MSICHANGANYE MAPENZI NA MASOMO-RC.

February 18, 2014
NA OSCAR ASSENGA,MUHEZA.
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu,Chiku Gallawa amewataka wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani hapa kuacha kujiingiza kwenye mapenzi wakiwa mashuleni kwani hali hiyo itawafanya kushindwa kufikia malengo yao.

Gallawa alitoa kauli hiyo  wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Potwe kwenye ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo,kusikiliza kero za wanannchi kupitia mikutano ya hadhara kwenye kata na vijiji mbalimbali wilayani hapa.

Alisema wanapaswa kutumia vizuri muda wao wakiwa shuleni kwa kujisomea kwa bidii ikiwemo kupenda masomo ya sayansi ili waweze kuongeza kasi ya wataalamu wa masomo hayo kwa siku zijazo kitendo ambacho kitaongeza hamasa ya wenzao wengine.

February 18, 2014

MANISPAA YA KINONDONI YAPITISHA BAJETI YA SHS.BILIONI 121



Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni limepitisha bajeti ya sh.bilioni 121 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya halmashauri kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.

Akitoa taarifa hiyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mheshimiwa Yusuph Mwenda alisema fedha hizo zimetokana na makusanyo ya vyanzo vya mapato , pesa kutoka ruzuku serikali kuu,Tamisemi,pesa za makusanyo ya ndani ya Halmashauri .Kwa sasa Halmashauri ina uwezo wa kujiendesha kwa asilimia 30 tofauti na hapo nyuma ambapo ilikuwa ikijiendesha kwa asilimia 20 tu.

Bajeti ya mwaka 2014/2015 ina lengo la kutekeleza mipango ya maendeleo na kuwaondolea umaskini wakazi wa kinondoni na kuboresha maisha yao.Imetolewa na Manispaa ya Kinondoni 

Na Dj sek blog
February 18, 2014
Wananchi wenye hasira kali wameteketeza kwa moto zaidi ya nyumba ishirini na kuvunja nyingine katika kijiji cha Kilombero mkoani Geita kutokana na mauaji ya watu watano yaliyotekelezwa kwa nyakati tofauti kwa kukatwa mapanga.
Tukio la Februari 6 la mwanamke Felista Mathias kuuawa kwa mapanga limewachochea zaidi wananchi hao kuvamia nyumba za wanaodaiwa kuhusika februari 17 wakati ukoo ya Kisumo ukitajwa kuhusika na mauaji yanayotokea kijijini humo ambapo mmoja wao Elias Kisumo amekamatwa.

Kumekuwa na matukio ya mauaji ya mapanga kwa wazee katika kijiji hiki, na matukio hayo yanahusisha ushirikina, uvamizi wa mifugo katika mashamba ya watu na hata visasi.

kuuwawa kwa mwanamke FELISTA MATHIAS mwenye umri wa miaka 55 sababu kubwa ni Ngombe wake kula mahindi shambani kwa Elias Kisumo na kudai alipwe fidia na baada ya kulipwa usiku vijana watano walimvamia mwanamke huyo na kumuua kwa mapanga.
February 18, 2014

JESHI LA POLISI LAKAMATA MENO YA NDOVU YENYE THAMANI SHILINGI MILIONI 17 SINGIDA

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SSP. Cordula Lyimo, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari leo juu ya kukamtwa kwa meno ya Tembo vipande 16 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 17 milioni.Vipande hivyo vimekamatwa februari 16 mwaka huu saa tano usiku kwenye kizuizi cha mazao cha kijiji cha Ukimbu wilaya ya Manyoni. Siku nne zilizopita,vipande vingine 21 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya shilingi 43 milioni,vilikamatwa eneo hilo hilo.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
JESHI la Polisi mkoa wa Singida limefanikiwa kukamata vipande 16 vya meno ya ndovu vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 17.
Meno hayo yamekamatwa siku nne (12/2/2014) toka meno mengine vipande 21 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 43 milioni, kukamatwa kwenye eneo lile lile la kizuizi cha mazao kilichopo katika kijiji cha Ukimbu kata ya Mgandu wilaya ya Manyoni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Singida.SSP.Cordula Lyimo amesema meno hayo yamekamatwa febr.16 saa tano usiku huko katika kizuizi cha mazao kilichopo katika kijiji cha Ukimbu,kata ya Mgandu tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni.
February 18, 2014

ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUJIRUSHA KWENYE MABANDA YA KUHIFADHIA CHUI

Mwanamume mmoja nchini China amenusurika kifo katika hifadhi ya wanyama pori nchini humo, baada ya kujirusha ndani ya hifadhi hiyo akisema alitaka 'kuwalisha' wanyama hao hatari.
 
Mwanamume huyo alitaka kujitoa uhai kwa kujirusha ndani ya chumba cha kuhifadhia Chui wakubwa wenye Milia au Tiger katika hifadhi ya wanyamapori nchini China.
 Wageni waliopigwa na mshangao, walitizama mwanamume huyo aliyejulikana tu kama Yang Jinhai, mwenye umri wa miaka 27 akiumwa, kugwaruswa na kubururwa na wanyama hao kabla ya walinzi kumuokoa.
 Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la China, Chengdu, watalii waliokuwa katika hifadhi hiyo walidhani kuwa bwana Yang alikuwa mmoja wa wafanyakazi wa hifadhi hiyo kwani walioshuhudia wanasema walimuona akibeba begi mabegani na kupanda mti kama aliyetaka kuwalisha wanyama hao wakubwa.
February 18, 2014
UONGOZI WA TPSF WATEMBELEA KIWANDA CHA TBL DAR LEO
 eneja wa Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Dar es Salaam, Calvin Nkya akieezea jinsi bia inavyopikwa kwa kutumia kompyuta, wakati ujumbe wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), ulipotembelea kiwanda hicho. Viongozi hao wa TPSF kutoka kushoto ni, aliyekaa ni Ofisa Mawasiliano, Rehema Mtingwa, Mkurugenzi Mtendaji Godfrey Simbeye, Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama, Louis Accaro na Mkurugenzi wa Sera, Edward Furaha.
 Nkya akiwaonesha viongozi hao wa TPSF, mtambo wa kutengenezea maji yaliyotumika kuwa safi kwa ajili ya matumizi mengine.
                                   Simbeye akioneshwa na Nkya matanki mbalimbali.
 Mpishi wa Bia wa TBL, Fadhili Sinkala akiwaonesha viongozi wa TPSF jinsi bia inavyopikwakwa kutumia kompyuta.

WATANO WALALAMIKIWA KAMATI YA MAADILI

February 18, 2014
Release No. 027
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 17, 2014

WATANO WALALAMIKIWA KAMATI YA MAADILI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewalalamikia wana familia watano wa mpira wa miguu kwa Kamati ya Maadili kuhusiana na udanganyifu katika mtihani wa utimamu wa mwili wa waamuzi na usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi.

Riziki Majala na Army Sentimea ambao ni wakufunzi wa waamuzi, na Oden Mbaga na Samwel Mpenzu ambao ni waamuzi wanadaiwa kughushi nyaraka kuhalalisha mtihani huo kinyume cha taratibu.

Naye Sabri Mtulla analalamikiwa na TFF kwa madai ya kuidanganya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji kuwa hakukuwa na pingamizi lolote juu ya usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi huku akijua wazi kuwa jambo hilo si kweli.

Kwa mujibu wa kanuni, malalamiko hayo yamefikishwa kwenye Kamati ya Maadili ambayo itachunguza ili kujiridhisha kama yana msingi au la. Ikibaini kuna kesi ndipo walalamikiwa watafika mbele ya kamati hiyo.

TWIGA STARS, ZAMBIA KUCHEZA MACHI 2
Mechi ya pili ya raundi ya kwanza kuwania Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Zambia (Shepolopolo) itachezwa Machi 2 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

Twiga Stars tayari imeingia kambini kujiandaa kwa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Twiga Stars chini ya Kocha Rogasian Kaijage inafanya mazoezi yake kwenye Uwanja wa Karume ambao ni wa nyasi za bandia kama ulivyo ule wa Azam Complex.

Shepolopolo iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Februari 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka.

Iwapo Twiga Stars itafanikiwa kuiondoa Shepolopolo itacheza na mshindi wa mechi kati ya Botswana na Zimbabwe. Zimbabwe ilishinda mechi ya kwanza ugenini.

Wachezaji wa Twiga Stars waliopo kambini ni Amina Ali, Anastazia Katunzi, Asha Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe Mlenzi, Everine Sekikubo, Fatuma Issa, Fatuma Makusanya, Fatuma Mustafa, Fatuma Mwisendi, Fatuma Omari, Flora Kayanda, Happiness Mwaipaja, Maimuna Mkane, Mwajuma Abdallah, Mwapewa Mtumwa, Pulkeria Charaji, Sherida Boniface, Sophia Mwasikili, Therese Yona, Vumilia Maarifa na Zena Said.
February 18, 2014

LULU AKIRI MAHAKAMANI KUWA MPENZI WA KANUMBA

Lulu
Dar es Salaam. Mwigizaji maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Kimemeta, amekiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na aliyekuwa mwigizaji mwenzake, Steven Kanumba na pia kuwa ugomvi na Kanumba siku ya tukio la kifo cha mwigizaji huyo, lakini akakana mashtaka ya kumuua bila kukusudia.
Lulu ambaye yuko nje kwa dhamana anakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akidaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia, kinyume cha Kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu (PC), April 7, 2012, nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican.
Jana Lulu alipandishwa kizimbani mahakamani hapo na kujibu mashtaka hayo kwa mara ya kwanza tangu alipofunguliwa kesi hiyo, ambapo alikana kumuua Kanumba bila kukusudia.Kesi hiyo namba 125 ya mwaka 2012 inasikilizwa na Jaji Rose Teemba.
Kukubali kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba, ni miongoni mwa mambo manane ambayo mshtakiwa huyo aliyakiri mahakamani hapo jana, kama mambo yasiyobishaniwa katika kesi hiyo.
Mambo mengine ambayo Lulu aliyakiri mahakamani hapo yaliyoko katika maelezo ya kesi hiyo ni pamoja na jina na anuani yake, kwenda nyumbani kwa Kanumba usiku wa tukio hilo, kuwa na ugomvi na Kanumba pia Kanumba kumzuia kutoka nje ya chumba alipojaribu kutoka ili akimbie.
Mengine ni kufanikiwa kutoka nje ya chumba cha Marehemu Kanumba, kumweleza mdogo wa Kanumba (Seth Bosco) kuwa Kanumba ameanguka, kukamatwa kwake na polisi eneo la Bamaga, saa 11 Alfajiri ya usiku wa tukio hilo na kwamba kweli anashtakiwa kwa kosa la kumuua Kanumba bila kukusudia.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI AMOS MAKALA KATIKA UKAKAGUZI WA SEKTA YA MAJI KATIKA WILAYA ZOTE YAHITIMISHWA KILOMBERO MOROGORO. .

February 18, 2014


 
Makala baada ya kukagua tanki la maji katika mji mdogo wa Mvomero wilaya ya Mvomero.PICHA/MTANDA BLOG
Mkazi wa mji mdogo wa Lupiro akiwa amepumzika katika pikipiki huku akimsubiri mhudumu wa kisima kilichopo kijiji hicho ili kuweza kupata huduma hiyo wakati wa ujio wa naibu waziri wa maji Amos Makala wa kukakagua miradi ya maji wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro.

Naibu waziri Amos Makala akizungumza jambo na wananchi wa kijiji cha Kibati juu ya miradi ya maji katika kijiji hicho kilichopo wilaya ya Mvomero.PICHA/MTANDA BLOG
 
Meneja wa kampuni ya Ruqman, Said Assey akimsikiliza naibu waziri wa maji Amos Makala kulia wakati akitoa maelekezo ya kurejea kazini baada ya kampuni hiyo kudaiwa kufanya mgomo wa kukataa kuendelea na kazi.PICHA/MTANDA BLOG
 
Mhandisi wa maji wilaya ya Mvomero Gabriel Ngongi kulia akitoa ufafanuzi wa jambo kwa Naibu waziri wa maji Amos Makala.
February 18, 2014

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI PEREIRA SIRIMA AZINDUA MKUTANO WA SIKU SITA WA MAKAMANDA WA JESHI LA POLISI NCHINI LEO MJINI MOSHI MKOANI KILIMANJARO

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz pamoja na Makamanda wengine wa Jeshi hilo, wakimsikiliza Naibu waziri wa mambo ya ndani, Pereira Sirima (hayupo pichani
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mikakati ya kukabiliana na uhalifu nchini pamoja na mikakati mingine ya Jeshi hilo wakati wa Uzinduzi wa mkutano wa siku sita wa makamanda wa jeshi la polisai uliofanyika leo katika ukumbi wa chuo cha taaluma ya polisi moshi (MPA
Naibu waziri wa Mambo ya ndani, Naibu waziri wa mambo ya ndani, Pereira Sirima, akizungumza na Makamanda wa Jeshi la Polisi nchini baada ya kuzindua mkutano wa siku sita wa makamanda hao ulioanza leo katika Ukumbi wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA).
February 18, 2014

KOCHA AHLY AGOMA KUJIUZULU ,AISUBIRI YANGA.

Wachezaji wa timu ya Yanga wakiwa mazoezini kujiandaa kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi kuu
KOCHA Mkuu wa Al Ahly ya Misri, Mohammed Youssef, ameziba masikio na kutupilia mbali kelele za mashabiki wanaomshinikiza ajiuzulu kutokana na matokeo mabaya na kesho Jumatano anaiingiza timu kambini.
Ahly inajiandaa na msimu mpya wa Ligi ya Mabingwa ambapo itaanza na Yanga mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam, lakini kesho kutwa Alhamisi itacheza mechi ya ‘Super Cup’ dhidi ya Safaxien ya Tunisia nchini Misri kwenye Uwanja wa Cairo.
Mechi hiyo ni kuashiria mwanzo wa msimu mpya wa mashindano ya kimataifa na hukutanisha bingwa wa Kombe la Shirikisho na wa Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita.
Mashabiki wa Al Ahly wanahofia kwamba mwenendo wa timu hiyo katika ligi yao ya ndani usije ukaiathiri na kukumbana na kipigo cha aibu kutoka kwa Yanga na wakaondoshwa mapema na kuwa timu ya pili ya Misri kuondoshwa mashindanoni na timu ya Tanzania ikiwa bingwa mtetezi. Simba iliitoa Zamalek mwaka 2003 wakati Wamisri hao wakiwa mabingwa watetezi.
BUNGE LA KATIBA VIPANDE.

BUNGE LA KATIBA VIPANDE.

February 18, 2014
Bunge Maalumu la Katiba, linaanza leo mjini hapa, huku kukiwa na mpasuko mkubwa miongoni mwa wajumbe, unaotokana na misimamo tofauti.
             
Kipengele kinachowagawa wajumbe hao ni Muundo wa Serikali uliopendekezwa katika Rasimu ya Katiba.

Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, iliyokutana kwa siku mbili Mjini Dodoma imeondoka na msimamo wa kutaka wajumbe wake wa bunge hilo kutetea hoja ya Serikali mbili huku Chadema na CUF vinataka Serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila hivi karibuni alikaririwa akitishia kwenda mahakamani kuzuia mchakato mzima wa Katiba hadi iundwe Serikali ya Tanganyika.

Msimamo wa CCM