March 05, 2014

TBL YAKABIDHI MAJENGO YA KIWANDA KWA CHUO KIKUU CHA KUMBUKUMBU YA STEPHANO MOSHI

Meneja wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya kaskazini,Salvator Rweyemamu (kulia) akimkabidhi mkataba wa kukabidhiana majengo ya TBL yaliyopo Moshi, kwa Katibu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi Kanda ya Kaskazini, Julius Mosi, katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki Moshi, mkoani Kilimanjaro. Majengo hayo yatakayotumika kwa ajili ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stephano
SMMUCO) yalikuwa ya Kiwanda cha Bia cha Kibo kilichonunuliwa na TBL.
Katibu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi Kanda ya Kaskazini, Julius Mosi akikabidhi mkataba kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stephano (SMMUCO) Prof,Arnod Temu kwa ajili ya kutmiwa na chuo hicho chini ya dayosisi hiyo iliyokabidhiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki Moshi, mkoani Kilimanjaro.Awali majengo hayo yalikuwa ya Kiwanda cha
Bia cha Kibo kilichonunuliwa na TBL.
Baadhi ya majengo yaliyokabidhiwa
Meneja wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya kaskazini,Salvator Rweyemamu, AKIELEZEA SABABAU ZA TBL kukabidhi majengo hayo kwa chuo hicho
Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stephano (SMMUCO) Prof,Arnod Temu akitoa shukurani kwa TBL
BAADHI YA WANANCHI WALIOHUDHURIA SHEREHE HIYO
Viongozi wa TBL, dAYOSISI NA cHUO WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
Ndani ya moja ya majengo hayo
Sehemu ya ndani ya moja ya majengo hayo
Viongozi wa TBL pamoja na viongozi wa chuo hicho wakitembelea maeneo
mbalimbali ya chuo hicho kujionea hali ilivyo kwa sasa.PICHA NA MDAU DICKSON BUSAGAGA
March 05, 2014

Wajumbe wa Bodi Wavutiwa na Teknolojia ya Utengenezaji Kadi ya Mwanachama NSSF

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF, Abubakar Rajabu (mwenye kofia nyeupe) akimkabidhi kadi ya uanachama wa NSSF, Ester Msalahi, ambaye ni mwalimu katika shule moja ya msingi ya binafsi. Kadi hilo iliandaliwa ndani ya saa moja kwa teknolojia mpya ya kisasa 'Mobile POS' ya utengenezaji kadi ya mwanachama wa shirika hilo
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF, Abubakar Rajabu (mwenye kofia nyeupe) akimkabidhi kadi ya uanachama wa NSSF, Ester Msalahi, ambaye ni mwalimu katika shule moja ya msingi ya binafsi. Kadi hilo iliandaliwa ndani ya saa moja kwa teknolojia mpya ya kisasa ‘Mobile POS’ ya utengenezaji kadi ya mwanachama wa shirika hilo
Wajumbe wa Bodi ya NSSF pamoja na viongozi wa shirika hilo wakipata maelezo juu ya Mobile POS inavyofanya kazi.
Wajumbe wa Bodi ya NSSF pamoja na viongozi wa shirika hilo wakipata maelezo juu ya Mobile POS inavyofanya kazi.
Mmoja wa wafanyakazi wa NSSF tawi la Ilala (katikati) aliyezungukwa akitoa maelezo namna Mobile POS inavyorahisisha kazi ya utengenezaji kadi ya mwanachama wa NSSF kwa muda mfupi.
Mmoja wa wafanyakazi wa NSSF tawi la Ilala (katikati) aliyezungukwa akitoa maelezo namna Mobile POS inavyorahisisha kazi ya utengenezaji kadi ya mwanachama wa NSSF kwa muda mfupi.
Meneja Kiongozi wa NSSF Temeke, Yahaya Mhamali (kulia) akitoa ufafanuzi juu ya teknolojia mpya ya kutoa huduma zote kwa wateja wao kwa kutumia tiketi maalumu ambayo mteja huchukua kwenye mashine maalumu anapofika kupata huduma anuai.
Meneja Kiongozi wa NSSF Temeke, Yahaya Mhamali (kulia) akitoa ufafanuzi juu ya teknolojia mpya ya kutoa huduma zote kwa wateja wao kwa kutumia tiketi maalumu ambayo mteja huchukua kwenye mashine maalumu anapofika kupata huduma anuai.

SIMBA WAIPANIA RUVU SHOOTING KESHO.

March 05, 2014
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amewataka wachezaji wake kutumia vizuri nafasi wanazopata ili washinde katika mechi yao dhidi ya Ruvu Shooting, mchezo unaotarajiwa kupigwa kesho katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Logarusic alisema timu yote inahitaji ushindi katika mechi yao hiyo, hivyo jambo kubwa ni kuona vijana wake wanakuwa makini zaidi uwanjani.

“Tumepoteza pointi muhimu katika mechi iliyopita kwasababu ya wachezaji kutotumia ipasavyo nafasi za wazi wanazozipata, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limetugharimu.

“Naamini wakati huu wachezaji wote wanafahamu jambo gani muhimu wanapaswa kufanya uwanjani kwa ajili ya kuwapatia maatokeo mazuri, maana mpira ni mchezo wa makosa,” alisema.