NANI KUKALIA USUKANI WA LIGI KUU LEO, YANGA AU MBEYA CITY?????
Na Reporter wa Sufianimafoto, Dar
TIMU
ya Mbeya City wakifungwa na Coastal na Yanga wakiibuka na ushindi dhidi
ya Ruvu Shooting katika mchezo wa LEO katika mechi ya Ligi Kuu Bara,
watakuwa wametoa mwanya kwa wanajangwani hao kukalia usukani wa ligi
hiyo.
Katika
mfulilizo wa ligi hiyo, Mbeya City watacheza na Coastal Union kwenye
Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku Yanga wakiwa katika Dimba la
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakaribisha Ruvu Shooting.
Ushindi
kwa Yanga utawawezesha kuongoza katika msimamo wa ligi hiyo kwa saa 24
kabla ya Azam FC keshokutwa kucheza na Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa
Chamazi, Dar es Salaam na kutegemea matokeo ya mchezo huo.
Azam
FC kwa sasa wanaongoza msimamo huo kutokana na kufikisha jumla ya
pointi 36, wakifuatiwa na Yanga na Mbeya City ambao kila mmoja ana
pointi 35 wakiwa na tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Yanga
wataingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kuifunga timu hiyo bao 1-0
katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo, ambayo kwa sasa
inashika nafasi ya tano ikiwa na pointi 25.