AINGIA KANISANI NA BASTOLA YANYE RISASI 8-KISARAWE...POLISI WA MKAMATA
Hofu imewakumba waumini wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Stephano, Kisarawe mkoani Pwani katika ibada ya Ijumaa Kuu baada mtu mmoja kukamatwa katikati ya ibada ya Ijumaa Kuu akiwa na bastola yenye risasi nane.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka kwa waumini na kuthibitishwa na polisi, mwanaume huyo ambaye si muumini wa kanisa hilo anadaiwa kutaka kufanya uhalifu kanisani hapo na alikamatwa baada ya waumini kushtukia mienendo yake isiyo kuwa ya kawaida.
WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA AFIWA NA MKWEWE
Spika
wa Bunge Anne Makinda akitoa pole kwa familia ya Marehemu akiwemo mke wa
Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda (kulia) ambaye alifiwa na baba yake
Mzazi, Mzee Abdallah Rehani , Nyumbani kwa marehemu,Tabata jijini Dar
es salaam Aprili 4, 2015 . Wengine pichani ni ndugu wa karibu wa Mama
Pinda.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.
Wilbroad Slaa katika mazishi ya babamkwe wake yaliyofanyika kwenye
Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015. Kushoto ni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif
Hamad.
Waombolezaji
wakisoma dua ya kumwombea marehemu Abdallah Rehani, Baba Mzazi wa Mke
wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Mzee Abdallah Rehani nyumbani
kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akimpa pole Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda katika mazishi ya baba mzazi wa mkewe, Marehemu Mzee
Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es
salaam, Aprili4, 2015.
Waombolezaji
wakizika mwili wa baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ,
Marehemu Abdallah Rehani kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es
salaam, Aprili 4, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika mazishi ya Baba Mkwe wake ,
Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
Aprili 4, 2015.
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad akishiriki katika
mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu
Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili
4, 2015.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akishiriki katika
mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu
Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili
4, 2015.
Katibu
Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad Slaa akishiriki katika mazishi ya baba
mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani
yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aorili 4,
2015.
Baadhi
ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali walioshiriki katika mazishi
ya Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah
Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
Aprili 4, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa rais wa Zanziba Seif Sharif
Hamad wakitoka kwenye eneo la makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
baada ya mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Marehemu Abdallah
Rehani Aprili 4, 2015. Kushoto ni Waziri Mkuu, Mstaafu, Frederick Sumaye
na mwenye koti jeusi katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,
Balozi Seif Iddi.(Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)
WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA AFIWA NA MKWEWE
Spika
wa Bunge Anne Makinda akitoa pole kwa familia ya Marehemu akiwemo mke wa
Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda (kulia) ambaye alifiwa na baba yake
Mzazi, Mzee Abdallah Rehani , Nyumbani kwa marehemu,Tabata jijini Dar
es salaam Aprili 4, 2015 . Wengine pichani ni ndugu wa karibu wa Mama
Pinda.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.
Wilbroad Slaa katika mazishi ya babamkwe wake yaliyofanyika kwenye
Makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015. Kushoto ni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif
Hamad.
Waombolezaji
wakisoma dua ya kumwombea marehemu Abdallah Rehani, Baba Mzazi wa Mke
wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu Mzee Abdallah Rehani nyumbani
kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Aprili 4, 2015.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akimpa pole Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda katika mazishi ya baba mzazi wa mkewe, Marehemu Mzee
Abdallah Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es
salaam, Aprili4, 2015.
Waombolezaji
wakizika mwili wa baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ,
Marehemu Abdallah Rehani kwenye Makaburi ya Segerea jijini Dar es
salaam, Aprili 4, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika mazishi ya Baba Mkwe wake ,
Marehemu Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
Aprili 4, 2015.
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad akishiriki katika
mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu
Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili
4, 2015.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi akishiriki katika
mazishi ya Baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, Marehemu
Abdallah Rehani kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aprili
4, 2015.
Katibu
Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad Slaa akishiriki katika mazishi ya baba
mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah Rehani
yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam Aorili 4,
2015.
Baadhi
ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali walioshiriki katika mazishi
ya Baba Mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda, Marehemu Abdallah
Rehani yaliyofanyika kwenye makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
Aprili 4, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa rais wa Zanziba Seif Sharif
Hamad wakitoka kwenye eneo la makaburi ya Segerea jijini Dar es salaam
baada ya mazishi ya baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Marehemu Abdallah
Rehani Aprili 4, 2015. Kushoto ni Waziri Mkuu, Mstaafu, Frederick Sumaye
na mwenye koti jeusi katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,
Balozi Seif Iddi.(Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)
MGAMBO SHOOTING YAICHAPA POLISI MORO BAO 4-0
USHINDI wa mabao 4-0 hii leo umetosha kabisa kuifanya Mgambo Shooting ya Tanga kunyakua pointi tatu zote muhimu kwenye mechi ya Ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Polisi Morogoro mchezo uliochezwa uwanja wa CCM Mkwakwani.
Viashirio vya ushindi huo vilianza kuonekana mwanzo wa mtanange huo ambapo Mgambo Shooting waliingia uwanjani hapo wakiwa na hari mpya katika mechi hiyo iliyokuwa na patashika ya aina yake.
Bao la kwanza la Mgambo shooting limefungwa na Full Maganga dakika ya 31 baada ya kumalizia faulu iliyopigwa na Mohamed Samata baada ya mchezaji wa polisi Moro Labani Kambole kumfanyia madhambi Malimi Busungu.
Bao la Pili limefungwa na Malimi Busungu baada ya kumalizika krosi iliyopigwa na Fully Maganga dakika 38 na kutinga wavuni na mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika mgambo 2-0,Polisi .
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo katika dakika ya 71 Mgambo waliongeza bao la tatu lililoweka kimiyani na Malimi Busungu huku Salim Azizi Gilla akiipatia Mgambo bao la nne na kuhitimisha karamu hiyo ya mabao
MAVETERAN KUCHUKUA KESHO KATIKA BONANZA VIWANJA VYA POPATLALY TANGA.
Katibu Mkuu wa Timu ya
Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe akiwaonyesha waandishi wa habari jana kombe ambalo
litashindaniwa katika bonanza la Maveteran litakalofanyika Jumatatu
likishirikisha timu saba,kushoto ni Katibu Msaidizi wa timu hiyo,Ramadhani
Sadiki na kulia ni Nahodha wa timu hiyo Thomas Semdoe
Katibu Mkuu wa Timu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe akiwaonyesha waandishi wa habari jana medali ambazo watapewa washindi katika bonanza la Maveteran litakalofanyika Jumatatu likishirikisha timu saba,kushoto ni Katibu Msaidizi wa timu hiyo,Ramadhani Sadiki na kulia ni Nahodha wa timu hiyo Thomas Semdoe
Katibu Mkuu wa Timu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe akiwaonyesha waandishi wa habari jana medali ambazo watapewa washindi katika bonanza la Maveteran litakalofanyika Jumatatu likishirikisha timu saba,kushoto ni Katibu Msaidizi wa timu hiyo,Ramadhani Sadiki na kulia ni Nahodha wa timu hiyo Thomas Semdoe
JUMLA ya timu saba kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini zinatarajiwa kushiriki katika bonanza la Maveteran ambalo linatarajiwa kufanyika kesho(Leo) Jumatatu ya Aprili 6 mwaka huu kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlaly mjini hapa.
Akizungumza jana, Katibu wa Klabu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe alisema ambao ndio waandaaji wa bonanza hilo alisema kuwa litashirikisha michezo mbalimbali.
Katibu huyo alizitaja timu hizo kuwa ni Zanzibar Veteran,Morogoro
Veteran,Mandingo Veteran,Disuza SC,Mango Garden Veteran ya Dar es Salaam,Tanga Middle Age Veteran na Kitambi Noma ya Dar es Salaam.
Aliitaja michezo ambayo itafanyika siku hiyo kuwa ni Mpira wa Miguu, Kurusha Tufe, Kuvuta Kamba na Kukimbiza Kuku ambapo bingwa atazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo Medali na kombe.
Aliongeza kuwa malengo kuu ya bonanza hilo ni kukuza vipaji vya soka sehemu ya kazi na kuendeleza undugu na kutangaza biasha pamoja na kuweka mahusiano mazuri na wafanyakazi wengine.
Aidha alisema wanamshukuru mdau wa michezo mkoani hapa,Yanga Omari kwa hatua yake nzuri ya kulidhamini bonanza hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa.
“Tunamshukuru sana mdau huyu kwa kuona umuhimu wa jambo hilo na kulifadhili lakini tunapenda kuwataka wadau wengine wajitokeze kulifadhili bonanza hili “Alisema Katibu huyo.
Bonanza hilo litaanza saa mbili asubuhi ambapo pia kutakuwa na mchezo wa kushindania kucheza mziki ambapo washindi wote watakabidhiwa zawadi na mgeni rasmi, Khalid Abdallah ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la soka nchini (TFF).
Akizungumza jana, Katibu wa Klabu ya Tanga Middle Age Veteran,Nuru Jumbe alisema ambao ndio waandaaji wa bonanza hilo alisema kuwa litashirikisha michezo mbalimbali.
Katibu huyo alizitaja timu hizo kuwa ni Zanzibar Veteran,Morogoro
Veteran,Mandingo Veteran,Disuza SC,Mango Garden Veteran ya Dar es Salaam,Tanga Middle Age Veteran na Kitambi Noma ya Dar es Salaam.
Aliitaja michezo ambayo itafanyika siku hiyo kuwa ni Mpira wa Miguu, Kurusha Tufe, Kuvuta Kamba na Kukimbiza Kuku ambapo bingwa atazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo Medali na kombe.
Aliongeza kuwa malengo kuu ya bonanza hilo ni kukuza vipaji vya soka sehemu ya kazi na kuendeleza undugu na kutangaza biasha pamoja na kuweka mahusiano mazuri na wafanyakazi wengine.
Aidha alisema wanamshukuru mdau wa michezo mkoani hapa,Yanga Omari kwa hatua yake nzuri ya kulidhamini bonanza hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa.
“Tunamshukuru sana mdau huyu kwa kuona umuhimu wa jambo hilo na kulifadhili lakini tunapenda kuwataka wadau wengine wajitokeze kulifadhili bonanza hili “Alisema Katibu huyo.
Bonanza hilo litaanza saa mbili asubuhi ambapo pia kutakuwa na mchezo wa kushindania kucheza mziki ambapo washindi wote watakabidhiwa zawadi na mgeni rasmi, Khalid Abdallah ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la soka nchini (TFF).
MAGWIJI WA KLABU YA BARCELONA WAANZA KUWASILI NCHINI
Nguli wa soka wa timu ya taifa ,Uholanzi na vilabu vya Ajax na Barcelona,Johan Cruyff (Kulia) akiongozana na mwenyeji wake,Rayco Garcia mara baada ya kuwasili katika uwanja a ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA)
Dixon
Busagaga (Kushoto) wa Globu ya Jamii na Busagaga's Orijino Blog akiwa
katika picha ya pamoja na waratibu wa ziara hiyo ya magwiji wa
Barcelona.
Mratibu
wa ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona nchini ,Royco
Garcia ,(kulia) akiwa na mdau wa soka wa mkoa wa Kilimanjaro na
Mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Hai,Harold Kifunda wakati wa
mapokezi ya gwiji wa soka wa timu ya taifa ya Uholanzi na vilabu vya
Ajax na Barcelona.
Dixon
Busagaga wa Globu ya Jamii akizungumza jambo na mratibu wa ziara ya
wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona nchini ,Royco Garcia ,uwanja
wa ndege wa Kimatifa wa Kilimanjaro wakati wa ujio wa gwiji wa soka wa
timu ya taifa ya Oholanzi na vilabu vya Ajax na Barcelona, Johan Cruyff.
Na Dixon Busagaga wa
Busagaga's Orijino Blog..
MCHEZAJI
wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi na vilabu vya ,Ajax na Balcelona,gwiji
Johan Cruyff amewasili jana majira ya saa 4:45 za asubuhi katika uwanja wa
ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ndege ya shirika la ndege la Qatar
Airways.
Baada
ya kuwasili uwanjani hapo ,Cruyff akiwa ameambatana na familia yake alipokelewa
na Rayco Garcia ,mratibu wa ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu ya
Barcelona ya nchini
Hispania watakao cheza mechi ya kirafiki dhidi ya wakongwe wa soka hapa nchini
jumamosi ijayo.
Akizungumza
na waandishi wa habari uwanjani hapo,Cruyff alisema anafurahi kufika Tanzania
kwa mara ya kwanza na kwamba amefurahia hali ya hewa ya Joto ukilinganisha na
nchi anayotoka ambayo kwa sasa ni msimu wa
baridi.
Alisema
ana matarajio makubwa baada ya kukanyaga ardhi ya Tanzania
ikiwemo kuona wanyama wa aina mbalimbali katika hifadhi ya taifa ya Serengeti
pamoja na kutembelea fukwe za bahari katika kisiwa cha Zanzibar kabla
ya mchezo huo wa kirafiki.
“Nasikia
furaha kufika Tanzania,na hali ya hewa ni nzuri,hali ya
joto,tunategemea kutembelea maeneo mengi
ya vivutio ,tunaenda kutizama wanyama katika hifadhi ya Serengeti na baadae
kutembea fukwe huko Zanzibar,tunategemea kuona vitu vingi vizuri.”alisema
Cruyff.
Kuhusu
mchezo wa Jumamoshi ,Cruyff alisema mashabiki wategemeee burudani toka kwa
wakongwe hao wa Barcelona
na kwamba mchezo huo hautakuwa wa ushindani isipokuwa wataonesha burudani
ambayo ni matarajio ya wengi.
“Kitu
cha kwanza ni kwamba mashabiki watapata Burudani,hatutacheza ili kushinda
ingawaje tutapenda kushinda ,lakini kikubwa ni kutoa burudani kwa
mashabiki,wafike tu uwanjani kufurahia mchezo”alisema
Cruyff.
Cruyff
ambaye ni mshindi mara tatu wa tuzo ya Ballon d’O ,1971,1973 na
1974 aliwataka wachezaji wa Tanzania
kujituma katika mazoeizi ni kuzingatia maelekezo ya walimu ili kujenga morali
ya timu na wachezaji kwa ujumla.
“Naweza
sema kwa wachezaji pekee ,wanapaswa kufanya mazoezi kwa bidii,wajaribu kujiweka
vizuri kila mara,na kitu kizuri katika michezo ni umoja wa timu ,mkishinda
mnashinda pamoja na mkipoteza mnapoteza pamoja”alisema
Cruyff.
Kuelekea
katika Pambano la Jumamosi tayari waratibu wa mashindano hayo walisema
maandalizi yanaendelea vizuri na kwamba baadhi ya wachezaji wa
Barcelona watakao shuka uwanjani siku
hiyo ni
pamoja na wakongwe Edaga Davis ,Deco,Patrick Kluivert na Simao
Sabrosa.
Historia ya
Cruyff.
Mdachi
Hendrik Johannes Cruijff alizaliwa Aprily
25 mwaka 1947
katika jiji la Amsterdam
nchini Uholanzi, akajulikana kama Johan
Cruyff ambaye hadi sasa ni meneja wa klabu ya Catalonia ya nchini
Hispania.
Cruyff ni miongoni mwa
wachezaji maarufu walio anzisha falsafa ya Total Football ambayo ilienea kote
duniani hatua iliyopelekea kuwa mmoja wa wachezaji wenye sifa kubwa katika
historia ya soka duniani.
Cruyff alikiongoza kikosi
cha timu ya taifa ya Uholanzi katika fainali za kombe la dunia la Fifa ,mwaka
1974 ambapo alifanikiwa kupata zawadi ya mpira wa dhahabu baada ya kuibuka
mchezaji bora wa mashindano.
Subscribe to:
Posts (Atom)