TANGAZO: MTOTO YUNUS HUSSEIN MKAZI WA MBEZI JUU KAPOTEA

March 14, 2018

                       
                                    YUNUS HUSSEIN  {ALIYEPOTEA}

MTOTO  YUNUS HUSSEIN PICHANI JUU MWENYE UMRI WA MIAKA 12 AMEPOTEA  NYUMBANI KWAO TOKEA TAREHE 8 MPAKA SASA HAJAONEKANA.
 HIVYO KWA YEYOTE ATAKAE MUONA MAHALA POPOTE ATOE TAARIFA KWA NAMBA ZIFUATAZO 0655090202/ 0655141464/ 06585000510
 AU ATOE TAARIFA KATIKA KITUO CHOCHOTE KILICHOPO KARIBU YAKE- MTOTO YUNUS ANAISHI MBEZI JUU JIJI DAR ES SALAAM NA RB NO NI MBJ/RB/236/2018.

SERIKALI YA SWEDEN YATOA BILIONI 66 KUKABARATI KITUO CHA KUZALISHIA UMEME CHA HALE HYDRO SYSTEMS WILAYANI KOROGWE

March 14, 2018
 Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt kulia wakati alipomtembelea ofisini kwake kufanya mazungumzo naye pia  alitembelea Kituo cha kufufua umeme kwa njia ya Maji kilichopo Hale wilayani Korogwe kushoto ni
 Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt akitembelea maeneo mbalimbali kwenye kituo hicho
 Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt wa pili kutoka kulia akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto wakiangalia kitu wakati walipotembelea kituo hicho
  Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt wa pili katikati akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto wakiangalia mitambo iliyopo kwenye kituo cha Kuzalisha Umeme Hale wilayani Korogwe Mkoani Tanga  wakati walipotembelea kituo hicho kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe,Rehema Bwasi
 Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt wa pili katikati akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto wakitembelea mitambo iliyopo kwenye kituo cha Kuzalisha Umeme Hale wilayani Korogwe Mkoani Tanga  wakati walipotembelea kituo hicho
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katika akiteta jambo na Meneja wa Pangani Hydro Systems Mhandisi Stephen Mahenda kulia ni  Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt kulia

Meneja Mwandamizi wa Uzalishaji Umeme kutoka Tanesco Makao Makuu Bakaya Mtamakaya akizungumza wakati ziara hiyo ya Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt kushoto kulia ni Meneja wa Uzalishaji wa Kituo cha Pangani Hydro Systems
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akizungumza kwenye kikao cha pamoja mara baada ya Balozi huyo wa Sweden kutembelea kituo hicho cha Uzalishaji wa Umeme kulia Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt


Meneja Uzalishaji wa Pangani Hydro Systems Mhandisi Stephen Mahenda kushoto akiteta jambo na  na Balozi wa Sweden nchini Katarina Rangnitt

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katika akiteta jambo na Balozi wa Sweden nchini Katarina Rangnitt kushoto
Balozi wa Sweden nchini Katarina Rangnitt akitembelea maeneo mbalimbali kwenye kituo hicho.

SERIKALI ya Sweden imetoa kiasi cha fedha Bilioni 66 za kitanzania sawa na  dola za Marekani milioni 30 ambazo zitatumika katika kukarabati mitambo katika Kituo cha Kuzalishia Umeme cha Hale Hydro System wilayani Korogwe mkoani Tanga.

Hayo yamebainishwa na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt wakati alipotembelea mgodi huo ambapo upo Hale wilayani Korogwe Mkoani Tanga.

Amesema kuwa Tanzania na Sweden zina historia za muda mrefu katika uhusiano wa kidplomasia na nyanja mbalimbali za uchumi na kijamii.

Amesema kuwa nishati ni jambo muhimu kwa maendeleo ya viwanda hivyo kwa kuona umuhimu wa jambo hilo kwa nia moja serikali ya Sweden imetoa kiasi hicho cha fedha katika kukarabati mgodi huo.

" Nishati ni jambo muhimu katika maendeleo ya viwanda na Tanzania tayari imeweka mikakati mizuri katika maendeleo ya viwanda hivyo,serikali ya Sweden imetoa kiasi hicho cha fedha kwa kukarabati mgodi huo "alisema.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella amemshukuru balozi huyo kwa serikali ya Sweden kufadhili mradi huo,pia amemkaribisha balozi huyo kuwekeza katika sekta mbalimbali za kijamii na uchumi.

" Nawashukuru serikali ya Sweden kwa kufadhili mradi huo na mheshimwa Rais ameweka mazingira mazuri ya uwekezaji mkoani Tanga haswa katika sekta ya viwanda hivyo karibuni Tanga mje kuwekeza" alisema.

Kwa upande wake Meneja wa Mtambo wa Uzalishaji Umeme wa Hale Mhandisi Steven Mahemba amesema kuwa mtambo huo umepunguza uzalishaji kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo uchakavu wa mitambo.

" Kituo hiki kimejengwa kuanzia mwaka 1962 na kumalizika mwaka 1964 na kina muda wa takribani miaka 52 hivyo pia kutokana na uchakavu wa miundombinu take imepunguza uzalishaji kutoka megawati 21 mpaka 4 hadi 8" alisema.

Ukarabati huo unatarajiwa kukamilika kwa muda wa miaka mitatu.

UNESCO YAWAFUNDA UJASIRIAMALI WALIMU KUFUNDISHA WANAFUNZI KUJITAMBUA

UNESCO YAWAFUNDA UJASIRIAMALI WALIMU KUFUNDISHA WANAFUNZI KUJITAMBUA

March 14, 2018
 Walimu wanaopatiwa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa(UNESCO) chini ya ufadhili wa program ya Malala wametakiwa kuhakikisha wanatumia elimu waliyopata kuwafanya wanafunzi hasa wa kike kujitambua na kukamilisha malengo yao. Kauli hiyo imetolewa na Ofisa Elimu wa mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu wakati akifungua semina hiyo inayoshirikisha wajumbe 64 wakiwemo walimu 40 na wakuu wa Shule 20 na maofisa elimu wanne kutoka wilaya nne za mkoa wa Tanga. Wilaya zinazohusika ni za Pangani, Muheza, Korogwe na Lushoto. Semina hiyo ni sehemu ya mradi wa kuwafanya watoto hasa wa kike kujitambua, kupunguza utoro na mimba za utotoni ili kufikia malengo yao ulioanza mwaka 2015. Mayasa alisema kwamba ili wawasaidie watoto hao wamalize masomo yao ni vyema walimu hao wakatambua umuhimu wa mafunzo hayo na kuwa karibu na watoto na kuishi nao kutambua shida zao na kuwasaidia kukabiliana nazo ili waweze kusonga mbele. Alisema kama walimu wakiamua kufanyakazi ya kufundisha tu bila kuwa karibu na watoto dhima ya kuwasaidia kufikia malengo hata ya kujiajiri wenyewe wakimaliza masomo haitafikiwa. Aliwataka walimu hao kusogeza elimu yao kwa wenzao na katika hilo kuweza kusaidia kufanya vyema kwa watoto katika masomo na pia utayari wa maisha. Aliwakumbusha walimu kusikiliza watoto kutambua shida zao na kujua namna ya kuwasaidia badala ya kubaki kulalamika kwamba watoto hao ni wakorofi au wanakiuka kanuni za shule. Alisema alishawahi kutembelea shule moja na kukuta mtoto ambaye anachelewa kufika shule lakini alipohoji aligundua kwamba kijana huyo wa kidato cha nne ana mama mgonjwa mahututi na lazima amhudumie kwa kuwa baba yake alikwishafariki. “Walimu walimshambulia yule mtoto, nikamuita pembeni na kujua tatizo lake” alisema Ofisa Elimu huyo ambaye pia alisema alikutana na kadhia hiyo pia kwa binti mmoja ambaye alilazimika kusaidia kuhamishwa kwake kupata hosteli kutokana na mazingira magumu aliyomo. Aliwataka walimu wanaochukua mafunzo hayo kubadilisha mtazamo na kuacha kuchukulia kazi kimazoea ili hata wafadhili nao waone fahari ya mchango wao katika elimu. Alisema kwamba kuendelea kuwa na shule dhaifu wakati kuna wafadhili wanapiga jeki si sawasawa; aliwataka walimu waamke na kuhakikisha kwamba mafunzo wanayoyapata yanawaondoa wanafunzi katika dhiki ya kujitambua na kujipanga kufikia malengo. Alisema miongoni mwa mambo yanayostahili kuangaliwa ni pamoja na kuhakikisha klabu zilizoanzishwa zinasonga mbele na kutoa matunda tarajiwa ili wafadhili nao wasichoke. Pamoja na mafunzo hayo kutakiwa kufika kwa wanafunzi pia amewataka kuambukiza elimu yao kwa walimu wenzao ili kuwa na moyo mmoja wa kusaidia watoto hasa wa kike ambao wanakumbana na vishawsihi vingi. Aliwataka walimu wengine pia kuiga Mkuu wa shule ya Kalemea ambaye pamoja na kuwa pembezoni amekuwa karibu na watoto na kiasi cha kutoa divisheni ya kwanza katika wilaya yake ya Lushoto. Katika mafunzo hayo ambayo yaliendeshwa na Mkufunzi kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Ofisa Miradi wa UNESCO Jeniffer Kota alisema kwamba lengo la semina hiyo ya ujasiriamali ni kutoa elimu kwa walimu namna ya kuwawezesha watoto wa kike kujitambua hivyo kupunguza utoro, mimba za utotoni na kuongeza maarifa ili waweze kumaliza shule angalau elimu ya msingi. Alisema elimu hiyo inayotolewa kwa wakuu wa shule na walimu wengine na maofisa elimu wilaya ni kuona kwamba walimu hao wanawafunza wengine ili kupeleka elimu kwa watoto nao waelewe thamani ya elimu na kuwa na uwezo wa kutimiza malengo na kujiajiri. Naye mgeni kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, wa idara ya elimu Simon Mombeyi aliwatafadhalisha walimu wanaochukua mafunzo hayo kuyafikisha kwa walimu wengine na kufikisha elimu hiyo kwa wanafunzi.; Alisema kwa kuwa lengo la msingi ni kuwezesha wafikie malengo wanayofikiria kwa kuwawezesha kujitambua na kubaki katika mstari. Alisema wanafunzi wa sekondari wana vishawishi vingi kwa kuwa wanapanga hivyo wanapojengewa uwezo wanaweza kudhibiti mihemko ya ujana na kumaliza elimu kama ilivyopangwa. Alisema rais amewekeza katika elimu na wao wanamsaidia lakini wanatakiwa kuwekeza kwa busara sana ili kufanikisha malengo hayo.
Ofisa Mradi wa Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO), Jennifer Kotta akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga.
Mgeni rasmi Ofisa Elimu wa mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu akitoa nasaha wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga. Kushoto ni Ofisa Mradi wa Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO), Jennifer Kotta na kulia ni Simon Mombeyi kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, wa Idara ya Elimu.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala wakisikiliza kwa umakini nasaha za mgeni rasmi (hayupo pichani) yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga.
Simon Mombeyi kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, wa Idara ya Elimu akizungumza jambo na washiriki wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga.
Mkufunzi wa mafunzo ya ujasiriamali kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Jacqueline Stenga akiendesha mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala kwa wajumbe 64 wakiwemo walimu 40 na wakuu wa Shule 20 na maofisa elimu wanne kutoka wilaya nne za mkoa wa Tanga yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani humo.
Mmoja wa washiriki mwalimu wa shule ya sekondari Mwera ya wilaya ya Pangani, Teresia Kapinga akiwasilisha taarifa wakati wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala kwa wajumbe 64 wakiwemo walimu 40 na wakuu wa Shule 20 na maofisa elimu wanne kutoka wilaya nne za mkoa wa Tanga yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani humo.
Pichani juu na chini ni washiriki wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala kwa wajumbe 64 wakiwemo walimu 40 na wakuu wa Shule 20 na maofisa elimu wanne kutoka wilaya nne za mkoa wa Tanga yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani humo.
Mgeni rasmi Ofisa Elimu wa mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu (wan ne kushoto) katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya siku nne ya ujasiriamali yanayotolewa na UNESCO chini ya ufadhili wa program ya Malala kwa wajumbe 64 wakiwemo walimu 40 na wakuu wa Shule 20 na maofisa elimu wanne kutoka wilaya nne za mkoa wa Tanga yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani humo.
--

KAMPUNI YA KILIMANJARO SAR LTD YAINGIA MAKUBALIANO NA HOSPTALI YA ST JOSEPH YA KUTOA HUDUMA KWA WATALII WALIPATA MATATIZO MLIMA KILIMANJARO

March 14, 2018
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kilimanjao SAR ,Ivan Braun akitia saini makubaliano ya Mashirikiano na Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi kuhusu uanzishwaji wa Kliniki ya utoaji matibabu kwa Wagonjwa wanaopata matatizo wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro na Meru,kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya St Joseph ,Sister ,Urbanie Lyimo huku zoezi hilo likishuhudiwa na Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba (aliyesimama kulia) ,Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi ,Raymond Mboya (katikati) na kushoto ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR,Amour Abdallah.
Zoezi hilo la utiaji saini pia lilifanywa na Mganga Mfawidi wa Hospitali ya St Joseph ,Sister Urbanie Lyimo kwa niaba ya Hospitali.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kilimanjao SAR ,Ivan Braun na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya St Joseph ,Sister ,Urbanie Lyimo wakibadilishana karatasi zenye makubaliano ya kushirikiana katika utoaji wa matibabu kwa Wagonjwa waliopata matatizo kutokana na hali ya muinuko katika Mlima mara baada ya kutia saini .
Mkuu wa wilaya ya Moshi akizungumza wakati wa Hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano hayo .
Baadhi ya Wauguzi na Madaktari katika Hosptali ya St Joseph wakifuatilia zoezi la utiaji saini wa makubaliano hayo .
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi,Raymond Mboya akizungumza wakati wa hafla hiyo .
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kilimanjao SAR ,Ivan Braun akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika Hosptali ya St Joseph mjini Moshi.
Mganga Mfawidi wa Hospitali ya St Joseph ,Sister Urbanie Lyimo akitoa wasifu wa Hosptali ya St Joseph wakai wa hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano ya mashirikiano na Kampuni ya Kilimanjaro SAR.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR,Amour Abdalah akizungumza katika Hafla hiyo.
Mgeni rasmi katika Hafla hiyo,Kippi Warioba na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na Wauguzi katika Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi.
Mgeni rasmi katika Hafla hiyo,Kippi Warioba na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR mara baada ya kukamilika kwa zoezi la utiaji saini .

NA Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini .

SEKTA ya Utalii nchini imepata suluhu ya Changamoto ya muda mrefu ya utoaji wa msaada wa kitabibu, utafutaji na uokoaji wa wageni wanaopata matatizo wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro na Meru .
Changamoto hiyo inafika kikomo rasmi baada ya kampuni ya Kilimanjaro SAR kuzindua Kliniki ya kwanza Afrika ya magonjwa yatokanayo na muinuko wa juu pamoja na utumiaji wa Helkopta kwa ajili ya uokoaji katika Hifadhi za Mlima Kilimanjarona Mlima Meru.
Mbali na uzinduzi huo Kilimanjaro SAR imeingia makubaliano na Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi ,kuanza kutoa huduma za kitabibu kwa wagonjwa watakao pata matatizo wakati wa kupanda Milima hiyo.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano kati ya Kampuni ya Kilimanjaro SAR na Hospitali ya St Joseph ,Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba aliyekuwa mgeni rasmi amesema hii ni fursa mpya kwa sekta ya Utalii kuutangaza vyema Mlima Kilimanjaro.
Huduma hii ya kwanza kutolewa barani Afrika inaiweka Tanzania katika nafasi ya pili katika Ramani ya Dunia, kuwa  na kliniki ya kipekee katika utoaji wa huduma kwa wapanda Mlima na kwamba kwa kiasi kikubwa itasaidia katika kuongeza idadi ya Watalii. 
Hata hivyo kuanza kwa huduma hiyo muhimu kwa sekta ya Utalii nchini ,bado ipo changamoto ya matumizi ya uwanja mdogo wa ndege wa Moshi hali inayowalazimu kutumia uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA).
Ulbanie Lyimo ni mganga Mfawidhi wa Hospitali ya St Joseph akaeleza faida itakayopatikana kutokana na kuingia makubaliano na kampuni hiyo ya Uokoaji ya Kilimanjaro SAR kuongeza maarifa katika utoaji wa matibabu kutoka kwa madaktari wa kigeni watakao hudumia wagonjwa wa Mlimani.
Kuanza kwa kliniki hii ni msaada kwa maiha ya wapandaji wa Mlima Kilimanjaro na Meru ikizingatiwa asilimia 75 ya magonjwa uwapo mlimani yanatokana na mbadiliko ya Hali ya Hewa kulingana na urefu wa Mlima.
RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASA ITAKAYOTUMIA UMEME SGR-KUTOKA MOROGORO HADI MAKUTUPORA- DODOMA KM 422 KATIKA ENEO LA IHUMWA NJE KIDOGO YA MJI WA DODOMA

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASA ITAKAYOTUMIA UMEME SGR-KUTOKA MOROGORO HADI MAKUTUPORA- DODOMA KM 422 KATIKA ENEO LA IHUMWA NJE KIDOGO YA MJI WA DODOMA

March 14, 2018
1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa itakayotumia umeme Standard Gauge (SGR) itakayotoka mkoani Morogoro hadi Makutupora Dodoma katika eneo la Stesheni ya Ihumwa nje kidogo ya mji wa Dodoma. Wengine katika picha ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na Balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke wakishuhudia.
2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifunua kitambaa wakati akiweka jiwe la msingi ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa itakayotumia umeme Standard Gauge (SGR) itakayotoka mkoani Morogoro hadi Makutupora Dodoma katika eneo la Stesheni ya Ihumwa nje kidogo ya mji wa Dodoma.
4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifunga kifuniko mara baada ya kutumbukiza karatasi ya majina ya viongozi mbalimbali waliofanikisha ujenzi huo kama kumbukumbu katika uwekaji wa jiwe la msingi la Reli ya Kisasa(SGR) itakayotoka mkoani Morogoro-hadi Makutupora Dodoma.
5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saruji iliyochanganywa na kokoto kwenye jiwe hilo la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka mkoani Morogoro-hadi Makutupora Dodoma yenye urefu wa km 422 katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saruji iliyochanganywa na kokoto kwenye jiwe hilo la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka mkoani Morogoro-hadi Makutupora Dodoma yenye urefu wa km 422 katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
7
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiweka saruji iliyochanganywa na kokoto kwenye jiwe hilo la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa mkoani Morogoro-hadi Makutupora Dodoma yenye urefu wa km 422 katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
9
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe pamoja Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya umeme kutoka mkoani Morogoro-hadi Makutupora Dodoma yenye urefu wa km 422 katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma. Wengine katika picha ni Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Pro. Makame Mbarawa,  Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Reli TRC Masanja Kadogosa pamoja na viongozi wengine.
10 11
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua mfano wa Reli hiyo ya Kisasa itakayotumia umeme mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
12
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua mfano wa Reli hiyo ya Kisasa itakayotumia umeme mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
13 14
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia baadhi ya wabunge waliofika kwenye uzinduzi wa Reli hiyo ya Kisasa SGR itakayo toka Morogoro hadi Dodoma.
16
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la Reli hio ya Kisasa katika eneo la Ihumwa Stesheni mkoani Dodoma.
17
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru madereva wa magari yatakayofanya kazi ya ujenzi wa reli hiyo ya kisasa SGR itakayo toka Morogoro hadi Dodoma.
18
Sehemu ya wananchi mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo za uwekaji wa jiwe la msingi.
19
Treni ya zamani ikipita katika Reli za zamani katika eneo la Ihumwa stesheni mkoani Dodoma.
20
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wakati akiwasili katika eneo la Ihumwa Stesheni kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi.
21
Mtendaji Mkuu wa Shirika la Reli TRC Masanja Kadogosa akitoa maelezo ya mradi huo wa Reli ya kisasa ya umeme kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli PICHA NA IKULU