WANACHAMA PSPF SASA RASMI KUPATA MIKOPO KUPITIA BENKI YA CRDB

February 27, 2017
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, (kushoto), akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dkt. Charels Kimei, wakati wa uzinduzi wa ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili ambapo CRDB sasa itawakopesha Wanachama wa PSPF kwenye maeneo ya elimu, viwanja na pesa za kuanzia maisha kwa watumishi wa serikali. Uzinduzi huo umefanyika Februari 27, 2017 makao makuu ya PSPF jijini Dar es Salaam.

NA K-VIS BLOG
WANACHAMA wa mfuko wa pensheni wa PSPF sasa wataanza kupata mikopo yao kupitia benki ya CRDB mara baada ya kuzinduliwa kwa  mpango  huo  baina ya taasisi hizo mbili jana jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini mpango huo  , Mkurugenzi Mkuu  wa PSPF, Bw Adam Mayingu , alisema kuwa mpango huo wa kutoa mikopo kwa wanachama ulianza tangu Desemba 2014 kwa kupitia taasisi nyingine za kifedha.
Alisema kuwa PSPF na benki ya CRDB wamekubaliana  kushirikiana katika kuendesha kwa pamoja huduma ya mikopo.Mikopo hiyo ni pamoja na mkopo wa elimu(education loan scheme), mkopo wa kuanzia maisha( startup life loan scheme) na mkopo wa viwanja(Nipo site na PSPF).
Alisema kuwa kwa upande wa mkopo wa elimu , mwanachama anaweza kukopa kwa ajili ya kujiendeleza kielimu katika ngazi yeyote ya elimu .Ngazi hiyo ni  stashahada, shahada, shahada ya uzamili na hata mafunzo ya ufundi.
Kwa upande wa mkopo wa kuanzia maisha, alisema mwanachama aliyepata ajira kwa mara ya kwanza huwa na mahitaji yake muhimu  na kwa kutambua hilo, PSPF kwa kushirikiana na CRDB wameanzisha  mpango huu ambapo mwanachama anaruhusiwa kukopa mishahara yake ya miezi miwili ili awaeze kujipanga na maisha mapya ya ajira.
Kuhusu mkopo wa viwanja  kwa wanachama, alisema  kuwa  huduma hii itawawezesha wanachama wa PSPF kukopa na kumiliki viwanja vya makazi ambavyo vinapataikana  maeneo mbali mbali ya nchi.
“Lengo  kubwa hapa ni kuwawezesha wanachama wa PSPF kumiliki viwanja vya makazi vilivyopimwa iii kuwaepusha dhdi ya ujenzi katika makazi holela, ambayo yamekuwa na gharama kubwa kuliko makazi yaliyopangiliwa”,alisema.
Alifafanua kuwa lengo kubwa la kuanzisha mikopo hiyo ni kuhakikisha kila mtanzania anatimiza ndoto  yake ikiwa ni katika masomo kupitia mkopo wa  elimu , ndoto yake nyingine kupitia mkopo wa kuanzia maisha au mkopo wa viwanja.
Hadi kufikia tarehe 17 Mwezi huu idadi ya wanachama walionufaika na mikopo  hiyo na idadi kwenye mabano ni  Elimu  (1,432)), mkopo wa kuanzia maisha ( 847), mkopo wa viwanja (58).
“Kwa kushirikiana na benki ya CRDB ambayo ina mtandao mkubwa wa matawi hapa nchini tunaamini watanzania wengi watanufaika na mikopo hii na kwa kufanya hivyo tutakuwa tunatakeleza juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha watanzania wengi zaidi wananufaika na huduma mbali mbali za Mifuko ya Hifadhi ya jamii”, alieleza.
Kw a upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk Charles Kimei, alisema azma yao ni kuhakikisha kuwa ushirikiano na wadau wanamkomboa kiuchumi mwananchi  hususan mwenye kipato cha chini  kwa kumpatia  mkopo wenye riba ya asilimia 14 tu kwa mwaka. Kuhusu marejesho alisema ni kuanzia mwaka mmoja hadi miaka mitano.
Ushirikiano wetu na PSPF  bado una muendeleo ulio mpana kwani kwa pamoja tunadhamiria hapo baadae kuingiza sokono mikopo kwa ajili ya wastaafu ‘pensioners’.
Alisema mpango huu wa utoaji wa mikopo kw wastaafu una lengo la kuleta faraja na kuwasaidia wastaafu katika kukidhi mahitaji yao mbali mbali ya kimaisha ikiwamo kulipia gharama za matibabu, ada za shule za watoto au wajukuaa  na kuendesha biashara ndogo ndogo zitakazosaidia kupunguza ukali wa maisha ya kila siku.
Dk Kimei alifafanua kuwa  nia yao ni kujenga mazingira mazuri kwa wastaafu walio wanachama wa PSPF ili kustaafu kusiogopwe na kuonekana ni mwanzo wa kuanza kwa kipindi cha maisha ya shida yasiyokuwa na  matumaini.
“Tunataka kujenga tabia ya kuwafanya wafanyakazi wanapopata barua za kustaafu wasihuzunike kama ilivyozoeleka”,alidokezaAlisema kuwa mwanachama wa PSPF anayetaka mkopo anatakiwa aende kwenye tawi lolote la benki ya CRDB ililopo karibu naye ili kupata huduma.
 Bw. Mayingu akitoa hotuba yake kuelezea ushirikiano huo ambao lengo lake  kubwa ni kupanuan wigo wa huduma kwa Wanachama wa Mfuko huo

 Dkt. Charles Kimei, akitoa hotuba yake kueleza jinsi benki yake ilivyofurahishwa na ushirikiano huo

 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi, akitoa hotuba ya ukaribisho
 Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Gabriel Silayo, (katikati), na Msaidizi Mtendaji wa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Bw.Keneth Kasigila, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Wateja wa Mashirika wa CRDB, Bw.Goodluck Nkini, (kushoto), wakati wa hafla hiyo.

BOHARI YA DAWA (MSD) YAPIGA HATUA KUWEZESHA UZALISHAJI DAWA KWA NJIA YA UBIA NA SEKTA BINAFSI (PPP)

February 27, 2017
 Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bwana, Laurean Bwanakunu (kushoto) na Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Mji wa Kibaha Bi.Jenifa Omolo wakibadilishana hati baada ya kusaini makubaliano ya umilikishwaji wa eneo la ardhi, lenye ukubwa wa mita za mraba 400,000 Dar es Salaam leo, ambayo itatumika kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha kuzalishia dawa na vifaa tiba Kibaha mkoani Pwani.

TAMKO LA WN-OMR - MMZ BW. JANUARY Y. MAKAMBA KWA VYOMBO VYA HABARI MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA AFRIKA TAREHE 3 MACHI, 2017

February 27, 2017



Kulia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Profesa Faustin Kamuzora, akitoa Tamko la Siku ya Mazingira Afrika kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Mkamba, Leo katika mkutano na waandishi wa Habari Mtaa wa Luthuli Jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira wa Ofisi hiyo Bw. Richard Muyungi.
Ndugu Wananchi,

Tarehe 3 Machi kila mwaka watanzania wote huungana na nchi nyingine za Afrika katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Afrika, ambayo huadhimishwa barani Afrika  kila mwaka. Siku hii imetengwa kwa lengo la kukumbuka umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira barani Afrika. Azimio la kuadhimisha Siku hii lilipitishwa na kuamuliwa na Baraza la Mawaziri wanaosimamia Mazingira wa nchi za Afrika kwenye mkutano uliofanyika Durban, Afrika Kusini Mwaka 2002. Siku hii iliamuliwa iwe kielelezo cha kukuza weledi kuhusu kupambana na uharibifu wa mazingira pamoja na kuenea kwa hali ya jangwa Afrika. Kuanzia wakati huo siku hii ilikuwa inaadhimishwa nchini Ethiopia kwenye makao makuu ya Umoja wa Afrika.
Ndugu Wananchi,
Kikao cha 12 cha Baraza la Mawaziri wa Mazingira (AMCEN) kiliamua kwamba maadhimisho ya siku hii yawe yanafanyika kikanda. Hivyo kuanzia mwaka 2009 maadhimisho ya siku  ya Mazingira Afrika yalianza kufanyika kikanda katika nchi za Afrika na ndipo, mwaka 2010 nchi yetu ikapata fursa ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho haya  yaliyofanyika jijini Arusha.  
Aidha, Umoja wa Afrika kwa kutambua juhudi na kazi iliyofanywa na Prof. Wangari Maathai kutokana na mchango wa mwanamke huyu katika hifadhi ya mazingira na  kuwezesha wanawake katika usimamizi endelevu wa maliasili na mazingira kwa ujumla waliamua tarehe 3 Machi kila mwaka iwe pia ni siku ya kumkumbuka yake iende sambamba na maadhimisho ya siku ya Mazingira Afrika. Hivyo tangu mwaka 2012 maadhimisho ya Siku ya Mazingira Afrika yamekuwa yakienda sambamba na maadhimisho ya Siku ya Wangari Maathai ili kutambua mchango wake katika utunzaji wa Mazingira. Mwanamke huyu alipata Tuzo ya heshima ya Nobel Laureate's green legacy kutokana na juhudi alizofanya.   

Ndugu Wananchi,
Tunapoadhimisha siku hii tutafakari kwa kina changamoto mbalimbali zinazochangia uharibifu mkubwa wa Mazingira. Changamoto hizo ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi, kuongezeka kwa hali ya jangwa na ukame, uchafuzi wa mazingira, ongezeko kubwa la idadi ya watu, kuwepo kwa shughuli za kiuchumi zisizoendelevu ambazo husababisha uharibifu wa mazingira. Hali hizo husababisha ongezeko la joto, ongezeko la ukame, mvua zisizotabirika, mafuriko, ongezeko la magonjwa mbalimbali ya mlipuko, upotevu wa bioanuai, uhaba wa chakula na hivyo kusababisha kuwepo kwa ongezeko la umaskini kwa jamii. 

Ndugu Wananchi,
Tunafahamu kabisa hali ilivyo sasa katika maeneo mengi nchini kwamba majira ya mvua yamebadilika na kusababisha ukame. Hivyo, inabidi tuhakikishe tunavilinda vyanzo vya maji kwa gharama yoyote ile. Aidha, katika kuadhimisha maadhimisho haya, kila mmoja awawajibike ipasavyo katika kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi yasiyoendelevu ya bioanuai na rasilimali zake. Hivyo kila mtu afanye shughuli za kiuchumi zisizoharibu mazingira ikiwa ni pamoja na  kutumia nyenzo za uvuvi endelevu, kutumia nishati jadidifu, majiko sanifu na banifu, nishati mbadala, kudhibiti uchafuzi, kupunguza uzalishaji wa taka na kusimamia ukusanyaji wa taka ili kuhakikisha miji yetu inakuwa safi.

Ndugu wananchi,
Natoa wito kwa watanzania tuadhimishe Siku ya Mazingira ya Afrika kwa kuendeleza na kusisitiza kampeni ya usafi katika maeneno yetu. Aidha, ninawagiza wananchi wote kuanzia ngazi ya Kaya, Mitaa, vikiwemo vikundi vya watu binafsi kushiriki kwenye shughuli za usafi ili kuhifadhi mazingira yetu. Nitumie fursa hii kuwakumbusha viongozi kuanzia  ngazi ya kijiji hadi mkoa kutumia fursa hii kuhuisha Kamati za Mazingira ili ziweze kusimamia shughuli za utunzaji mazingira katika maeneo yao. Aidha, mikoa, halmashauri za wilaya, sekta zote, pamoja na taasisi mbalimbali, mashirika yasiyo ya kiserikali  na wananchi wote kwa ujumla kushiriki katika shughuli za hifadhi na usafi wa mazingira  wakati wote. 
RC MRISHO GAMBO ATEMBELEA NYUMBANI KWA HAYATI EDWARD SOKOINE

RC MRISHO GAMBO ATEMBELEA NYUMBANI KWA HAYATI EDWARD SOKOINE

February 27, 2017

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo wikiendi hii alipata nafasi ya kutembelea nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani Hayati Edward Moringe Sokoine huko Monduli juu Wilayani Monduli. 

Mh.Gambo alipata wasaaa wa kuzungumza na wajane wa kiongozi huyo mkubwa wa Kitaifa aliyefariki kwa ajali ya gari mwaka 1984 eneo la Dumila huko Mkoani Morogoro, Mkuu wa mkoa alipata wasaa wakuzungumza na familia hiyo pamoja na wakazi majirani wanaozunguka familia hiyo na kusema maneno machache ambapo Alisema 

"Kutembelea maeneo haya ambapo zipo kumbukumbu za mashujaa wetu waliolipigania Taifa letu kwa uzalendo mkuu, inatusaidia sisi viongozi vijana kuzirudia hadhiri zetu za uongozi ili tuweze kuwatumikia wananchi wanyonge kwa Uadilifu na uwajibikaji,ili kuacha alama katika nafasi tulizopewa na kuwatumikia wananchi kama walivyofanya wazee wetu hawa." 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo,Akisalimiana na Mjane wa Hayati Sokoine.
Kutoka Kulia ni Diwani wa Monduli juu akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli na pia ni Diwani wa Monduli Mjini Mh:Issack Joseph,akisalimiana na Mjane wa Hayati Sokoine .
Mh: Gambo akiwa ameambatana na Mjane wa Sokoine Pamoja na watumishi mbalimbali wa Serikali,Wakitoa Heshima kwenye kaburi la Hayati Sokoine.  
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh: Mrisho Gambo akipanda mti wa kumbukumbu nyumbani kwa Hayati Sokoine.Picha na Msumbanews.com

Serikali kutoa matrekta ili kuinua kilimo biashara kwa wanawake.

February 27, 2017


SERIKALI imeahidi kutoa pembejeo za kilimo cha kisasa yakiwemo matrekta kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kupitia taasisi inayojihusisha na kuendeleza wanawake katika kilimo Tanzania (CAWAT) ili waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo cha kisasa hususani cha kibiashara.
 
Ahadi hiyo ya Serikali ya serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha kwa Niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akizungumza kwenye harambee kukusanya fedha kwa ajili ya kuwezesha mradi wa kuwajengea uwezo wanawake waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo biashara iliyoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Land O’ Lakes kwa kushirikiana na CAWAT na kufanyika jijini Dar es salaam mwshoni mwa wiki.
 
“Serikali ipo tayari kutoa pembejeo hizo za kilimo cha kisasa yakiwemo matrekta bora kabisa ambayo yataolewa kwa vikundi vya kina mama wanachama wa CAWAT ambao wataonyesha nia na uwezo wa kutekeleza kilimo cha kisasa hususani cha kibiashara. Zaidi wanufaika hao watahakikishiwa soko la uhakika kwa kile watakachozalisha,’’ alisema Ole Nasha ambae pia yeye binafsi alitoa mchango wa mil. 2 kwenye harambee hiyo.

Alisema serikali ipo tayari kushirikiana na taasisi yeyote nchini yenye nia ya dhati katika kuleta mabadiliko yenye tija yatakayoliwezesha taifa kuongeza kasi yake katika kuelekea uchumi wa viwanda na mapinduzi ya kilimo.

Hatua hiyo ya serikali inakwenda sambamba na ahadi ya Benki ya Maendeleo ya kilimo nchini (TADB)kwa CAWAT ambapo kupitia Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wake Bw Francis Assenga, ilitangaza kwenye warsha hiyo kwamba ipo tayari kushirikiana na CAWAT ili kutoa ushauri utakaoambatana na fursa ya kutenga sh milioni 600 kwa ajili ya kuwajengea uwezo wanawake katika kuendesha kilimo hicho cha kibiashara kupitia taasisi hiyo.

"Kupitia ushirikiano wetu huo na CAWAT ni wazi kwamba TADB tunakwenda kufanya mabadiliko makubwa kwenye sekta ya kilimo hasa cha kisasa kupitia wanawake nchini. Baada ya kupitia malengo ya CAWAT tumelizika moja kwa moja kuwa tuna kila sababu ya kushirikiana nao ili kuifikisha hii nchi kwenye uchumi wa viwanda kupitia kilimo,’’ alisema.

Katika harambee hiyo kiasi cha pesa zaidi ya milioni 27 kilipatikana ikiwa ni ahadi na taslimu, huku pia ikielezwa kuwa Balozi za Japan na Switzerland hapa nchini zimeonyesha nia ya kusaidia miradi mbalimbali itakayoendeshwa na taasis hiyo ya CAWAT.

Awali wakizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa taasisi ya CAWAT Dk Victoria Kisyombe pamoja na Mkurugenzi Mradi kutoka taasisi ya Land O’ Lake Dr Rose Kingamkono walisema kwa sasa taasisi ya CAWAT ipo kwenye mchakato wa awali wa kuanza kujitegemea yenyewe kiuendashaji bila kutegemea msaada iliyokuwa ikiupata kutoka shirika la msaada la Marekani USAID. 

 Mkurugenzi Mradi kutoka taasisi ya Land O’ Lake Dr Rose Kingamkono akizungumza kwenye harambee ya kukusanya fedha  kwa ajili ya kuwezesha mradi wa kuwajengea uwezo wanawake waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo biashara iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya washiriki wa harambee hiyo.
 Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha  akizungumza kwenye harambee hiyo.  Ole Nasha alimuwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye harambee hiyo iliyofanyika kwa mafanikio makubwa!
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini  (TADB) Bw Francis Assenga akizungumza kwenye harambee hiyo.Benki hiyo ilitangaza nia yake ya kutenga sh milioni 600 kuwezesha miradi ya taasisi  ya CAWAT.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa taasisi inayojihusisha na kuendeleza wanawake katika kilimo Tanzania (CAWAT)  Dk Victoria Kisyombe (Kushoto) akipeana mkono wa pongezi na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) Bw Francis Assenga kwenye harambee hiyo ikiwa ni ishara kuanza kwa ushirikiano baina ya taasisi hizo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mradi kutoka taasisi ya Land O’ Lake Dr Rose Kingamkono.
 Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa taasisi za CAWAT, Land O’ Lake, SAGCOT pamoja na maofisa wa juu wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) kwenye harambee hiyo.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha akipeana mkono wa pongezi na Meneja Uhusiano wa Mfuko wa pesheni wa PPF, Lulu Mengele ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa mfuko huo kwenye harambee hiyo.

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA WAWAKILISHI WA SEKTA BINAFSI KUJADILI MCHAKATO WA TATHMINI YA ATAHRI KWA MAZINGIRA.

February 27, 2017


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January Makamba  akiwa katika kikao  na wawakilishi wa sekta binafsi wakizungumza kuhusu masuala ya ufanisi katika mchakato wa Tathmini ya athari za Mazingira. Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Profesa Faustin Kamuzora. Kikao hiko kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam



Baadhi ya Wadau wa sekta binafsi waliohudhuria kikao hiko wakiwa pamoja na Watumishi na Wataalamu toka Ofisi ya Makamu wa Rais na Baraza la Usimamizi wa mazingira(NEMC) wakimsikiliza Mh. Waziri January Mkamba(hayupo pichani) wakati wa kikao hiko.




Mmoja wa Wadau toka sekta binafsi za wenye mahoteli, viwanda na fukwe Bi. Lathifa K. Sukes akichangia jambo katika kikao hiko. (PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI OMR)