SPIKA MAKINDA APONGEZWA, PINDA AFUNGA MKUTANI WA KUHIFADHI WANYAMAPORI

SPIKA MAKINDA APONGEZWA, PINDA AFUNGA MKUTANI WA KUHIFADHI WANYAMAPORI

November 09, 2014

unnamed
unnamed2Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwenye viwanja  vya  Bunge mjini Dodoma Novemba 7, 2014 katika tafrija  ya kumpongeza Spika kwa kuteuliwa kuwa Rais wa Mabunge ya  SADEC . Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Anna Abdallah na wapil kulia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela  Kairuki na kushoto ni Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dr. Pindi Chana. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed3Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Spika wa Bunge Anne Makinda  (kushoto) wakimsikiliza Naibu Waziri wa katiba na Sheria, Angela Kairuki  (katikati) alipotoa maelezo kuhusu zawadi ya picha  ambayo wabunge walimzawadia Spika Makinda katika tafrija ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa spika wa Mabunge ya SADEC iliyofanyia kwenye viwanja vya Bunge mjioni Dodoma Novemba 7, 2014.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) unnamed4Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Spika wa Bunge Anne Makinda  (kushoto) wakimsikiliza Naibu Waziri wa katiba na Sheria, Angela Kairuki  (katikati) alipotoa maelezo kuhusu zawadi ya picha  ambayo wabunge walimzawadia Spika Makinda katika tafrija ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa spika wa Mabunge ya SADEC iliyofanyia kwenye viwanja vya Bunge mjioni Dodoma Novemba 7, 2014.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) unnamed5Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu (kushoto) na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Arusha  ambako alifunga Mkutano wa kupiga vita ujangili wa wanayamapori  na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori uliofanyika mjini Arusha Novemba 8, 2014.(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed6 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza  na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu (wapili  kushoto) na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri (kulia) baada ya kufunga Mkutano wa kupiga vita ujangili wa wanayamapori  na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Mbunge wa Kahama, James Lembeli.Wapili kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Dkt Richard Sezibara(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed7 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza  na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu (wapili  kushoto) na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri (kulia) baada ya kufunga Mkutano wa kupiga vita ujangili wa wanayamapori  na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Mbunge wa Kahama, James Lembeli.Wapili kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Dkt Richard Sezibara(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Rais Kikwete afanyiwa upasuaji wa tezi dume Marekani, hali yake inaendelea vyema

Rais Kikwete afanyiwa upasuaji wa tezi dume Marekani, hali yake inaendelea vyema

November 09, 2014

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dkt. Jakaya
Mrisho Kikwete akizungumza na  Dkt.Edward Shaeffer wa hospitali ya
Johns Hopkins na Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi(kulia) baada
ya kuwasili katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore,
Maryland,  Marekani kwa upasuaji Jumamosi asubuhi. Upasuaji huo
uliochukua muda wa saa moja na nusu ulifanyika salama.(Picha na Fred Maro) unnamed2 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na daktari Bingwa
Mpasuaji Edward Shaeffer muda mfupi kabla ya kuingia kwenye chumba cha
upasuaji uliofanyika katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyopo
Baltimore Maryland Marekani Jumamosi asubuhi.Upasuaji huo uliochukua
muda wa saa moja na nusu ulifanyika salama.
…………………………………………………………………
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete alfajiri ya jana, Jumamosi, Novemba 8, 2014, alifanyiwa
upasuaji wa tezi dume (prostrate) katika Hospitali ya Johns Hopkins
iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.
Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya madaktari waliomfanyia
uchunguzi wa afya yake kujiridhisha kuwa Rais alikuwa anahitaji
matibabu ya aina hiyo.
Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha saa moja
unusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa. Hali ya Mheshimiwa
Rais Kikwete inaendelea vizuri, bado yuko wodini akiendelea kuwa chini
ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba.
Wananchi wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais Kikwete
kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.
Imetolewa na
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS, IKULU
DAR ES SALAAM,
NOVEMBA 9, 2014

Mh. Lowassa azindua helkopta ya kanisa la ufufuo na uzima

November 09, 2014

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono waumini Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima,Kawe jijini Dar es Salaam leo.Picha zote na Othman Michuzi.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwasili kwenye viwanja vya kawe lilipo Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima leo.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwa kwenye kwenye jukwaa kuu na mwenyeji wake,Ambaye ni Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,Mchungaji Josephat Gwajima (kushoto),Kawe jijini Dar es Salaam leo.Wengine pichani ni Askofu Eliud Isanje (wa pili kulia) na Mchungaji Elifuraha Laswai (kulia).
Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,Mchungaji Josephat Gwajima akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Helkopta iliyonunuliwa na Mchungaji huo kwa ajili ya kutoa huduma za kiroho.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwahutubia waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima,wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa Helkopta itakayotumiwa na Mchungaji huyo katika kazi zake za kiroho,hafla hiyo imefanyika leo kwenye viwanja vya Kawe,Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akijadiliana jambo na baadhi ya wachungaji waliohudhulia kwenye hafla hiyo.
wakielekea kwenye uzinduzi rasmi wa Helkopta.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Helkopta ya Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima (kulia kwa Mh. Lowassa).
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mtoto wa Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiiingia ndani ya Helkopta hiyo kuashiria kuizindua rasmi kwa safari mbali mbali za kihuduma ya kiroho,itakayotumiwa na Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiteta jambo na rubani wa Helkopta hiyo muda mfupi baada ya kuizindua.
Helkopta iliyozinduliwa ikipaa kuondoka uwanjani hapo na baadae kurudu mara baada ya kuzinduliwa na Mh. Lowassa.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimsikiliza kwa makini Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima wakati akimuelezea kuhusu vitabu vyake alivyoviandika kabla ya kuvizindua rasmi.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikata utepe kwenye vitabu viliyoandikwa na Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima (kushoto)
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akionyesha moja ya vitabu viliyoandikwa na Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima (kushoto) wakati alipovizindua rasmi leo.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono waumini Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima,Kawe jijini Dar es Salaam leo.