MOTO WAMWAKIA PROFESA TIBAIJUKA
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka. PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam/Mbeya. Viongozi
wa vyama vya siasa na wanaharakati wa masuala ya ardhi, wamesema
kuzomewa kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa
Anna Tibaijuka ni matokeo ya makosa yanayowafanywa na Serikali
kuwapendelea wawekezaji wa nje na kuwapuuza wananchi.
Kauli
hiyo imekuja siku moja baada ya Profesa Tibaijuka kuzomewa na wananchi
waliokerwa na kitendo cha kumruhusu mwekezaji kuendelea kumiliki shamba
la Kapunga, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya lenye ukubwa wa hekta 7,370.
Wananchi
hao walikasirishwa na kitendo cha Profesa Tibaijuka kubadili msimamo
wake awali wa kumpokonya ardhi mwekezaji huyo kwani mara ya kwanza
alishawaeleza viongozi wa vijiji kuwa serikali itawarudishia eneo lao.