WAKULIMA NJOMBE WAFURAHIA MBEGU BORA YA MUHOGO WAWASHUKURU WATAFITI SERIKALI

May 09, 2018

Na: Calvin Edward Gwabara,Njombe.

Wakulima Mkoani Njombe w amewashukuru watafiti na Serikali kwa kuwezesha kupatikana kwa mbegu bora za muhogo ambazo zinauwezo wa kustawi kwenye maeneo ya baridi hasa nyanda za juu kusini baada ya utafiti wa mwaka mmoja ulifanywa na watafiti kutoka kituo cha utafiti wa kilimo cha Mikocheni MARI na chuo kikuu cha Dar es salaam.

Wakulima na wakazi wa kata ya Lupembe Mkoani Njombe wakifurahia mavuno makubwa ya mbegu za Muhogo zinazostawi kwenye maeneo ya baridi kali.

Wakiongea kwa furaha wakati wa zoezi la kuvuna mihogo hiyo ambayo ilipandwa mwaka mmoja uliopita wakulima hao wamesema sasa wamepata zao la biashara la uhakika baada ya zao la la chai kusumbua biashara yake .











Akiongea kwa niaba ya wakulima wenzake bwana Mapambano Luhongori Mkazi wa kijiji cha Lupembe wilaya ya njombe mkoani humo amesema kuwa Zao la Muhogo sasa litakuwa mkombozi kwa wakulima wengi ambao wamekuwa na shauku ya kulima zao hilo ili kuweza kunufaika na fursa kubwa ambazo wanazipata wakulima wa mikoa mingine kama vile Mara, Geita na Pwani.






‘’ Kutokana na uhitaji na soko kubwa la muhogo mkoani njombe nimejaribu mara kadhaa kulima zao la muhogo bila mafanikio lakini siamini macho yangu leo kuona katika eneo hilihili ambalo tulipanda mbegu hizi bora za watafiti kwenye shamba darasa imetoka mihogo mingi na mizuri kiasi hiki, ila nimegundua kuwa mbegu tulizokuwa tunatumia za kienyeji hazifai ukanda wetu’’ Alisema Luhongoli mkulima kutoka mkoa huo.




Mtafiti kiongozi wa Utafiti huo Dkt. Joseph Ndunguru akifafanua jambo kwa wakulima mara baada ya kuvuna baadhi ya mashina hayo kwenye kila aina 75 walizopanda eneo hilo.

Kwa upande wake Bi Rehema Malekela ambaye pia alishiriki kuanzia mwazo wa utafiti mpaka wakati huu wa kuvuna amesema kilimo cha zao hilo kilikuwa kidogo sana ambapo familia zimekuwa zikilima mashina machache kuzunguka nyumba kwaajili ya vitafunywa vya chai tu baada ya kuona zao hilo haliwezi kuwapatia tija kama wakulima wa maene mengine nchini.

Bi Malekela ameongeza kuwa wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani waislamu hupata shida sana kupata muhogo na hivyo kuwalazimu baadahi ya wafanyabiashara wengi kwenda kufuata mihogo kwenye mikoa mingine inayozalisha zao hilo kwa wingi na kuja kuiuza mkoani humo kwa bei kubwa.

“ Kwakweli ukifunua moyo wangu na moyo wa kila mtu unayemuona hapa aliyekuja kushiriki zoezi hili utaona furaha isiyo na kifani ndio maana unaona tumejitokeza kwa wingi watu kutoka Tarafa nzima kuja kushuhudia kupatikana kwa zao linguine la biashara kwenye eneo letu” Alisema Bi. Malekela kwa niaba ya wakina mama wengine.




Mamia ya wakulima na wakazi wa Kata ya Lupembe na maeneo mengine waliojitokeza kuangalia matokeo hayo ya utafiti kuona kama wanaweza kulima Muhogo kwenye ukanda huo wa baridi kali.







Aliongeza kuwa kingine kikubwa wanachowashukuru watafiti hao ni kuwaahidi kuwapelekea mbegu hizo kila mkulima kupitia vikundi vyao na kuwafundisha namna ya kuchakata muhogo na kupata bidhaa mbalimbali kama vile clips,Biskuti,Maandazi na aina zingine za vyakula ili kuongeza thamani ya zao hilo.






Kwa upande wake mtafiti kiongozi wa utafiti huo kutoka Kituo cha utafiti wa Kilimo Mikocheni MARI Dkt. Joseph Ndunguru amesema kuwa kwa muda mrefu wakulima kwenye maeneo ya baridi wamekuwa hawalimi zao hili hali ambayo imekuwa ikiwakosesha fursa mbalimbali zitokanazo na zao hilo ambazo wakulima wa maeneo yenye joto wanazipata kwa kuzalisha muhogo.






Amesema katika utafiti huo wamepeleka mbegu aina 75 za muhigo katika maeneo matatu ya utafiti huo ambayo ni Mkoa wa Njombe ambapo wanaangalia aina za muhogo kati ya hizo ambazo zitastawi na kuvumilia baridi hadi la nyuzijoto 16 -22C na eneo linguine ni mkoa wa Dodoma kuangalia aina ya mihogo itakayoweza kuvumilia ukame na Mkoa wa Pwani katika eneo la Chambezi ambapo wanaangalia changamoto ya joto na magonjwa.










Dkt. Joseph Ndunguru na Dkt. Gladness Temu wakiwa wamebeba moja ya mashina ya mbegu hizo yaliyovunnwa hivi karibuni katika eneo la Chambezi ambalo walikuwa wakiangalia mbegu zinazostawi kwenye eneo la Joto na magonjwa.

‘’ Kwakweli tumepata mafanikio makubwa sana kwa mfano kwa Mkoa wa Njombe kwenye baridi ,aina 47 kati ya aina 75 tulizopanda kwenye shamba hili kwenye eneo lenye bardi zaidi tum eona zimefanya vizuri sana nah ii ni kutuonyesha kuwa sasa wakulima wa eneo hilo wanaweza kunufaika na kilimo hiki’’ Alisema Dkt. Ndunguru.

Mtafiti huyo ameongeza kuwa pamoja na kufanya vizuri kwa aina hizo 47 lakini wamegundua kuwa katika eneo hilo shina linatoa mihogo mingi sana lakini haiwezi kukomaa kwa muda wa mwaka mmoja kama ilivyo kwenye maeneo yenye joto na hivyo kuhitaji muda zaidi ya mwaka mmoja ili inenepe na kukomaa vizuri.

Kwa upande wake mtafiti kutoka Chuo kikuu cha Dar es salaam Dkt. Gladness Temu ambaye ni mtafiti katika mradi huu amesema kuwa katika kipindi chote cha utafiti huo wamekuwa wakitembelea shamba hilo na kuchukua takwimu mbalimbali muhimu ambazo zitakuja mwishoni kusaidia katika hitimisho na mapendekezo kwa wakulima.


Dkt. Gladness Temu akiinua shina la Muhogo walilovuna huko Chambezi hivi karibuni.

Amesema miongoni mwa taarifa hizo ni pamoja na kuangalia kama mbegu hizo zinashambuliwa na magonjwa ya batobato na michirizi ya kahawia magonjwa mabayo ni hataro sana kwa mihogo kwa sasa lakini hayakujitokeza kabisa kwenye shamba hilo hali ambayo inawafanya kuamini uzalishaji utakuwa mkubwa sana katika eneo hilo.

‘’ Katika kuhakikisha magonjwa hayo hayatokei kabisa tutawaletea mbegu bora na safi ili waanze kilimo hicho bila magonjwa nah ii itawasaidia sana sasa kuwa wazalishaji wa mbegu za muhogo wazuri maana eneo lao halina magonjwa hayo kwa sasa’’ Alisistizia Dkt. Gladness.
Mradi huu wa utafiti unafanywa kwa kushirkiana na nchi Tatu za Tanzania,Kenya na Hispania kwa ufadhili wa shirikala la maenedeleo la umoja wa Ulaya kupitia kwa shirikala la chakula na kilimo duni
ani FAO.




Baadhi ya wafanyakazi wa kituo cha utafiti wa Kilimo Mikocheni cha jijini Dar es salaam MARI wakifurahi wakati waliposhirikiana kuinua shina moja la Muhogo huko Chambezi Bagamoyo.


MKAZI WA ZANZIBAR ASHINDA BIDHAA ZENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 1 KUTOKA JUMIA

May 09, 2018
MKAZI wa visiwani Zanzibar, Bi. Patricia Philipo amejishindia vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka Jumia kupitia kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ katika mwezi uliopita wa Aprili.

Mshindi huyo alipatikana kupitia kampeni iliyoendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. Wateja walitakiwa kupendekeza mtu wao wa karibu ambaye waliona anastahili nyumba yake kupendezeshwa na Jumia kwa kupatiwa ofa ya vyombo vya ndani.

Bi. Patricia Philipo aliibuka mshindi baada ya mchumba wake Bw. Mwalim Juma Kumpendekeza ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa.

“Mimi ni mteja mzuri wa Jumia kwa sababu naitumia mara kwa mara kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali ambazo zimekuwa zikinifika mpaka ninakoishi Zanzibar. Baada ya kuliona hili shindano, niliona ni vema nimpendekeze mwenzangu ashinde. Ukizingatia tupo kwenye maandalizi ya ndoa yetu, suala la mahari pamoja na vyombo vya ndani ni gharama hivyo ushindi wake ungekuwa na mchango mkubwa kwenye shughuli yetu,” alisema Bw. Juma ambaye ni mchumba wa mshindi wa kampeni hiyo, Bi. Patricia.

“Sikuwa na wasiwasi kwamba endapo angeshinda asingeweza kupatiwa zawadi zake. Kwa sababu hapo nyuma kulikuwa na mashindano kadhaa kama vile ‘Treasure Hunt’ kipindi cha Mobile Week, wateja walikuwa wanashinda simu na kukabidhiwa bila ya ubabaishaji wowote,” alimalizia Bw. Juma.

Akielezea furaha yake mara baada ya kutangazwa mshindi Bi. Patricia Philipo amesema kuwa, “kusema ukweli hapo mwanzo sikutarajia kama ningeweza kushinda kutokana na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wangu. Kuna wakati nilitaka kukata tamaa kwa sababu mwenzangu alikuwa ameniacha mbali, mashabiki wake walikuwa wanamuunga mkono na kuwashirikisha wengine kwa kiasi kikubwa.”

“Lakini niliongeza bidii na kumuomba Mungu ili niweze kufanikiwa. Na kweli ilifika mahala mpinzani wangu akakata tamaa. Hapo ndipo mimi nilipoongeza bidii zaidi na kufanikiwa kuibuka mshindi,” aliongezea Bi. Patricia na kuhitimisha, “nina furaha kubwa katika kipindi hiki kwani zawadi niliyoshinda ni kubwa. Vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja si jambo la kawaida. Jumia wameweka alama kubwa katika maisha yangu na nawaombea waendelee kuwajali wateja wao kwa bidhaa bora, ofa lukuki pamoja na kuwa waaminifu.”

Kampeni ya ‘Big Home Makeover’ kutoka Jumia iliyodumu kwa takribani mwezi mmoja, ilikuwa na dhamira ya kuwawezesha wateja wake kununua vyombo vya ndani kwa gharama nafuu. Lakini pia ilitoa fursa ya kumzawadia mteja mmoja aliyependekezwa na mtu wake wa karibu vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni mmoja.

“Tunampongeza mshindi wetu Bi. Patricia kwa ushindi aliojipatia lakini pia tunawasihi wateja wetu kuchangamkia bidhaa mbalimbali kwenye mtandao wetu. Kupitia mtandao unaweza kuokoa muda na gharama pamoja na usumbufu wa kufuata bidhaa. Lakini cha muhimu ni njia salama na ya uhakika, Jumia inawapatia fursa wateja wake kufanya manunuzi na kisha kulipia baada ya kuridhika na mzigo aliofikishiwa,” alisema Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey.

“Hivi sasa kupitia mtandao wetu tunaendesha kampeni ya kutoa punguzo kubwa la bei ambalo hauwezi kupata sehemu yoyote. Kwa mfano, simu zinazouzwa Jumia ni pungufu ya shilingi 50,000 tofauti na ukienda kwenye maduka moja kwa moja, vivyo hivyo kwa bidhaa nyinginezo, kila bidhaa utakayoiona basi ujue imepunguzwa kiasi hicho! Tunawasihi watanzania wasicheze mbali na jumia ili kuweza kunufaika na mambo haya mazuri,” alihitimisha Geofrey.

Mchumba wa mshindi, Bw. Mwalim Juma aliyependekeza mchumba wake ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa hundi iliyofanyika Dar es Salaam jana.

Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey.akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa mshindi huyo akikabidhiwa hundi yake.

Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey ( kulia), akimkabidhi Bi.Patricia Philipo mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 1 baada ya kuibuka mshindi. Katikati Mchumba wa mshindi, Bw. Mwalim Juma aliyependekeza mchumba wake ashinde zawadi ya vyombo hivyo.


(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)