WAZIRI UMMY AMUAGA BALOZI WA SWITZERLAND

July 30, 2024

 

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ametoa shukrani kwa nchi ya Switzerland kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kusaidia Sekta ya Afya hasa kwenye uboreshaji wa Utoaji wa huduma za Afya ya Msingi nchini. 

Waziri Ummy amesema hayo leo Julai 29, 2024 wakati akiagana na Balozi wa 'Switzerland' nchini Tanzania Mhe. Didier Chassot katika ofisi ndozo za Wizara ya Afya Jijini Dar Es Salaam aliyedumu kwa muda wa Miaka Minne nchini. 

"Tanzania na Uswisi zina ushirikiano wa muda mrefu wa maendeleo kupitia Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi (SDC), maeneo ya sasa ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uswisi ni pamoja na kuendelea kuchangia katika Mfuko wa Afya wa pamoja ambapo kupitia awamu ya ufadhili wa moja kwa moja wa Kituo cha Afya (DHFF) Mwaka 2021-2025." Amesema Waziri Ummy 

Waziri Ummy amesema nyanja nyingine wanayoshirikiana na Uswisi ni katika kuchangia kutokomeza Malaria ifikapo mwaka 2030, mpango wa kulinda Afya za vijana (SYP) pamoja na kutoa msaada kwa nafasi ya usimamizi wa ubia na uhamasishaji wa rasilimali ili kusaidia Wizara ya Afya. 

Waziri Ummy ameiomba Serikali ya Uswisi kuiunga mkono na kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa kuendelea kuchangia Mfuko wa Afya wa pamoja na kusaidia utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote ili Watanzania wapate huduma za Afya bila kikwazo cha fedha. 

Kwa upande wake Balozi wa Switzarland Mhe. Didier Chassot ameihakikishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea kushikiana hasa katika upande wa Sekta ya Afya ikiwemo kuchangia katika Mfuko wa Afya wa pamoja. "Nitaenda kumweleza mwenzangu anaekuja baada yangu jinsi tulivyokuwa tunashirikiana na Serikalinya Tanzania hasa katika kuchangia Mfuko wa Afya wa pamoja lakini pia na ombi hilo la kusaidia kufanikisha Bima ya Afya kwa Wote." Amesema Balozi Chassot

Balozi Chassot ameishukuru Tanzania kwa kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake ambapo pia ameelezea jinsi Watanzania walivyo wakarimu.

DKT BITEKO AWAKEMEA WATUMISHI WANAOKWAMISHA WAFANYABIASHARA

DKT BITEKO AWAKEMEA WATUMISHI WANAOKWAMISHA WAFANYABIASHARA

July 30, 2024

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka watumishi Serikalini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na misingi ya utoaji wa huduma ili kuleta matokeo Chanya na sio kuwakwamisha watu wanohitaji huduma.

Dkt. Biteko ametoa agizo hilo (Julai 30,2024) wakati akizindua Sera Taifa ya Biashara katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka Serikalini na sekta binafsi.

Amesema katika baadhi ya ofisi kuna watu mahiri wa kuandaa maandiko lakini utekelezaji wa majukumu yao hauna uhalisia na hauendani na nyaraka walizoziandaa na hivyo nyaraka hizo kubaki kwenye makablasha.

“ Tunaweza kuwa wazuri sana wa kuandika kutoa matamko na kutoa ahadi lakini hali halisi haibadiliki, Hakuna faida ya kuwa na afisa anayejipanga kumkwamisha mfanyabiashara ili tu aitwe bosi, Tunatakiwa kuwa na nyaraka inayotuunganisha wote vinginevyo sera hii itabaki kuwa kitabu cha hadithi kwenye kabati,” Amesema Dkt.Biteko

Amewahimiza watumishi serikalini kuwahakikishia watu wote wanapata huduma hizo pasipo kuwekewa vikwazo suala ambalo litawajengea heshima mbele za watu wanaotafuta huduma hizo, “Uwepo wa sera ya taifa ya Biashara utasababisha mabadiliko makubwa katika nyaraka na sheria mbalimbali za nchi na hivyo sekta zote za serikali zinatakiwa kuisoma sera hii na kuisimamia.“ Amesema Dkt. Biteko

Katika hate nyingine, Dkt. Biteko amewataka watanzania kutumia fursa ya Sera hii kuwa nyezo ya kuimarisha nguvu za kiushindani kitaifa, kikanda na kimataifa huku akiainisha hifadhi ya mazingira na kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Aidha amewataka watanzani kutembea kifua mbele wakiamini kuwa wanao uwezo wa kushindana na kushindanisha bidhaa kwa kuboresha bidhaa hizo ili kuvutia masoko ya ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia kuwa sera hii ni ya biashara na siyo sera ya Wizara ya Viwanda na Biashara.

Dkt. Biteko pia amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan haipendi kuona ama kusikia kero dhidi ya wafanyabiashara hivyo, wadau wote wana ni umuhimu kutumia fursa hiyo kuboresha huduma kupitia sera hii mpya.

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe, Dkt. Selemani Jafo amesema mabadiliko ya kibiashara duniani yanasababisha mabadiliko ya  biashara na mitaji kuwawezesha watanzania kushiriki katika ujenzi wa Uchumi huku akiwashukuru wadau wa maendeleo kwa mchango wao katika maandalizi ya Sera hiyo.

Awali akitoa salamu za Bunge na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda na Biashara, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Mariam Ditopile ameipongeza Serikali kwa hatua ya kupata sera hiyo na kushauri kwa kuwa na uratibu wa pamoja katika masuala yanayoendana na kuondoa urasimu unaosababisha kukosekana kwa tija.

Kwa upande wake, Balozi wa Norway hapa nchini, Mhe. Tone Tinnes amesema ni wazi kuwa Tanzania imekuwa kivutio cha biashara na imeongeza mauzo ya bidhaa zake poamoja na uwekezaji wa mitaji wa moja kwa moja kutoka nje ya nchini.

Amesema suala la manufaa zaidi ni uwekezaji katika kuboresha masuala ya jinsia, vijana na  hifadhi ya mazingira.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binfasi nchini (TPSF), Raphael Maganga amesema serikali imeonesha nia na nguvu ya kimfumo katika kusimamia biashara kwa kuunganisha uratibu wa biashara na kuja sera inayolenga kuwaunganisha wahitaji na kuunganisha wafanyabiashara wadogo na wale walio katika sekta rasmi.

Uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Biashara umebeba Kaulimbiu Ushindani wa Biashara katika kuchochea kasi ya mabadiliko ya Jamii ya kiuchumi yanayoongozwa na viwanda.

.
.
.
.
.
.
.
.
.

MELI ILIYOBEBA MAGARI 300 YATUA BANDARI YA TANGA NA KUWEKA REKODI YA AINA YAKE

July 30, 2024



Na Bashiru Hamis, TANGA

HISTORIA mpya imeandikwa katika Bandari ya Tanga baada ya leo Meli iliyobeba magari 300 ya MV Annegrit kupitia kampuni ya kubwa iliamua kutumia Bandari ya Tanga kupitisha mizigo yake kupitia Kampuni Seafront Shipping Services (SSS) ambapo meli hiyo ikitokea nchini China ikitumia siku 21 kufika kwenye Bandari ya Tanga

Ujio wa Meli hiyo ambayo kwa mara ya kwanza imeingiza idadi kubwa ya Magari ambayo yatashushwa katika Bandari ya Tanga ulishuhudiwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhandisi David Kihenzile.

Akizungumza mara baada ya kuipokea meli hiyo Mhandisi Kihenzile ujio wa meli hiyo katika Bandari ya Tanga ni kutokana na juhudi zilizofanywa na Serikali katika kuboresha Bandari hiyo ambapo kiasi cha Bilioni 429 zilitumika

Alisema uwekezaji huo umekuwa ni chachu kubwa ya kuifungua Bandari hiyo huku akiwashauri wadau mbalimbali kutumia bandari ya Tanga kwa ajili ya kusafirisha mizigo yao na kuleta ameli za abiria kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa kwenye Bandari.

“Ujio wa Meli hii ni matunda makubwa ya uwekezaji ambayo yamefanywa na Serikali kwani katika Bandari hii kumefanyika uwekezaji wa Bilioni 429 katika maboresho ya Bandari hiyo leo tumeshuhudia meli kubwa kutoka China ikiwa imetumia siku 21 kutua Tanga ikiwa imebeba magari 300”Alisema

Alisema katika uwekezaji huo fedha hizo zilisaidia kuongeza kina kutoka mita 3 mpaka 13 zamani meli hiyo isingeweza kupaki hapo ilipo lakini pia imewasaidia kufanya upanuzi na eneo la kuingilia na kutokea meli kwa takribani Upana mita 73.

Aidha alisema pia fedha hizo zimesaidia kuongeza eneo la kugeuzia meli kwenye kipenyo cha takribani mita 800.

“Nitumia nafasi hii kutoa rai kwa sababu bado mzigo unaohudumiwa hapa hautoshi idadi ya meli hazitoshi wanajikuta sehemu ya mzigo mwengine tunavizia kwenye bandari za majirani zetu zikishusha ndio zije hapa tunataka meli za aina hii zitoke moja kwa moja ulaya, china na maeneo ya mbalimbali zije hapa kwetu moja kwa moja”Alisema.

Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian aliwataka wafanyabiashara kuitumia Bandari hiyo kwa sababu wakiitumia mizigo yao itatoka kwa haraka hakuna usumbufu wa kuambiwa subiri meli nyengine zinapakua.

Hii ni kwa mara ya kwanza wamefanikiwa kuleta meli hiyo yenye shehena ya mizigo mchanganyiko inayokadiriwa kuwa na tani 14,000 kutoka chini moja kwa moja hadi Bandari ya Tanga.

Ambapo inaweka alama ya kipekee kuwahi kutokea kwa meli ya mizigo mchanganyiko kuweza kushusha kiwango kikubwa cha mizigo mchanganyiko, zaidi ya magari 500 na aina nyingine ya mizigo mchanganyiko kuweza kushushwa katika bandari ya Tanga.

Baadhi ya mizigo itaelekea katika nchi Jirani kama Zambia,Zimbabwe,Jamhuri ya watu wa kongo (D.R.C) ,Malawi ,Rwanda na kadhalika. Pia mizigo mingine itabaki hapa nchini kwa maana ya (Local goods).

“Kimsingi haya ni mafanikio makubwa na muhimu kwa maendeleo ya Bandari ya Tanga. Bandari ya Tanga inatarajia pia kupokea aina nyingi ya mizigo kuelekea nchi za Jirani, na hii itafanya wafanyabiashara, watoa huduma za usafiri, mawakala wa forodha, jamii za wafanyabiashara wa ndani, kwa pamoja kunufaika kwa kiwango cha juu kutokana na meli zitakazokuwa zinatia nanga bandari ya Tanga moja kwa moja kutoka bandari za Kimataifa

Awali akizungumza Meneja Mkuu wa Kampuni ya Uwakala wa Meli Seafront Shipping Services (SSS) Neelakandan CJ alisema kutakuwa na meli za mizigo mchanganyiko kuanzia 3 mpaka 4 kipindi cha hivi karibuni, ambazo tayari zimepangwa kuingia bandari ya Tanga mwezi wa nane(8).