MBARAWA AMKABIDHI NAIBU SPIKA MWONGOZO WA WATUMIAJI WA HUDUMA NA BIDHAA ZA MAWASILIANO

February 08, 2018
  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akionesha Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma Februari 8, 2018.

  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto) akimkabidhi Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa pili kulia) Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa niaba ya Wabunge. Wakishuhudia  watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano Mhandisi Anjelina Madete na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma Februari 8, 2018.

  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) akimweleza Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa kwanza kulia) umuhimu wa Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa Wabunge mara baada ya kumkabidhi Mwongozo huo kwa niaba ya Wabunge ili waweze kusoma, kuelewa na kuelimisha wananchi namna ya kutumia vema huduma na bidhaa za mawasiliano nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma.

  Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa kwanza kulia) kuhusu Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma
UNICEF YATOA MSAADA WA LAPTOP 200 KWA WIZARA YA AFYA ZANZIBAR

UNICEF YATOA MSAADA WA LAPTOP 200 KWA WIZARA YA AFYA ZANZIBAR

February 08, 2018

1a 1b 1d
Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo kushoto na akikabidhiwa Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kutoka kwa Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar
2
Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kwa Wizara ya Afya Zanzibar ili zisaidie kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar
3
Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kutoka shirika la UNICEF ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.
Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar
……………..
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limetoa msaada wa Komputa aina ya Laptop 200 kwa Wizara ya Afya ya Zanzibar ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.
Laptop hizo zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 400 zimetolewa ikiwa ni mwendelezo wa UNICEF kuiunga mkono Serikali katika kuimarisha huduma za matibabu hasa ya akinamama na watoto.
Akikabidhi Msaada huo katika Ukumbi wa Wizara hiyo Mnazi mmoja Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin amesema upatikanaji wa taarifa sahihi ni jambo muhimu linalofaa kupewa kipaumbele.
Amesema uwepo wa taarifa sahihi za Wajawazito na watoto huisaidia Serikali kujua idadi ya ongezeko la watu wake hali inayopelekea kupanga mipango vyema ya matibabu kulingana na idadi ya watu husika.
Amewataka Watendaji kwa ujumla kuunga mkono juhudi zinazotolewa na UNECO ili kuhakikisha afya za Watoto na Wajawazito zinaimarika.
Francesca ameongeza kuwa Shirika hilo la UNICEF litaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika juhudi zake za kimatibu na kuipongeza Srikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kutoa matibabu bure kwa wananchi wake.
Amefahamisha kuwa Zanzibar inapiga hatua mbele kwa upande wa Matibabu na kupongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuwashajiisha Wajawajizito kushiriki huduma hizo muhimu katika maisha yao. “Zanzibar zaidi ya asilimia 99 ya Wajawazito hushiriki katika Kliniki mbalimbali walau mara moja katika kipindi chao cha ujauzito. Hii inawezekana kwamba imechangiwa na juhudi za Serikali za kuyafanya matibabu bure”Alipongeza Francesca.
Kwa upande wake Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo amelishukuru Shirika la UNICEF kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar hasa katika sekta ya Afya.
Amemuahidi Mwakilishi huyo kwamba Msaada uliotolewa utatumika vyema ili kutimiza malengo ya Shirika hilo.
“Cha bure mara nyingi vitu vya bure havitunzwi vyema lakini Laptop hizi lazima tujitahidi kuutumia vyema..Laptop ziendelee kudumu na taarifa zinazohitajika zote kuanzia Dawa, Wajawazito, Watoto nakadhalika zote ziwekwe kwenye mfumo unaotakiwa”Alisema Waziri Kombo.
Waziri Kombo amesema Zanzibar inaendelea kupokea pongezi kutoka pande zote za Dunia kwa namna Serikali inavyojitahidi katika kutoa huduma bora za matibabu na hivyo msaada huo utazidi kuimarisha huduma hizo.
Laptop hizo zitagawiwa katika Vituo vyote vya matibabu Unguja na Pemba ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.
IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR
NAIBU WAZIRI KANGI LUGOLA ASIKITISHWA NA UTENDAJI WA DUWASA

NAIBU WAZIRI KANGI LUGOLA ASIKITISHWA NA UTENDAJI WA DUWASA

February 08, 2018

1
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Kangi Lugola akisalimiana na Uongozi wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA) alipofanya ziara ya kutembelea Ofisi hizo mjini Dodoma.
2
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Kangi Lugola akifafanua jambo alipokua akiongea na Wafanyakazi wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA) mjini Dodoma.
3
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Kangi Lugola akielekeza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA) David Palangyo wakati wa ziara ya kutembelea mabwawa ya kuhifadhi maji taka yanayotumiwa na DUWASA katika eneo la Swaswa mjini Dodoma.
4
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Kangi Lugola akiwa pamoja na Ujumbe toka DUWASA akikagua mabwawa ya kuhifadhi maji taka katika eneo la Swaswa na Ilazo mjini Dodoma ambapo alifanya ziara.
5
Sehemu ya mabwawa ya kuhifadhia maji taka inayotumiwa na Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA) katika eneno la Swaswa.
………………………………………………………………………….
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola hii leo amefanya ziara ya kushtukiza katika Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) ikiwa ni pamoja na kutembelea miundombinu ya Mamlamka hiyo.
Waziri Lugola amesikitishwa na namna Mamlaka hiyo ilivyoshindwa kuhimili kiasi cha maji taka yanayozalishwa katika Mji huo wa Dodoma na kutitiririka katika  makazi ya watu bila kutibiwa (Treated).
Katika ziara hiyo Naibu Waziri Kangi Lugola ameitaka Mamlaka hiyo kuja na mpango wa haraka wa kudhibiti maji hayo kwa lengo la kudhibiti usafi wa Mazingira na Ustawi wa Wananchi. “DUWASA mmekuwa mkitiririsha maji taka bila kuyatibu kwenye makazi ya watu, na kwenye kilimo cha mpunga, na mmepelekea baadhi ya watu kuyahama makazi yao.” Lugola alisisitiza.
Aidha Waziri Lugola ameitaka DUWASA kuhakikisha mabwawa mawili yaliyotelekezwa eneo la Swaswa yanakarabatiwa ili kuhimili kiwango cha uharibifu wa mazingira kabla ya tarehe 31/12/2018, na kuwataka kuimarisha ulinzi kuzunguka mabwawa yote ili watu wasichepushe maji katika mashamba yaliyopo pembezoni mwa mabwawa hayo.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Lugola ameitaka Mamlaka hiyo ya DUWASA kutumia gari ya matangazo na kushirikiana na viongozi wa Serikali za mitaa kutoa elimu kwa wananchi wa maeneo hayo juu ya athari ya matumizi ya  maji hayo machafu
DUWASA pia imetakiwa kupata kibali kutoka kwa Mamlaka ya Bonde la Maji ya Wami-Ruvu cha kutiririsha maji taka kwenye mazingira na kuhakikisha maji hayo yanatibiwa kwa kiwango kinachoruhusiwa kwa mujibu wa sheria na kufanya Tathmini ya Kimkakati ya Mazingira kuendana na ongezeko la watu.
Nae Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Bw. David Pallangyo amesema kuwa walipokea mabwawa hayo  kutoka kwa iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) mwaka 2002 na kukiri kutiririsha maji hayo bila kuyatibu katika mazingira.
Bw. Palangyo amebainisha kuwa Ofisi yake ina mkakati wa muda mrefu wa kujenga mabwawa makubwa zaidi eneo la Nzuguni ili kukidhi mahitaji ya sasa na kuendana na ongezeko la idadi ya watu baada ya Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi.

MSTAHIKI MEYA SELEBOSI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI LEO JIJINI TANGA.

February 08, 2018
 Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga(CCM) Alhaji Mustapha Mhina Selebosi akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani leo kwenye ukumbi wa Halmashauri kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudi Mayeji  kushoto ni Naibu Meya wa Jiji hilo,Mohamed Haniu
 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudio Mayeji akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo,Alhaji Mustapa Mhina Selebosi anayefuata ni Naibu Meya Mohamed Haniu na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga,Meja
 Naibu Meya Mohamed Haniu akizungumza katika kikao hicho kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi
Waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakifanya dua kabla ya kuanza kikao hicho
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia  na Naibu Mstahiki Meya Mohamed Haniu wakipitia taarifa mbalimbali wakati wa kikao hicho leo
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akisisitiza jambo kwenye kikao hicho kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji na kushoto ni Naibu Meya wa Jiji la Tanga ,Mohamed Haniu
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Hamisi Mkoba akipitia kabrasha wakati wa kikao hicho 
 Katibu wa CCM wilaya ya Tanga katika akifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa kikao hicho

 Baadhi ya waheshimiwa maduwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho kwa umakini
 Sehemu ya wataalamu katika halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho

 Diwani wa Kata ya Maweni (CCM) Calvas Joseph akiuliza swali katika kikao hicho
 Sehemu ya waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakiangalia makabrasha kabla ya kuanza kikao hicho

Sehemu ya wataalamu kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga wakiwa makini kufuatilia taarifa mbalimbali kulia ni Ramadhani Possi

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE WA SHIMUTA

February 08, 2018
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirikisho la Michezo la Mashirika  ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) mjini Dodoma.
Akizungumza baada ya kikao na Makamu wa Rais, Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi alisema wamekutana na Makamu wa Rais na kumkabidhi ripoti ya mashindano ya mwaka 2016-2017 na 2017-2018.
Pamoja na kumkabidhi Ripoti hiyo, pia walimueleza Makamu wa Rais ambaye ni Mlezi wa Shirikisho, changamoto na mipango mbali mbali ya kuboresha shirikisho hilo. Pichani Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi ambaye aliongozana na Uongozi na Wajumbe wa Shirikisho kukutana na Makamu wa Rais kwenye makazi yake, Kilimani mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe kutoka Shirikisho la Michezo la Mashirika ya umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania mara baada ya kumaliza mazungumzo kwenye makazi yake Kilimani, mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE WA SHIMUTA

February 08, 2018
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirikisho la Michezo la Mashirika  ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) mjini Dodoma.
Akizungumza baada ya kikao na Makamu wa Rais, Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi alisema wamekutana na Makamu wa Rais na kumkabidhi ripoti ya mashindano ya mwaka 2016-2017 na 2017-2018.
Pamoja na kumkabidhi Ripoti hiyo, pia walimueleza Makamu wa Rais ambaye ni Mlezi wa Shirikisho, changamoto na mipango mbali mbali ya kuboresha shirikisho hilo. Pichani Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi ambaye aliongozana na Uongozi na Wajumbe wa Shirikisho kukutana na Makamu wa Rais kwenye makazi yake, Kilimani mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe kutoka Shirikisho la Michezo la Mashirika ya umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania mara baada ya kumaliza mazungumzo kwenye makazi yake Kilimani, mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE WA SHIMUTA

February 08, 2018
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirikisho la Michezo la Mashirika  ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) mjini Dodoma.
Akizungumza baada ya kikao na Makamu wa Rais, Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi alisema wamekutana na Makamu wa Rais na kumkabidhi ripoti ya mashindano ya mwaka 2016-2017 na 2017-2018.
Pamoja na kumkabidhi Ripoti hiyo, pia walimueleza Makamu wa Rais ambaye ni Mlezi wa Shirikisho, changamoto na mipango mbali mbali ya kuboresha shirikisho hilo. Pichani Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bw. Khamis Mkanachi ambaye aliongozana na Uongozi na Wajumbe wa Shirikisho kukutana na Makamu wa Rais kwenye makazi yake, Kilimani mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe kutoka Shirikisho la Michezo la Mashirika ya umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania mara baada ya kumaliza mazungumzo kwenye makazi yake Kilimani, mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

DIAMOND NA HAMISA WAMALIZA TOFAUTI ZAO

February 08, 2018
Na Karama Kenyunko , Globu ya Jamii
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul “Diamond Platzum” mapema leo asubuhi amefika katika viunga vya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Ustawi wa Jamii kwenye mahakama ya watoto kwa ajili ya usuluhishi juu ya matunzo ya mtoto wake aliyezaa na mlimbwende Hamisa Mobeto.

Alianza kuingia Diamond akafuatiwa na Hamisa baada ya muda kidogo ambapo walikaa kwa zaidi ya saa moja.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza usuluhushi huo, Diamond alisema,
 
“Kiasi cha pesa tunavyoviandika kama kama hivi, tunazungumza tu, lakini watoto hawahitaji mahitaji mengi, wakati mwingine mtoto wako una uwezo wa kumpa hadi Shilingi milioni 100 na huwezi kusema simpi kwa sababu niliandikisha nitampa Laki Moja haimsaidii”.

Alisema wao kama wazazi wameweka mazingira mazuri ya kumlea mtoto wao kwa kadri ya uwezo wataokapata, kiasi kitakachomfanya akue katika malezi bora wakipata watakula nae wakikosa watalala

“Nyuma ya stori hii nimejifunza kwamba siyo kila mtoto ambaye haishi na baba au mama yake basi asiyeishi nae anatatizo nae, hata mi nimejifunza pia kwa mimi na baba yangu,kuna vitu wazazi wanavifanya vinakuwa siyo fresh,vinatengeneza story, mtoto baadae akikua hajui story ya nyuma anajua mzazi mmoja anamatizo akajua dingi noma lakini siyo tu”.

Aidha Diamond amesema ni vema wazazi wote wawili watumie busara kuangalia namna gani wanasuluhisha ugomvi hasa hasa pale wanapokuwa wameitilafiana, watumie busara kutafuta njia ya kusuluhisha bila kuwaumiza watoto

"Nitahakikisha mtoto wangu akue katika mazingira mazuri, asome kadri ya uwezo nitakaokuwa nao, kwani maisha ni kupanda na kushuka kuna wakati unakuwa hauna unasema leo mie sina basi mambo yanakuwa Bundasiliga leo mnakula mihogo maisha ndivyo yalivyo amesema Diamond.

Amesema, “Kiumakini hakukuwa na vita kati yetu sisi wawili, ila kwa upande wa mwenzangu kulikuwa na watu wanaingiza chuki ilimradi kutengeneza mazingira ya kumkomoa Diamond kitu ambacho tumeona hakimsaidii mtoto.

“Tumekubaliana na tumeyamaliza na tumeweka misingi mizuri ya kumlea mtoto wetu, kwani mwisho wa siku hata mahakama haiwezi kunambia nimlipe Milioni 5 nitaitoa wapi, nina kazi mie, Mahakama imenipa kazi au kuna mtu amenipa kazi...? au eti mtoto umjengee nyumba, ulinipa mie nyumba alisema Diamond.

Alipohojiwa baada ya kumalizika kwa usuluhishi, wakili wa Hamisa Mobeto,Walter Goodluck amesema, "leo tulikuja kwa usuluhishi na wamesuluhishwa Ila sasa wamesuluhishwa nini na nini hilo tutalijua badae", amesema

Novemba 10, mwaka jana na Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama hiyo upande wa watoto ya watoto, Devotha Kisoka, aliitupilia mbali kesi aliyofunguliwa Mobeto juu ya matunzo ya mtoto Prince Abdul kwa kuwa ilifunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.

Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine akiiomba matunzo ya mtoto.

Pia alikuwa akiiomba mahakama imuamuru Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.
Msanii wa Bongo Fleva, Nasbu Abdul ‘Diamond Platinumz’ akifika katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwaajili ya usuruhisho wa matunzo ya mtoto wao aliyezaa na Hamisa Mobeto.
Hamisa Mobeto akiwa kwenye mahakamani kisutu leo
Msanii wa Bongo Fleva, Nasbu Abdul ‘Diamond Platinumz’ akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoka ustawi wa jimii kwa ajili ya kwaajili ya usuruhisho wa matunzo ya mtoto wao aliyezaa na Hamisa Mobeto leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
 
Chanzo www.mtaakwamtaa.co.tz

WIZARA YA MALIASILI, ARDHI NA TAMISEMI KUAMUA HATMA YA MGOGORO WA PORI LA AKIBA MKUNGUNERO – DK. KIGWANGALLA

February 08, 2018


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi aliyekuwa akimunesha mpaka wa kijiji hicho na Pori la Akiba Mkungunero wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Na Hamza Temba - Kondoa, Dodoma
..........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla jana tarehe 7 februari, 2018 ametembelea Pori la Akiba Mkungunero katika Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma na kuwataka wananchi wanaozunguka pori hilo kusubiri uamuzi wa Serikali  utakaoshirikisha Wizara yake,  Wizara ya Ardhi na Tamisemi katika kujibu maombi yao ya kutaka kupewa sehemu ya ardhi katika pori hilo kwa ajili ya kuendesha shughuli za kibinadamu.

Dk. Kigwangalla ambaye aliongozana na Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, alitembelea vijiji vinne vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko na kufanya mikutano ya hadhara kwa ajili ya kujiridhisha na  kujifunza juu ya mgogoro uliopo baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero.

"Nimefika hapa leo kujifunza juu ya mgogoro huu, nimejionea hali halisi lakini pia nina maelezo ya wataalamu ambayo yapo kwenye maandishi naomba niende nikayasome, niyatafakari ili niweze kushauriana na wenzangu na mwisho wa siku tuweze kuja na suluhu ya namna ya kuondokana na changamoto ambazo zimekuwepo.

"Niwaombe sana wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhu ya mgogoro huu ni vema tukafuata sheria zilizopo, tuzingatie mipaka iliyowekwa ili tusiingie kwenye migogoro, lakini kwa sasa siwezi kwa namna yeyote ile kutamka neno la kujibu maombi ya mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na wananchi yaliyotolewa hapa leo.

"Kama Serikali tutakaa, Wizara yangu, Wizara ya Ardhi na Tamisemi ili tujue kiini cha mgogoro huu tufanye uamuzi kuwa ni maeneo gani yaongezwe katika hifadhi kwa ajili ya wananchi au ni vitongoji vipi vifutwe, tutaleta majibu, na jambo hili tutalifanya kwa uadilifu mkubwa bila kumuonea mtu ili kumaliza mgogoro huu," alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Awali akimkaribisha Waziri huyo kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Ikengwa, Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Ashatu Kijaji alisema kutokana na ukweli kuwa Serikali ya awamu ya tano inasikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi, ni vema Waziri huyo akatumia hekima na kuangalia uwezekano wa kuwapa wananchi hao Kilomita 12 za mraba kutoka kwenye hifadhi hiyo kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kibinadamu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi alisema mgogoro baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero ulinza mwaka 2006 kufuatia zoezi la kuanzishwa kwake  pamoja na lile na uwekagi wa vigingi vya mpaka  na vijiji jirani kutoshirikisha wananchi na viongozi wa halmashauri za vijiji hoja ambayo ilipigwa na Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso

Aidha alisema wananchi wa vijiji hivyo wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya kilimo na ufugaji, hivyo akamuomba Waziri huyo pamoja na Serikali kwa ujumla kutumia busara  kuwamegea wananchi wa vijiji hivyo eneo la Kilomita 12 za mraba kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

Naye Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso alisema Pori la Akiba Mkungunero lilianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 307 la mwaka 1996 baada ya kupandishwa hadhi kutoka Pori Tengefu. Alisema mchakato wa kupandisha hadhi pori hilo ulishirikisha wananchi na viongozi wa vijiji na wilaya ambapo mihutasari mbalimbali ilisainiwa.

Alisema pori hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazochochea mgororo huo ikiwemo kijiji kimoja cha Kisondoko  kusajiliwa kimakosa ndani ya hifadhi hiyo pamoja na malalamiko mbalimbali ya wananchi kuwa hawakushirikishwa kwenye uanzishwaji wa pori pamoja na madai mengine kuwa pori hilo limeingilia mipaka ya vijiji hivyo.

Pori la Akiba Mkungunero ambalo lina ukubwa wa Kilimita za Mraba 557.9 lina umuhimu mkubwa kiuchumi na kiikolojia kwa kuwa ni chanzo muhimu cha mto Tarangire ambao ni uhai wa hifadhi ya Taifa ya Tarangire na ikolojia nzima ya ziwa Manyara. Pori hilo pia ni sehemu ya mapito na mazalia ya wanyamapori pamoja na makazi ya wanyamapori adimu duniani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa muda mfupi baada ya kuwasili wilayana humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa ramani ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kulia) akiteja jambo na Meneja wa Pori la Akiba Mkungunero, Emannuel Bilaso wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi wakati wa ziara yake ya kikazi jana katika Pori la Akiba Mkungunero Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea mabango ya malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Kisondoko kuhusu Pori la Akiba Mkungunero na vijiji jirani wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko wilayani Kondoa jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na mmoja wa wahifadhi wa Pori hilo wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.