UVUNAJI WA MAZAO YA BAHARI UMEPUNGUA KUTOKA TANI 481 HADI TANI 316 MKOANI TANGA

January 10, 2014


 Tanga.
HALI ya uvunaji wa  mazao ya baharini katika mkoa wa Tanga imepungua kutoka tani 481 zilizopatikana mwaka 2011/2012 zenye thamani ya fedha za kitanzania 4,821,440,915.15 zilizosafirishwa nje ya nchini hadi kufikia tani 316 kwa mwaka 2012/2013 ambapo upungufu huo wa tani 165.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu,Chiku Gallawa wakati akizungumza na TANGA RAHA BLOG ambapo alisema upungufu huo umesababishwa na hali ya soko la mazao kama Pweza kwa nchi Ulaya kupungua.

BAADA YA KUZUSHIWA KIFO MWAKA JANA D.DOCTOR AKANUSHA HABARI HIZO.

January 10, 2014

MSANII D.DOCTOR AKIWA KATIKA POZI LEO
                       Na Oscar Assenga,Tanga.
MSANII nguli wa mziki wa Bongofleva mkoani Tanga, Dominick Mndeme “D.Doctor amejitokeza hadharani na kukanusha habari zilizokuwa zimeenezwa kuwa amefariki dunia kwa kusema sio kweli.

Akipiga stori na  TANGA RAHA BLOG,D.Doctor alihabarisha kuwa habari hizo zilivumishwa Desemba 29 mwaka jana na mmoja kati ya wasanii nguli wa jijini Tanga ambaye ni rafiki yake wa karibu kitendo ambacho kilimshangaza sana.

January 10, 2014

D.DOCTOR :AWASAA WASANII KUWA WABUNIFU.

Na Oscar Assenga,Tanga.
WASANII wa mziki wa BongoFleva nchini wametakiwa kuwa wabunifu na kubadilika kutokana na mazingira ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuutangaza mziki huo kitaifa na kimataifa kama ilivyokuwa kwa nchini nyengine duniani.

Wito huo ulitolewa na Msanii wa mziki huo mkoani Tanga,Dominick Mndeme “D.Doctor wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambapo alisema kutokuwa na umakini kwa wasanii wengi  kumewafanya kutoka na kuonekana kuwika kwa muda fulani na baadae kupotea kwenye tasnia hiyo kitendo ambacho kinachangia pia kushusha mziki huo.
January 10, 2014

YANGA SC WAKUTANA NA ROBERTO CARLOS UTURUKI

Na Baraka Kizuguto, Antalya

WACHEZAJI wa Yanga SC wamepata fursa ya kukutana na beki wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Roberto Carlos ambaye kwa sasa ni kocha wa klabu ya Sivasspor iliyopo Ligi Kuu nchini hapa.
Yanga imefikia katika hoteli ya Sueno Beach Side eneo la Manavgat pembeni kidogo ya jiji la Antalya leo asubuhi imeanza mazoezi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika.
Roberto Carlos katikati akiwa na Mkwasa na Nizar kushoto

Timu ilipokelewa na wenyeji majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za huku ikiwa ni sawa na saaa 12 kwa saa za Afrika Mashariki na moja kwa moja kikosi kilielekea katika mji wa Manavgat ambapo ndipo ilipo hoteli ya Sueno Beach Side ambapo msafara mzima umefikia.
Sueno Hotel Beach Side ni hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano, ambayo ina jumla ya vyumba 760, mabwawa ya kuogelea,viwanja viwili vya mpira vya mazoezi kimoja kikiwa na nyasi za kawaida na kingine nyasi za bandia.
January 10, 2014

COASTAL UNION NDANI YA MUSCAT

Msafara wa Coastal Union baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Muscat, Oman jana kwa mwaliko wa klabu ya Fanja ya Oman. Coastal itakuwa huko Januari 23 kwa mazoezi na mechi za kujipima nguvu.
Wachezaji wa Coastal kutoka kulia Razack Khalfan, Jerry Santo na Haruna Moshi 'Boban'
Kipa Shaaban Kado na Razack Khalfan kushoto
January 10, 2014

AZAM FC YAVULIWA UBINGWA KOMBE LA MAPINDUZI, YAPIGWA 3-2 MBELE YA RAIS MWINYI AMAAN

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
NDOTO za Azam FC kubeba kwa mara ya tatu mfululizo Kombe la Mapinduzi, leo zimeyeyuka baada ya kufungwa mabao 3-2 na KCC ya Uganda katika Nusu Fainali ya michuano hiyo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Shujaa wa timu ya Watunza Jiji la Kampala leo alikuwa ni William Wadri aliyefunga bao la tatu dakika ya 45 na ushei, akiunganisha krosi ya Habib Kavuma.
Kabla ya hapo, Tony Odur aliifungia bao la kusawazisha KCC na kuwa 2-2 dakika ya 51, akiunganisha pia krosi ya Habib Kavuma.
Kipre Tchetche akimtoka mchezaji wa KCC katika mchezo wa leo

Kipa Mwadini Ali alidaka mechi zote nne za awali bila kufungwa hata bao moja, lakini leo amekubali kufungwa mabao matatu rahisi na KCC.
Hadi mapumziko, tayari Azam FC walikuwa mbele kwa mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Joseph Lubasha Kimwaga yote dakika za 16 na 32.
Kinda huyo aliyepandishwa kutoka akademi ya Azam msimu huu, alifunga bao la kwanza kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa na beki wa kulia Erasto Nyoni kutoka wingi ya kulia.
Bao la pili Kamwaga aliitokea krosi ya chini ya mshambuliaji hatari wa Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche kutoka kushoto na kuteleza nayo hadi nyavuni.
Mzee Mwinyi aliishuhudia Azam ikipigwa 3-2
Baada ya kupata bao hilo, Azam walionekana kutaka kuwadharau wapinzani wao, walioitumia vyema fursa hiyo kupata bao moja kabla ya mapumziko, lililofungwa na Ibrahim Kiiza dakika ya 37.
Kazi bure; Joseph Kimwaga akipongezwa na Himid Mao baada ya kufunga bao la pili, lakini mabao yake hayakuwa na faida leo

Kipindi cha pili, mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog kuwatoa wachezaji wote wa safu ya mbele Kipre Tchetche, Joseph Kimwaga na Brian Umony na kuwaingiza Muamad Ismail Kone, Ibrahim Mwaipopo na Farid Mussa yaliigharimu timu.
Wachezaji wote walioingia walishindwa kucheza vizuri kama waliotoka na ndipo KCC ilipoutumia mwanya huo kutoka nyuma na kushinda mechi.
Kwa matokeo hayo, KCC inasubiri mshindi wa mechi ya usiku kati ya Simba SC ya Dar es Salaam na URA ya Uganda pia ikutane naye katika fainali Jumatatu.
Mchezaji Joseph Kimwaga alikabidhiwa king’amuzi na rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi baada ya kutajwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Malika Ndeule, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Himid Mao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Kipre Tchetche, Brian Umony na Joseph Kimwaga
January 10, 2014

MTUNZI na mwimbaji wa bendi ya Extra Bongo 'Next Level Wazee wa Kizigo' Ramadhani Masanja 'Le General Banza Stone' anatarajiwa kutambulishwa rasmi kurejea kwake upya jukwaan Januari 25 mwaka huu katika onyesho maalumu litakalofanyika katika Ukumbi wa Meeda Club Cnza jijini Dar es Salaam.
Kwa muda wa miezi miwili Banza alikuwa yu mgonjwa hali iliyomsababishwa kushindwa kupanda jukwaani kabla ya hivi karibuni kujikongoja na kushiriki kwenye ziara ya 'Mafahari Watatu' katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa akiwa na  Extra Bongo.
Kwa mujibu wa msemaji wa bendi hiyo Juma Kasesa, mara baada ya kumalizika kwa ziara hiyo Banza amepewa mapumziko maalumu ya wiki tatu kuimarisha afya yake na kufanya mazoezi tayari kujiandaa kurejea jukwaani kwa kishindo kuwapa burudani wapenzi na mashabiki wa muziki wa dansi waliokuwa waki -mis sauti na tungo zake.

MOTO WAUNGUZA BOHARI YA KUFIDHIA DAWA VINGUNGUTI.

January 10, 2014

                                                    January 10, 2014
Moto ulivyozuka kwenye Bohari ya kuhifadhia dawa katika Kampuni ya Tpower Technics Vingunguti Dar es Salaam
CHANZO.AMANITANZANIABLOG


January 10, 2014
*ABIRIA WALIOKWAMA KITUO CHA TRENI DODOMA BADO WAENDELEA KUSOMA, SASA KUSAFIRISHWA KWA MABASI
 Abiria waliokwama na treni Dodoma wakusubiri mabasi kwa ajili ya usafiri wa kuelekea mikoa ya Morogoro, Dar es saalam na Kigoma baada ya abiria hao kukodishiwa mabasi na shirika la Reli kutokana na kushindwa kuendelea na safari baada ya njia ya Reli kukumbwa na mafuriko katika eneo la Gulwe na Godegode wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma. Hapa abiria hao wakiendelea kusota katika Kituo cha Treni mjini Dodoma.
 Abiria hao wakiwa katika kituo hicho hawajui la kufanya kutokana na kukosa chakula katika stesheni ya reli mkoani Dodoma walipotangaziwa kuanza kusafirishwa kwa mabasi lakini mpaka kufikia leo jioni zaidi ya abiria 900 kati ya 1600 walikuwa bado hawapatiwa usafiri huo.
  Mfanyakazi wa shirika Reli kituo cha Dodoma akiandika tangazo katika ubao wa matangazo lililowataka abiria waliokuwa wanaelekea mikoa ya kanda ya ziwa kurudishiwa nauli zao kutokana na usafiri wa treni kusitishwa kwa muda usiojulikana.
 Askari wa kuzuia Ghasia (FFU) wakiangalia usalama kwa abiria wa treni waliokwama kutokana na treni kushindwa kuendelea na safari tangu juzi mara baada ya kufika kituo cha reli mkoani Dodoma kutokana na maji ya mvua iliofunika reli wilayani Mpwapwa.
Na John Banda, Dodoma
SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limelazimika kuwasafirisha abiria waliokwama katika kituo cha Treni cha Dodoma kwa mabasi, kwa siku mbili katika Stesheni mkoani Dodoma waliokuwa wanasafiri kwa Treni kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa, kutokana na kushindikana kwa ukarabati  unaoendelea kufanyika mpaka sasa ambao umeonekana kushindikana kutokana na wingi wa maji yaliyopo kwenye eneo hilo la Gulwe na Godegode lililopo Wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Stesheni hii Masta wa Kituo cha Reli Dodoma, Zakaria Kilombele alisema kuwa kutokana na hali hiyo ya ukarabati huo unaoendela kwa hivi sasa kwenye njia hiyo ya relishirika limeamua kuwasafisha abiria hao waliokwama kwa kutumia mabasi.

D.DOCTOR :AWASAA WASANII KUWA WABUNIFU.

January 10, 2014
Na Oscar Assenga,Tanga.
WASANII wa mziki wa BongoFleva nchini wametakiwa kuwa wabunifu na kubadilika kutokana na mazingira ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuutangaza mziki huo kitaifa na kimataifa kama ilivyokuwa kwa nchini nyengine duniani.

Wito huo ulitolewa na Msanii wa mziki huo mkoani Tanga,Dominick Mndeme “D.Doctor wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambapo alisema kutokuwa na umakini kwa wasanii wengi  kumewafanya kutoka na kuonekana kuwika kwa muda fulani na baadae kupotea kwenye tasnia hiyo kitendo ambacho kinachangia pia kushusha mziki huo.