KOROGWE WATAWADHWA KUWA MABINGWA WA COPA COCA COLA MKOA.
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
TIMU ya soka wilaya ya Korogwe leo imetawadhwa kuwa mabingwa wapya wa Mashindano ya Vijana ya Copa Coca Cola ngazi ya mkoa baada ya kufanikiwa kuichapa Muheza mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.
Mchezo huo ambao ulianza majira ya saa nane mchana ulikuwa mkali na wenye upinzani wa hali ya juu kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu na kuonyesha kandanda nzuri na la kuvutia ambapo hadi timu zote zinakwenda mapumziko,Korogwe walikuwa wakiongoza bao 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote ziliingia uwanjani hapo zikiwa na hari ya mchezo baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Mabao ya Korogwe yalifungwa na Erick Msagati ambaye alipachika mabao yote kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.
TIMU ya soka wilaya ya Korogwe leo imetawadhwa kuwa mabingwa wapya wa Mashindano ya Vijana ya Copa Coca Cola ngazi ya mkoa baada ya kufanikiwa kuichapa Muheza mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.
Mchezo huo ambao ulianza majira ya saa nane mchana ulikuwa mkali na wenye upinzani wa hali ya juu kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu na kuonyesha kandanda nzuri na la kuvutia ambapo hadi timu zote zinakwenda mapumziko,Korogwe walikuwa wakiongoza bao 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote ziliingia uwanjani hapo zikiwa na hari ya mchezo baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Mabao ya Korogwe yalifungwa na Erick Msagati ambaye alipachika mabao yote kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.
CHIZA ADAM KINDA WA MIAKA 12 ALIYEKUSUDIA KURITHI NAMBA YA SULEIMAN KASSIM SELEMBE KATIKA TIMU YA TAIFA YA ZANZIBAR (ZANZIBAR HEROES) .
NA MASANJA MABULA,PEMBA.
Kwa wale ambao walikuwa wakifuatilia kwa karibu michuano ya
vijana waliochini ya umri wa miaka 15 iliyomalizika hivi karibuni katika shehia
za Tondooni na Makangale Wilaya ya Micheweni waliridhika na kiwango
kilichooneshwa na kinda Chiza Adam wa timu ya Chuo Kids .
Kinda huyo anayemudu kucheza nafasi ya kiungo mshambauliaji
(namba nane)aliiwezesha timu yake kuibuka bingwa wa michuano hiyo iliyoandaliwa
na mwandishi wa makala haya na kupata ufadhili kutoka shirika la habari la
Korea CTS , chini ya usimamizi wa mchungaji Samwel E. Maganga wa kanisa la TAG .
Katika michuano hiyo kinda huyo alionesha uwezo mkubwa na hivyo
kuwa ni gumzo kwa mashabiki waliokuwa
wakifuatilia michuano hiyo ambayo ilizishirikisha timu tisa ambapo pia aliibuka
kuwa mchezaji bora .
Uwezo mkubwa wa kupiga chenga ,kumiliki mpira , kutoa pasi za mwisho pamoja na kufunga mabao
ulisababisha viongozi na wachezaji wa timu pinzani kuumiza vichwa kutafuta
mbinu za kumzuia ili asisababishe madhara katika lango la timu zao .
Pia uwezo wake wa kupanda na kushuka , kukimbia na mpira na
kupiga mpira akiwa katika mwendo ni moja ya vitu alinavyo navyo kinda huyo
ambaye pia ni mwanafunzi wa darasa la tano katika Skuli ya Msingi ya Makangale,
vitu ambavyo ni adimu kwa wachezaji
wengi hapa nchini .
“ Wakimkapa huyo anayeitwa ‘Selembe’ katikati , Chuo Kids hawawezi
kufunga bao , lakini hakabiki ni majanja ajabu kwani anatumia akili zaidi na
hatabiriki atafanya nini na kwa wakati gani , huyu dogo ni hazina ya taifa kwa
siku za baadaye ” alisikika mlezi wa Timu ya Maji Maji ya Tumbe Hamad Haji wakati
wa fainali ya michuano hiyo .
Akizungumza na makala haya Chiza amesema kuwa lengo lake ni
kutaka kuichezea Timu ya Taifa ya Zanzibar ( Zanzibar Heroes) huku akitamani
kufuata nyayo za mshambuliaji wa timu ya Coastal Union ya Tanga Suleiman Kassim
Selembe .
Amesema kuwa amekuwa akifuatilia sana kila inapocheza timu
ya Taifa ya Zanzibar na pia hufarajika kusikia au kuona kinsi mchezaji huyo
anavyokimbia na mpira pamoja na staili ya uchezaji wake .
“ Nimeanza kumfuatilia Selembe tangu akiwa na Timu ya Azam
FC na kipindi hicho nikuwa naishabikia Azam , lakini mara baada ya Selembe
kuhamia timu ya Coastal Union , mimi siku hizi naipenda Coastal ” alifahamisha
.
Ameeleza kwamba siku zote amekuwa anajaribu kuiga uchezaji
wa Seremba , jambo ambalo lilimfanya abadilishe namba kutoka kiungo mkabaji na
kuwa kiungo mshambuliaji na wakati mwengine kucheza kuingo wa Pembeni ( namba
saba ) .
Staili hiyo ya kumuiga mchezaji huyo , Chiza amelezimika kubadili hata jina na
kutaka aitwe Selembe pindi awapo
uwanjani ambapo baadhi ya wachezaji wenzake amegombana nao kwa kushindwa
kumuita Seremba na badale yake kumuita Chiza .
Aidha Kinda huyo ambaye pia ni shabiki wa klabu ya
Barcelona alisema pamoja na
kuishabikiana kuipenda klabu ya Coastal Union pia ndoto zake mbali na kuichezea
timu ya Taifa ya Zanzibar , anatamani kucheza soka la kuliwa katika viwanja vya
Nocamp .
“ Kwa Ulaya naipenda timu ya Barcelona , kwani inacheza
mzuri ambapo wachezaji wote wanashambulia , wanacheza pasi fupi fupi naaimini
juhudi zangu ndizo zitakazotimiza ndoto yangu
hiyo ”alieleza Chiza anayevaa jezi namba kumi (10) ambayo inavaliwa na Lionel Messi .
Chiza ambaye ni mtoto wa pili katika familia ya Adam Pesa
Mbili Shija na mama Fortinata Majaliwa yenye watoto wawili alizaliwa mwaka 2001
katika Kijiji cha Mbuzini Unguja na alihamia Pemba baada ya akiwa na umri wa
miaka wa nane baada ya wazazi wake kudai kwamba hafuatilii masomo ambapo
anajishughulisha zaidi na mpira .
Kwa upande wake Kocha wa Timu ya Chuo Kids Stanslausi Markus
Stanslausi (Kibabu) aliiambia makala
haya kwamba Chiza ni moja ya wachezaji wenye nidhamu ya hali ya juu ,
anasikiliza na anafuata kile anachofundishwa pia ni mwepesi ya kushika
mafundisho .
Amesema kuwa kutokana na sifa alizonazo kinda huyo kwa
amemteuwa kuwa Kocha Msaidizi wa Timu hiyo akimsaidia Ali Makame Ali na wameweza
kushirikiana na kuweza kuipa mafanikio timu yao .
“ Anaweza kufika mbali kisoka kwani anajituma , ana nidhamu
ya hali ya juu awawapo ndani na nje ya uwanja , msikivu na mwepesi wa kushika mafundisho ,
hizi ndiyo sifa alinajaaliwa kuwa nazo kijana huyo ”alifahamisha kibabu .
Amesema kuwa katika mshindano hayo Chiza alifunga mabao
watano , huku akitengeneza pasi za
mwisho kumi ambazo zilizaa magoli kwenye
michezo yote kumi iliyocheza timu yake kuanzia kwenye makundi , nusu fainali na
fainali .
Kibabu aliongeza kwamba michuano hiyo imemsaidia katika
kuibua vipaji kwani amebaini kuwepo kwa vijana ambao wanauwezo wa kucheza mpira
na wanaweza kufika mbali ikiwa wataendelezwa zaidi .
“ Michuano hii imenisaidia kubaini vipaji vya wachezaji
ambao walikuwa wamejifika , nawaombeni wapenda michezo kujitokeza kwa ajili ya
kuzifadhili timu hizi ili tuweze kufanikisha azma ya kuinua vipaji na kuzalisha
ajira kwa vijana ”alieleza .
Hata hivyo ametoa wito kwa makampuni na wadau mbali mbali wa
michezo kujitokeza kwa ajili ya kumdhamini na kumuendeleza Kinda huyo ambaye ameonyesha uwezo mkubwa ili
kutimiza ndoto yake ya kuitumikia timu ya Taifa ya Zanzibar .
Nazo taarifa ambazo zimepatikana na mwandishi wa makala haya
zinesema kuwa wafanyakazi wa Shirika la CTS kutoka Korea wameahidi kumtafutia
mawakala kinda huyo ili wamuendelezwe zaidi kisoka .
Subscribe to:
Posts (Atom)