RAIS KIKWETE ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA AKIWA NA WAJUKUU

October 08, 2015
Keki iliyoandaliwa kwa ajili ya sherehe za miaka 65 ya kuzaliwa kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete na miaka 55 ya kuzaliwa mdogo wake Yusufu Mrisho Kikwete jana jioni jijini Dar es salaam. Rais Kikwete na mdogo wake walisherehekea siku zao za kuzaliwa kwa kukata na kula keki na wajukuu wao na wa jamaa, ndugu na marafiki waliowaalikwa kwenye sherehe hii fupi iliyojaa furaha na bashasha.
Keki
Wajukuu wakimchukua babu wakamwimbie na kukata naye keki
Mjukuu akiogoza wajukuu wenzie kumwimbia babu
Wajukuu wakimwimbia babu
Wajukuu wakimsaidia babu kupuliza mishumaa
Babu akikata keki huku wajukuu wakiisubiri kwa hamu
Wajukuu wakiendelea kusubiri keki
Babu akiwalisha wajukuu keki
Kila mjukuu alipata keki
Keki ya babu taaamuu.....
Mufti Mkuu wa Taanzania na wageni wengine waalikwa wakishuhudia babu akiwalisha keki wajukuu
Sasa ni zamu ya babu kulishwa keki na wajukuu
 "....We love you babu..."
Karibu keki babu...
Babu akiendelea kulisha keki wajukuu
Bibi, Mama Salma Kikwete, akimsaidia Babu kuhakikisha kila mjukuu kapata keki
Kila mjukuu anapata keki
Babu na bibi wakiendelea kuandaa keki
Selfie zilikuwepo pia

MWENYEKITI wa chama cha DP mchungaji Christopher Mtikila azikwa kijijini kwake Milo Wilaya ya Ludewa

October 08, 2015

MWENYEKITI wa chama cha DP mchungaji Christopher Mtikila amezikwa kijijini kwake Milo Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo.
Vilio vyatawala  huku aliyekuwa mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe na Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi  watao ya Moyoni wasema alikuwa kiungo mhimu katika Taifa . 

Wakati Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji  Mutungi  akiwataka watanzania hasa viongozi wa vyama vya siasa kumuenzi Mchungaji Mtikila kwa kuenzi Amani wakati huu wa kuelekea katika uchaguzi mkuu octoba 25 mwaka huu ,Filikunjombe asema mbali ya ukorofi wa Mtikila kwa kile alichokiamini ila kwake alikuwa ni mshauri mkubwa wa Ubunge wake katika jimbo la Ludewa.

Wakitoa salamu za rambi rambi wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika leo  kijijini kwake Milo Wilaya ya Ludewa ,Jaji Mutungi alisema kuwa katika enzi za uhai wake marehemu Mtikila alikuwa akisimamia kile anachokiamini.

Alisema kuwa mbali ya misimamo yake ya kusimamia alichokiamini bado alikuwa ni mtu wa kujenga hoja na ambae hakupenda kuhatarisha Amani ya nchi hakuwa anapenda njia za mkato katika kupata majibu ya kile asichokiamini.

" Njia za mkato marehemu hakupenda kabisa kwani hata Kama jambo la kutisha ambalo wengine huogopa yeye alikuwa tayari kwenda mahakamani kusaka Haki yake bila kuhatarisha Amani ya nchi Mimi nafikiri kila mmoja akafuata misingi yake katika kudai Haki bila kuvuruga amani naamini tutafanikiwa.
" Alisema kuwa kuna mapungufu yanaweza kujitokeza ila Jambo la msingi kila mmoja kutanguliza kwanza amani ya nchi badala kuipa kisogo Amani na kupenda machafuko katika nchi".
Hivyo aliwataka watanzania bila kujali itikadi zao za vyama kuendelea na siasa huku wakitanguliza Amani ya nchi.
Mbunge aliyemaliza muda wake wa jimbo la Ludewa ambae ni mgombea Ubunge wa jimbo hilo Bw Filikunjombe alisema kuwa pamoja na Mchungaji Mtikila enzi za uhai wake alisimamia jambo ambalo 
alikuwa akiamini ila kwake amekuwa msaada mkubwa katika ushauri wa kuwatumikia wananchi wa Ludewa .
Alisema Mchungaji Mtikila hakuwa tayari kumuunga mkono mbunge wa Ludewa ambae hakuwa msaada wa kimaendeleo kwa wananchi ila kwa upande wake alikuwa akimuunga mkono na hata kutosimamisha mgombea katika jimbo la Ludewa. 
" Mchungaji Mtikila hakuwa tayari kuungana na mbunge asiyefanya Kazi za maendeleo jimboni Ludewa ila kwangu alikuwa akiniunga mkono na hata kunipingeza kwa Kazi nzuri ..... Kicho chake ni pigo kubwa kwa Taifa hasa kwa wana Ludewa ambao tulijivunia sana uwepo wake"

Hata hivyo alisema njia pekee kwake ya kumuenzi Mchungaji Mtikila ni kuendelea kuwatumikia vema wananchi wa Ludewa kwa kuleta maendeleo zaidi Kama alivyohitaji katika uhai wake.
Filikunjombe alisema katika kuamini kwake na kusimamia anachokiamini hadi mauti inamkuta alikuwa akitetea kuwepo kwa nchi ya Tanganyika na ndio maana kazikwa na bendera ya Tanganyika na kudai kuwa hakuna na kosa kupigania Tanganyika kwani Tanganyika inahitajika.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr Rerema Nchimbi alisema kuwa Mkoa wa Njombe umepoteza kiongozi makini na kuwa katika kumuenzi ni vema kwa vyama vya siasa kuendesha kampeni za amani na utulivu zaidi na kuwa wakati taifa linaelekea katika uchaguzi mkuu ni vema kila chama kumuenzi Mtikila kwa kulinda Amani .
Naibu Katibu mkuu wa DP Taifa Abdul Mluya alisema kuwa suala la kifo cha mwenyekiti wake ni utata mtupu na bado wanaendelea kuchunguza.

Wakati huo huo Chopa ya Filikunjombe aliyotumia kufaria kwenda katika mazishi hayo iliwafanya wananchi kuacha kusikiliza Salam mbali mbali za viongozi na kukimbilia kutazama na kumlaki Mgombea huyo Ubunge jimbo la Ludewa.
 Mkuu  wa mkoa wa Njombe Dr Rehema Nchimbi kulia akiwa na Deo Filikunjombe mgombea  ubunge jimbo la Ludewa na mbunge aliyemaliza muda  wake katikati kushoto ni msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi leo  wakati wa mazishi ya Mchungaji Mtikila 
 Mchungaji Patrick Mgaya aliyekuwa  safari moja na marehemu Mtikila wa pili kulia akiwa katika mazishi hayo 
 Waombolezaji wakiwa msibani 

 Filikunjombe akitoa salamu zake wakati wa mazishi ya Mtikila 
 Wananchi wakimsikiliza Filikunjombe



 Filikunjombea akitoa mkono wa pole  kwa wafiwa  katikati ni mjane Mama Georgina  Mtikila 

 Filikunjombe akiwasili msibani kwa chopa 

 Jaji Francis Mutungi kushoto Bw MGaya na Askofu Mtetemela na Filikunjombe wakiwa msibani 
 Filikunjombe akijiandaa kubeba jeneza 

 Mjane  wa Mtikila  akiweka shada la maua 

KENYA-TANZANIA BUSINESS FORUM ON OCTOBER 6, 2015 IN NAIROBI, KENYA IN PICTURES

October 08, 2015
 Executive Director of Tanzania Investment Centre Ms. Juliet Kairuki welcomes the President of Republic of Kenya H.E. Uhuru Kenyatta to the Forum
 President of the Republic of Kenya  H.E. Uhuru Kenyatta arrives at the venue of the Kenya-Tanzania Business Forum. He is escorted by Kenyan Minister of Industrialization and Enterprise Development
 Kenyan Minister of Industrialization and Enterprise Development and Managing Director of Intercontinental Hotel, Nairobi welcome the President of the United Republic of Tanzania
 Ms Juliet Kairuki , CEO of Tanzania Investment Centre welcomes President of the United Republic of Tanzania HE. Dr Jakaya  Kikwete
 Their Excellencies Dr. Jakaya Kikwete and Uhuru Kenyatta enter the conference room
Permanent Secretary Ministry of Industry and Trade Mr Uledi Musa deliver his remarks
 The two Presidents stand at attention as Nationa Anthems are played

 President Jakaya Kikwete delivers his keynote address during the forum
 Godfrey Simbeye (CEO of the Tanzania Private Sector Foundation) extends a hand  to the Managing Director of Kenya Investment Authority Dr . Moses Ikiara
 From left, Juliet Kairuki CEO of Tanzania Investment Centre; Mr. Godfrey Simbeye (CEO of Tanzania Private Sector Foundation) and Dr Moses Ikiara (CEO of Kenya Investment Authority-Keninvest) take timr off for a souvenir photo during the forum
 CEO of Kenya Association of Manufacturers ( in red) Ms Phyllis Wakiaga and other delegates await the arrival of the Kenya and Tanzania Presidents at the forum. 


 Senior members of the Tanzanian delegation at the forum  
 Kenya Police Brass band play  the National Anthems during the business forum. They are also famous for playing Tanzanian top hits like Diamond's "You are my number one" to the surprise of many a Tanzanian listening to them
 Prominent Kenyan business moguls including  Great  Chris Kirubi the richest  business magnet in Kenya owning  virtually most of the companies in HACO industries, and Kenya Airways shareholder engage President Kikwete post delivery of his key note address
 Mr Geodfrey Simbeye Simbeye (CEO of TPSF) greets the President  of Kenya H.E. Uhuru Kenyatta in Nairobi
 Ms. Juliet Kairuki with the Permanent Secretary, Ministry of Trade and Industry from Tanzania Mr. Musa Uledi
 TIC’ EXD listens attentively to speech of the CEO of Kenya Investment Authority
 Kenyan investor seeks clarity on some issues from Executive Director of Tanzania Investment Centre.
Mrs Juliet Kairuki addressing the audience