KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA TANGA YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAJI MUHEZA.

November 08, 2023

Mjumbe wa kamati hiyo Ndugu, Omari AyubuW wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Tanga akizungumza wakatiwa ziara hiyo

 







Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga ikiongozwa na Mjumbe wa kamati hiyo Ndugu, Omari Ayubu imetembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Muheza Mjini unaosimamiwa na TANGA UWASA.


Akisoma taarifa ya mradi kwa viongozi na wajumbe wa ziara hiyo, Mhandisi Violet Kazumba kutoka kitengo cha Miradi amesema kuwa, Utekelezaji wa mradi huu ni muendelezo wa miradi ambayo imetekelezwa katika eneo la Muheza mjini lengo kuu ikiwa ni kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi, ambapo mradi huu unatarajiwa kunufaisha wakazi wapatao 11,000 katika maeneo ya Tanganyika, Kwemkabara na Masuguru ambao kwa sasa wanapata huduma ya maji kwa mgao.


"Mradi unagharama ya Shilingi Mil.638 na unatekelezwa kwa njia ya mfumo wa Force Acount, ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 80 na baadhi ya wananchi wa maeneo husika wameanza kunufaika na mradi huu kwa kupata huduma ya maji kupitia vituo saba (7) vya kuchotea maji vilivyojengwa na kukarabatiwa katika maeneo mbalimbali" Alisema Mhansi Kazumba.


Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa na kukagua mradi huo Mjumbe wa kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga Ndugu, Omari Ayubu ameipongeza TANGA UWASA kwa kazi nzuri inayoendea kufanyika katika kuhakikisha wananchi wa Muheza wanapata huduma ya majisafi.


"Nawapongeza wenzetu wa TANGA UWASA kwa kazi nzuri na jitihada zao katika kuhakikisha wananchi wanapata maji na niwatake wananchi tuwe walinzi wazuri wa miundombinu ili tufanikishe upatikanaji wa huduma nzuri na kwa wakati wote", alisema.


Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga inafanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo lengo ni kuhakikisha ilani ya chama cha mapinduzi inatekelezwa na wananchi wanapata huduma pasipo changamoto yoyote.





DC SAME AENDELEA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI NA KUZITOLEA MAJIBU

November 08, 2023

 Na Ashrack Miraji Same kilimanjaro


MKUU wa Wilaya ya Same Kasilda mgeni ameendelea na ziara zake kusikiliza na kutatua kero za wananchi ambapo akiwa Kata ya Njoro amepokea kero ya ubovu wa barabara, kukosekana kwa nishati ya umeme kwenye baadhi ya Vitengoji pamoja na upatikanaji wa maji safi na salama.

Mgeni amepokea kero hizo wakati wa mkutano wa hadhara wa wakazi wa kata hiyo uliofanyika katika Kijiji cha Emuguri ambacho asilimia kubwa ya wakazi wake ni wafugaji ambapo walitumia mkutano huo kuwasilisha kero hizo.

Akitolea ufafanuzi hoja hizo mkuu huyo wa Wilaya amesema tayari Serikali ya imeshatoa zaidi ya Sh.bilioni tisa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya barabara kwenye Wilaya ya Same na miongoni mwa barabara zilizo kwenye mpango wa matengenezo ni barabara kutoka makao makuu ya kata hadi kwenye kijiji hicho cha Emuguri ambayo ipo kwenye bajeti ya mwaka huu 2023/2024 ambayo muda wowote itaanza kutengenezwa.

Upande wa nishati ya Umeme wananchi walihoji kuwa baadhi ya vitongoji kwenye kata hiyo havina umeme, ambapo kwa mujibu wa wataalam vitongoji vyote vipo kwenye mpango wa kufikishiwa umeme kwa bajeti ya mwaka huu ambapo serikali emetenga zaidi ya shilingi Milion 700 atika baejeti ya mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na miradi ya Umeme kuhakikisha ifikapo mwaka 2025 maeneo yote ya Wilaya ya Same yemefikiwa na huduma.

Kuhusu maji safi amesema Serikali imeanza taratibu za kutaka kuchimba kisima kikubwa kupunguza changamoto iliyopo pia kijiji hicho cha Emuguri ni kati ya vijini 16 vya wilaya ya Same vitakavyo nufaika na mradi mkubwa wa Same, Mwanga-Koroge ambao kwa awamu ya kwanza utakamilika Juni mwakani mradi huo utagharimu zaidi ya shilling Milion 137.

“Kwa niaba ya wakazi wa Same tunamshukuru Sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutujali wananchi wake na kuridhia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na sisi wasaidizi wake ahadi yetu ni kuimarisha usimamizi kuhakikisha fedha zote zinazo tolewa na serikali zinatumika kama ilivyoekusudiwa kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyo kubalika."

Aidha mkuu huyo wa wilaya amewataka wakazi wa Same kuwa walinzi wa miundombinu inayotekelezwa kwenye wilaya hiyo kuhakikisha inadumu kwa muda mrefu,na kusisitiza pia utunzaji wa mazingira hasa maeneo ya vyanzo vya maji.





REA YATENGA BILIONI 10 KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI VIJIJINI

November 08, 2023

 Na Veronica Simba – REA


Wakala wa Nishati Vijijini (REA), katika Mwaka huu wa Fedha (2023/24), umetenga shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kusambaza mitungi ya gesi ya LPG, majiko na vifaa vyake katika maeneo ya vijijini kwa njia ya ruzuku.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameyasema hayo wakati akiwasilisha Taarifa ya Wakala kwa Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, Novemba 7, 2023.

Alisema kuwa, kiasi cha mitungi kati ya 200,000 hadi 500,000 inatarajiwa kusambazwa katika maeneo ya vijijini kutegemea kiwango cha ruzuku kitakachotolewa.

Akielezea Mradi wa usambazaji gesi ya kupikia kwa ujumla, Mhandisi Saidy alisema unategemewa kusambaza mitungi ya gesi 70,020 ambapo hadi kufikia Agosti 15 mwaka huu, mitungi 23,806 (sawa na asilimia 34) ilikuwa imeshasambazwa kwa wananchi mbalimbali kupitia kwa Wabunge ambao ni wawakilishi wao.

“Lengo la Serikali kupitia REA katika utekelezaji wa Mradi huo ni kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika maeneo yao,” alifafanua.

Aidha, Mkurugenzi Mkuu alieleza kuwa, katika hatua nyingine, REA inatekeleza Mradi wa usambazaji gesi asilia kwa ajili ya kupikia katika mikoa ya Lindi na Pwani kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), ambapo alisema Mkataba umesainiwa na maombi ya fedha za awali, yapo Wizara ya Fedha kwa ajili ya uhakiki.

“Mkataba huu una jumla ya shilingi bilioni 6.8 ambapo unatarajiwa kuunganisha wananchi 980 na nishati ya kupikia katika maeneo ya Mnazi Mmoja mkoani Lindi na Mkuranga mkoani Pwani.”

Alisema kuwa, katika Mwaka huu wa Fedha (2023/24), REA imetenga shilingi bilioni 18.5 kwa ajili ya kuiwezesha TPDC kujenga miundombinu ya kusambaza gesi asilia katika maeneo yaliyopo pembezoni mwa Mkuza wa Bomba Kuu la kusafirisha gesi asilia linalopita katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Pwani ili wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo waweze kutumia gesi asilia kwa ajili ya kupikia.

Mkurugenzi Mkuu pia alieleza kuhusu Mradi wa ufungaji mifumo ya kupikia katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 300 ambapo alisema Wakala unalenga kujenga mifumo hiyo kwa Taasisi 100.

Akifafanua, alisema kuwa Mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati akifungua Kongamano la Nishati ya Kupikia jijini Dar es Salaam, Novemba 2022.

Kuhusu usambazaji wa majiko banifu, alieleza kuwa kupitia ruzuku ya Dola za Marekani milioni sita iliyotolewa na Benki ya Dunia, Serikali kupitia REA inatarajia kusambaza majiko banifu 70,000 yaliyotengenezwa kwa teknolojia yenye ubunifu wa kupunguza matumizi ya kuni na mkaa pamoja na kupunguza uharibifu wa mazingira.

Naibu Waziri Kapinga alitembelea Makao Makuu REA jijini Dodoma na kuzungumza na Menejimenti yake ikiwa ni mara ya kwanza tangu ateuliwe kushika wadhifa huo.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kulia), akiwasilisha Taarifa ya Utendaji Kazi wa Wakala hiyo kwa Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga (katikati), Novemba 7, 2023. Naibu Waziri alitembelea Makao Makuu ya REA jijini Dodoma na kuzungumza na Menejimenti ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu ateuliwe kushika wadhifa huo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka.

Naibu Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge anayewakilisha Vijana Mbinga, Judith Kapinga akiwasha jiko la gesi muda mfupi kabla ya kugawa majiko hayo kwa umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni. Mheshimiwa Kapinga aligawa majiko hayo ikiwa ni sehemu ya Mpango Maalumu wa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuwawezesha wananchi wa vijijini kupitia Wabunge wao, kutumia nishati safi ya kupikia.

Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), wakiwa katika picha ya pamoja. Wanawake hawa wamejiwekea utaratibu wa kuchanga fedha na kununua majiko na mitungi ya gesi ambapo hugawa katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha wanawake waishio vijijini kutumia nishati safi ya kupikia.

Mitungi yenye majiko ya gesi ikiwa imeandaliwa tayari kwa kugawiwa kwa umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoani Ruvuma hivi karibuni ikiwa ni Mpango maalumu wa uwezeshaji wanawake waishio vijijini kutumia nishati safi ya kupikia. Uwezeshaji huu kwa njia ya ruzuku unatolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

UTEUZI: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MUDA HUU NA KUVUNJA BODI YA TCRA

November 08, 2023

 

MPANGO WA TAIFA WA MAENDELEO UWE NA SURA YA UTAIFA KWA VITENDO

November 08, 2023


Na Mwandishi Wetu Dodoma.

MBUNGE wa Viti Maalumu Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe Neema Lugangira ametaka Mpango wa Taifa wa Maendeleo uwe na sura ya Utaifa kwa vitendo badala ya kuyagawa maeneo nchini.

Lugangira aliyasema hayo wakati akichangia mpango huo Bungeni na alisema wanapojadili mpango wa maendeleo ya Taifa anaamini ni muhimu kwa Serikali kuhakikisha maendeleo ya Taifa yanatawanywa kwenye maeneo yote ya nchi.

Alisema kwa kufanya hivyo kutapelekea wao kuweka mipango thabiti ambayo itatafuta nyenzo na njia mbalimbali za kiunua mikoa ambayo ipo kwenye hali ya umaskini.

Mbunge Lugangira alisema ili mikoa hiyo nayo iweze kuendelea kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi na kuchangia pato la Taifa jambo ambalo Rais Dkt Samia Suluhu amekuwa akilisema mara nyingi hata katika ziara yake alipokwenda mkoani Kagera alisema kwa Jiographia na mambo yake haupaswi kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa umaskini nchini.

Alielekeza ifanyike tathimini mbalimbali na kuona namna ya kuihusisha kwenye Serikali ili mkoa huo na pamoja na mikoa mengine yenye kufanana na hiyo iweze kuinuka kiuchumi.

“Mh Mwenyekiti katika hotuba ya mpango wa maendeleo ya Taifa haijaeleza wazi namna gani Serikali imejipanga kuweka mikakati dhabiti ya kuinua mikoa yenye hali ya umaskini na haijaweka mipango mahususi wa kuona namna gani ya kutawanya maendeleo ya nchi yetu”Alisema

Alieleza kwamba kwa harakarahaka anajielekeza kwa Mkoa wa Kagera ambao unapakana na nchi tatu za Afrika Mashariki Uganda, Rwanda na Burundi ikiwemo uwepo wa asilimia kubwa zaidi ya ziwa Victoria pia wana Ranchi Tano na una ardhi yenye rutuba pamoja na misimu miwili ya mvua lakini bado inashangaza kuona mkoa unaongoza kwa umaskini.

“Hivyo kama nchini tunaweza kujiuliza kwanini ipo hivyo jambo la kwanza wameshindwa kuona nambna wanaweza kutumia maeneo ya kimkakati ili yaweza kufungua uchumi wa Taifa letu”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Mkoa wa Kagera unaweza kuwa kitovu cha Taifa cha kuunganisha Biashara kwa nchi za Ukanda wa nchi Afrika Mashariki (Rwanda, Burundi na Uganda) na ili kufanya hivyo lazima uwepo wa kiwanja cha Ndege cha Kimataifa.

Aidha, Lugangira alimpongeza Mhe Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuunda wizara mahususi ya Ofisi Rais inayosimamia mipango na uwekezaji na kuunda tume ya mipango.

Pia alitumia nafasi hiyo kuwapongeza Waziri mwenye dhamana ya wizara hiyo Profesa Kitila Mkumbo na pamoja na Lawarance Mafuru naye kwa kuteuliwa wote kuongoza wizara hiyo kwani ni majembe na wanatosha

Alisema jambo ambalo hawana na hawaelewi hilo litatekeleza vipi,hawana soko kuu la biashara za mazao ya mifugo,kilimo na uvuvi na tatu hakuna mkakati dhabiti wa kuona zile Ranchi tano zinaweza kuwekewa mikakati ili kuchangia maendeleo,hawana viwanda vya kutosha vya samaki

Mbunge huyo alisema pia fedha za misaada pamoja na miradi ya maendeleo kutoka kwa wadau wa maendeleo na mashirika ya kimataifa hayatawanywi ipasavyo kwenye nchi yetu unakuta ni maeneo machache hayo hayo wadau wanakwenda halihali Serikali inapaswa kuweka jitihada za makusudi kuhakikisha inatawanywa kwenye nchi yetu.

Alisema kwamba suala lingine ni kuwa mkoa wa Kagera ni ya sita kwa wingi wa watu bado Hospitali ya Mkoa wa Kagera ni sawa sawa na ya wilaya hadi kufikia kwamba hivi karibuni hadi miezi 18 iliyopita ndio walipata vifaa tiba kwa ajili ya watoto njiti kupitia jitihada zake kwa kushikrikiana na Shirika la Doris Molel Foundation.

“Leo hii watoto 780 wameweza kuokolewa maisha yao na hii inaonyesha mkoa huu kwenye sekta ya afya bado wako nyuma na mkoa huo ndio mara nyingi unapata kadhia nyingi kunapotokea milipuko ya magoinjwa hapa nchini lakini bado uwekezaji wa sekta ya afya kwenye mkoa huo haujaridhisha”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba mkoa huo hawana hata chuo kikuu kwenye mkoa huo ambacho kingweza kupata wanafunzo kutoka nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, Uganda, Burundi, Rwanda,

“Mh Mwenyekiti jambo lingine ni kwamba Serikali ilipoandaa Sagoti ya Tanzania ilikuwa na lengo la kuona namna gani ya uwekezaji utakapofanyika ili kuweza kuimarisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kwenye mikoa ya nyanda za juu kusini ili miaka kadhaa Taasisi kama hiyo iweze kuanzishwa kwenye mikoa mengine ya kanda nyengine hivyo jambo hilo linachangia kupelekea maendeleo kwenye sehemu moja ya nchi na amikoa mengine kuendelea kubaki kuewa nyuma”Alisema

Mbunge Lugangira alisema Mkoa wa Kagera hadi leo ndio unaongoza kwa idadi ya watoto wenye utapiamlo lakini hawana mradi wowote wenye kupambana na hali hiyo lakini wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuwapelekea Mkuu wa mkoa Fatuma Mwasa na Katibu Tawala wa Mkoa huo (RAS) Toba Nguvila ambao wamekuwa na maono makubwa ya kuendelea mkoa huo kutoka uliopo ili uweze kuchangia pato la mkoa huo.

Mbunge huyo alisema kwamba alimuona Waziri Profesa Kitila Mkumbo atakapohitimisha hoja hiyo awaeleza bayana kwamba mpango wa maendeleo ya Taifa unakuwa wa vitendo kwa nchi ya Tanzania bila kuacha maeneo mengine nyuma kama vile Mkoa wa Kagera na Mengineyo kwa kufanya hivyo wanaweza kusema sasa wana mpango wa maendeleo ya Taifa


BODI YA TASAC YAUNGA MKONO NA KUPONGEZA JITIHAZA ZA TPA KUJENGA BANDARI YA KUHUDUMIA MZIGO MCHAFU KISIWA CHA MGAO

November 08, 2023







BODI ya Wakurugenzi ya Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeunga mkono na kupongeza jitihada za Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) kujenga Bandari ya kuhudumua mizigo Mchafu eneo la Kisiwa -Mgao.

Ujenzi huo unatarajiwa kufanyika katika kisiwa hicho kilichopo katika Halmashauri ya wilaya ya Mtwara Mkoani Mtwara ikiwa ni mkakati wa kusogeza huduma karibu na wananchi.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Capt. Mussa Mandia akiwa katika ziara hiyo ya kukagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na TASAC chini ya usimamizi wa Bodi hiyo.

SERIKALI YAWEKA UKOMO BEI ZA UNUNUZI WA BIDHAA

November 08, 2023

 Na. Peter Haule, WF. Dodoma


Serikali imeeleza kuwa imeweka ukomo wa bei za bidhaa ambazo Serikali inanunua kwa kuzingatia bei za soko ili kudhibiti ununuzi wa bidhaa hizo kwa gharama kubwa kuliko zilizopo Sokoni.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Asia Abdulkarim Halamga, aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu kushusha gharama za ununuzi na kuagiza bidhaa hususani magari kulingana na bei ya Soko.

Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali imeweka msisitizo katika Sheria ya manunuzi kwa kuweka ukomo wa bei za bidhaa ambazo Serikali inafanya manunuzi kwa kuzingatia bei za soko.

“Ukomo wa bei za manunuzi ambayo Serikali inafanya si tu kwa magari lakini pia kwa bidhaa nyingine, kuanzia mfumo wenyewe wa manunuzi ambapo Afisa Masuuli anapotaka kulipa kwa gharama za juu kuliko bei ya soko inayotambulika atakuwa amekiuka Sheria”, alisema Dkt. Nchemba.

Akizungumzia suala la kuagiza bidhaa moja kwa moja kutoka viwandani bila kupitia kwa Wakala, Dkt. Nchemba alisema kuwa kuna baadhi ya mazingira yakiwemo ya viwango vya ubora vya baadhi ya bidhaa, Sheria inamruhusu Afisa Manunuzi kununua moja kwa moja lakini hutokea kwa baadhi ya maeneo wanunuzi wenyewe hawapendi Taasisi nunuzi kwenda moja kwa moja kiwandani kwa kuwa viwanda hivyo vinaushirikiano wa moja kwa moja kwa wale wanaofanya nao biashara ambao ni matawi yao au mawakala.

Hata hivyo alisema kuwa mtazamo wa Serikali ni kuendelea kupunguza matumizi ya magari ambapo Serikali iliweka utaratibu kwa wale wenye sifa ya kuwa na magari wakopeshwe ili kuipunguzia Serikali mzigo wa kuyaendesha na kuyafanyia huduma za matengenezo.

Kuhusu Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) kuchelewesha ununuzi wa magari ya Serikali, Dkt. Nchemba alisema kuwa ucheleweshaji huo ulisababishwa na Mabadiliko ya aina (models) za magari yanayotumiwa na Serikali ambapo upatikanaji wa aina mpya huweza kuchukua muda mrefu zaidi kutegemea na idadi ya mahitaji kwa Serikali.

Alieleza kuwa sababu nyingine ni athari za kiuchumi zinazoathiri mnyororo wa uzalishaji na usafirishaji mfano UVIKO-19, iliyosababisha viwanda vinavyozalisha vipuri vya magari kufungwa na kusababisha changamoto ya uhaba wa vifaa vya TEHAMA ambavyo kwa sehemu kubwa ya magari ya kisasa hutumia teknolojia kubwa ya umeme na changamoto ya usafirishaji wa magari, ikiwemo uhaba wa wasafirishaji na ukosefu wa makasha ya kusafirisha mizigo.

Aidha, Mhe. Dkt. Nchemba, alisema kuwa, kwa sasa mnyororo wa ununuzi wa magari duniani umeanza kuimarika na magari yote yanafika kwa wakati na kukabidhiwa kwa Taasisi zilizoagiza, hivyo upatikanaji wa magari kwa wakati umerejea.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akijibu swali bungeni kuhusu Serikali kushusha gharama za bidhaa inazoagiza na kununua hususani magari kulingana na bei ya Soko.

BENKI YA LETSHEGO FAIDIKA YAPATA FAIDA YA SH.BILIONI 1.3 KABLA YA KODI.

November 08, 2023

 Benki ya Letshego Faidika ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa taasisi ya kifedha ya Faidika (Faidika Microfinance) na Benki ya Letshego (Letshego Bank) imepata faida ya Sh1.3 billioni ikiwa ni ongezeko la asilimia 234 kwa kipindi cha robo ya mwaka ya utendaji wake mpaka Septemba 30 mwaka huu.


Faida hiyo ni ya kwanza tangu taasisi hizo mbili kuunganishwa mwezi Juni mwaka huu ambapo mwaka 2022 katika kipindi hicho hicho walipata hasara ya Sh981 milioni huku robo ya awali ya mwaka 2023, kabla ya kodi, Letshego ilikuwa hasara ya Sh464 milioni.

Mafanikio katika utendaji wa benki hiyo mpaka kufikia robo ya kwanza yametokana na uwekezaji katika huduma bora na za kisasa na kufanya mageuzi chanya ya kifedha ndani ya robo moja tu.

Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Letshego Faidika Bw Baraka Munisi alisema, "Tumefurahishwa na mabadiliko chanya ya faida kabla ya kodi katika kipindi kifupi. Baada ya muunganiko na kufanya kazi pamoja , sasa tunalenga kutumia faida za ufanisi mkubwa wa uendeshaji na nguvu kuelekea kutoa faida endelevu kwa wadau wetu."

Bw Munisi aliongeza kuwa baada ya muungano huo Juni mwishoni mwaka huu, mali jumla ya Benki iliongezeka kwa asilimia 213 hadi Sh108 bilioni ikilinganishwa na Sh34 bilioni katika robo ya pili ya mwaka 2023.

Alisema kuwa upande wa mikopo nayo iliongezeka kwa asilimia 465 katika kipindi hicho hicho hadi kufikia Sh 72.7 bilioni ikilinganishwa na Sh12.8 bilioni katika robo ya pili ya mwaka 2023.

“Katika kipindi kama hicho pia, robo ya tatu inayomalizika tarehe 30 Septemba 2023, amana za benki ziliongezeka kwa asilimia tisa ikilinganishwa na robo iliyopita,” alisema.

Kwa mujibu wa Bw Munishi kutokana na ukuaji wa kitabu cha mikopo na ufanisi wa ukusanyaji na kurejeshwaji, kiwango cha mikopo isiyolipika kwa benki kiliboreshwa kutoka asilimia 44 hadi 18 robo kwa robo wakati mali zenye faida kwa jumla ziliongezeka hadi asilimia 72 kutoka asilimia 59 robo kwa robo. Kiwango cha gharama kwa mapato kiliboreshwa hadi asilimia 83 kutoka asilimia 176 katika robo iliyopita.

Bw Munisi alithibitisha azma ya Benki ya Letshego Faidika kuwa moja ya benki za kati zinazoongoza nchini Tanzania katika kipindi cha miaka mitatu hadi mitano.

"Nina matumaini na nimehamasishwa kuhusu mustakabali wa benki yetu huku tukiendelea kuwa na lengo la kutoa utendaji endelevu pamoja na mifumo imara ya utawala wa kiwango cha dunia, kutoa thamani inayoweza kupimika na inayoweza kuhisika kwa wateja na wadau wetu wote.

“Nawapongeza wafanyakazi, wateja, wanahisa, Benki Kuu ya Tanzania, Tume ya Ushindani ya Haki, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na washirika wetu wa biashara kwa ushirikiano na msaada wao unaendelea,” alisema.

Alisema kuwa benki hiyo inaendelea kuwa na azma ya kujenga uthabiti wa biashara ili kukabiliana na changamoto za masoko yanayojitokeza na vile vile kuhakikisha kuwa inaendelea kuboresha maisha ya wateja na wanachama wa jamii kupitia bidhaa na huduma rahisi, nafuu, na zinazofaa.

"Nawashukuru wafanyakazi wote kwa kazi ngumu, uaminifu, na jitihada zisizochoka kwa miaka michache iliyopita kwa kufanikisha mchakato huu kwa Pamoja! Tuko hakika #TunaNguvuPamoja,” alisema Munisi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Letshego Faidika Bw Baraka Munisi akisisitiza jambo wakati wa kutangaza utendaji wa taasisi hiyo wa mwaka mpya wa fedha na kuweza kupata faida bila kodi ya Sh1.3 bilionibila kodi.

OPERESHENI MAALUM YA DCEA YABAINI KIWANDA CHA KUTENGENEZA BISKUTI ZENYE BANGI JIJINI DAR

November 08, 2023

 *Pia wanasa kilo 423 za bangi, yatoa tahadhari ya ulaji vyakula kwa wanafunzi


Na Said Mwishehe, Michuzi TV

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imekamata kilo 423.54 za bangi iliyosindikwa maarufu kama Skanka huku pia kubaini uwepo wa kiwanda cha kutengeneza biskuti zilizochanganywa na bangi katika eneo la Kawe jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Novemba 8, 2023 jijini Dar es Salaam Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema wamekamata Skanka baada ya kufanyika operesheni maalum zilizofanyika kwenye mipaka na fukwe za Bahari ya Hindi.

Amefafanua kilo 158.54 zilikamatwa eneo la Kigamboni na Kawe jijini Dar es Salaam zikiwa zimehifadhiwa ndani ya mabegi ya nguo tayari kwa kusafirishwa , kilo 265 zilikamatwa katika matukio tofauti mikoa ya nyanda za juu Kusini zikiwa zimefichwa ndani ya magari kwa kuchanganywa na bidhaa nyingine ikiwemo maboksi yenye matunda aina ya Apples zikisafirishwa kuelekea jijini Dar es Salaam.

Pia amesema Mamlaka hiyo imekata watu wanaojihusisha na utengenezaji wa biskuti kwa kuchanganya na Skanka katika eneo la Kawe huku akifafanua katika tukio hilo watuhumiwa walikutwa wakiendelea na uzalishaji wa biskuti hizo kwa kutumia mtambo mdogo wa kusaga skanka na vifaa vya kutengeneza biskuti za bangi.

Akifafanua zaidi mbele ya waandishi wa habari , amesema Mamlaka imebaini maeneo yanayotumika kama masoko ya kusambazia na kuuza Skanka kwenye fukwe ya Bahari ha Hindi .

"Kutokana na operesheni hizo meongeza katika operesheni hizo watu 16 wamekamatwa ambapo kati yao sita wamefikishwa mahakamani na 10 watafikishwa baada ya taratibu za kisheria kukamilika."

Akifafanua kuhusu Skanka( Skunk) amesema ni jina la mtaani linaloitambulisha aina ya bangi yenye kiwango kikubwa cha sumu ikilinganishwa na bangi ya kawaida.

Ameongeza dawa hiyo ya kulevya hutokana na kilimo cha bangi mseto ambapo asilimia 75 ni bangi aina ya Sativa na asilimia 25 ni bangi aina ya Indica."Kiwango cha sumu kilichopo kwenye sanka ni zaidi ya asilimia 45 ukilinganisha na bangi ya kawaida ambayo kiwango chake cha sumu ni kati ya asilimia 3 mpaka 10.

"Hivyo Skanka ina madhara makubwa zaidi kwa mtumiaji ikiwemo kuamsha na kuzidisha magonjwa ya afya ya akili kwa haraka.Imebainika kuwa watu wasiowaaminifu huchanganya sanka kwenye vyakula kama vile biskuti, keki, jamu , sharubati , tomato souce pia kwenye sigara na shisha.

" Lengo la kufanya hivyo ni kurahisisha uuzwaji wa dawa hizo kwa kuficha na kuongeza idadi ya watumiaji wa dawa za kulevya hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya vyakula hivyo hupendwa na watoto, "amesema.

Lyimo amesema wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo wanapaswa kuwa makini na vyakula hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya vyakula hivyo hupendwa na watoto.

Pamoja na hayo amesema Mamlaka hiyo inaendelea kufanya operesheni dhidi ya wasafirishaji na wazalishaji wa dawa za kulevya katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha dawa za kulevya haziendelei kuwepo nchini.

" Tunawaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za wahalifu wa dawa za kulevya kwa kupiga namba ya bure ya 119 ambapo taarifa zitapokelewa kwa usiri mkubwa na kufanyiwa kazi."

Hata hivyo alipoulizwa Mamlaka inampango gani wa kuchukua hatua kwa baadhi ya wauza shisha ambao wanachanganya na bangi, amejibu kuwa kwa sasa wapo katika mchakato wa kuwepo kwa sheria hivyo itakapokamilika Mamlaka itatoa taarifa kuhusu shisha.

Alipoulizwa ni hatua gani zinachukuliwa na Mamlaka hiyo kudhibiti uzalishaji wa biskuti zinazochanganywa na bangi pamoja na aina nyingine ya vyakula, amejibu wameendelea kuchukua hatua ikiwa pamoja na kuvunja mtandao wa wazalishaji wa biskuti hizo akitolea mfano wote waliokuwa wanahusika na kiwanda kilichopo Kawe wamekamatwa na kesi iko mahakamani na wengine wamefungwa.

Amesisitiza Mamlaka imeendelea na mapambano dhidi ya dawa za kulevya na hivyo kusababisha dawa za kulevya kupungua nchini na matokeo yake waraibu wa dawa hizo wanalazimika kutumia dawa mbadala pamoja na dawa za Waraibu

Aidha amesema kutokana na kufanyika kwa operesheni ya kutokomeza dawa za kulevya nchini hivi sasa wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa hizo kuingiza bangi kutoka nchi nyingine lakini Mamlaka imeimarisha ulinzi mipakani ili kuhakikisha hakuna dawa za kulevya zinazoingia nchini.






Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo
 

BODI YA WAKURUGENZI TBS YAFANYA ZIARA BANDARI YA BAGAMOYO NA MBWENI

November 08, 2023

 


NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

BODI ya Wakurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetembelea katika bandari ya Bagamoyo na Mbweni kwa lengo la kutazama mambo yanavyofanyika katika ukaguzi wa bidhaa na changamoto zinazopatikana ili kuboresha shughuli za ukaguzi katika bidhaa zinazoingia kupitia bandari hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa habari katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi TBS, Prof. Othman Chande amesema kuwa wamefika mahali hapo na wamegundua changamoto kadhaa mojawapo ikiwa ni jinsi upakuaji mizigo husika unavyofanyika.

"Mafuta yanavyoingia hapa yanatupwa baharini watu wanasukuma kutoa nje hii mbinu siyo nzuri sana , ila kwa sasa inabidi tuende nayo tu hivyohivyo Amesema Prof.Chande.

Naye Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki Bw.Fransis Mapunda amesema kuwa wanaishukuru Bodi ya wakurugenzi ya TBS kuwatembelea na kuwapa muongozo jinsi ya kutatua changamoto wanazopitia hasa katika kuhakikisha bidhaa zinazoingia nchini zinakidhi matakwa ya viwango.

Amesema katika Bandari hiyo wana ofisi ambayo imekuwa ikikagua mizigo inayoingia na inayopitia hapo kwenda visiwani Zanzibar na sehemu nyingine mbalimbali.

Pamoja na hayo Bw. Mapunda ametoa wito kwa wafanyabiashara kutumia ofisi ya TBS kupitisha mizigo yao kwani ni kituo rasmi kilichowekwa na serikali ili kuepuka hasara itakayopatikana baada ya kukamatwa kwa yule ambaye anakiuka utaratibu uliowekwa.

"Mizigo inayofika katika bandari hii ikichukua muda mrefu, inachukua masaa sita inakua imesha shughulikiwa itoke katika eneo hili hivyo basi natoa wito kwa wafanyabiashara wapitie kupitisha mizigo yao tuweze kuikagua kwa maana wakipitisha sehemu nyingine ile mizigo ikikamatwa itakua hasara kwao kwani itaenda kuteketezwa". Amesema Bw. Mapunda

Kwa Upande wake Mfanyabiashara wa Mafuta Bw.Frank Kimaro ameipongeza TBS kwa kuwapatia huduma nzuri ambayo haina usumbufu kwao kama wafanyabiashara hivyo amewaomba wafanyabiashara ambao wamekuwa wakienda kinyume na utaratibu uliowekwa na TBS kuacha kutumia njia zisizo sahihi na kuweza kupitia TBS ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara.

"Ukiomba kibali ndani ya masaa mawili kila kitu kinakuwa kimeshasoma na changamoto ya mizigo midogomidogo labda kuhusu batch namba mengine wanatusaidia maafisa wa TBS"Amesema.

SEMA, STROMME FOUNDATION WAJIVUNIA MAFANIKIO MIAKA MIWILI MRADI WA ELCAP MKOANI SINGIDA

November 08, 2023

 



Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga, akifunga kikao kazi cha kutathimini utekelezaji wa mradi wa ELCAP wa miaka mitano ulioanza Septemba 20, 2021 ambao unatarajia kumalizika Mwezi Juni, 2026/ unao tekelezwa na Shirika la SEMA kwa kushirikiana na Shirika la Stromme Foundation Tanzania.


............................................................................





Na Dotto Mwaibale, Singida
SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA) lenye makao yake makuu mkoani Singida kwa kushirikiana na Shirika la Stromme Foundation Tanzania kupitia mradi wa Kilimo Biashara wa ELCAP katika kipindi cha miaka miwili ya utekelezaji wa mradi huo wamepata mafanikio makubwa ya uongezaji uzalishaji wa mazao kwa kutoa elimu za teknolojia mbalimbali za kilimo.

Mkurugenzi wa SEMA, Ivo Manyaku akizungumza Novemba 7, 2023 kwenye kikao kazi cha kutathimini utekelezaji wa mradi huo wa miaka mitano ulioanza Septemba 20, 2021 ambao unatarajia kumalizika Mwezi Juni, 2026 umekuwa na mafanikio makubwa kwa wakulima.

Alisema lengo la mradi huo ni kuwawezesha wakulima wadogo kuzalisha kwa ubora zaidi na kupata mazao mengi katika eneo dogo.


Manyaku alisema mradi huo ni mahususi kwa vijana na wanawake na ni muendelezo wa vikundi vilivyokuwa vikitumika katika mradi wa awali wa kuweka na kukopa na sasa wanawatoa katika eneo hilo na kuwaingiza kwenye uzalishaji wenye tija na kuongeza thamani kupitia mazao ya kilimo ambayo ni mahindi, alizeti, mtama na mbaazi.

Aidha, Manyaku alisema kupitia mradi huo wamefanikiwa kuwatafutia wakulima masoko kwa kuwaunganisha na wadau mbalimbali na wafanyabiashara .

Akitaja mafanikio mengine kuwa kabla ya kuanza kwa mradi huo wakulima walikuwa wakipata magunia ya mahindi kati ya sita hadi saba kwa heka moja lakini sasa wanapata magunia 15 hadi 20 na akamtaja mmoja wa wakulima hao kutoka Wilaya ya Ikungi kuwa alipata magunia 10 katika nusu heka.

Alisema lengo la mradi huo ni kuwafikia wakulima 6000 na kati ya hao asilimia 40 wawe vijana na asilimia mbili watu wenye ulemavu na kuwa umejikita kuhakikisha kuwa teknolojia wanazo wapa zinaendelea kuwasaidia wakulima hata baada ya mradi huo kumalizika.

Alisema pamoja na kuwa na lengo la kuwafikia wakulima 6000 lakini kwa kupitia mnyororo wa thamani wanatamani kuwafikia wakulima 10,000 katika wilaya ambazo unafanyika mradi huo ambazo ni Iramba, Ikungi na Manyoni na kuwa gharama ya mradi huo ni Sh.Bilioni 4.5.

Alisema mradi huo unatekelezwa na SEMA kwa kushirikiana na Stromme Foundation na nchi ya Norway pamoja na washirika wao wa kimkakati, NGI, CSFS na NMBU ambao wanawawezesha kuwapa teknolojia.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga ambaye alikuwa mgeni rasmi alishiriki kikao hicho na alitoa maoni yake namna ya kuboresha zaidi mradi huo ambapo alipongeza mashirika hayo kwa kuusaidia Mkoa wa Singida katika sekta ya kilimo.

“Katika mradi huu ni Singida peke yake ndiyo inasaidiwa kuhakikisha inaboresha kilimo ili kuongeza uzalishaji na hasa kwa kutumia teknolojia inayokwenda kuhifadhi maji katika mashamba yetu na kurutubisha ardhi na kuboresha maisha ya familia zetu,” alisema Mganga.

Alisema kwa kuwa mradi huo una walenga wakulima wadogo hasa wanawake na vijana katika wilaya za Ikungi, Iramba na Manyoni anaamini kutokana na kuwa wepesi wa kuelewa watakwenda kuleta mabadiliko chanya kwenye familia zao kwani wakiwezeshwa kupata mikopo na mbegu bora mashamba yao yanakwenda kuwa dhahabu katika Mkoa wa Singida.

Pamoja na mambo mengine alishauri mradi huo uweze kufika mpaka shule za msingi na sekondari.kwa ajili ya lishe kwa wanafunzi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Bajeti Wizara ya Kilimo, Mohammed Chikawe aliyashukuru mashirika hayo kwa kuungamkono jitihada za Serikali katika sekta ya kilimo mkoani hapa na kueleza mradi huo unatekelezwa vizuri ambapo alitumia nafasi hiyo kuwaomba wadau hao wa maendeleo kuusambaza na kwenye mikoa mingine ili nayo iweze kupata teknolojia hiyo ya uzalishaji wa mazao na kuongeza thamani pamoja na kuwatafutia masoko kama ilivyofanya katika Mkoa wa Singida.

Wajasiriamali na wanufaika wa mradi huo Anna Ntandu kutoka Wilaya ya Ikungi na Rehema Mwaliwa kutoka Kata ya Iseke wilayani Ikungi waliyashukuru mashirika hayo kwa kuwapa mafunzo ya kilimo biashara ambayo yamewakomboa kiuchumi na kuweza kujikimu kimaisha na kusomesha watoto wao.

“Changamoto kubwa tuliyonayo ni vifaa vya kufanyia kazi, mtaji na masoko ya uhakika kwa mfano mimi nalazimika kutumia sufuria kwa ajili ya kuoka mkate badala ya oveni naomba tunapo hitimu mafunzo tuwe tunawezeshwa vifaa hivyo hata kwa kukopeshwa,” alisema Mwaliwa.
Mkurugenzi wa SEMA, Ivo Manyaku akitoa taarifa ya mradi huo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Bajeti Wizara ya Kilimo, Mohammed Chikawe, akizungumza kwenye kikao hicho.

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa SEMA, Daniel Chacha, akizungumza kwenye kikao hicho.

Mwakilishi wa Shirika la CSFS kutoka Zambia, Gibson Simusokwe, akitoa mada kwenye kikao hicho.

Mwakilishi kutoka Shirika la NGI la , Nchini Norway Profesa Gerard Cornelissen, akizungumza kwenye kikao hicho.

Mwakilishi wa Shirika la NMBU kutoka Nchini Norway, Profesa. Jan Mulder, akizungumza kwenye kikao kazi hicho.

Mratibu wa miradi wa ELCAP, Alunas Maxwell, akiongoza kikao kazi hicho.

Meneja wa Miradi ya Stromme Foundation Tanzania , Doreen Matekele, akizungumza kwenye kikao hicho.

Mjasiriamali mnufaika na mradi huo, Anna Ntandu akiyashukuru mashirika hayo kwa kuwapa mafunzo ya kilimo biashara.

Mnufaika na mafunzo ya kilimo biashara, kutoka Kata ya Iseke wilayani Ikungi, Rehema Mwaliwa akitoa shukurani baada ya kupata mafunzo hayo.

Washiriki kutoka Stromme Foundation Kampala Uganda wakiwa kwenye kikao kazi hicho.

Kikao kikiendelea.

Kikao kazi kikiendelea..

Taswira ya kikao kazi hixmafunzo hicho.

Mgeni rasmi wa kufunga kikao hicho, Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga, akikagua bidhaa za wajasiriamali walionufaika na mradi huo.

Picha ya pamoja na wadau wa mradi huo kutoka Norway.

Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la SEMA.