AINGIA KANISANI NA BASTOLA YANYE RISASI 8-KISARAWE...POLISI WA MKAMATA

April 05, 2015

Hofu‬ imewakumba waumini wa ‪Kanisa‬ ‪Katoliki‬ la Mtakatifu Stephano, ‪‎Kisarawe‬ mkoani ‪‎Pwani‬ katika ibada ya Ijumaa Kuu baada mtu mmoja kukamatwa katikati ya ibada ya Ijumaa Kuu akiwa na bastola yenye risasi nane.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka kwa waumini na kuthibitishwa na polisi, mwanaume huyo ambaye si muumini wa kanisa hilo anadaiwa kutaka kufanya uhalifu kanisani hapo na alikamatwa baada ya waumini kushtukia mienendo yake isiyo kuwa ya kawaida.

WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA AFIWA NA MKWEWE

April 05, 2015

Spika wa Bunge Anne Makinda akitoa pole kwa familia ya Marehemu akiwemo mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda (kulia) ambaye alifiwa na baba yake Mzazi, Mzee Abdallah Rehani , Nyumbani kwa marehemu,Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015 . Wengine pichani ni ndugu wa karibu wa Mama Pinda.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa katika mazishi ya babamkwe wake yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015. Kushoto ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad.
Waombolezaji wakisoma dua ya kumwombea marehemu Abdallah Rehani, Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Mzee Abdallah Rehani nyumbani kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akimpa pole Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika mazishi ya baba mzazi wa mkewe, Marehemu Mzee Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam, Aprili4, 2015.
Waombolezaji wakizika mwili wa baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda , Marehemu Abdallah Rehani kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam, Aprili 4, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika mazishi ya Baba Mkwe wake , Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad akishiriki katika mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akishiriki katika mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad Slaa akishiriki katika mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aorili 4, 2015.
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali walioshiriki katika mazishi ya Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa rais wa Zanziba Seif Sharif Hamad wakitoka kwenye eneo la makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam baada ya mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Marehemu Abdallah Rehani Aprili 4, 2015. Kushoto ni Waziri Mkuu, Mstaafu, Frederick Sumaye na mwenye koti jeusi katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi.(Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)

WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA AFIWA NA MKWEWE

April 05, 2015

Spika wa Bunge Anne Makinda akitoa pole kwa familia ya Marehemu akiwemo mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda (kulia) ambaye alifiwa na baba yake Mzazi, Mzee Abdallah Rehani , Nyumbani kwa marehemu,Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015 . Wengine pichani ni ndugu wa karibu wa Mama Pinda.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa katika mazishi ya babamkwe wake yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015. Kushoto ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad.
Waombolezaji wakisoma dua ya kumwombea marehemu Abdallah Rehani, Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Mzee Abdallah Rehani nyumbani kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akimpa pole Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika mazishi ya baba mzazi wa mkewe, Marehemu Mzee Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam, Aprili4, 2015.
Waombolezaji wakizika mwili wa baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda , Marehemu Abdallah Rehani kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam, Aprili 4, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika mazishi ya Baba Mkwe wake , Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad akishiriki katika mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akishiriki katika mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad Slaa akishiriki katika mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aorili 4, 2015.
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali walioshiriki katika mazishi ya Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa rais wa Zanziba Seif Sharif Hamad wakitoka kwenye eneo la makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam baada ya mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Marehemu Abdallah Rehani Aprili 4, 2015. Kushoto ni Waziri Mkuu, Mstaafu, Frederick Sumaye na mwenye koti jeusi katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi.(Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)

MGAMBO SHOOTING YAICHAPA POLISI MORO BAO 4-0

April 05, 2015
NA MWANDISHI WETU,TANGA.

USHINDI wa mabao 4-0 hii leo umetosha kabisa kuifanya Mgambo Shooting ya Tanga kunyakua pointi tatu zote muhimu kwenye mechi ya Ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Polisi Morogoro mchezo uliochezwa uwanja wa CCM Mkwakwani.

Viashirio vya ushindi huo vilianza kuonekana mwanzo wa mtanange huo ambapo Mgambo Shooting waliingia uwanjani hapo wakiwa na hari mpya katika mechi hiyo iliyokuwa na patashika ya aina yake.

Bao la kwanza la Mgambo shooting limefungwa na Full Maganga dakika ya 31  baada ya kumalizia faulu iliyopigwa na Mohamed Samata baada ya mchezaji wa polisi Moro Labani Kambole kumfanyia madhambi Malimi Busungu.

Bao la Pili limefungwa na Malimi Busungu baada ya kumalizika krosi iliyopigwa na Fully Maganga dakika 38 na kutinga wavuni na mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika mgambo 2-0,Polisi .

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo katika dakika ya 71 Mgambo waliongeza bao la tatu lililoweka kimiyani na Malimi Busungu huku Salim Azizi Gilla akiipatia Mgambo bao la nne na kuhitimisha karamu hiyo ya mabao


MAVETERAN KUCHUKUA KESHO KATIKA BONANZA VIWANJA VYA POPATLALY TANGA.

April 05, 2015
Katibu Mkuu wa Timu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe akiwaonyesha waandishi wa habari jana kombe ambalo litashindaniwa katika bonanza la Maveteran litakalofanyika Jumatatu likishirikisha timu saba,kushoto ni Katibu Msaidizi wa timu hiyo,Ramadhani Sadiki na kulia ni Nahodha wa timu hiyo Thomas Semdoe

Katibu Mkuu wa Timu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe akiwaonyesha waandishi wa habari jana medali ambazo watapewa washindi katika bonanza la Maveteran litakalofanyika Jumatatu likishirikisha timu saba,kushoto ni Katibu Msaidizi wa timu hiyo,Ramadhani Sadiki na kulia ni Nahodha wa timu hiyo Thomas Semdoe


JUMLA ya timu saba kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini zinatarajiwa kushiriki katika bonanza la Maveteran ambalo linatarajiwa kufanyika kesho(Leo) Jumatatu ya Aprili 6 mwaka huu kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlaly mjini hapa.
Akizungumza jana, Katibu wa Klabu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe alisema ambao ndio waandaaji wa bonanza hilo alisema kuwa litashirikisha michezo mbalimbali.

Katibu huyo alizitaja timu hizo kuwa ni Zanzibar Veteran,Morogoro
Veteran,Mandingo Veteran,Disuza SC,Mango Garden Veteran ya  Dar es Salaam,Tanga Middle Age Veteran na Kitambi Noma ya Dar es Salaam.

Aliitaja michezo ambayo itafanyika siku hiyo kuwa ni Mpira wa Miguu, Kurusha Tufe, Kuvuta Kamba na Kukimbiza Kuku ambapo bingwa atazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo Medali na kombe.

Aliongeza kuwa malengo kuu ya bonanza hilo ni kukuza vipaji vya soka sehemu ya kazi na kuendeleza undugu na kutangaza biasha pamoja na kuweka mahusiano mazuri na wafanyakazi wengine.

Aidha alisema wanamshukuru mdau wa michezo mkoani hapa,Yanga Omari kwa hatua yake nzuri ya kulidhamini bonanza hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa.

  “Tunamshukuru sana mdau huyu kwa kuona umuhimu wa jambo hilo na kulifadhili lakini tunapenda kuwataka wadau wengine wajitokeze kulifadhili bonanza hili “Alisema Katibu huyo.

Bonanza hilo litaanza saa mbili asubuhi ambapo pia kutakuwa na mchezo wa kushindania kucheza mziki ambapo washindi wote watakabidhiwa zawadi na mgeni rasmi, Khalid Abdallah ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la soka nchini (TFF).

MAGWIJI WA KLABU YA BARCELONA WAANZA KUWASILI NCHINI

April 05, 2015

Nguli wa soka wa timu ya taifa ,Uholanzi na vilabu vya Ajax na Barcelona,Johan Cruyff (Kulia) akiongozana na mwenyeji wake,Rayco Garcia mara baada ya kuwasili katika uwanja a ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA)


Dixon Busagaga (Kushoto) wa Globu ya Jamii na Busagaga's Orijino Blog akiwa katika picha ya pamoja na waratibu wa ziara hiyo ya magwiji wa Barcelona.


Mratibu wa ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona nchini ,Royco Garcia ,(kulia) akiwa na mdau wa soka wa mkoa wa Kilimanjaro na Mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Hai,Harold Kifunda wakati wa mapokezi ya gwiji wa soka wa timu ya taifa ya Uholanzi na vilabu vya Ajax na Barcelona.


Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii akizungumza jambo na mratibu wa ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona nchini ,Royco Garcia ,uwanja wa ndege wa Kimatifa wa Kilimanjaro  wakati wa ujio wa gwiji wa soka wa timu ya taifa ya Oholanzi na vilabu vya Ajax na Barcelona, Johan Cruyff.


Na Dixon Busagaga wa Busagaga's Orijino Blog..

MCHEZAJI wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi na vilabu vya ,Ajax na Balcelona,gwiji Johan Cruyff amewasili jana majira ya saa 4:45 za asubuhi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ndege ya shirika la ndege la Qatar Airways.

Baada ya kuwasili uwanjani hapo ,Cruyff akiwa ameambatana na familia yake alipokelewa na Rayco Garcia ,mratibu wa ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona ya nchini Hispania watakao cheza mechi ya kirafiki dhidi ya wakongwe wa soka hapa nchini jumamosi ijayo.

Akizungumza na waandishi wa habari uwanjani hapo,Cruyff alisema anafurahi kufika Tanzania kwa mara ya kwanza na kwamba amefurahia hali ya hewa ya Joto ukilinganisha na nchi anayotoka ambayo kwa sasa ni msimu wa baridi.

Alisema ana matarajio makubwa baada ya kukanyaga ardhi ya Tanzania ikiwemo kuona wanyama wa aina mbalimbali katika hifadhi ya taifa ya Serengeti pamoja na kutembelea fukwe za bahari katika kisiwa cha Zanzibar kabla ya mchezo huo wa kirafiki.

“Nasikia furaha kufika Tanzania,na hali ya hewa ni nzuri,hali  ya joto,tunategemea kutembelea maeneo mengi ya vivutio ,tunaenda kutizama wanyama katika hifadhi ya Serengeti na baadae kutembea fukwe huko Zanzibar,tunategemea kuona vitu vingi vizuri.”alisema Cruyff.

Kuhusu mchezo wa Jumamoshi ,Cruyff alisema mashabiki wategemeee burudani toka kwa wakongwe hao wa Barcelona na kwamba mchezo huo hautakuwa wa ushindani isipokuwa wataonesha burudani ambayo ni matarajio ya wengi.

“Kitu cha kwanza ni kwamba mashabiki watapata Burudani,hatutacheza ili kushinda ingawaje tutapenda kushinda ,lakini kikubwa ni kutoa burudani kwa mashabiki,wafike tu uwanjani kufurahia mchezo”alisema Cruyff.

Cruyff ambaye ni mshindi mara tatu wa tuzo ya Ballon d’O ,1971,1973  na 1974 aliwataka wachezaji wa Tanzania kujituma katika mazoeizi ni kuzingatia maelekezo ya walimu ili kujenga morali ya timu na wachezaji kwa ujumla.

“Naweza sema kwa wachezaji pekee ,wanapaswa kufanya mazoezi kwa bidii,wajaribu kujiweka vizuri kila mara,na kitu kizuri katika michezo ni umoja wa timu ,mkishinda mnashinda pamoja na mkipoteza mnapoteza pamoja”alisema Cruyff.

Kuelekea katika Pambano la Jumamosi tayari waratibu wa mashindano hayo walisema maandalizi yanaendelea vizuri na kwamba baadhi ya wachezaji wa Barcelona watakao shuka uwanjani siku hiyo ni pamoja na wakongwe Edaga Davis ,Deco,Patrick Kluivert na Simao Sabrosa.

Historia ya Cruyff.
Mdachi Hendrik Johannes Cruijff alizaliwa Aprily 25 mwaka 1947 katika jiji la Amsterdam nchini Uholanzi, akajulikana kama Johan Cruyff ambaye hadi sasa ni meneja wa klabu ya Catalonia ya nchini Hispania.

Cruyff ni miongoni mwa wachezaji maarufu walio anzisha falsafa ya Total Football ambayo ilienea kote duniani hatua iliyopelekea kuwa mmoja wa wachezaji wenye sifa kubwa katika historia ya soka duniani.

Cruyff alikiongoza kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi katika fainali za kombe la dunia la Fifa ,mwaka 1974 ambapo alifanikiwa kupata zawadi ya mpira wa dhahabu baada ya kuibuka mchezaji bora wa mashindano.