UVCCM YAWATAKA WAHANDISI ZANZIBAR KUJENGA BARABARA ZENYE UBORA

August 16, 2017
Meneja Mradi wa Barabara yenye urefu wa km 35  ya Ole Ngeneja Mhandisi Amin Khalid Abdallah akitoa ufafanuzi juu ya maendeleo ya mradi huo kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipokwenda kukagua ujenzi wa barabara hiyo wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba. (Picha zote na Fahad Siraji)
Daktari dhamana katika hospitali ya Chakechake Dkt.Ali Habib Ali akimpokea Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipowasili hospitalini hapo kuangalia wagonjwa na kuwafariji wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akimpatia baadhi ya vifaa tiba Bi, Salha Issa Nassor alipotembelea katika wodi ya kina mama waliojifungua alipowatembelea wagonjwa na kuwafariji katika Hospitali ya Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) (kulia)) akiwasili katika ukumbi wa mkutano Tawi la CCM Wawi kuzungumza na Vijana wa CCM wilayani ChakeChake Mkoa wa Kusini Pemba.
 Vijana wakifuatilia mkutano huo.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na Vijana wa CCM wilayani ChakeChake Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa mkutano Tawi la CCM Wawi, wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC)  wakati akizungumza na maafisa Wadhamini wa mabaraza ya mji na madiwani, katika ukumbi wa skuli ya Chekechea Mdungu Wilayani ChakeChake Mkoa wa Kusini pemba.
Maafisa wadhamini wa mabaraza ya Mji na Madiwani wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.

Na Mathias Canal, Kusini Pemba

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umekemea baadhi ya wahandisi wasiowajibika ipasavyo kwa kujenga barabara chini ya kiwango ilihali serikali imewalipa fedha zao kadri ya makubaliano.

UVCCM imesema kuwa serikali inapaswa kuwachukulia hatua za kisheria wahandisi wa kariba hiyo ikiwemo kuwanyima tenda sambamba na kuwafikisha mahakani kwani wanaisababishia hasara kubwa serikali kwa kufanya marekebisho ya barabara mara kwa mara.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 alipokuwa akikagua ujenzi wa barabara ya Ole-Vitongoji na Mfukiwa-Kengei wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilayani Chakechake Mkoa wa Kusini Unguja.

Barabara hiyo yenye jumla ya urefu wa Kilomita 35 inatarajiwa kukamilika katika hatua za awali mwishoni mwa mwezi Agosti 2017 huku ukamilisho wote ukitaraji kufika ukomo Disemba 2018.

Shaka amepongeza namna barabara hiyo inavyojengwa kwa viwango ambayo itakuwa na uwezo wa kudumu kwa muda mrefu pasina kufanyiwa marekebisho ya mara kwa mara kama ambavyo baadhi ya barabara zimekuwa zikiharibika na kufanyiwa marekebisho jambo ambalo linaiingizia serikali hasara.

Hadi kufika hatua ya ukamilisho barabara hiyo itagharimu Dola za kimarekani shilingi Milioni 11 ambazo ni sawa na zaidi ya Bilioni 24.4

Hakuna serikali popote duniani yenye uwezo wa kuajiri  vijana wote nchini badala yake serikali nyingi zinafanya kazi ya kuweka miundo msingi ya wananchi kuweza kujiajiri.

DC ASIA ABDALLAH AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA MTANDAO WA TTCL 4G LTE

August 16, 2017
 Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah akizungumza wakati wa uzinduzi wa mitandao wa TTCL 4G LTE katika Mkoa wa Iringa eneo la ofisi za kampuni hiyo.
 Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah akizindua huduma ya mtandao wa simu wa TTCL kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa bi Amina Masenza

Na Fredy Mgunda, Iringa.

Watanzania wametakiwa kuanza kuutumia mtandao wa simu wa TTCL kwa kuwa umeboreshwa kwa kiwango kikubwa na huduma zao zinazingatia wateja wake ili kuendelea kiinufaisha serikali kwa kuwa mtandao huo unamilikiwa na serikali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa TTCL 4G mkuu wa wilaya ya kilolo Asia Abdallah alisema kuwa wananchi wanapaswa kuunga mkono mtandao huu wa kizalendo ambao unahuduma nyingi nzuri.

“Ukiangalia utagundua kuwa mtandao wa TTCL inahuduma ya pesa ambazo zina makato madogo sana kulinganisha mitandao mingine hivyo nawasiii wananchi wa mkoa wa iringa kuanza kutumia huduma za mtandao huu wa kizalendo” alisema Abdallah

Abdallah aliwataka wananchi kuanza kuvithamini vitu vya wazawa kwanza ili kuleta maendeleo ya maendeleo kwenye kampuni na taasisi za kizalendo  ndio maana mkuu wa mkoa wa Iringa na wakuu wa wilaya wote wa mkoa huu wameamua kujiunga na mtandao huu wa TTCL.

“Mimi,mkuu wa mkoa ,mkuu wa wilaya Richard Kasesela  na viongozi wengine wamejiunga na mtandao huu wa TTCL 4G ambao unakasi kubwa kwenye upande wa internet na huduma nyingine ziboreshwa na zimekuwa bora sana” alisema Abdallah

Aidha Abdallah alisema kuwa kampuni hii ya kizalendo imekuwa ikihudumia jamii kwa njia tofautitofauti za kimaendeleo hasa kwa kuunga mkono kwenye michezo mbalimbali hapa nchini.

“Kama unakumbuka hivi karibuni kulikuwa na mshindano ya Ritta kabati challenge cup ambapo kampuni hii ya kizalendo ilichangia zaidi ya milioni mbili kufanikisha kuendesha mashindano hayo hivyo utagundua kuwa TTCL imekuwa ikirudisha faida kwa wananchi”alisema Abdallah

Abdallah alisema kuwa TTCL wana bando kuwa kwa gharama nafuu hivyo naomba wananchi wanaopenda kutumia mitandao ya kijamii wanapaswa kujiunda na mtandao huu kwa kuwa unagharama nafuu na internet yake inakasi nzuri kulingana na mitandao mingine.

Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya TTCL nchini Waziri Kandamba alisema kuwa TTCL imekuja kuboresha maisha ya watanzania wanaopenda kutmia mitandao ya simu kwa kuwa wamejipanga kufanya kazi kishindani tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

“Leo tumefanya uzinduzi wa mtandao wenye kasi kubwa 4G LTE ambao utakuwa unakata kiu kwa wanaopenda kutumia mitandao ya kijamii kwa kuwa tumeboresha huduma zetu zote katika mtandao huu” alisema kandamba

UVCCM YAWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTENGANISHA SIASA NA MAENDELEO

August 16, 2017
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na Viongozi Mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akisaini kitabu cha wageni Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akionyesha ilani ilani ya CCM mwaka 2015-2020 na maelekezo ya namna ya utekelezaji wakati akizungumza na Viongozi Mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba Ndg Abdallah Rashid Ali akielezea namna Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inavyotekeleza ilani ya CCM mbele ya Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.