January 09, 2014

MOTO WAMWAKIA PROFESA TIBAIJUKA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka. PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam/Mbeya. Viongozi wa vyama vya siasa na wanaharakati wa masuala ya ardhi, wamesema kuzomewa kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ni matokeo ya makosa yanayowafanywa na Serikali kuwapendelea wawekezaji wa nje na kuwapuuza wananchi.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Profesa Tibaijuka kuzomewa na wananchi waliokerwa na kitendo cha kumruhusu mwekezaji kuendelea kumiliki shamba la Kapunga, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya lenye ukubwa wa hekta 7,370.
Wananchi hao walikasirishwa na kitendo cha Profesa Tibaijuka kubadili msimamo wake awali wa kumpokonya ardhi mwekezaji huyo kwani mara ya kwanza alishawaeleza viongozi wa vijiji kuwa serikali itawarudishia eneo lao.

TUZO ZA MAKOCHA ZAJA MACHI 2014

January 09, 2014

Na Daud Julian, Morogoro 

TUZO ya makocha wa mpira wa miguu Tanzania ‘Tanzania Football Coaches Awards 2014’ inatarajiwa kutolewa mapema mwezi machi, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na TANGA RAHA BLOG, ofisa mtendaji wa tuzo hizo, Fredrick Luunga alisema lengo hasa ni kuthamini mchango wa makocha wazawa na wa kigeni katika kuendeleza mchezo wa soka hapa nchini.
Luunga alisema kwa miaka mingi, makocha wamekuwa wakifanya kazi hiyo katika mazingira magumu na wamekuwa hawathaminiwi vya kutosha kutokana na mchango wanaoutoa katika kupigania maendeleo ya mchezo huo.
Alisema, anaamini tuzo hiyo itakayokuwa ikitolewa kila mwaka, itasaidia kuibua ari mpya na kuwaongezea morali ya kufanya kazi makocha.

TFF YAISHAURI WILAYA YA HANDENI JUU YA UWANJA WA AZIMIO ULIOPO MJINI HUMO

January 09, 2014

 Msemaji wa TFF, Boniface Wambura, pichani.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

SHIRIKISHO la Soka nchini (TFF), limesema ili Uwanja uweze kutumiwa katika mechi za Ligi Kuu unahitajika kuandaliwa vizuri, ikiwa ni pamoja na kuwa na eneo zuri la kuchezea, uzio na maeneo ya kukaa kwa mashabiki na wahusika wengine.

Maneno ya TFF yanaweza kuwa majibu kwa Wilaya ya Handeni inayojipanga kuhakikisha uwanja wao wa Azimio uliyopo wilayani humo unaweza kutumiwa katika mechi za ligi kuu, kwa kupitia timu ya Mgambo Shooting yenye maskani yake Kabuku wilayani Handeni.
January 09, 2014

KWA MARA YA KWANZA QATAR KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2022 KATIKA MAJIRA YA BARIDI.

 KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amedai kuwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar 2022 haitafanyika mwezi Juni na Julai kama ilivyozoeleka badala yake itafanyika majira ya baridi. Kumekuwa na mijadala mikubwa toka Qatar walipopewa uenyeji wa kuandaa michuano hiyo Desemba mwaka 2010 kutokana na hofu ya joto kali katika majira ya kiangazi katika ukanda huo ambalo linaweza kuwa hatari kwa wachezaji na mashabiki watakaohudhuria. Akihojiwa na Radio France, Valcke amesema badala ya kufanyika kipindi hicho michuano hiyo inaweza kusogezwa mbele ya kati ya Novemba 15 na Januari 15. Valcke aliendelea kudai kuwa kama michuano hiyo ikichezwa kati ya Novemba 15 na kumalizika Desemba muda huo hali ya hewa itakuwa nzuri tofauti na Juni na Julai.

BASI LA KAMPUNI YA MTEI LACHOMWA MOTO NA WANANCHI WENYE HASIRA BAADA YA KUGONGA BODABODA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WATATU

January 09, 2014

Basi la kampuni ya Mtei Express T.742 ACU linavyoonekana baada ya kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali wa kitongoji cha Ijanuka kijiji cha Kisasida manispaa ya Singida,kutokana na kugonga pikipiki aina ya sky go T.368 BXZ na kuua abiria watatu waliokuwa kwenye pikipiki hiyo.Basi hilo lilikuwa likitoka Singida mjini kuelekea Arusha mjini jana (9/1/2014).Picha na Nathaniel Limu





January 09, 2014
*RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA MNARA WA KUMBUKUMBU YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kuweka jiwe la msingi Ujenzi   wa Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar, katika viwanja vyaKisonge Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka kwa Bw. Habib Nuru mshauri wa Ujenzi wa kampuni ya Hab Consult ya Dar es Salaam,baada ya kuweka jiwe la msingi Mnara wa kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisonge,Michenzani Mjini Unguja leoasubuhi.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi   Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisonge,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.
January 09, 2014
NOAH YAUA WAWILI MKATA NA KUJERUHI NANE 
Na Oscar Assenga, Handeni.
WATU wawili wamefariki dunia hapo hapo na wengine nane kujeruhiwa
baada ya gari aina ya  Noah walilokuwa wamepanda kutaka kulipita gari
lililkuwa mbele yake na kukutana na gari lori aina ya Volvo na
kugongana uso kwa uso na kusababisha vifo hivyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Costastine Massawe  athibitisha
kutokea tukio hilo leo na kueleza tukio hilo lilitokea majira ya saa
tano mchana wakati gari hilo aina ya Noah T266 AXZ lililokuwa
likitokea Kabuku kwenda Mkata ambapo lilipofika eneo la kwamgogo ndio
lilipotaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na ndipo alipkutana na
lori aina ya  Volvo na kugongana nalo.

Massawe amtaja dereva wa gari aina ya Noah aliyesababisha ajali hiyo
kuwa ni Abdallah Selehe (60) mkazi wa kata ya Hale wilayani Korogwe
mkoani Tanga ambaye alikimbizwa kwenye hospitali ya Mkata Handeni
akiwa hajitambui akiwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi.

Aliwataja watu waliofariki dunia katika ajali hiyo kuwa ni wanawake
wawili ambao walikuwa miongoni mwa abiria waliokuwepo kwenye gari hilo
aina ya Noah ambapo kwa mujibu wa kamanda masawe majina yao haya
kuweza kupatikana mara moja.

Kamanda Massawe alisema chanzo cha ajili hiyo ni dereva za gari hilo
aina ya Noah kutaka kulipita gari lililokuwa mbele yake kwenye kona na
ndio ambapo alipokutana uso kwa uso na lori hilo na kusababisha ajali
hiyo.

    "Ajali nyingi zinatokea kutokana na madereva kutokuwa makini kwani
wengi wao wanasababisha ajali hizo kwa kutaka kuyapita magari yaliyopo
mbele yao bila kufikiria kufanya hivyo ni kukiuka sheria za usalama
barabarani "Alisema Kamanda Massawe.

Aidha kamanda  Massawe alitoa wito madereva mkoani Tanga kutii sheria
bila kuruti kwa kufuata sheria za usalama barabarai na kuwataka abiria
kuacha kushabikia mwendokasi badala yake watoe taarifa kwa jeshi hilo
ili hatua kali ziweze kuchukuliwa zidi yao

ABIRIA ZAIDI YA 2000 WANAOTUMIA USAFIRI WA TRENI WAKWAMA MKOANI DODMOA.

January 09, 2014


Na Omary Mlekwa aliyekuwa Dodoma
ZAIDI ya Abiria elfu mbili waliokuwa wanasafiri kutoka mkoani Kigoma kuelekea mikoani wamekwama jana kusafiri kwa saa tisa katika mkoani Dodoma  hali iliopelekea abiria hao kuandamana hadi ofisi ya mkuu wa mkoa  kutafuta msaada
Imedaiwa kuwa abiria hao ambao walikuwa wakielekea jijini Dar es Salaamu walitumia zaidi ya  wiki mbili njia waliamua kuandama hadi ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dodoma mara baada ya kufika kaituo cha mamala yarely mkoani hapa na kupta taarifa kuwa hawaweze kuendelena safari kutokana na miundombinu ya Treli  
Wakizungumza kwa jazba mbele ya mkuuu wa mkoa wa Dodoma Dkt Rehema Nchimbi baadhi ya abairia walisema wameanza safari tangu Januari 2 mwaka huu lakini mpaka sasa hawajaweza kufikia jijini Dar es Saalamu  na kila siku wanmekuwa wakidanganywa na uongozi wa shirika hili huku wakiendelea kuteseka njiani