Dkt Mpango avutiwa na ubunifu wa programu ya IMBEJU katika kuchochea ujumuishi wa kiuchumi nchini

May 19, 2023

 

Arusha. Tarehe 18 Mei 2022 - Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Mpango ameipongeza Benki ya CRDB pamoja na taasisi yake ya CRDB Bank Foundation kwa ubunifu iliokuja nao kupitia programu ya IMBEJU ambapo amesema ni wenye manufaa makubwa kwa Taifa.

Dkt. Mpango amesema hayo wakati wa uzinduzi wa semina maalum ya elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanahisa wa Benki ya CRDB pamoja na umma iliyobeba kaulimbiu ya “Ushirika wa Benki ya CRDB na Serikali kuwezesha Vijana na Wanawake” iliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC).

Katika semina hiyo iliyoambatana na maonyesho ya biashara changa za vijana, Dkt. Mpango ameshuhudia bunifu za baadhi ya vijana zinazoendelezwa kupitia programu ya IMBEJU. Dkt. Mpango amepongeza akisema semina hiyo pia ni fursa kwa vijana kuonekana na wawekezaji.
“Nimefurahi kuona mmewaalika vijana wenye biashara changa pamoja na wanawake katika semina hii. Kwa kufanya hivi mmewapa fursa ya kuonekana na wawekezaji watarajiwa kwani naamini wapo wanahisa ambao wanaweza kuwekeza katika hizi biashara zao kama ambavyo wamewekeza katika Benki ya CRDB,” amesema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango pia amepongeza jitihada za Benki ya CRDB kushirikiana na Serikali kuyawezesha makundi ya kiuchumi bara na visiwani kupitia programu hiyo ya IMBEJU na kwamba sio mara ya kwanza kwani benki hiyo inashirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutoa mikopo isiyo na riba kupitia programu ya INUKA na Uchumi wa Bluu.

Aidha, Dkt. Mpango aliipongeza Benki ya CRDB kwa mafanikio makubwa iliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita yaliyoshuhudia benki hiyo ikiendelea kutengeneza faida inayoiwezesha kutoa gawio kwa wanahisa wake.
“Nimefurahisha kusikia mwaka huu Bodi ya Wakurugenzi imekuja na pendekezo la ongezeko la asilimia 25 la gawio kwa kila hisa. Wanahisa wa Benki ya CRDB mnastahili kutembea kifua mbele kwa ongezeko hili,” ameongezea Dkt. Mpango huku akibainisha kuwa Serikali nao itanufaika na ongezeko hilo kwani ina hisa ndani ya Benki ya CRDB.

Dkt. Mpango ametumi anafasi hiyo kuziomba taasisi za fedha na bennki za biashara nchini kupunguza riba ya mikopo kama ilivyofanywa kwenye kilimo ambako baadhi zinatoa mikopo hiyo kwa asilimia 9.

“Naamini riba hiyo inaweza kushuka zaidi ya hapo. Punguzeni riba pia kwenye sekta nyingine mfano wachimbaji wadogo wa madini, wafugaji na wakulima. Riba kubwa ni kati ya sababu zilizolifanya Jiji la Dar es Salaam kushika nafasi ya 500 kati ya majiji 1,000 duniani katika kukuza biashara ndogo tofauti na majirani zetu Kenya ambao jiji lao la Nairobi lilikuwa miongoni mwa majiji 160 bora katika ripoti hiyo yam waka 2022,” aemesema Dkt. Mpango.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alimweleza Makamu wa Rais kuwa dhamira ya benki hiyo ni kuifanya programu ya IMBEJU kuwa endelevu ndio maana wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuwafikia vijana na wanawake wengi zaidi.

“Tunaamini mafanikio ya programu hii yapo katika ushirikiano, ndio maana tangu mwanzoni tulianza kwa kushirikiana na wenzetu wa COSTECH (Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia) na ICTC (Tume ya TEHAMA) na hivi karibuni tumesaini mkataba na Shirika la Care International,” amesema Nsekela akiainisha kuwa mpaka sasa vijana 709 na wanawake zaidi ya 4,000 wameshanufaika na programu hiyo.

Nsekela amebainisha kuwa lengo la kuijumuisha programu ya IMBEJU katika semina ya wanahisa wa benki hiyo ni kuwaonyesha kwa vitendo mwelekeo wa mkakati mpya wa Benki ya CRDB wa miaka mitano kuanzia mwaka 2023 – 2027 ambao umejikita katika kuleta mageuzi thabiti katika biashara ya benki hiyo kupitia huduma, bidhaa na programu bunifu katika soko.
Mwaka huu, Benki ya CRDB imepata leseni ya kutoa huduma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na leseni ya kampuni tanzu ya CRDB Insurance. Nsekela amesema kwa hatua hiyo, Benki sasa inatoa huduma katika nchi tatu ambazoni Tanzania, DRC na Burundi ambako ilifungua tawi miaka 10 iliyopita.

“Tunayo CRDB Bank Foundation ambayo imejikita kuwahudumia vijana na wanawake. Kwa hatua zote za kimkakati tunazozichukua, tunaamini miaka michache ijayo, ufanisi wetu utaongezeka hivyo kuongeza thamani ya uwekezaji wa wanahisa wetu,” amesema Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay amesema ikiwa benki ya kizalendo inayomilikiwa na Watanzania kwa zaidi ya asilimia 80, wanajivunia kuendelea kuwekeza katika ubunifu uliochangia kukua kwa thamani ya uwekezaji wa wanahisa wake ikiwamo Serikali.
Katika semina hiyo mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwamo faida za kuwekeza katika hisa. Dkt. Laay aliwataka Watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji katika hisa husasan za Benki ya CRDB ili nao wanufaika na gawio nono ambalo limekuwa likitolewa na benki hiyo kila mwaka.
 
Dkt Laay pia alitumia fursa hiyo kuwaalika wanahisa wa Benki ya CRDB kuhudhuria Mkutano Mkuu utakaofanyika kesho katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) na kupitia mtandao. “Mkutano utaanza saa 3 asubuhi, watu wa mtandaoni wataweza kujiunga kupitia link https://escrowagm.com/crdb/login.aspx au kupitia SimBanking App,” amesema Dkt. Laay.

Benki ya CRDB imeweka mwongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yake ya www.crdbbank.co.tz, mitandao ya kijamii ya Instagram na Twitter, na maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa wanahisa wote.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi wa Kyaro Assistive Tech, Colman Ndetembea inayozalisha vifaa vya usaidizi kwa ajili kusaidia watu wenye ulemavu, wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU. Wengine pichani ni kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, Mweneykiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wa kumkaribisha Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU, uliofayika leo kwenye Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Esther Mwamapa akizungumza wakati wa kumkaribisha Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU, uliofayika leo kwenye Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).






Dkt Mpango avutiwa na ubunifu wa programu ya IMBEJU katika kuchochea ujumuishi wa kiuchumi nchini

May 19, 2023
Arusha. Tarehe 18 Mei 2022 - Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Mpango ameipongeza Benki ya CRDB pamoja na taasisi yake ya CRDB Bank Foundation kwa ubunifu iliokuja nao kupitia programu ya IMBEJU ambapo amesema ni wenye manufaa makubwa kwa Taifa.

Dkt. Mpango amesema hayo wakati wa uzinduzi wa semina maalum ya elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanahisa wa Benki ya CRDB pamoja na umma iliyobeba kaulimbiu ya “Ushirika wa Benki ya CRDB na Serikali kuwezesha Vijana na Wanawake” iliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC).

Katika semina hiyo iliyoambatana na maonyesho ya biashara changa za vijana, Dkt. Mpango ameshuhudia bunifu za baadhi ya vijana zinazoendelezwa kupitia programu ya IMBEJU. Dkt. Mpango amepongeza akisema semina hiyo pia ni fursa kwa vijana kuonekana na wawekezaji.
“Nimefurahi kuona mmewaalika vijana wenye biashara changa pamoja na wanawake katika semina hii. Kwa kufanya hivi mmewapa fursa ya kuonekana na wawekezaji watarajiwa kwani naamini wapo wanahisa ambao wanaweza kuwekeza katika hizi biashara zao kama ambavyo wamewekeza katika Benki ya CRDB,” amesema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango pia amepongeza jitihada za Benki ya CRDB kushirikiana na Serikali kuyawezesha makundi ya kiuchumi bara na visiwani kupitia programu hiyo ya IMBEJU na kwamba sio mara ya kwanza kwani benki hiyo inashirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutoa mikopo isiyo na riba kupitia programu ya INUKA na Uchumi wa Bluu.

Aidha, Dkt. Mpango aliipongeza Benki ya CRDB kwa mafanikio makubwa iliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita yaliyoshuhudia benki hiyo ikiendelea kutengeneza faida inayoiwezesha kutoa gawio kwa wanahisa wake.
“Nimefurahisha kusikia mwaka huu Bodi ya Wakurugenzi imekuja na pendekezo la ongezeko la asilimia 25 la gawio kwa kila hisa. Wanahisa wa Benki ya CRDB mnastahili kutembea kifua mbele kwa ongezeko hili,” ameongezea Dkt. Mpango huku akibainisha kuwa Serikali nao itanufaika na ongezeko hilo kwani ina hisa ndani ya Benki ya CRDB.

Dkt. Mpango ametumi anafasi hiyo kuziomba taasisi za fedha na bennki za biashara nchini kupunguza riba ya mikopo kama ilivyofanywa kwenye kilimo ambako baadhi zinatoa mikopo hiyo kwa asilimia 9.

“Naamini riba hiyo inaweza kushuka zaidi ya hapo. Punguzeni riba pia kwenye sekta nyingine mfano wachimbaji wadogo wa madini, wafugaji na wakulima. Riba kubwa ni kati ya sababu zilizolifanya Jiji la Dar es Salaam kushika nafasi ya 500 kati ya majiji 1,000 duniani katika kukuza biashara ndogo tofauti na majirani zetu Kenya ambao jiji lao la Nairobi lilikuwa miongoni mwa majiji 160 bora katika ripoti hiyo yam waka 2022,” aemesema Dkt. Mpango.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alimweleza Makamu wa Rais kuwa dhamira ya benki hiyo ni kuifanya programu ya IMBEJU kuwa endelevu ndio maana wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuwafikia vijana na wanawake wengi zaidi.

“Tunaamini mafanikio ya programu hii yapo katika ushirikiano, ndio maana tangu mwanzoni tulianza kwa kushirikiana na wenzetu wa COSTECH (Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia) na ICTC (Tume ya TEHAMA) na hivi karibuni tumesaini mkataba na Shirika la Care International,” amesema Nsekela akiainisha kuwa mpaka sasa vijana 709 na wanawake zaidi ya 4,000 wameshanufaika na programu hiyo.

Nsekela amebainisha kuwa lengo la kuijumuisha programu ya IMBEJU katika semina ya wanahisa wa benki hiyo ni kuwaonyesha kwa vitendo mwelekeo wa mkakati mpya wa Benki ya CRDB wa miaka mitano kuanzia mwaka 2023 – 2027 ambao umejikita katika kuleta mageuzi thabiti katika biashara ya benki hiyo kupitia huduma, bidhaa na programu bunifu katika soko.
Mwaka huu, Benki ya CRDB imepata leseni ya kutoa huduma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na leseni ya kampuni tanzu ya CRDB Insurance. Nsekela amesema kwa hatua hiyo, Benki sasa inatoa huduma katika nchi tatu ambazoni Tanzania, DRC na Burundi ambako ilifungua tawi miaka 10 iliyopita.

“Tunayo CRDB Bank Foundation ambayo imejikita kuwahudumia vijana na wanawake. Kwa hatua zote za kimkakati tunazozichukua, tunaamini miaka michache ijayo, ufanisi wetu utaongezeka hivyo kuongeza thamani ya uwekezaji wa wanahisa wetu,” amesema Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay amesema ikiwa benki ya kizalendo inayomilikiwa na Watanzania kwa zaidi ya asilimia 80, wanajivunia kuendelea kuwekeza katika ubunifu uliochangia kukua kwa thamani ya uwekezaji wa wanahisa wake ikiwamo Serikali.
Katika semina hiyo mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwamo faida za kuwekeza katika hisa. Dkt. Laay aliwataka Watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji katika hisa husasan za Benki ya CRDB ili nao wanufaika na gawio nono ambalo limekuwa likitolewa na benki hiyo kila mwaka.

Dkt Laay pia alitumia fursa hiyo kuwaalika wanahisa wa Benki ya CRDB kuhudhuria Mkutano Mkuu utakaofanyika kesho katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) na kupitia mtandao. “Mkutano utaanza saa 3 asubuhi, watu wa mtandaoni wataweza kujiunga kupitia link https://escrowagm.com/crdb/login.aspx au kupitia SimBanking App,” amesema Dkt. Laay.

Benki ya CRDB imeweka mwongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yake ya www.crdbbank.co.tz, mitandao ya kijamii ya Instagram na Twitter, na maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa wanahisa wote.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi wa Kyaro Assistive Tech, Colman Ndetembea inayozalisha vifaa vya usaidizi kwa ajili kusaidia watu wenye ulemavu, wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU. Wengine pichani ni kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, Mweneykiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wa kumkaribisha Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU, uliofayika leo kwenye Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Esther Mwamapa akizungumza wakati wa kumkaribisha Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati alipowasili katika ufunguzi wa Semina ya Wanahisa ya Benki ya CRDB ambayo mwaka huu imebeba ujumbe wa uwezeshaji wa vijana na wanawake kupitia program ya IMBEJU, uliofayika leo kwenye Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).





DC MWOGELO AIPONGEZA BENKI YA NMB KWA KUBORESHA SEKTA YA MADINI NCHINI

May 19, 2023

MKUU wa wilaya ya Korogwe Joketi Mwogelo akizungumza leo wakati akifungua kikao cha Klabu za Madini Mkoani Tanga (NMB Mining Club) kilichofanyika wilayani Korogwe 
MKUU wa wilaya ya Korogwe Joketi Mwogelo akizungumza leo wakati akifungua kikao cha Klabu za Madini Mkoani Tanga (NMB Mining Club) kilichofanyika wilayani Korogwe 
MKUU wa wilaya ya Korogwe Joketi Mwogelo akizungumza leo wakati akifungua kikao cha Klabu za Madini Mkoani Tanga (NMB Mining Club) kilichofanyika wilayani Korogwe 
Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Praygod Mphuru akkizungumza wakati wa halfa hiyo

Mkuu wa wilaya ya Korogwe Joketi Mwogelo akiteta jambo na Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Praygod Mphuru katika mara baada ya kufungua kikao cha klabu ya wachimbaji wa madini mkoani Tanga (NMB Mining Club mkoa wa Tanga) jana kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Mikopo kutoka Benki ya NMB Makao Makuu Mashaga Changarawe kulia ni Kaimu Afisa Madini Mkoa wa Tanga Jared Obado

Mkuu wa wilaya ya Korogwe Joketi Mwogelo kulia akitete jambo na Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Madaraka Jijini Tanga Elizaberth Chawinga mara baada ya kufungua kikao cha Klabu za Madini Mkoani Tanga (NMB Mining Club) kilichofanyika wilayani Korogwe 
Sehemu ya Washirki wa kikao hicho wakifuatilia mijadala 
Sehemu ya Washiriki wa Kikao hicho wakifuatilia majadiliano
Wadau wa Sekta ya Madini wakiwa kwenye kikao hicho
Kikao kikiendelea
Umakini ukiendelea kufuatilia mijadala mbalimbali kwenye kikao hicho


Na Oscar Assenga,Korogwe

MKUU wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga Joketi Mwogelo ameipongeza Benki ya NMB nchini kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanaboresha sekta ya madini kutokana na kugusa mnyororo mzima wa thamani ya sekta hiyo

Mwogelo aliyasema hayo wakati akifungua kikao cha Klabu za Madini Mkoani Tanga (NMB Mining Club) kilichofanyika wilayani Korogwe ambapo alisema hatua inapaswa kupongeza kutokana na kwamba imekuwa ni benki ya kwanza kuona fursa hiyo na hivyo kuamua kujikita kwenye sekta hiyo.

Alisema hatua ya kuanza kutoa elimu kwao ni jambo muhimu kwa sababu kuna wachimbaji wadogo wanaweza kuchimba bila kuwa na dira yoyote ,kujua fursa za kifedha zilizopo jinsi ya kuweka fedha na jinsi ya kurithisha vizazi vijavyo kwa hiyo wamechokifanya ni kuipa hadhi sekta ya madini.

“Lakini pia ni kuunga mkono juhudi,jitihada, dira na mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita na wao Korogwe wana madini hivyo hii ni fursa ya kuendelea kuwezesha wananchi wao kiuchumi baada ya kuzitambua ili iweze kuwa na tija lazima wapate elimu kama hii”Alisema

Mkuu huyo wa wilaya alisema kwamba kwa hilo wanaipongeza benki hiyo kutokana na kwamba wamekuwa mfano bora wanavyounga mkono jitihada za serikali hivyo yatakayoibuiliwa wanajitahidi kwenye msukumo wa serikali na wao watatoa ushirikiano wa hali ya juu.

Hata hivyo alisema kwamba anaaamini baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo yatawawezesha wachimbaji hao kwenda kubadilika na hivyo kuweza kuzalisha mabilionea wengine watakaotoka wilayani humo kupitia sekta ya madini.

Awali akizungumza katika kikao hicho Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Praygod Mphuru alisema kwamba kukutana na wachimbaji hao wa madini imekuwa ni fursa muhimu kwao na hivyo kuweza kuongeza wigo wa wadau muhimu ambao watashirikiana nao.

Aidha alisema kwamba wameona kuwakutananisha wadau hao ili kuwapitisha kwenye mafunzo jinsi ya kupata mitaji ya biashara zao na jinsi ya kufanya biashara zao za madini kisasa ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Kaimu Meneja huyo alisema pia wanawafundisha jinsi ya kutenegeneza warithi wa biashara zao sambamba na namna ya kuweka rekodi ya biashara zao ili wanapofanya mahesbabu wajue wamepata faida au hasara”Alisema

Hata hivyo kwa kwa upande wake Meneja wa NMB tawi la Madaraka Tanga Elizaberth Chawinga aliwakaribisha wadau wa sekta ya madini kuchangamkia fursa zilizopo kwenye benki hiyo kutokana na wao kuamua kuingia kwenye sekta hiyo kwa miguu miwili .

Alisema kwamba sababu madini kwenye mnyororo mzima wa thamani na wamejikita huko ambapo watapata fursa ya kufungua akaunti na kutoa vifaa vya kisasa vya kuchimbia kwa wanakopeshwa kwa riba nafuu kabisa na watawasimamia hata kama watakuwa wanasafirisha madini kutoka nchini kwenda nje ya nchi.

WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA BENKI YA CRDB KWA KUTOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA JESHI LA POLISI KUIMARISHA USALAMA KWA WATALII JIJINI ARUSHA

May 19, 2023

 

 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohammed Mchengerwa (wa pili kushoto) akiwa katika pikipiki zilizokabidhiwa na Benki ya CRDB kwa Kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia jijini Arusha kwa ajili ya kusaidia katika doria na kuimarisha ulinzi na usalama kwa watalii. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia), Mkuu wa Wilaya Arusha, Felician Mtahengerwa (wa kwanza kulia), na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo.
 
========   ========   =========

Arusha Tarehe 18 Mei 2023 - Serikali imeipongeza Benki ya CRDB kwa kutoa msaada wa pikipiki 15 kwa Jeshi la Polisi mkoani Arusha ili kuimarisha doria zitakazoongeza usalama kwa watalii wanaokuja nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Utalii na Maliasili, Mohamed Mchengerwa alipopokea pikipiki hizo zenye thamani ya TZS 40 milioni kwenye hafla fupi iliyofanyika katika Kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia kilichopo jijini hapa.
Waziri amesema sekta ya utalii ina umuhimu mkubwa katika uchumi na maendeleo ya wananchi nchini kwani ndiyo inayoongoza kwa kuliingizia taifa fedha nyingi za kigeni, ikiwa ya pili kwa kuchangia kwenye Pato la Taifa (GDP), na ya tatu kwa kutoa ajira.

“Ripoti za Benki Kuu Tanzania (BOT) zinaonyesha sekta ya utalii inaendelea kuimarika baada ya kuathiriwa na janga la UVIKO-19. Mapato yatokanayo na utalii kwa Machi yalifikia Dola za Marekani bilioni 2.787 ikilinganishwa na dola milioni 885 kipindi kama hicho mwaka 2021. Katika mwezi huo, jumla ya watalii 1,574,630 waliingia nchini,” amesema Mchengerwa na kuongeza huku akipongeza jitihada kubwa zilizofanywa na Rais Samia katika kuitangaza Tanzania kupitia filamu ya Royal Tour.

“Kipeeke kabisa naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa msaada huu wa pikipiki 15 ambao Benki yetu ya CRDB imeutoa kwa kituo chetu hichi. Pikipiki hizi zitawawezesha askari kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Askari watakabiliana haraka na dharula jambo litakalosaidia kuimarisha usalama kwa watalii na kuifanya nchi yetu kuwa kivutio kikubwa hivyo wageni wengi kuja kuitembelea.” 
Mwaka 2020, sekta ya utalii ilichangia asilimia 10.6 kwenye pato la taifa ila kiasi hichi kilishuka hadi asilimia 5.7 mwaka 2021 kutokana na athari za UVIKO-19 hivyo kuilazimu Serikali kuchuku ahatua za makusudi kuifufua kwa kufuata taratibu za Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufanya matangazo kimataifa kwa Rais Samia Suluhu Hassan mwenyewe kurekodi filamu ya ‘The Royal Tour.’

Ili kuhakikisha usalama wa watalii wanaokuja nchini, Serikali ilianzisha kitengo maalum cha utalii na diplomasia kwa ajili ya kuwahudumia watalii na wanadiplomasia wanaofika nchini kutalii ama kuwekeza kwa haraka.

Kwa kuwa jiji la Arusha ndio kitovu cha utalii nchini, kituo hicho kimejengwa huko na askari wake walipewa mafunzo ya ziada ndani na nje ya nchi juu ya namna bora ya kuhudumia watalii. Vituo vingine vidogo vimefunguliwa katika wilaya za Arumeru, Karatu, Monduli na Longido.
Akikabidhi pikipiki hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kila mmoja anafahamu umuhimu wa amani, utulivu na usalama katika maendeleo ya nchi kiuchumi, kijamii na kisiasa hivyo ni jukumu la jamii nzima kushiriki kuuimarisha.

“Pamoja na kuwepo hali ya amani na utulivu nchini, bado baadhi ya matukio ya uhalifu hujitokeza kama vile vile uporaji wanaofanyiwa raia hata watalii wanaokuja kutembelea vivutio vilivyopo nchini. Ili Jeshi la Polisi litekeleze majukumu yake kwa ufanisi linahitaji vitendea kazi vya kutosha,” amesema Nsekela.

Mkurugenzi huyo amesema wanayo furaha kubwa kukabidhi pikipiki hizo ili kuwasaidia askari kukimbizana na wahalifu wanaowapora watalii au kusafirisha mihadarati hivyo kuharibu sifa njema za jiji hili la kitalii.
“Tunaamini matumizi sahihi ya pikipiki hizi yatasaidia kudhibiti uhalifu jijini hapa na tunaahidi tutaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini kupunguza baadhi ya changamoto zinazokwamisha ufanisi wake ili nchi yetu iendelee kuwa salama kwa biashara na uwekezaji,” amesema Nsekela.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Edith Swebe, amesema jitihada zinazoendelea kuutanga utalii wa Tanzania umelifanya Jiji la Arusha kupokea wageni wengi wanaoongeza haja ya askari polisi kuwapo katika kila eneo.
“Tunachokifanya sasa hivi ni kusimamia mradi wa utalii salama ambao unahitaji askari kuwapo kila walipo wageni. Pikipiki hizi tunazozipokea zitasaidia kuwafikisha askari kwenye maeneo ambako magari hayawezi kufika kwa urahisi zikiwamo barabara nyembamba. Jeshi la Polisi linaaminimazingira salama ni kivutio cha utalii,” amesema Edith ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa kamanda wa Mkoa wa Simiyu.

Hata hivyo, ameiomba Serikali na wadau wengine wa utalii kuliwezesha jeshi hilo kupata pikipiki nyingine 10 zitakazofanya kata zote 25 za Jiji la Arusha kuwa na pikipiki moja ya doria itakayosaidia utekelezaji wa mradi wa utalii salama.