kuingia katikati ya Jiji.

Mabula ambae alikuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza katika uongozi uliomalizika mwaka jana, amebainisha kuwa utekelezaji wa ujenzi wa maegesho hayo unatarajiwa kufanyika kwa uharaka zaidi ambapo amewahimiza wawekezaji mbalimbali kujitokeza ili kushirikiana na halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa ajili ya kufanikisha ujenzi huo.

Suala la magari makubwa kuingia katikati ya Jiji la Mwanza huku yakiwa na mizigo, linalalamikiwa na madereva wa magari madogo ya mizigo kwa kile wanachoeleza kuwa wanaingiliwa katika shughuli ambazo wao wangezifanya na hivyo kujiingia kipato ambapo wameiomba halmashauri ya Jiji la Mwanza kutoruhusu magari hayo kuingia katikati ya Jiji.
Bonyeza PLAY Hapa chini Kusikiliza 

Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula.
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula akiongea na wanahabari ofisini kwake.