DKT. MPANGO AIAGIZA WIZARA YA VIWANDA KUTATUA CHANGAMOTO YA SOKO LA MATUNDA TANGA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Philip Mpango ameigiza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa wa Tanga kuchukua hatua za mapema katika kukabiliana na changamoto ya soko la matunda yanayozalishwa mkoani humo.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na Wananchi wa Kabuku Wilaya ya Handeni akiwa ziarani mkoani Tanga leo tarehe 21 Februari 2024.
Ameuagiza uongozi wa mkoa wa Tanga kufanya tathimini na kutambua kiasi cha matunda yanayozalishwa katika eneo hilo.
Aidha Makamu wa Rais amemuagiza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kukutana na wamiliki wakubwa wa viwanda vya kuchakata matunda (Bakhresa na Jambo Product) ili waweze kutumia matunda yanayozalishwa Wilaya ya Handeni na Tanga kwa ujumla katika bidhaa zao.
Halikadhalika Makamu wa Rais amewasihi wananchi wa Kabuku na Watanzania kwa ujumla kuongeza jitihada katika utunzaji wa mazingira ili kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
Amesema athari za uharibifu wa mazingira zimepelekea ongezeko la joto kupita kiasi, ongezeko la mvua ambayo imepelekea uharibifu wa miundombinu na mlipuko wa magonjwa.
Amesema ni muhimu watanzania kutambua uhifadhi ya mazingira ni jukumu la kila mmoja kwa kuacha kukata miti ovyo, kuacha kuchoma misitu pamoja na kupanda miti na kuitunza.
Makamu wa Rais amewasisitiza wananchi wa Kabuku kuhakikisha wanazingatia elimu kwa watoto ili kuwa na kizazi bora na chenye maarifa kwa manufaa ya Taifa.
Pia amewaasa wananchi wa eneo hilo kuzingatia lishe kwa kuwa ndio msingi wa afya bora ya mwili na akili.
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema Wizara imepokea shilingi bilioni 25 kwaajili ya ujenzi wa mradi mkubwa wa kutoa maji eneo la Segera hadi Kabuku mkoani Tanga kwa lengo la kukabiliana na adha ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.
Waziri Aweso amesema mradi huo unatarajia kukamilika mwanzoni mwa mwaka 2025 ambapo tayari mkandarasi anaendelea na kazi.
Aidha Waziri Aweso ametoa wito kwa mkandarasi kuhakikisha anafanya kazi na kukamilisha kwa wakati pamoja na kuwashirikisha wananchi na viongozi wa eneo husika wakati wote wa ujenzi wa mradi huo.
Aidha ameahidi kwamba Wizara ya Maji itahakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa TAMISEMI Deogratius Ndejembi amesema tayari Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) imepokea shilingi bilioni 30 ambazo zitaanza kushughulikia changamoto mbalimbali za barabara hapa nchini.
Ameongeza kwamba kwa upande wa Wilaya ya Handeni, Serikali tayari imetenga fedha kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Sindeni – Kwedikazo ya kilometa 37.7 kwa kiwango cha lami.
Amesema katika Wilaya hiyo TARURA itaanza mchakato mara moja wa kuhakikisha barabara zilizoharibiwa na mvua zinatengenezwa ili ziweze kupitika vema.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Philip Mpango akizungumza na wananchi wa Kabuku Wilaya ya Handeni wakati akiwa ziarani mkoani Tanga tarehe 21 Februari 2024.
BILIONI 988 KUTUMIKA KUBORESHA MIUNDOMBINU DAR ES SALAAM
Bilioni 988/ kutumika kuboresha miundombinu Dar es Salaam
Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia imesaini mkataba wa mradi wa kuboresha miundombinu katika jiji la Dar es salaam (DMDP)awamu ya pili utakao gharimu bilioni 988.83.
Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo jijini Dar es salaam Waziri wa fedha Mwigulu Nchema amesema dhamira ya serikali ni kuhakikisha miundombinu katika jiji inaimarika.
Amesema mkataba huo wa DMDP II unaashiria dhamira ya serikali ya kuimarisha miundombinu na kukuza ustawi wa kiuchumi kwa wakazi wa jiji hilo.
“Hatua hii itawezesha serikali ya Tanzania kupata mkopo kutoka benki ya Dunia wenye thamani ya dolla za kimarekani milioni 361.1 sawa na shilingi bilioni 988.093 kutekeleza mradi DMDP kwa awamu ya pili”amesema.
Amesema mradi huo wa DMDP II ni muendelezo wa utekelezaji wa mpango wa tatu wa taifa wa maendeleo wa miaka mitano 2021/22 mpaka 2025/26,lakini pia ni utekelezaji wa irani ya uchaguzi ya CCM na ajenda ya serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Kwa upande wake waziri wa nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa amesema watahakikisha fedha hizo zinaenda zilipokusudiwa kwani ni dhamira ya Rais kuona jiji la Dar es salaam linakuwa jiji la kibiashara.
Amesema fedha hizo zitaenda kujenga miundombinu ya barabara,ujenzi wa madampo makubwa ya takataka,masoko 18,vituo vya mabasi 9 pamoja na mifereji ya maji ya mvua ili kuzuia mafuriko pindi mvua kubwa zinaponyeesha.
“Tunakwenda kufanya usimamizi wa hizi fedha ili zilafanye lililokusudiwa na kazi ianze mara moja lakini pia tutafanya ushawishwi kwa Rais ili kurudisha hadhi ya jiji la Dar es salaam”Amesema.
Naye,Mkurugenzi mkaazi wa benki ya Dunia nchini Nathan Belete amesema wataendelea kushirikiana na serikali katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika kuinua uchumi wa nchi kwani kwa zaidi ya miaka 15 wameweza kufanya mambo mengi ya maendeleo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa wabunge wa Dar es salaam Dkt Faustine Ndugulile amesema hawatakubali upotevu wa fedha hizo wala kazi zilizokusudiwa kufanywa chini ya kiwango hivyo ametoa rai kuanza kwa mchakato wa kazi hizo mapema ili ifikapo mwezi April wakandarasi waangie kazini.
“Asilimia 10 ya watanzania nyumbani kwao ni Dar es salaam lakini pia asiliamia 70 ya uchumi wa nchi unatokea hapa hivyo kipaumbele lazima kiwe barabara kwani hakuna mashamba hapa”Amesema Ndugulile.
TAFITI ZINAZOHUSU CHAKULA NA LISHE KUFANYIWA UCHUNGUZI WA KIMAABARA
Tafiti zinazohusu chakula na lishe kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara
Serikali kupitia Wizara ya Afya imepanga kuweka sharti kwa kufanya uchunguzi wa kimaabara kwenye tafiti zozote nchini zinazohusisha masuala ya chakula na lishe katika Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC).
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema hayo jana Februari 20, 2024 wakati wa ziara yake ya kukagua na kuona kazi zinazofanywa na Taasisi ya Chakula na Lishe kwa upande wa Maabara iliyopo Mikocheni Jijini Dar Es Salaam.
“Tunampango wa kufanya uchunguzi wa kimaabara kwa mtu yeyote au shirika lolote linalofanya tafiti zinazohusu masuala ya chakula na lishe, lazima zithibitishwe na ushahidi wa kisayansi baada ya sampuli kuchukuliwa na kuletwa katika maabara hii, isiwe tu ni tafiti za kwenye makaratasi.” Amesema Waziri Ummy.
Waziri Ummy amesema maabara hiyo ya chakula na lishe ni moja ya maabara kubwa na zinazoaminika katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika ambapo amefurahishwa na kazi wanazofanya ikiwa ni pamoja na kuja na ushahidi wa kisayansi.
“Lakini pia kuna utafiti ambao wameufanya na kushauri kwamba wataalamu wa Afya wanashauri na kuelekeza watoto wa umri chini ya miezi Sita wasipewe chakula kingine chochote zaidi ya maziwa na mama”. Amesema Waziri Ummy.
Maabara hiyo imegawanyika katika sehem Tatu ambayo ni maabara ya chakula (food chemistry) ambayo inafanya uchunguzi wa viinilishe (macro and micro nutrients), maabara inayofanya uchunguzi wa viashiria vya viini lishe mwilini (micronuient biomarkers), na maabara inayofanya uchunguzi wa hali ya lishe (body composition) ikiwa ni pamoja na kugundua kama chakula kimeharibika.
Mwisho, Waziri Ummy ametoa wito kwa Watanzania kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi, kupunguza matumizi ya sukari na chumvi ili kuepuka kupata magonjwa yasiyoambukiza kwa kuwa yamekuwa yakiongezeka kila siku.
CCM YAUPONGEZA UBALOZI WA UINGEREZA KUHAMIA DODOMA
Chama Cha Mapinduzi kimeumepongeza Ubalozi wa Uingereza nchini kwa kuitikia wito wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuzitaka ofisi za ubalozi mbalimbali zilizopo Tanzania kuhamia Dodoma.
Pongezi hizo, zimetolewa leo, tarehe 21/2/2024, jijini Dodoma na Katibu wa NEC wa Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid, wakati akizungumza na ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza, katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma.
Ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza, ukiongozwa na Mkuu wa Ofisi ya Dodoma, Bi. Godfrida Magubo, mapema leo, umetembelea Ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha na kuitambulisha Ofisi ya Ubalozi huo, iliyopo Dodoma, ambayo ilifunguliwa Januari 2024.
‘’Chama Cha Mapinduzi kinawashukuru na kuwapongeza sana kwa kuunga mkono juhudi za kuhamia Makao Makuu ya Nchi hapa Dodoma,’’ Rabia alisema akiwapongeza.
Aidha, ameutaka Ubalozi wa Uingereza wawe mabalozi wa kuhamasisha ofisi zingine za ubalozi mbalimbali nchini kuhamia Dodoma.
Ndg. Rabia ameongeza kusema, ‘’ Chama na Serikali tumehamia Dodoma moja kwa moja, na hatukusudii kurudi nyuma, hivyo natoa wito kwa ofisi zingine za ubalozi wa nchi mbalimbali kuhamia Dodoma kama ninyi mlivyofanya’’.
Katibu wa NEC Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza wamezungumza na kujadiliana mambo mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Uingereza.
CCM WAMPA KONGOLE RAIS SAMIA KWA KUIMARISHA DEMOKRASIA
NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR.
DC SIMANJIRO AWATAKA VIONGOZI KUIFUATA JAMII
MASESA AWAASA MADEREVA KUPUNGUZA MWENDOKASI WAWAPO NDANI YA HIFADHI YA MIKUMI
Na Richard Mrusha Mikumi.
WATUMIAJI wa Vyombo vya moto wametakiwa kupunguza mwendokasi zaidi pindi wanapopita kwenye Hifadhi ya taifa ya mikumi ili kuepuka kugonga wanyama na kusababisha hasara kubwa ya kukosa fedha kutokana na utalii unaofanyika kwenye Hifadhi hiyo.
Hayo yamesemwa februari 19,2024 na kamishna mkuu Msaidizi wa hifadhi ya Taifa Mikumi Kamanda ,Augustine Masesa wakati akizungumza na waandishi wa Habari kwenye ofisi za Makao makuu ya Hifadhi hiyo zilizopo mikumi mkoani Morogoro.
Kamanda Masesa Amesema pamekuwepo na changamoto kubwa ya wanyama kugongwa kutokana na mwendo kasi wa magari yanayokatisha kwenye Hifadhi hiyo licha kuwataka kutembea mwendo mdogo lakini wanakwenda mwendokasi kwa kufanya hivyo inasababisha madhara ya mara Kwa mara Kwa wanyama wetu
"Kama shirika ama Hifadhi Sasa tunafikiria kufunga kamera (CCTV) katika Hifadhi hii ya mikumi ili kudhibiti na kubaini wanaokwenda Kwa spidi kubwa kwani tunaamini kufanya hivi kutaokoa wanyama wetu kuwa salama zaidi."Amesema
Pia katika hatua nyingine Kamanda Masesa ametoa rai Kwa watanzania na hasa kupitia nyakati za sikukuu mbalimbali na likizo kujitokeza na kutembelea Hifadhi ya taifa ya mikumi ili kujionea vivutio mbalimbali vilivyopo hususani wanyama kama Simba , tembo,Swala,chui,viboko,mamba ikiwa sehemu ya Kukuza utalii wetu
Amesema hakuna mahala kwingine unaweza kuona wanyama hao Kwa ukaribu zaidi ya Hifadhi ya taifa ya mikumi hivyo nivema tukajenga tabia ya kutembelea na si kuwaachia wageni tu japo katika siku za hivi karibuni pamekuwepo na ongezo la watalii wa ndani kutembelea Hifadhi hiyo.
Pia akizungumzia royal tour ambayo ilizinduliwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwanza Amesema wanamshukuru sana kiongozi huyo mkuu wa nchi kwani imeleta chachu na matunda yake yanaonekana kwani watalii wameongezeka ukilinganisha na huko nyuma .
Masesa Amesema watalii wengi ambao wanakuja kutembelea Hifadhi ya taifa Mikumi wanatoka Zanzibar Asubuhi na Ndege na kufika Hifadhi ya mikumi baada ya kutalii jioni wanarudi kulala Zanzibar hali ambayo kama Hifadhi inawapa hamasa Sasa ya kukaribisha wawekezaji ili kujenga hoteli kubwa za nyota tano ili watalii waweze kulala hifadhini pindi wanapokuja kutalii.
Aidha Amesema wanaendelea kuimarisha miundombinu na zaidi ujenzi wa kiwanja cha ndege ili Kuruhu ndege kubwa kutua na kuongeza idadi kubwa ya watalii lakini Kwa kifupi royal tour imelipa na mambo yanakwenda vizuri .
"Kikubwa watanzania waendelea kuja kutembelea vivutio vyetu na Kwa musimu huu wa sikuku ya pasaka basi watumie fursa hii kuja na watapata huduma zote ndani ya Hifadhi ikiwemo sehemu za maradhi, chakula , lakini Kuna utalii wa michezo na kubwa zaidi na chautofauti wataona wanyama Kwa karibu zaidi."Amesema